Mwiba,

Kwanza napenda nikushukuru kwa uchambuzi wako yakinifu, ila mimi nilikuwa na swali moja tuu . Tafadhali nakuomba unipe maana( definition ) ya neno nchi .
Mbona dogo hilo ,ni rahisi unapoulizwa unatoka nchi gani ukasema ninatoka Tanzania na ikawa umemaliza na uliemjibu ikawa ameridhika ingawa hakuna Nchi inayoitwa Tanzania.
Ila ikiwa suala hilo hilo umeulizwa na msomi anefahamu Jiografia atakuuliza Tanzania bara(MainLand) au Zanzibar (Visiwani ) na ninaposema hakuna nchi inayoitwa Tanzania ninamaanisha Nchi iliyopo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Tanzania ni kifupi ila sijui kama unafahamu kirefu chake ndio nikasema hakuna kitu hicho Nchi iitwayo Tanzania labda kwa vichwa mchungu.
Natumai umefarijika la unataka maana kwa kilugha basi ni eneo la ardhi na zamani kulikuwa na Sukuma land matebele Land na nyenginezo hizo zikimaanisha eneo la ardhi la jamii ya watu fulani ,unajua ukitazama ramani za zamani sana hutaweza kuiona Tanganyika ila Zanzibar ilikuwepo ,Tanganyika nafikiri ilianza kuitwa hivyo kati ya miaka aliyozaliwa Nyerere.
Ila sasa wameongezea ili Nchi iwe Nchi sijui uwe na jeshi,uwe na mahakama,uwe na chombo cha kutunga sheria na mambo kibao ambayo kimsingi hayahitajiki ili uweze kuwa Nchi kwani hayo yote ni mambu ya kisasa na kisiasa ,mgawanyiko wa Urusi nchi zilizojitenga hazikuwa na mambo hayo tena sio kuwepo japo moja lakini hayakuwa na hata kipande ya mambo ambayo unataka yakamilike ili uweze kuwa nchi ,kilichowasaidia ni kule kule kwa zamani kuitwa Sukuma Land au Matebele Land na leo hii nchi hizo zilizojimegua kutoka Russia zimeweza kutengeneza mambu ya kisasa ili ziweze kutambuliwa. Zanzibar inayo mambo kibao ambayo hawa wa urusi hawakuwa nayo sasa iweje wazuke wazushi waseme Zanzibar sio Nchi kama si dharau ni kitu gani.Au mpaka iwepo Tanganyika ndio mjue kama Zanzibar ni nchi ,yaani hata kudai kurudi kwa Tanganyika huru mnataka wawasemee WaZanzibari.
 
Kwa hiyo Wazanzibar hawatambui uhalali wa Katiba nzima, si ndio? Ila wanavikubali vile vipengele vinavyowapa over-representation kwenye cabinet ya Muungano, na kwenye Bunge (wabunge woooote wa Zanzibar wana represent kaeneo kadogo kuliko wilaya moja ya Kahama) na wanakubali vipengele vinavyowafanya wabunge wao wapige kura kuhusu mambo ya watu wa Bara and so on and so forth (manake Bara hawana Bunge lao).

Sasa mtu ambae anakubali vipengele fulani fulani tu vya Katiba huyo utamwita jina gani huyo mtu?

Halafu Mwiba, je wewe unajua kile kipengele alicho kinukuu Pinda, Ibara ya Kwanza, unajua kilipitishwa vipi, na kilitakiwa kipitishwe vipi? Umesema kin Pinda hawana jibu, wewe unalo?
Wewe wacha kukurupuka ,sio waZanzibari peke yao wanayoibeza katiba bali Vyama vingi vya kisiasa vimesikika vikidai Katiba mpya ,sasa hawa nao niwaZanzibari au tuwaite punguani ,Katiba hii ni ya Chama kimoja,katiba hii imetokana na kutungwa kwenye mfumo huo wa Chama kimoja hivyo mambu yake mengi humo yatakuwa yakupitishwa bila kupingwa wala kuhojiwa maana ulikuwa ukianza kuhoji utaonekana wewe si mwenzetu au sio ?
Unapoambiwa kuondolewa kwa Raisi wa Zanzibar kuwa makamo wa kwanza kulipitishwa kimizengwe ,tatizo ni hilo hapo wote ni wa Chama kimoja na unapoonyoosha kidole kupinga baada ya kikao utaitwa pembeni kupewa maneno yako kama unataka kubalkia mbunge au unataka kurudi nyumbani kubaka inzi,tunaposema Katiba haifai basi fahamu kuwa mambo mengi yalipita bila kupingwa na sizani kama lipo lililopingwa labda lile la kina Kiwete ambalo walitaka kuirudisha Tanganyika huru.
Hivyo ndugu utanielewa nisemapo Katiba ya Tanzania haifai na misingi kuwa haifai ilijadiliwa na mtu mmoja tu ambae alikusanya mawazo mwenyewe akayachuja mwenyewe akaongezea mwenyewe mradi akayasanifu vile anavyotaka mwenyewe mtu mmoja mwenyewe ni CCM ndio ukamsikia Pinda kusema ngoja mambo haya atayarudisha CCM maana kwenye vyama vingi hayahusiki ni mambo yalioratibiwa na kukarabatiwa na CCM .
Upinzani wanaposema KATIBA itungwe upya sio wapumbavu wanajua chanzo cha KATIBA hii ni kulinda maslahi ya CHAMA TAWALA wanajua ndani yake kuna hatari kubwa ambayo inalinda vyanzo vya CCM ,wao ndio walioisimamia KATIBA hii bila ya kuwepo upinzani ndani yake si unakumbuka wakati ule wa Chama kimoja kulikuwa na picha ya Mgombea Uraisi mmoja tu katika karatasi ya kupigia kura upande wa Picha kuna NDIO na upande uliokuwa hauna Picha kuna HAPANA ,sasa maana yake unaijua ?
Ukiweka tiki kwenye NDIO inamaana umemkubali ndio yeye tu na ukiweka tiki kwenye HAPANA maana yake HAPANA mwengine, ila yeye tu.
Hivyo Raisi alikuwa hakataliki utakapoweka tiki kwa vyovyote vile utakuwa umemkubali na hiyo ndio maana ya Katiba iliyotungwa chini ya mfumo wa Chama kimoja.
Na ndio hapo sio WaZanzibari tu wanayoiona katiba hiyo haina faida kwao bali hata WaTAnganyika wengi wanaamini kuna upungufu mkubwa ndani ya Katiba inayotumika hivi sasa.
 
CUF wamvaa Mwinyi
na Mwandishi Wetu, Zanzibar

SIKU moja baada ya Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, mzee Ali Hassan Mwinyi, kueleza kuwa haelewi kuwa Zanzibar ni nchi au la, baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, kikiwamo Chama cha Wananchi (CUF), wamemjia juu na kusema anajua ukweli wa suala hilo.

Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Bimani, alisema chama hicho kimeshtushwa na kauli ya Mwinyi kuwa hajui Zanzibar kama ni nchi au la, kwa sababu amewahi kuwa rais wa Zanzibar na wa Jamhuri ya Muungano.

Alisema kauli hiyo inaweza kumpotezea sifa rais huyo mstaafu, kwani ni mmoja wa wazee wanaotajwa kuweza kuleta ufumbuzi wa tatizo hilo.

Hata hivyo, alisema msimamo wa CUF unabaki pale pale kwamba Zanzibar ni nchi na itaendelea kubaki hivyo hadi mwisho wa dunia.

"Mzee Mwinyi katuacha njia panda, lakini tunafahamu anajua ukweli, huwezi kuwa rais usifahamu mamlaka ya nchi unayoiongoza," alisema Bimani.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa NCCR - Mageuzi Zanzibar, Ambar Khamis, alisema Mwinyi anajua ukweli ila ameogopa kutoa msimamo huo hadharani.

"Inawezekana Rais mstaafu Mwinyi, hataki kueleza ukweli, kwa kuhofia asije akaziudhi pande mbili za Muungano. Wakati huu waasisi wa Muungano hawapo, yeye ndiye tulitarajia atuonyeshe njia, sasa kama yeye anakosa msimamo, nani mwingine anaweza kutusaidia kupata ukweli wake?" alihoji.

Alisema hakuna njia nyingine kwa sasa zaidi ya kuanzishwa kwa mahakama ya kikatiba, ili suala hilo likajadiliwe na kutolewa uamuzi.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Hamad Mussa Yussuf, alisema hakuna njia ya kutatua mvutano huo wa kikatiba zaidi ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuitisha mgogoro wa kikatiba.

Alisema Katiba ya Muungano na ya Zanzibar zinaonyesha kuwa zina mvutano katika kuitambua Zanzibar, kama nchi na kuwataka viongozi wakuu kuchukua hatua hiyo.

Tangu kuibuka mjadala juu ya Zanzibar ni nchi au si nchi, kumekuwa na mjadala mkubwa mitaani na wanasiasa kuitisha mikutano ya hadhara hapa Zanzibar na kupinga wazi kauli ya Waziri Mkuu Pinda aliyesema bungeni kuwa Zanzibar si nchi.

Wakati huo huo, CUF imelitaka Baraza la Wawakilishi kupitisha azimio la kuyarejesha katika mamlaka ya Zanzibar mambo yote 11 yaliyoongezwa katika orodha ya mambo ya Muungano, ambayo hayakuwamo katika makubaliano ya awali.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa chama hicho, Ismail Jussa Ladhu, katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Magomeni, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Jussa alisema makubaliano ya awali ya mambo ya Muungano yaliyokuwemo katika hati ya makubaliano hayo (Article of Union) yalikuwa 11, lakini baadaye yaliongezwa hadi kufikia 22.

Katika mkutano huo, Jussa alisema mkataba wa Muungano ambao aliuita kuwa ndiyo nguzo kuu na sheria mama ya Muungano, hautoi fursa kwa mamlaka yoyote kuongeza orodha ya mambo ya Muungano.

"Makubaliano ya Muungano ni mkataba wa kimataifa baina ya mataifa mawili, Zanzibar na Tanganyika. Hakuna mamlaka yenye uwezo wa kubadilisha makubaliano hayo isipokuwa mataifa hayo mawili yakikubaliana kufanya mabadiliko kwa utaratibu ule ule uliotumika mwanzo kufikia makubaliano hayo," alisema.

Alisema mambo ambayo yanapaswa kurejeshwa katika mamlaka ya Zanzibar ni fedha za kigeni, sarafu, mabenki, maliasili ya mafuta na gesi asilia, Baraza la Mitihani la Taifa na Elimu ya Juu.

Mambo mengine ni usafiri na usafirishaji wa anga, leseni za viwanda, utafiti, takwimu, vyama vya siasa na Mahakama ya Rufaa pamoja na utabiri wa hali ya hewa nchini.

Katika hatua nyingine, Jussa alifurahishwa na kitendo cha hivi karibuni cha Baraza la Wawakilishi kuchukua uamuzi wa kuliondoa suala la mafuta na gesi asilia katika orodha ya mambo ya Muungano.

Alisema kwa kutumia utaratibu huo huo Baraza linaweza kupitisha azimio la kuyarejesha katika mamlaka ya Zanzibar mambo mengine yote ya Muungano ambayo yameongezwa kinyume cha sheria.

Katika hali ya kushangaa, Jussa alisema uchumi na maendeleo si suala la Muungano, na hivyo Zanzibar imeachiwa jukumu la kuwaendeleza watu wake katika mambo kama elimu, afya, maji, ujenzi, nishati, kilimo, mawasiliano, uchukuzi, tawala za mikoa, ajira, habari, utamaduni na michezo, lakini nyenzo kuu za uchumi za kuwezesha kuyaendeleza mambo hayo zimedhibitiwa na upande wa Bara.

Alisema ni lazima Zanzibar iheshimiwe kama nchi kamili iliyoshirikiana na Tanganyika kuunda Jamhuri ya Muungano, au kama si hivyo, basi nchi hizo mbili zikubaliane kurudi katika hadhi zao kama zilivyokuwa kabla ya Muungano.
-------------------------------------
Hao ni CUF kama nilivyosema mwanzoni kuwa wanaoweza kulikabili suala hili na kuwajibu vitimba kwiri na uchovu wao ni CUF.Na Muungano utajengwa na kudumishwa na CUF na si vinginevyo mafisadi hawana hasara na maisha ya mtu wao wanajali maslahi yao binafsi tu ,Mwinyi amejitokeza kwa ajili ya kutaka kumtayarishia Mwanawe aende nae akawe Raisi wa Zanzibar maana kule kila ukiitetea CCM na kuweza kuwa tayari kuuwa basi ndio unapopewa zana za mauaji na serikali ya Muungano kwenda kuuwa uwatakao ili CCM ibakie madarakani ,halafu mnatarajia WaZanzibari wauone muungano ni lulu.
 
Hapana,

Tatizo sio muungano ila viongozi wasioona mbali na m bele. Soma shairi langu hapa chini:



Laiti nchi ingeliwa


Laiti nchi ingeliwa, nami nisingelala njaa,
Iwe ya utamu wa muwa, au ukali wa chang'aa,
Nami nisingechelewa, cha kwangu kujimegea,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Wajinga ndio waliwa, ni nani asiyejua?
Udamisi wabakia, ujinga kubishania,
Kitu kisichowasaidia, na hakitowasaidia,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Utawala usofaa, tena uliolemaa,
Ujinga huutumia, madarakani kubakia,
Na kura yake ni njaa, wasonacho kuhadaa,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Pilau huwapikia, wakala na kuvimbiwa,
Shibe mwana malevya, hata ya leo tu ikiwa,
Huabudu waheshimiwa, japokuwa wawaibia,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Vitenge huwagawia, shangwe wakazipewa,
Mtu alichoibiwa, iweje kuzawadiwa?
Kweli wajinga waliwa, na wachache wanajua,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Laiti inglikuwa, nchi hii ni haluwa,
Mie ningeliibugia, kila siku kuamkia,
Yangekuwa mazoea, kula,kullala na waa,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Mwanaharamu tambua, mwanasiasa akiwa,
Hana lililo uluwa,Ila vyote kuvamia,
Sio wa kuaminiwa, Wala kudhaminiwa,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Lakini kumbe balaa,Nchi ikiwa na njaa,
Kula haitotufaa,Na kunywa haijanyewa,
Na upwa mgaagaa,Maji tele, kiu baa,
Nisingelilala njaa,laiti nchi yaliwa!

Na miti ilipojaa,Viotani tumejaa,
Kujenga sio ukubwa,Na udogo sio jaa,
Kama huna manufaa,Binadamu ni kinaya,
Nisingelilala njaa,laiti nchi yaliwa!

Zanzibar nashangaa,Dubai bado haijawa,
Kisa wote twatambua,Viongozi wasiofaa,
Madungayembe kadhaa,Kisingizioi popobawa,
Nisingelilala njaa,lati nchi yaliwa!

Sasa watuhadaa,Zanzibar kula yafaa,
Mega wee na megua,Meno yote utang'oa,
Hakilikiki kisiwa,Msitufanye vichaa,
Nisingelilala njaa,laiti nchi yaliwa!

Tunahitaji bidhaa,Na huduma maridhia,
Visiwa kuendelea,Na bara Tanzania,
Heshima kujijengea,Kote katika dunia,
Nisingelilala njaa, laiti nchi yaliwa!

Siyo Mzee,
Dar es salaam
 
CUF wamvaa Mwinyi

na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

SIKU moja baada ya Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, mzee Ali Hassan Mwinyi, kueleza kuwa haelewi kuwa Zanzibar ni nchi au la, baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, kikiwamo Chama cha Wananchi (CUF), wamemjia juu na kusema anajua ukweli wa suala hilo.

Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Bimani, alisema chama hicho kimeshtushwa na kauli ya Mwinyi kuwa hajui Zanzibar kama ni nchi au la, kwa sababu amewahi kuwa rais wa Zanzibar na wa Jamhuri ya Muungano.

Alisema kauli hiyo inaweza kumpotezea sifa rais huyo mstaafu, kwani ni mmoja wa wazee wanaotajwa kuweza kuleta ufumbuzi wa tatizo hilo.

Hata hivyo, alisema msimamo wa CUF unabaki pale pale kwamba Zanzibar ni nchi na itaendelea kubaki hivyo hadi mwisho wa dunia.

“Mzee Mwinyi katuacha njia panda, lakini tunafahamu anajua ukweli, huwezi kuwa rais usifahamu mamlaka ya nchi unayoiongoza,” alisema Bimani.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa NCCR - Mageuzi Zanzibar, Ambar Khamis, alisema Mwinyi anajua ukweli ila ameogopa kutoa msimamo huo hadharani.

“Inawezekana Rais mstaafu Mwinyi, hataki kueleza ukweli, kwa kuhofia asije akaziudhi pande mbili za Muungano. Wakati huu waasisi wa Muungano hawapo, yeye ndiye tulitarajia atuonyeshe njia, sasa kama yeye anakosa msimamo, nani mwingine anaweza kutusaidia kupata ukweli wake?” alihoji.

Alisema hakuna njia nyingine kwa sasa zaidi ya kuanzishwa kwa mahakama ya kikatiba, ili suala hilo likajadiliwe na kutolewa uamuzi.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Hamad Mussa Yussuf, alisema hakuna njia ya kutatua mvutano huo wa kikatiba zaidi ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuitisha mgogoro wa kikatiba.

Alisema Katiba ya Muungano na ya Zanzibar zinaonyesha kuwa zina mvutano katika kuitambua Zanzibar, kama nchi na kuwataka viongozi wakuu kuchukua hatua hiyo.

Tangu kuibuka mjadala juu ya Zanzibar ni nchi au si nchi, kumekuwa na mjadala mkubwa mitaani na wanasiasa kuitisha mikutano ya hadhara hapa Zanzibar na kupinga wazi kauli ya Waziri Mkuu Pinda aliyesema bungeni kuwa Zanzibar si nchi.

Wakati huo huo, CUF imelitaka Baraza la Wawakilishi kupitisha azimio la kuyarejesha katika mamlaka ya Zanzibar mambo yote 11 yaliyoongezwa katika orodha ya mambo ya Muungano, ambayo hayakuwamo katika makubaliano ya awali.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa chama hicho, Ismail Jussa Ladhu, katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Magomeni, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Jussa alisema makubaliano ya awali ya mambo ya Muungano yaliyokuwemo katika hati ya makubaliano hayo (Article of Union) yalikuwa 11, lakini baadaye yaliongezwa hadi kufikia 22.

Katika mkutano huo, Jussa alisema mkataba wa Muungano ambao aliuita kuwa ndiyo nguzo kuu na sheria mama ya Muungano, hautoi fursa kwa mamlaka yoyote kuongeza orodha ya mambo ya Muungano.

“Makubaliano ya Muungano ni mkataba wa kimataifa baina ya mataifa mawili, Zanzibar na Tanganyika. Hakuna mamlaka yenye uwezo wa kubadilisha makubaliano hayo isipokuwa mataifa hayo mawili yakikubaliana kufanya mabadiliko kwa utaratibu ule ule uliotumika mwanzo kufikia makubaliano hayo,” alisema.

Alisema mambo ambayo yanapaswa kurejeshwa katika mamlaka ya Zanzibar ni fedha za kigeni, sarafu, mabenki, maliasili ya mafuta na gesi asilia, Baraza la Mitihani la Taifa na Elimu ya Juu.

Mambo mengine ni usafiri na usafirishaji wa anga, leseni za viwanda, utafiti, takwimu, vyama vya siasa na Mahakama ya Rufaa pamoja na utabiri wa hali ya hewa nchini.

Katika hatua nyingine, Jussa alifurahishwa na kitendo cha hivi karibuni cha Baraza la Wawakilishi kuchukua uamuzi wa kuliondoa suala la mafuta na gesi asilia katika orodha ya mambo ya Muungano.

Alisema kwa kutumia utaratibu huo huo Baraza linaweza kupitisha azimio la kuyarejesha katika mamlaka ya Zanzibar mambo mengine yote ya Muungano ambayo yameongezwa kinyume cha sheria.

Katika hali ya kushangaa, Jussa alisema uchumi na maendeleo si suala la Muungano, na hivyo Zanzibar imeachiwa jukumu la kuwaendeleza watu wake katika mambo kama elimu, afya, maji, ujenzi, nishati, kilimo, mawasiliano, uchukuzi, tawala za mikoa, ajira, habari, utamaduni na michezo, lakini nyenzo kuu za uchumi za kuwezesha kuyaendeleza mambo hayo zimedhibitiwa na upande wa Bara.

Alisema ni lazima Zanzibar iheshimiwe kama nchi kamili iliyoshirikiana na Tanganyika kuunda Jamhuri ya Muungano, au kama si hivyo, basi nchi hizo mbili zikubaliane kurudi katika hadhi zao kama zilivyokuwa kabla ya Muungano.
 
Mwiba,
Tatizo la Tanzania umeliweka kwa Wabara na Wazanzibar hapo kidogo mimi nakuwa mgumu kukubaliana na wewe pamoja na kwamba una sababu za maana kuweka hoja zako.
Wanaokalia Uchumi wa nchi hizi mbili hadi leo hii ni Viongozi. Uongozi wa Karume unavuna wasichokipanda huko Unguja na Pemba huku Bara tunao kina Mkapa ambao walihakikisha wanachukua kila kilicho pandwa. Hakuna mmoja wetu anayefaidika na kitu chochote, hivyo sidhani kama ni uungwana kutumia jina la Bara na Visiwani wakati adui wa haki zetu tunamruka kutafuta mchawi nje..

Kama jamiii moja ni muhimu tutazame matatizo ya Uongozi Tanzania kama TAIFA moja kwanza kabla hatujafika mbali. Madini ya Bara hayawapi manufaa wananchi wa bara wala sehemu zinazochimbwa zaidi ya kuwaachia Mashimo. Kilio ulichonacho wewe leo hii ndio wanacho hata wakazi wa Bulyanhulu, Mafia na kwingineko ambako rasilimali zao zinachotwa.
Mimi nadhani tatizo kubwa la Muungano sio mgao isipokuwa Uongozi wetu sote bara na Visiwani ambako kila mmoja wao anatazama maslahi yake. Tukianza kutenganisha makosa haya na Muungano nadhani tutafikia suluhu fulani kwa sababu ni MUHIMU kwanza kutambua Zanzibar ni nchi Kwa tafsiri yetu wenyewe sio ya mkoloni) na kuwapa madaraka yanayohusiana na Utawala mdogo ndani ya Jamhuri kama zilivyo nchi nyingezo ktk Muungano uwe wa Breat Britain, USA, Canada, Australia na kadhalika... Tusiige mfano mmoja tu.
Miungano ya nchi hizo imezifanya kuwa imara zaidi na hakuna hata mtu mmoja anaweza kusema leo ati Scotland sio nchi, ama Ontario sio nchi Canada ama Texas sio nchi Marekani kulingana na tafsiri ya katiba ya nchi hizo. sasa baada ya kuwa na tafsiri kamili ndipo nguvu ya serikali hujengwa kutazama maslahi ya eneo linalohusika. tatizo la Tanzania kwa sababu hatuna serikali tatu tumejenga Uhasama. Serikali kuu bado inapewa madaraka ama mamlaka ya territorial kiasi kwamba tumeshindwa kufahamu sheria inayoiziunganisha nchi hizi. Hadi leo hii kweli bado tumefikia kwamba mtu anataka kuipindua serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kisheria imeshindikana kupatiwa ufumbuzi kwa sababu hawajui (kisheria) kama Zanzibar ni nchi..Huo mwanzo.

Tunapoongelea haya maswala ya mgao wa kiuchumi ni lazima tuwe makini sana. Mkuu hadi sasa hivi sikubaliani na ukweli kwamba madai ya Zanzibar yanaleta mantiki hasa pale tunapozingatioa kwamba hadi sasa Zanzibar wanafaidi mengi toka Bara kwa msemo usemao Changu Changu chenu chetu..Na bara wamekuwa ktk mfumo huo kukubali matokeo ya kutokuwa na serikali tatu.
Mimi naomba kitu kimoja tu. Msomi yeyote toka Zanzibar anambie Zanzibar haifaidiki vipi na Madini ya Bara kwa sababu hakuna madini yanayomilikiwa na serikali ya Bara isipokuwa watu binafsi ambao wanalipa Kodi... Je, ni ktk mchanganuo upi Wazanzibar wameweza kuona kwamba mchango wa madini kama kodi haufiki Zanzibar. Wameweza kutenganisha vipi mkusanyiko wa kodi zote na kutenga madini kuwa hawapewi kinachoingia kama kodi wakati Zanzibar ina wabunge wake ktk bunge la Taifa...
Naomba kueleimishwa katika hilo maanake yawezekana mimi natazama shilingi tofauti kabisa na ile walioishika Wazanzibar!

mkandara,
nilipotea muda kutokana na shughuli za hapa na pale na bado hazijaisha ila nimetupa macho na kuuona huu mjadala, japo kwamba imeniwia tabu kuusoma na kuupima kimantiki wote , lakini , nimeona nidandie hapa njiani.,
umeomba uelimishwe ni vipi zanzibar hainufaiki na muungano ,, lakini umeshindwa kuonesha ni vipi zanzibar inanufaika na muungano?, nakuomba usiuegemeze uchumi wa nchi za kiafrika na kodi, japo kama kodi ni moja ya vipengele vya uchumi wa nchi yoyote duniani, na pia nakuomba ichukulie zanzibar kwamba iliungana na tanganyika as a free state ambayo kama haikuungana basi leo hii tungekuwa tunaongelea zanzibar yenye benki kuu inayotambulika, balozi fungamano na nchi za nje , msaada wa asilimia 100 as a free state, independent authority ya kupata misaada n.k., sasa kwenye maongezi yako si vyema ukaifananisha zanzibar na mkoa wa dodoma as far as history and zanzibar status b4 union is concerned!
hamna haja ya kufichana ,muungano hausaidii lolote kwa wazanzibari, ninachoomba ni marekebisho ambayo yatarejesha hadhi ya zanzibar kimataifa, niliwahi kuongea kipindi cha nyuma , "hakuna serikali ya muungano bali kuna serikali ya tanganyika iliyobeba jina la muungano", je yupo anaebisha?
 
Zanzibar debate in new twist
By Salma Said, Zanzibar
THE CITIZEN

Debate on the Union yesterday took a new turn after the opposition Civic United Front (CUF) urged representatives in the Isles legislature to pass a motion to remove 11 matters said to have been irregularly incorporated into the original Articles of Union.

CUF argues that the additional matters were not part of the 11 Articles of Union as agreed upon when Tanganyika and Zanzibar merged to form the United Republic of Tanzania in 1964.

Addressing a public rally in Zanzibar, CUF director of foreign affairs and cooperation Ismail Jussa said the additions were made without following the law and were therefore invalid.

He said the Union Constitution had no provisions for other matters to be added in the original document.

The Union agreement is a binding contract between the former two states. No authority has the powers to change such an agreement unless the two sides agree to do so using the same procedures that led to the Union, he said.

He listed the added matters as banking, foreign exchange, oil and gas, currency, civil aviation, higher education, research, statistics, industrial licenses, meteorological issues, Court of Appeal and political parties.

Mr Jusa said the House of Representatives had done commendably well to remove oil and gas from Union matters, insisting that the same method be used to implement his party's proposal.

While debating the Water, Construction, Energy and Land ministry's budget, CCM and CUF Representatives supported remarks by minister Mansour Yusuf Himid oil, if discovered, will remain the property of Zanzibar, just as minerals are to the Mainland.

Mr Jusa wondered why economy and development were not part of Union matters, living the Zanzibar government struggling to improve the welfare of its people.

Institutions such as the Bank of Tanzania and Tanzania Revenue Authority do not see themselves as Union institutions, he lamented.

He added that Zanzibar has to be respected as a country that merged with the former Tanganyika to form the Union or else the two partners should abandon the merger and return to their former status.

Mr Jussa said the misunderstanding by Prime Minister Mizengo Pinda and many academicians on the Mainland is due to taking the Union Constitution as the principal document.

He said the Union Constitution is full of significant mistakes resulting from misinterpretation of an international contract that formed the Union.

He resented those who call for an end to the debate on the Isles status. Earlier, CUF vice-chairman Mr Machano Khamis Ali said Zanzibaris should thank Mr Pinda for awakening them on the issue.

He also called President Amani Karume to make a formal statement on the Isles status.
 
Date::7/28/2008
Umoja wa Mataifa unaitambua Tanzania siyo nchi ya Zanzibar

Frederick Katulanda, Mwanza
Mwananchi

SAKATA la hadhi ya Zanzibar kama ni nchi au la, limezidi kupamba moto baada ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Dk Asha-Rose Migiro, naye kujitosa katika mjadala huo kwa kusema nchi inayotambuliwa na Umoja huo ni Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na wala si Zanzibar.

Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Mwanza katika hoteli ya Tilapia, Dk Migiro alisema katika kanuni za UN nchi zinatambulika kutokana na uanachama wake na kwa Tanzania wao wanaitambua Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni mwananchama wao na siyo Tanganyika wala Zanzibar.

''Kila nchi inastaili yake ya kujiunga, hapa sisi tunaitambua Jamhuri ya Muungano na wala si vinginevyo,'' alisema Dk. Migiro.

Alisema mjadala unaoendelea hapa nchini ni masuala ya ndani ya nchi na kwamba si mjadala wa kwanza kwa nchi wanachama wa UN kwani nyingi zimekuwa katika migogoro kama hiyo wakijadiliana na wengine hata kufikia uamuzi wa kuvunja muungano wao.

''Mfano nchi kama Marekani ambayo inayo majimbo mengi inatambulika kama mwananchama wa Umoja wa Mataifa, huo ni mfumo wake, na mfumo wa utawala uliopo Tanzania ni ule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na uwakilishi wake Umoja wa Mataifa ni kupitia Jamhuri ambayo inatambulika kama Tanzania iliyo mwanachama wao,'' alieleza Dk Migiro.

Sakata la hadhi ya Zanzibar lilishika kasi baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutoa kauli bungeni akisema kwamba Zanzibar si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mara baada ya kauli hiyo, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walianza kumshambulia kwamba amekosea kudai kuwa Zanzibar si nchi.

Baadaye Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Iddi Pandu Hassan, alitoa kauli ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) akisema kwamba Pinda alikuwa ameteleza kwani anajua fika kuwa Zanzibar ni nchi.

Katika maswali ya papo hapo kwa Waziri Mkuu, wabunge walimuuliza kama kweli alikuwa ameteleza, aliweka msisitizo kwamba ni kweli Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa katiba ya nchi.

Pinda aliwaagiza Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, Johnson Mwanyika na wa SMZ kukutana kwa nia ya kutoa tafsiri sahihi kuhusu maneno ambayo yanachanga watu ya ''state, nchi na sovereign''.

Kauli ya Pinda iliilazimu SMZ kutoa tamko la serikali kupitia kwa Naibu Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Ali Juma Shamuhuna, kwamba visiwa hivyo vya Unguja na Pemba ni nchi.

Jaribio la tatu la kumtaka Pinda kueleza kama Zanzibar si nchi liligonga mwamba bungeni baada ya Spika kusema kwamba mjadala huo ulikuwa umefungwa kutokana na ukweli kwamba Waziri Mkuu alikuwa amekwisha kulitolea maelezo. Pinda alisema anafikiri suala hilo sasa litachukuliwa na chama chake, CCM, na kulitolea tamko.

Mvutano huo ukizidi kuumuka, jana Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, alisema chama hicho hakitatoa tamko kuhusu hadhi ya Zanzibar kama alivyotaka Waziri Mkuu kwa kuwa hakioni haja ya kufanya hivyo.

Makamba aliliambia gazeti hili jana kuwa kauli ya Pinda ni maoni ambayo utekelezaji wake unategemea haja na sababu za msingi.

''Katika kikao chake chochote (Kikso cha Kamati Kuu), CCM haitajadili na kutoa tamko la hadhi ya Zanzibar kama alivyotaka Pinda kwani haijaona haja ya kufanya hivyo,'' alisema Makamba.

Akithibitisha kauli yake kwamba agizo la Pinda ni maoni, Makamba alisema tangu aitoe bungeni Julai 24 mwaka huu, hajawasiliana na CCM kwa ajili ya utekelezaji.

"Pinda anatoa maoni na mimi sijawasiliana naye kwa barua wala ana kwa ana kama mtendaji wa CCM na kujadili kauli hiyo," alisema Makamba.

Makamba alitoa kauli hiyo kufuatia gazeti hili kumtaka aseme endapo agizo la Pinda kwa CCM kutolea tamko suala la Zanzibar ni moja ya agenda za Kikao cha Kamati Kuu ya CCM ambayo inatarajiwa kukutana wiki hii.

Pinda aliitwisha CCM mzigo wa kutolea tamko suala hilo baada ya hoja hiyo kumfika shingoni na kuamini kwamba kwa jinsi suala hilo linavyochukuliwa, baadhi ya watu hawamtakii mema.

Uamuzi wa Pinda wa kuelekeza hoja ya hadhi ya Zanzibar kwa CCM aliufikia bungeni Julai 24, mwaka huu baada kukataa kujibu maswali ya wabunge yaliyomwelekeza kwenye hoja hiyo.

Wa kwanza alikuwa ni Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Juma Mnyaa aliyemtaka Waziri Pinda kutumia uzoefu wake wa kufanya kazi Ikulu na taaluma yake ya sheria kueleza nini kiko juu kati ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Mkataba wa Muungano.

Baada ya swali hilo, Pinda ambaye amejizolea umaarufu wa kujibu maswali ya wabunge kwa utulivu na umakini, alishusha pumzi na kusema: "Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mnyaa hanitakii mema, leo (Julai 24) nimesikia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imezima maandamano dhidi ya Pinda, sasa sikutaka sana kuliendeleza hili.

''Chochote nitakachokujibu nitakuwa nikizidi kuendeleza malumbano juu ya jambo hili, tayari niliagiza wanasheria wakuu wakae na kuliangalia hili, sasa kuanza tena kulijadili, ahaa�''


Hata hivyo, Pinda alisema kutokana na mwelekeo wa mjadala huo kuchukua taswira tofauti, ni vema CCM ikalichukua suala hilo, kulijadili na kutolea kauli.


Kauli ya Pinda ilipingwa na Mbunge wa Konde (CUF), Dk. Ali Tarab Ali, ambaye alihoji mantiki ya CCM kutolea kauli suala hilo kwani si la kisiasa bali la wananchi.

Tarab alipendekeza mjadala wa kitaifa kuhusu suala la Muungano kabla ya mambo hayajaharibika badala ya kuiachia CCM.

Naye mbunge wa Chambani (CUF), Salim Hemed Khamisi, alijaribu kuibua suala hilo kwa mlango wa nyuma pamoja na Spika wa Bunge kulizima ingawa hakugusia suala la Muungano hasa kama Zanzibar ni nchi au la.

Tangu Pinda atoe kauli kwamba Zanzibar si nchi, umeibuka mjadala mkali ambao unaonyesha kuutikisa Muungano, kutokana na baadhi ya wanasiasa kutaka Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Amani Abei Karume, atoe kauli juu ya utata huo.

Miongoni mwa wanasiasa kwa upande wa CCM waliojitokeza kuzungumzia suala hilo njia ya Bunge ni Mkuu Kitengo cha Propaganda, Hizza Tambwe, aliyemuunga mkono Waziri Mkuu kwamba Zanzibar si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hadi sasa Wazanzibari bila kujali itikadi zao za vyama wameungana kumjia juu Pinda kwa kusema ameshusha hadhi ya visiwa hivyo, huku wengine wakienda mbali wakimtaka Rais Karume aitoe Zanzibar kwenye Muungano.

Katika hatua nyingine, akizungumzia taarifa zaa ufisadi zilizozagaa hapa nchini, Dk Migiro alisema wao kama UN wamekuwa watazamaji tu kutokana na kuwa ni suala la ndani ya nchi, lakini wamekuwa wakifuatilia kwa ukaribu zaidi ili kujua hatma yake.

Alisema kuwajibika kwa kiongozi kama ilivyokuwa kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa ni sehemu ya demokrasia na uwajibikaji kwa mtu yoyote anayejali na kuheshimu utawala bora na sheria.

''Sisi kama Umoja wa Mataifa tunaangalia kwa makini kwa sababu inapotekea amani ikavujika katika nchi tunaingilia kwa sababu msingi mikuu ya UN ni amani na usalama na maendeleo ya nchi, hivyo inapotokea jambo ndani ya nchi Umoja wa Mataifa huwa hauingilii bali unayatazama kwa makini kama hili la kujiuzulu kwa viongozi,'' alisema.
 
Ni sawa kabisa alivyosema huyo mwanamama ambae anatafuta umaarufu lakini nampa muda subiri jawabu kutoka kwa WaZanzibar na asipoangalia basi anaweza akanuka mivi.
Vipi amesema kama inavyotakiwa na sivyo ilivyoandikwa kwenye kichwa cha habari ,inataka mtu anesoma between the line na kuweza kung'amua mapema yaliokusudiwa.
Gazeti limeandika Inatambuliwa Tanzania wakati sio ukweli Mwanamama katika maneno yake yote hajateleza na kusema kuwa inatambuliwa kama Tanzania bali kila alipohusisha alisema inatambuliwa kama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,hivyo vichwa mchungu wasioweza kutofautisha na kupandwa na jazba wanaweza kukurupuka na kusema ..mnaona hata umoja wa Mataifa hawaitambui Zanzibar ,naona ndio hivyo matumbili yakitaka kufa miti yote huwa inateleza.
Ila naona ni harakati za akina kakakazi wa Kikwete Butiama team wakizidi kuwateketeza wahafizina baada mshiko wa Kikwete kupigwa na chini jambo ambalo limepeleka kauli zake zote na ahadi za ndani na nje ya nchi za kusawazisha mpasuko wa Zanzibar kuonekana ni uwongo mbaya sana kwa kiongozi.
Hivyo msiwe na pupa Zanzibar ipo na inawakilishwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama alivyosema mwanamama na nawashangaa sana watu wanaokurupuka ni sehemu nyingi tu inasemwa kama Zanzibar inawakilishwa ila sijasikia Tanganyika kama inawakilishwa msifanye zarau jitahidini kukamata chenu na mujitahidi katika kuirudisha Tanganyika huru mtegemea cha ndugu hufa masikini kuna hatari muungano ukavunjika wakati mafisadi wameshawateka WaTanganyika wote na huo utakuwa wakati mgumu kuidai kurudi kwa Tanganyika huru na pimeni kwa kituo ili muone ukweli hawa watu ambao hivi sasa wanashika kasi katika kuiteka Tanganyika kila sehemu wamo katika future plan na wakifanikiwa itawawia vigumu sana kwa akina Ztto na wenziwe kupata pumzi na upenyo wa kuwafurusha mafisadi kwani mafisadi watakuwa wameshateka kila kitu ,hizi mbio wanaisaka Zanzibar ambayo nahisi wameona kama hawakuisakama Zanzibar basi huenda mipango yao isifanikwe.
Kuweni macho na wanaozima hoja za kuitangaza na kuidai Tanganyika huru ,uhuru wake umetekwa na mafisadi au hamuoni maana inawezekana mna macho lakini hamna mkionacho ,mnabaki kutumuwa mijicho kumbe hamuoni chochote,poleni sana.
 
Hata akifufuka Nyerere wacha kisumo alieko hai,hawa ndio mafisadi waliojificha lakini Tanganyika inakuja mafisadi tafuteni pa kujificha la si hivyo mtakwenda Jela tu.
 
Baadhi ya Kampuni za zenj zinazofaidi Muungano...
Image651.jpg

 
Ni sawa kabisa alivyosema huyo mwanamama ambae anatafuta umaarufu lakini nampa muda subiri jawabu kutoka kwa WaZanzibar na asipoangalia basi anaweza akanuka mivi.
Vipi amesema kama inavyotakiwa na sivyo ilivyoandikwa kwenye kichwa cha habari ,inataka mtu anesoma between the line na kuweza kung'amua mapema yaliokusudiwa.
Gazeti limeandika Inatambuliwa Tanzania wakati sio ukweli Mwanamama katika maneno yake yote hajateleza na kusema kuwa inatambuliwa kama Tanzania bali kila alipohusisha alisema inatambuliwa kama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,hivyo vichwa mchungu wasioweza kutofautisha na kupandwa na jazba wanaweza kukurupuka na kusema ..mnaona hata umoja wa Mataifa hawaitambui Zanzibar ,naona ndio hivyo matumbili yakitaka kufa miti yote huwa inateleza.
Ila naona ni harakati za akina kakakazi wa Kikwete Butiama team wakizidi kuwateketeza wahafizina baada mshiko wa Kikwete kupigwa na chini jambo ambalo limepeleka kauli zake zote na ahadi za ndani na nje ya nchi za kusawazisha mpasuko wa Zanzibar kuonekana ni uwongo mbaya sana kwa kiongozi.
Hivyo msiwe na pupa Zanzibar ipo na inawakilishwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama alivyosema mwanamama na nawashangaa sana watu wanaokurupuka ni sehemu nyingi tu inasemwa kama Zanzibar inawakilishwa ila sijasikia Tanganyika kama inawakilishwa msifanye zarau jitahidini kukamata chenu na mujitahidi katika kuirudisha Tanganyika huru mtegemea cha ndugu hufa masikini kuna hatari muungano ukavunjika wakati mafisadi wameshawateka WaTanganyika wote na huo utakuwa wakati mgumu kuidai kurudi kwa Tanganyika huru na pimeni kwa kituo ili muone ukweli hawa watu ambao hivi sasa wanashika kasi katika kuiteka Tanganyika kila sehemu wamo katika future plan na wakifanikiwa itawawia vigumu sana kwa akina Ztto na wenziwe kupata pumzi na upenyo wa kuwafurusha mafisadi kwani mafisadi watakuwa wameshateka kila kitu ,hizi mbio wanaisaka Zanzibar ambayo nahisi wameona kama hawakuisakama Zanzibar basi huenda mipango yao isifanikwe.
Kuweni macho na wanaozima hoja za kuitangaza na kuidai Tanganyika huru ,uhuru wake umetekwa na mafisadi au hamuoni maana inawezekana mna macho lakini hamna mkionacho ,mnabaki kutumuwa mijicho kumbe hamuoni chochote,poleni sana.

Kazi kweli kweli
 
Ngoja niwaambieni,
wanaoshabikia kuuendeleza mjadala wa zanzibar ni nchi si lolote zaidi ya uhuni na uzandiki na zaidi zaidi wananufaika na kuvunjika kwa muungano.
Huu ni ulevi wa kimadaraka... badala ya kuboresha muungano wao wanahubiri kuuvunja.... them think can survive one on but will take couple to acomplish unification...
tufike mahala viongozi kama Seif, Shamhuna na wengineo wenye mawazo mgando tuwaepuke kwani wanaelekea kubaya ambapo ndipo walipopachagua...
 
NYERERE WAS RIGHT....! Jana tarehe 28 majira ya saa mbili na robo usiku nikiwa na redio yangu mkulima, nilisikiliza kipindi kilichorushwa hewani na TBC maarufu kama WOSIA WA BABA....!
Katika maneno ya mwalimu utagundua kuhusu mjadala unaoendelea. Vile vile hotuba ya SISI WAZANZIBARI WAO WATANGANYIKA nayo inabidi iambatane na ile ya jana.
KUNA MASLAHI BINAFSI NA SI YA WANANCHI KTK HOJA HII...!
 
naomba mtu anipe: (akitenganisha bara na visiwani)
1. faida/hasara za muungano huu
2. faida/hasara za kuuvunja

Naomba legacy ye nyerere isiwe mojawapo ya vigezo.
 
Gazeti limeandika Inatambuliwa Tanzania wakati sio ukweli Mwanamama katika maneno yake yote hajateleza na kusema kuwa inatambuliwa kama Tanzania bali kila alipohusisha alisema inatambuliwa kama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,hivyo vichwa mchungu wasioweza kutofautisha na kupandwa na jazba wanaweza kukurupuka na kusema ..mnaona hata umoja wa Mataifa hawaitambui Zanzibar ,

Do. Hapa Mheshimiwa Mwiba umeeleza. Ndivyo ilivyo hivyo.
 
Ngoja niwaambieni,
wanaoshabikia kuuendeleza mjadala wa zanzibar ni nchi si lolote zaidi ya uhuni na uzandiki na zaidi zaidi wananufaika na kuvunjika kwa muungano.
Huu ni ulevi wa kimadaraka... badala ya kuboresha muungano wao wanahubiri kuuvunja.... them think can survive one on but will take couple to acomplish unification...
tufike mahala viongozi kama Seif, Shamhuna na wengineo wenye mawazo mgando tuwaepuke kwani wanaelekea kubaya ambapo ndipo walipopachagua...
Sasa ikiwa juhudi zote za kuuboresha zinagonga ukuta unategemea nini ,maana kinachoonekana sio kuboresha ni kuboronga ,vipi nafasi ya Raisi wa Zanzibar ambayo kwa ukweli ndio moja ya mhimili mkuu wa Muungano mnakwenda kuichezea.
Zanzibar haikuunganishwa Zanzibar imeungana ,sasa tofauti ya Kuungana na kuunganishwa sijui kama mtaiona.
 
Dk. Migiro either ameboronga au amekuwa misquoted.

Nchi haiwezi kuwa mwanachama wa UN kama nchi hiyo si nchi sovereign, that is true.

Lakini at the same time kutokuwa mwanachama wa U.N hakumaanishi kwamba wewe si nchi sovereign. U.N ni taasisi ya kimataifa kama nyingine nyingi, kuna nchi sovereign kama Switzerland ambazo kutokana na principles zake za neutrality na interests zake za banking zimeamua kutokuwa member wa U.N and many international organizations such as the E.U, NATO, SHENGEN and what not.Hii ni kwa sababu wa Swizi hawataki mikataba ya taasisi hizi iwafunge, hawataki ku abide to U.N resolutins ambazo zinaweza kuwa na implications kwenye banking industry yao na vitu kama hivyo.

Kwa hiyo kuleta issue ya uanachama wa U.N, which insinuates that as a criteria ya ku determine kama Zanzibar ni nchi au siyo at best ni upotoshaji.

Mwandishi anaruka left right and center lakini haja address swala muhimu, nini kinafanya nchi kuwa nchi?
 
Hivi wanataka Makamu wa Rais wa Jamhuri awe "BALOZI" wa Zanzibar nchini Tanzania? Na akina Dr. Hussein wawe "WAAMBATA" wa kijeshi au?
 
Back
Top Bottom