Muuza magazeti aliyedaiwa kuuawa maandamano Chadema aibuka

Mkuu kuzomea ndiyo adhabu yake ni kifo??? mbona Waziri Mkuu alizomewa lakini hakuna aliyeuawa?? sembuse polisi!!.....

Mkuu kuna post ililetwa humu kwamba watu 10 wamekamatwa kutokana na zomea zomea iliyompata Pinda!!Kama ni kweli,hatujui watapewa adhabu gani
 
Katika tafrani hiyo, kijana Zona, ambaye alikuwa anasoma magazeti aliuawa wakati Polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa CHADEMA.

Polisi walidaiwa kutumia risasi za moto na mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji.

Watu wengine waliojeruhiwa katika tafrani hiyo wameelezwa kuwa ni mwendesha baiskeli, Hashim Seif ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni akiwa anapita na baiskeli yake na kijana mwingine aliielezwa kuwa ni muuza matunda, Frank Valimba aliyejeruhiwa kwa kupigwa risasi tumboni.

Kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi wa madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, jeraha lililokutwa kwenye kichwa cha marehemu huyo lilitokana na kurushiwa kitu kizito.

Waw! Risasi za polisi zina akili sana, zenyewe huwa zinajetuhi tu miguuni na tumboni. Inashangaza hivi vitu vizito kwa nini havijifunzi kutoka risasi za polisi!
 
Kwa jinsi mwandishi alivyo andika inamaana huyo mmbeba mizigo hana dhamani kuliko muuza magazeti
 
Hilo ndo tatizo lako! hushughulishi huo mpira wa duara juu ya shingo yako,mwenyewe unaita kichwa,kufikiri na kuona beyound bounderies! unaamua moyo wako ukubali unachohisi ww kuwa ni sahihi! Think twice!
You dont seem to think even once so why cant think ten times to boost you empty head instead of telling noble thinks to think twice? Mh! stupid joke.
 
Huyu mwandishi wa hii habari ana udhaifu mkubwa sana. Aliyeuwawa na polisi ni Zona na hata huyo anayesema 'hakufa' anakiri aliyeuwawa ni Zona. The only pieace of infomation ya kusahihisha ni 'occupation' ya merehemu. Alichotakiwa kusema ni kwamba 'ajira' ya marehemu Zona haikuwa kuuza magezeti bali kubeba mizigo.

Hujagundua siku hizi ili kuuza gazeti inabidi utafute namna ya kuihusisha Chadema(au tukio la Chadema) na story yako. Anyway simlaumu mwandishi ndicho analipwa kufanya... Anamtumikia mwenye mbwa!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
This is clear evidence ...Ubarikiwe Kamanda kwa ushujaa wako...Ukweli utatuweka huru daima.......walioua ni Polisi na siyo Raia.Haya Nchimbi na Mwema here we go:rockon:
 
Utii wa sheria Bila shuruti Polisi Mupo juu ya sheria?Hivi mtu akikuzomea unampiga risasi?:A S 39:
 
Kumbe Polisi walighadhabika baada ya wafuasi wa CDM kuwazomea? kazi kweli kweli.

Kwa hiyo, mwananchi yeyote akimzomea polisi anastahili kupigwa risasi? Lakini pamoja na yote kwenye habari hii, nilicho-confirm kulingana na maelezo ya huyu muuza magazeti ni kwamba marehemu Ali aliuwawa kwa risasi na sio kitu kizito. RPC Moro nae anahitaji 'kuisadia polisi' hapa.
 
kwani alolazimisha kuandamana wakati polisi wamezuia ni nani? Tafakari,chukua hatua,usiwe unapenda kila unachokiona!
Kweli nyani haoni ***** lake!Hujiulizi! Hivi kwa nini walioandamana kama wameihalifu sheria ya nchi, mbona hawapelekwi sehemu husika?
 
kwani alolazimisha kuandamana wakati polisi wamezuia ni nani? Tafakari,chukua hatua,usiwe unapenda kila unachokiona!
Kama issue ni waandamanaji mbona wanaua wasoma magazeti na kujeruhi waendesha baiskeli. Mimi nafikiri kama maandamano ni ualifu basi wangesubiri wakati waandamanaji wamebeba mabango yao wawashamulie halafu wakatangaze kwenye vyombo vya habari kuwa tumeua waandamanaji kadhaa ambao walifanya uhalifu wa kuandamana.
 
Back
Top Bottom