Muungano wetu: Mgao wa Fedha za IMF na Zanzibar kupewa asilimia 18, ni sahihi?

Habari zenu wakuu?
Kama nitamkwaza mtu naomba nisamehewe lakini siwezi kukaa kimya.

Serikali imetoa mpangilio wa matumizi ya mkopo wa IMF , Tsh Trillion 1.3 za kitanzania.

Kama ifuatavyo;

(i). Sekta ya maji- Billion 139.4
(ii). Elimu -Billion 368.9
(iii). Afya - Billion 90.2
(iv).Jamii yenye maisha duni - Billion 5.5
(v). Makundi maalum - Billion 5
(vi). Shughuli za uratibu - billion 5

(vii). SERIKALI YA ZANZIBAR - BILLION 231

********************************************

* Yani Tanzania bara tupo zaidi ya million 55 ila jamii yenye mazingira magumu inapewa billion 5 wakati kwa takwimu za harakaharaka nadhani inakadiriwa waTz wenye maisha duni ni zaidi ya million 7. ni dhahiri hiyo hela haitoshi kbsa maana hata watu wa tasafu wanalipwa kiduchuuuuuu.

*Zanzibar ina wakazi zaidi ya 1 million kwanini fedha zote hizi ziende kwao ilihali serikali ingepunguza walau billion 100 na kuzijaza kwenye yafuatayo...

-mikopo ya vijana yenye riba nafuu au 0% riba

-kuongeza hela kwenye hiyo bajeti ya afya ili hospitali za wilaya na zahanati za kata vijijini vikapata vifaa pungukiwa.

-basi jamani hata walimu kadhaa wajengeeni nyumba za kukaa hata mbili tatu za kuzuga na hyo bilion 100

HAYO NI BAADHI AMBAYO YAPO KICHWANI KWANGU ILA NAJUA KILA MTU ANA YAKE AKILINI.

Ni nini faida ya muungano kwa Tanzania bara?


mzalendo wa kweli.
Hapa kwetu lita ya mafuta ya kula imefika 9000
mkate- 1300
soda -700
mchele wa kawaida 1kg-2200


Chanzo ya picha ya budget -TBC
maoni yaliongezewa - Mzalendo wa kweli

Nawasilisha.

Haya yote kayataka baba wa Taifa, akili yake haikuwaza sawasawa
 
Duh, kwa hiyo wakati wa kulipa, Zanzibar itabidi walipe hiyo Bil 231 au nani atalipa hiyo hela, maana ni mkopo ujue.

Bila shaka, Zanzibar hairuhusiwi kukopa, mkopo ukija wa JMT nao wanapewa chao, ila kuna tatizo, formula ipi inatumika? Sbb Zanzibar ina watu wachache sana, sasa naona hela kama kubwa sana inaenda huko.
 
Kero za Wazanzibar ni kupewa tu! hakuna hata siku moja wamedai kuwajibika.
Hawajui muungano unaendeshwaje lakini wanajua kugawana
Laah!
Kipindi cha siasa za unafiki nadhani ndiyo kinaelekea mwisho wake. Tutakapoondokana na hali hiyo, hapo ndipo tutakapoanza kwenda mbele kwa uhakika.
Nafarijika kwamba hakuna tofauti kati yetu kuhusu Muungano.
 
Tukome kiherehere! Kila siku watu kama kina Kikwete wamekaa kimya. Walifikiri raisi atatoka bara milele wakati kwenye katiba wameweka kipengele lazima makamu atoke Zanzibar. Hapo acha watukamue vya kutosha labda tutaelewa vizuri. Tunajidai eti tunawachagulia rais then what? Halafu nina swali kuntu... Hivi hizi hela huwa zinakaguliwa na CAG wetu? Au tunatoa then zinapotelea kinyemela nyemela Zanzibar maana nauona mwanya mweupeeeeee usio na kiulizi. Hazitakaa zifikishwe bunge la muungano na kule Zanzibar hatutakaa tusikie maana upinzani na serikali wanakula meza moja. Zidumu fikra za mwenyekiti Nyerere! ZIDUMU
 
Tuanzishe utaratibu wa Zenj kukopa Tanganyika na warudishe kwa ribà! Tanganyika ikope kwa jina LA muungano nà badala ya kugawana na Zanzibar wao wakopeTanganyika!! Mgao ni wa kutumia tu lakini mkopo ni wa kutumia na kurejesha!! Kwa Sasa kama ambavyo sekta ya Elimu inavyopata mgao na kutumia bila kurejesha ndivyo Zanzibar inavyopata mgao na kutumia bila kurejesha!!
 
Tuanzishe utaratibu wa Zenj kukopa Tanganyika na warudishe kwa ribà! Tanganyika ikope kwa jina LA muungano nà badala ya kugawana na Zanzibar wao wakopeTanganyika!! Mgao ni wa kutumia tu lakini mkopo ni wa kutumia na kurejesha!! Kwa Sasa kama ambavyo sekta ya Elimu inavyopata mgao na kutumia bila kurejesha ndivyo Zanzibar inavyopata mgao na kutumia bila kurejesha!!

Andika katiba mpya tufuate maoni yako
 
Hivi karibuni, kuna taarifa zilizowekwa wazi kwenye baadi ya vyombo vya habari, juu ya mgawanyo wa mikopo ya nje, kati ya Tanzania bara na Zanzibar.

Mkopo wa pesa ya Uviko 19, tunaambiwa Zanzibar ilipata 18%. Mkopo wa kutoka Japan, tunaambiwa Zanzibar imepata 30%.

Mkataba wa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, umeweka wazi kanuni ya mgawanyo wa mikopo na misaada kutoka nje, ambapo Zanzibar inastahili kupewa 4.5%.

Kama ni kweli Zanzibar ilipata 18% badala ya 4.5%, na pia ilipata 30% badala ya 4.5%, waliohusika wote, wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Katibu Mkuu Wizara ya fedha, walistahili wasimamishwe mara moja, na kama tungekuwa na Bunge, lilistahili kuunda kamati kuchunguza ukweli wa jambo hili, na kuchunguza uhusika wa Rais katika ukiukaji huu wa kanuni za Muungano.

Jambo la kujiuliza:

1) kwa hali hii ya sasa, ambapo nchi haina bunge linalowakilisha wananchi, nani ataihoji serikali?

2) kama trend itaendelea hivi, mpaka kufikia 2025, hali itakuwaje?

3) kama hiki ndicho kinachoendelea, hatuoni kuna njama za kuitumia Tanganyika kuijenga Zanzibar, na kuifanya Tanganyika kuwa 'kubwa jinga?'

4) Hali ikiendelea hivi, na bunge hatuna, nani ataweza kuhoji juu ya jambo hili?

5) Je, hatuoni kuwa kama hali hii ni kweli, mikopo hii inailenga Zanzibar, na Tanzania bara inatumika tu kama daraja, huku kisheria deni likiwa la kwake?

6) Japo hatuombei, kama kukiwa na njama ambazo zikafanya siku moja Muungano ufe, hatuoni hasara itakayokuwepo kwa Tanzania bara kwa sababu madeni haya yote mkopaji ni yeye, na hivyo ndiye atakayewajibika kulipa?
Watanganyika Wana hoja, wasikilizwe!

Wazanzibar Wana manung'uniko, wasipuuzwe!
 
Back
Top Bottom