Shadrack K. Lwila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2016
- 4,925
- 14,277
Mkuu hili swali sio la hovyo hata kidogo linahitaji tija ya kulifikiria sana kwa kina.Hili swali linaonekana la hovyo lakini linahitaji kufikiri sana. Nadhani sasa tuanze kuuliza yale maarifa tulipewa shuleni na vyuoni kama ni sahihi.
Kama ni mgandamizo tuu ambao unachangiwa na mawingu vipi kipindi cha masika ambacho hudumu hata miezi mitatu?
Anyway lazima tuanze upya kupitia elimu na maarifa yetu ikiwezekana tuwavunze vijana wetu kutafiti na kufikiri
Mfano wa mfanano wa swali kama hilo alilouliza mtoa mada, ambalo uwa najiuliza pia ni kuwa kama mvua inafanyika kwa kupitia mvuke kupanda juu, kisha mvua inajiunda kwenye mawingu na kisha kuyeyuka na kurudi chini kama mvua tena, na huo mzunguko ufanyika tena na tena. Ni sawa tu,lakini vipi kuhusu kiangazi mbona mvuke pia upanda juu lakini haurudi tena chini kama mvua???