Phillemon Mikael
Platinum Member
- Nov 5, 2006
- 10,518
- 8,583
Ninapokumbuka muziki na siasa namkumbuka msanii aliyevuma sana nchini , wakati huo hapakuwa na Diamond wala nani , huyu ni MARLAW alikuwa na kipaji sana na kuelekea kampeni za urais 2010 nyimbo zake zilikuwa HITS kwenye radio top ten zote
Mwaka 2010 alipata deal la kampeni akazunguka nchi nzima akiimba nyimbo zake HIT kwa kubadilisha na kuweka maneno ya kisiasa
Alipata pesa nyingi na kampeni zikaisha , kufikia mwaka 2011 mambo yalikuwa ni tofauti kwani hakuna mtu aliyetaka kusikiliza nyimbo zake wala show zake taratibu alipotea kwenye ramani ya muziki na kubakia zilipendwa. Bahati mbaya waliomtuma hawajamkumbuka kwani hata kampeni zilizofuatia za 2015 na sasa 2020 hakuna aliyekumbuka kumpa deal MARLAW
Tunayo tasnia yetu ya Bongo Movie ambayo kati ya mwaka 2005 hadi 2015 ilikuwa kwa kasi ,tatizo likaanza mwaka 2015 pale Bongo movie walipoanza kutumika kisiasa ..walipata deal kubwa sana na wakadhulumiana pesa ..kampeni ziliisha na wengi bongo movie wana miaka sita hawajatoa movie hata moja ...wanaishi kwa kuuzana , kupiga mizinga , kula pesa za rambi rambi na kusubiri kampeni ....leo tasinia ya filamu imefika sehemu mbaya kabisa ..hakuna maendeleo yoyote ..wakati ilikuwa inakuwa kwa kasi na walifikia hadi kupewa maeneo ya viwanja kwa ajili ya maendeleo yao.
Tunapoangalia haya basi ni vigumu kuacha kumuangalia DIAMOND na wasafi yake anayoimiliki kwa ubia na wafanyabishara wengine .., imegeuka kituo cha propaganda na yeye mwenyewe kageuka "capt john komba " tunatambua kuwa kalipwa vizuri na moja ya deal ni kukubaliwa kufungua vituo vya radio mikoani kwa kasi ya moto ..kwani ndani ya kampeni za mwaka huu pekee kafungua mikoa minne ndani ya siku 60 ikiwamo Mwanza , Mbeya na Arusha. Hii sio kawaida wakati vituo vingi tu vyenye uwezo maombi yao ya kufungua kwenye mikoa mingine yamekaliwa kwa miaka sasa yeye ndani ya miezi miwili kafungua vituo kama uyoga ili vitumike kwenye propaganda
Naona Kampeni zimeisha na anatangaza tena kuanza ziara nchi nzima ya "FIESTA" Wenyewe wanaita WASAFI TOUR ...Tofauti na ziara hii na ile ya kampeni ni kuwa wakati kwenye kampeni aliimba bure hii sasa atalipisha kiingilio....
MABIBI NA MABWANA KARIBUNI KWENYE WASAFI TOUR 2020
MUZIKI NA SIASA !!!
Mwaka 2010 alipata deal la kampeni akazunguka nchi nzima akiimba nyimbo zake HIT kwa kubadilisha na kuweka maneno ya kisiasa
Alipata pesa nyingi na kampeni zikaisha , kufikia mwaka 2011 mambo yalikuwa ni tofauti kwani hakuna mtu aliyetaka kusikiliza nyimbo zake wala show zake taratibu alipotea kwenye ramani ya muziki na kubakia zilipendwa. Bahati mbaya waliomtuma hawajamkumbuka kwani hata kampeni zilizofuatia za 2015 na sasa 2020 hakuna aliyekumbuka kumpa deal MARLAW
Tunayo tasnia yetu ya Bongo Movie ambayo kati ya mwaka 2005 hadi 2015 ilikuwa kwa kasi ,tatizo likaanza mwaka 2015 pale Bongo movie walipoanza kutumika kisiasa ..walipata deal kubwa sana na wakadhulumiana pesa ..kampeni ziliisha na wengi bongo movie wana miaka sita hawajatoa movie hata moja ...wanaishi kwa kuuzana , kupiga mizinga , kula pesa za rambi rambi na kusubiri kampeni ....leo tasinia ya filamu imefika sehemu mbaya kabisa ..hakuna maendeleo yoyote ..wakati ilikuwa inakuwa kwa kasi na walifikia hadi kupewa maeneo ya viwanja kwa ajili ya maendeleo yao.
Tunapoangalia haya basi ni vigumu kuacha kumuangalia DIAMOND na wasafi yake anayoimiliki kwa ubia na wafanyabishara wengine .., imegeuka kituo cha propaganda na yeye mwenyewe kageuka "capt john komba " tunatambua kuwa kalipwa vizuri na moja ya deal ni kukubaliwa kufungua vituo vya radio mikoani kwa kasi ya moto ..kwani ndani ya kampeni za mwaka huu pekee kafungua mikoa minne ndani ya siku 60 ikiwamo Mwanza , Mbeya na Arusha. Hii sio kawaida wakati vituo vingi tu vyenye uwezo maombi yao ya kufungua kwenye mikoa mingine yamekaliwa kwa miaka sasa yeye ndani ya miezi miwili kafungua vituo kama uyoga ili vitumike kwenye propaganda
Naona Kampeni zimeisha na anatangaza tena kuanza ziara nchi nzima ya "FIESTA" Wenyewe wanaita WASAFI TOUR ...Tofauti na ziara hii na ile ya kampeni ni kuwa wakati kwenye kampeni aliimba bure hii sasa atalipisha kiingilio....
MABIBI NA MABWANA KARIBUNI KWENYE WASAFI TOUR 2020
MUZIKI NA SIASA !!!