Nchi Yetu Ni Huru Na Hawa Cuf Tutapambana Nao Kwa Hoja Na Nguvu Zote Lakini Suala La Muafaka Kwa Sasa Wasahau Tanzania Ina Mengi Ya Kujadili Na Kuyafanyia Kazi Zaidi Ya Huo Muafaka
Asante sana msemaji wa CCM (Maana ndio kazi Shy uitakayo),basi tusubiri tuone maana wahenga walisema "ASIYE FUNZWA NA MAMAYE HUFUNZWA NA ULIMWENGU"
 
Jamani Hiyo Zanzibar Sio Mali Ya Cuf Au Lipumba Au Nani

Zanzibar Ni Moja Ya Nchi Zinazounda Tanzania Na Ni Mali Ya Watanzania

Huyu Anayesema Mambo Sio Shwari Nawasi Wasi Na Uzalendo Wake Anapotosha Watu Kwa Makusudi Kwa Dhamira Zile Zile Changanishi Ambazo Kwa Asili Watanzania Hatuna Hulka Hizo

pia anyesema zanzibar ni shwali nina wasi wasi naye na nina wasiwasi na uzalendo wake halisi katika kutetea haki na uhuru wa wananchi wake. anapotosha watu kwa hulka zile zile za kifisadi za kudai tanzania kuna amani wakati kila kukicha haki ya mnyonge inanyongwa tena waziwazi. ni mtanzania gani siyejua kuwa zanzibar kuna mpasuko. hata rais mwenyewe alikili, sasa iweje wewe useme kuwa hamna au inawezekana kuwepo na mpasuko bado mambo yakawa shwali kwa mtazamo wako? au kuna haja ya kuingia darasani kubukua maana ya neno shwali na si shwali?

woga wa watanzania ndio unaotuponza. ila...
 
Nchi Yetu Ni Huru Na Hawa Cuf Tutapambana Nao Kwa Hoja Na Nguvu Zote Lakini Suala La Muafaka Kwa Sasa Wasahau Tanzania Ina Mengi Ya Kujadili Na Kuyafanyia Kazi Zaidi Ya Huo Muafaka

kama walikuwa na mengi ya kujadili kwa nini waliliongelea kwa masaa nane mfululizo kule butiama? si ndio waliolianzisha.
 
NI NGUMU SANA KUKAA MEZA MOJA NA WAASI VIONGOZI WA CUF NI WAASI NA HILO LITAMBULIKE LEO , KESHO NA HATA MILELE HATA WAO WANATAMBUA HILO

SASA TUTAKAAJE MEZA MOJA NA WAASI ?

1 ) WAMESAIDIA KUUWA RAIA KULE PEMBA WAKATI WA UCHAGUZI

2 ) MWEMBECHAI NAPO WANA MKONO WAO

3 ) NA KUNA MENGI MENGI YA KUJADILI HUMU

HAWA NI WAASI HATUWEZI KUKAA MEZA MOJA NA WAASI MPAKA WAO WENYEWE MAAMUE KUWEKA SILAHA CHINI NA WATAMKE KWA MAANDISHI NA KUWEKA SAHIHI HII NCHI NI YA AMANI , UPENDO NA UMOJA ULIOJENGWA NA BABA WA TAIFA AMBAYE ALIKUWA MUASISI NA MWANACHAMA HAI WA CCM

are you alright?

waasi kadiri ya nani? na muasi ni mtu gani?

you better go to rest rather than showing your intelligence eh! i mean...here.
 
are you alright?

waasi kadiri ya nani? na muasi ni mtu gani?

you better go to rest rather than showing your intelligence eh! i mean...here.

Unapoteza muda na shy ? Inasemekana ni mtoto wa nje ya ndoa na sasa ana laana kwa kuwa kapatikana katika kitanda cha haramu.Majuzi nimeona Lunyungu kamksema nikadhani ni utani mie nikafuatilia naambiwa mbali ya hilo shy ana u mental kidogo .Lakini pia ni mlamba miguu wa majamaa na anajitangazia kwamba yeye ana close ties na usalama kwamba yeye ni informer and he is waorking on damaging Jambo Forum .Ukweli ni mwingi hapa kutokana na maandiko yake .Si akili ya kawaida hii .
 
are you alright?

waasi kadiri ya nani? na muasi ni mtu gani?

you better go to rest rather than showing your intelligence eh! i mean...here.

Tatizo la CCM ni wahuni na tatizo la CUF ni wachochezi wa uvunjaji amani.

Kwanini CUF wasipoelewana na CCM wanakimbilia maneno ya uvunjaji Amani??? kwani Amani imejingwa na CUF??? Viongozi gani hawa wanaposhidwa kuelewana yani alternative yao ni VITA na kuvunja amani.Inamaana hata hawana plan B wao ni maguvu tu Ni rahisi sana kuona CUF hawana kitu na msiwape nchi .

Chama chenye kilicho na maono ya kivitavita kisipewe nafasi
 
Mie mashaka yangu makubwa ni kuwa CCM wameliacha hivi swala la Zanzibar kwa makusudi kabisa ili kuzitoa fikra zetu juu ya yale ambayo tumekuwa tunayapigia kelele kutaka majibu na hatua za kisheria zichukuliwe.
Mambo ya BOT,RICHMOND,KIWIRA nk. nani atayazungumza wakati kutakuwa na vurugu Zanzibar? Hilo wanalijua kabisa na ndio maana hakuna tamko la Kuhusu ufisadi wowote lililotolewa au kuchukuliwa hatua.
Kashfa za Ufisadi ni mbaya kwa viongozi hawa binafsi,na wanauhakika zikishughulikiwa kama inavyopaswa ni sawa na KIFO kwao,kwanini wasitumie usanii ktk kufuta (hata kama utaleta adhari za aina yeyote kwa Wazanzibar)Fikra zote za kuwachukulia hatua?
Lazima tuamke na kuwa macho na njama zozote za KUTUSAHAULISHA yale tuliyoanza tayari kupambana nayo.
 
If history is our best guide not only to know where we are going but also have a profound sense of where we are, then I can safely say that our President has missed HIS BIGGEST opportunity of leaving behind a credible legacy-If he was interested anyway!.

Whether we like it or not, spin or what, Zanzibar is a scar on our sovereignity as a nation and unless we get serious leaders who are prepared to take some hard and painful decisions, Zanzibar will remain a painful reminder of what has characterised our continent since independence. utawala wa mabavu. This was an opportunity to get this matter adressed for once and for all. The Zanzibar polity is cut down in the middle, so it would be naivity and stupidity of the highest order to think kwamba CCM can govern confortably sidelining the other group. Quality ya kiongozi bora ni kucontain zelouts na mafisadi wengineo. Unfortunately wamemzidi nguvu JK! So sad and dissapointing.

Swala la Zanzibar halihitaji ushabiki kama wengi wetu tunavyo display humu. Ni swala ambalo linagusa ile long cherished nerve ya upendo na amani. Watanzania tumeanza kuwa wanafiki kwa kufanya uovu na kuhubiri amani, kuwanyima watu haki yao kwa kutumia ukuta wa upendo na mshkamano. Jamani naomba nisiwe quoted lakini as day goes by, these slogans however sweet they are-zinaelekea ukingoni. Jeshi na polisi halitatuletea AMANI tukiipoteza.

Hatuwezi kuomba amani na upendo udumu Tanzania wakati tunatekeleza matendo ya kifisadi na uonevu. Hata huyo Mungu hatuelewi. Ni dhahiri kwamba tumeamua kuitoa kafara hii amani tuliyo nayo mwenye altare ya mafisadi wachache ambao wanaamini wana hati miliki ya kuwatawala watanzania wote.

Uongozi ni msalaba. JK amedhihirisha kwamba philophy yake ya uongozi ni questionable. Iam not a politician but Zanzibar question is likely to HAUNT our conscious for hundred years to come! We have failed ourselves to build a more perfect union beneficial for all of us.

JK, kama unapita JF, think again what you have presided over in Butiama and how do you want the nation and People to remember you. It is sad that the greatest history of man, is that he never learns from history. Indeed Tanzanians/Africans we have proved big time that we have never learn anything from the scourge of dictatorship and injustice.

Peace and love to you all!
 
CUF ni Chama kilichotulia kabisa na kinachofanywa na CUF ,CCM hakijui inabaki kubahatisha tu ,CUF hawataki kabisa serikali ya mseto mnaweza kusema ni ile hadisi ya sungula lakini siyo,ni mitego ya kumnasa ndege mjanja CCM ,na kusema kweli CCM imenasa na inazidi kujizonga na mitego ya CUF ,ingawa ni tabu kuiona kwa karibu ,itakubidi upekeche bongo kweli kweli na kuchanganua kwa kina kisha upime.

CUF hawakutaka serikali ya mseto ila walijua kabisa kwamba CCM Zanzibar hawapo tayari kwa hilo ,sasa kwa kuwaweka pembeni zaidi CUF wakavulumisha dongo hilo hilo la kuona ni vyema kuwepo mseto na kamati ya CCM ikaingia malaini na kukubali.

Kilichotokea ni CCM kupinga ,fahamu kuwa haifahamiki CCM Zanzibar japo akina makamba wamejaribu kuchora kuwa ni wale wa CCM kutoka Zanzibar ndio wamepinga.Waliloliona CUF limetokea.

Tayari CUF imefanikiwa kuichafua CCM mbele ya macho ya kimataifa na hili si jambo dogo katika siasa za kimataifa na hata za ndani siku hizi,niliwa kusikia wateja walitaka mafisadi washitakiwe na hili la muafaka lifikie mwisho na wote walitarajia kufikia mwisho ,ili wapate nguvu kuipiga jeki bajeti ya Tanzania ,Je mwelekeo wao au mtazamo wao utakuwa ule ule wa kuipiga jeki Bajeti ya Tanzania.

Mwalimu Julius alitwambia tufunge mkaja kwa muda wa miezi kumi na nane sasa Muungwana nae ajitayarishe kuwafahamisha wananchi ni muda gani tutahitajika kufunga mkaja na CU hawajaanza kutia tifu.
 
Tatizo la CCM ni wahuni na tatizo la CUF ni wachochezi wa uvunjaji amani.

Kwanini CUF wasipoelewana na CCM wanakimbilia maneno ya uvunjaji Amani??? kwani Amani imejingwa na CUF??? Viongozi gani hawa wanaposhidwa kuelewana yani alternative yao ni VITA na kuvunja amani.Inamaana hata hawana plan B wao ni maguvu tu Ni rahisi sana kuona CUF hawana kitu na msiwape nchi .

Chama chenye kilicho na maono ya kivitavita kisipewe nafasi

mimi ninachokiangalia hapa ni kuwa leo watasema cuf chama cha waasi, kesho watasema chadema chama cha makabila, keshokutwa watasema TLP chama cha vichaa, mtondo watasema hili na lile na lile.

sasa kama cuf ni waasi, mbona hakijafutwa, mbona hawaachii raia waamue kwa uchaguzi ulio huru, that's where i am trapped and that is where i disagree to agree.
 
Tatizo la CCM ni wahuni na tatizo la CUF ni wachochezi wa uvunjaji amani.

Kwanini CUF wasipoelewana na CCM wanakimbilia maneno ya uvunjaji Amani??? kwani Amani imejingwa na CUF??? Viongozi gani hawa wanaposhidwa kuelewana yani alternative yao ni VITA na kuvunja amani.Inamaana hata hawana plan B wao ni maguvu tu Ni rahisi sana kuona CUF hawana kitu na msiwape nchi .

Chama chenye kilicho na maono ya kivitavita kisipewe nafasi

Makapu kidogo umenichanganya hapa .Hivi CUF kusema maamuzi wanawaachia wananchi na wanachama wa Chama hao ni kuvunja amani? Amani nadhani inavunjwa na CCM kwa uwafanya Watanzania wa Zanzibar ni wajinga kiasi hicho .Mara zote ni CCM wamekuja na maneno mara CUF ya waarabu, mara wameleta silaha nchini , mara chama cha kidini etc etc .Nashangaa Makapu nisaidie kufafanua tafadhali.
 
na Edward Ibabila (Butiama) na Saada Said (Zanzibar)

MKUTANO wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliomalizika jana kijijini Butiama, umeonyesha dalili za wazi za kuhofia kuundwa kwa serikali ya mseto kabla ya mwaka 2010.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka ndani ya kikao hicho, zinaonyesha kwamba pamoja na wajumbe wa CCM na wa Chama cha Wananchi (CUF) kwenye kamati ya muafaka, kukubali kuundwa kwa serikali ya mseto Zanzibar kabla ya uchaguzi ujao wa mwaka 2010, mpango huo umepingwa na wanachama wengi wa CCM kutoka visiwani Zanzibar.

Kikao hicho kiliendelea mpaka usiku huku ajenda ya suala la muafaka likizua mvutano mkubwa miongoni mwa wajumbe wa kikao hicho hasa wale wa kutoka Zanzibar.

Kabla ya kujadiliwa suala hilo, kikao hicho kilijadili ajenda ya hali ya kisiasa, usalama ndani ya chama na serikali na suala la hali ya uchumi kabla ya wajumbe kupumzika.

Baada ya hapo, wajumbe waliingia kujadili ajenda ya muafaka Zanzibar na mmoja wa wajumbe alilidokeza Tanzania Daima kuwa mjadala huo uliwagawa huku wajumbe kutoka Zanzibar wakipinga kuwepo kwa serikali ya mseto visiwani humo.

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Amani Abeid Karume ndiye anayetajwa kuwaongoza baadhi ya wanachama wa chama hicho kupinga kuwapo kwa serikali ya mseto visiwani Zanzibar.

Habari hizo zinaeleza Rais Karume hayuko tayari kwa sasa na hususan kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, kuunda serikali ya umoja wa kitaifa itakayokuwa na Waziri Kiongozi atakayetokana na CUF.

CUF kimeshajadili mapendekezo yaliyotokana na mazungumzo ya muafaka na wamekubaliana na ajenda zote, ikiwemo ya kuanzishwa kwa serikali ya mseto kabla ya mwaka 2010.

Ajenda nyingine iliyodaiwa kuzua mjadala mkubwa ni ya baadhi ya wana CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi kufilisiwa na kunyang’anywa mali zao.

Akifungua kikao hicho juzi, Rais Jakaya Kikwete, aliwatoa hofu baadhi ya watu, hususani wanaotuhumiwa kwa ufisadi kuwa, chama hicho hakina mpango wa kutaifisha mali zao.

Rais Kikwete alisema ingawa kikao hicho kitajadili masuala mazito yanayohusu chama na serikali, lakini hakitajadili mageuzi ya kisera au kiitikadi.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete ilionyesha dhahiri kuwagawa wajumbe wa mkutano huo, ambao baadhi yao walitaka wanachama waliotuhumiwa kwa ufisadi watoswe.

Kutokana na kauli hiyo, habari kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa kikao hicho zinaeleza kuwa, wengi wamekatishwa tamaa na kuelezea kauli hiyo kama ni ya kuwataka wanaowatuhumu viongozi kwa rushwa kuacha kufanya hivyo.

Wakielezea jinsi kauli hiyo ya Kikwete ilivyopokelewa ndani ya kikao hicho, walisema wana CCM ambao wanatuhumiwa katika kashfa ya Richmond na EPA, ambao kwa muda wote kabla ya kutolewa kwa kauli hiyo, walikuwa kimya huku wakionekana wazi kuwa na wasiwasi, walichangamka na kuwa miongoni mwa watu walioshangilia.

Aidha, habari zilieleza kuwa baadhi ya wajumbe walikuwa na matarajio makubwa kuwa kashfa ya Richmond na EPA zingekuwa miongoni mwa ajenda muhimu katika vikao hivyo.

Walisema kama ajenda hizo zingejadiliwa, kwa vyovyote vile yangetokea maamuzi mazito dhidi ya wanachama wa chama hicho, ambao kwa namna moja au nyingine wanahusishwa katika tuhuma hizo.

Habari zinaeleza kabla ya kuanza kwa kikao hicho, baadhi ya wajumbe walilumbana vikali huku wengi wakitaka waliohusika katika kashfa hizo wapewe adhabu kali, ikiwa ni pamoja na kufilisiwa mali zao na kufutiwa uanachama.

Katika malumbano hayo, wajumbe wachache walionekana kutounga mkono hoja hiyo kwa madai kuwa itazidisha makundi ndani ya chama, jambo ambalo walidai litaathiri mshikamano wa chama hicho.

Wakati huo huo, Chama cha Wananchi (CUF) kimesema hakitaki kuingizwa katika serikali kwa ajili ya kutaka umaarufu na madaraka, lakini kinataka kuundwe serikali yenye sura ya umoja wa kitaifa kwa lengo la kuwakutanisha Wazanzibari wote.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, alipozungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Garagara, Jimbo la Mtoni.

Alisema kutokana na uzoefu alioupata, chama chake kimeona ni busara kuingizwa katika serikali kwa sababu kitakuwa karibu zaidi na mwenendo wa kazi za serikali kwa kuwa mwafaka uliopita wakati wa Dk. Salmin Amour haukutekelezwa.

Alisema muafaka mwingine ambao ulitiwa saini na kusimamiwa na Rais Amani Abeid Karume pia ulishindwa kutekelezwa, hivyo mazoea yanaonyesha kutokuwepo uaminifu, lakini CUF ikiwemo ndani ya serikali, itafanya kazi pamoja na CCM, hivyo mambo yanayokwama yataweza kukwamuliwa. “Wenye dhana kuwa sisi tunataka madaraka No, hatutaki madaraka, tunataka kufanya kazi karibu na wenzetu, ili kuijenga nchi yetu, wale wenye kufikiri tunaingia kwenye serikali kwa mlango wa nyuma, hawatujui lengo letu, sisi lengo letu jamani ni kuishi kwa amani katika nchi hii, hatutaki madaraka, tunataka kuondosha chuki na uhasama wa muda mrefu,” alisema Maalim Seif.

Alisema Zanzibar kumekuwepo na chuki na uhasama kwa miaka kadhaa hivi sasa, hivyo kuwepo kwa serikali ya pamoja ambayo itawawakilisha wananchi wote itamaliza hali hiyo.

Maalim Seif alisema nchi haiwezi kwenda na kupata rehema na baraka iwapo kuna watu wenye roho mbaya na chuki dhidi ya wenzao, hivyo ni vema kukaa pamoja na maslahi ya taifa na vizazi vijazo na sio busara kuendeleza kuzozana mara kwa mara jambo linalochangia kukosekana amani na baraka.

Katibu Mkuu huyo wa CUF alisema hakuna baraka inayoweza kuingia katika nchi kama kuna mivutano na chuki miongoni mwa wananchi na viongozi.

“Mimi ni muumini sana, naamini kabisa na nina hakika tukikaa pamoja nchi yetu itapata baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwani hivi sasa hatupati baraka kutokana na mivutano na chuki zilizopo, tukaeni kuijenga nchi yetu jamani, wenzangu CCM nchi hii… nchi hiii… haya,” alisema.

Alisema iwapo Rais Salmin na Rais Karume wangeuchukua ushauri wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Zanzibar leo hii kusingekuwa na mgogoro kama huu kwa kuwa mwaka 1995 alishauri kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa, lakini alipuuzwa.

Katika hatua nyingine, Maalim Seif alisema endapo CCM hawatatoa jibu la kuwaridhisha wananchi, chama chake na ulimwengu utafahamu nani mwenye dhamira mbaya kwa Tanzania, kwani CUF imeingia katika mazungumzo kwa dhamira njema na kuzingatia maslahi ya taifa lake.

Aidha, baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani Zanzibar wameanza kupiga debe kushirikishwa katika serikali ya mseto kabla hata ajenda hiyo kufikiwa utekelezaji wake.

Hali hiyo imeanza kujitokeza siku chache baada ya Maalim Seif kutangaza kamati ya pamoja ya mazungumzo imekubaliana kuunda serikali ya umoja wa kitaifa, kama hatua ya kumaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar.

Katibu Mkuu wa TADEA, Juma Ali Khatib alisema hatua ya mazungumzo iliyofikiwa katika muafaka huo ni muafaka katika kujenga umoja wa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Hamad Mussa Yussuf, alisema suala la serikali ya mseto ni jambo linalohusu katiba, hivyo ni vema vyama vyote vikashirikishwa kabla ya hatua ya utekelezaji.

Alisema matatizo ya Zanzibar yatapata ufumbuzi wa kudumu kama katiba itaandikwa upya na sheria zote za uchaguzi kurekebishwa.

Msimamo huo hauna tafauti na kauli ya Naibu Katibu Mkuu wa NLD, Rashid Ahmed Rashid ambaye alisema chama chake kinasubiri maamuzi ya Halmashauri Kuu ya CCM, ili kiweze kuchukua hatua, kwa vile vyama vya CCM na CUF havina haki kubadilisha katiba peke yao bila ya ridhaa ya wananchi wote.

Hata hivyo, Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Ambar Khamis, alisema hatua za mazungumzo zinazoendelea zinafaa kungwa mkono, lakini mjadala wa utekelezaji wake, lazima na viongozi wa kambi ya upinzani washirikishwe.

Source: Tanzania Daima
 
CUF ni Chama kilichotulia kabisa na kinachofanywa na CUF ,CCM hakijui inabaki kubahatisha tu ,CUF hawataki kabisa serikali ya mseto mnaweza kusema ni ile hadisi ya sungula lakini siyo,ni mitego ya kumnasa ndege mjanja CCM ,na kusema kweli CCM imenasa na inazidi kujizonga na mitego ya CUF ,ingawa ni tabu kuiona kwa karibu ,itakubidi upekeche bongo kweli kweli na kuchanganua kwa kina kisha upime.

CUF hawakutaka serikali ya mseto ila walijua kabisa kwamba CCM Zanzibar hawapo tayari kwa hilo ,sasa kwa kuwaweka pembeni zaidi CUF wakavulumisha dongo hilo hilo la kuona ni vyema kuwepo mseto na kamati ya CCM ikaingia malaini na kukubali.

Kilichotokea ni CCM kupinga ,fahamu kuwa haifahamiki CCM Zanzibar japo akina makamba wamejaribu kuchora kuwa ni wale wa CCM kutoka Zanzibar ndio wamepinga.Waliloliona CUF limetokea.

Tayari CUF imefanikiwa kuichafua CCM mbele ya macho ya kimataifa na hili si jambo dogo katika siasa za kimataifa na hata za ndani siku hizi,niliwa kusikia wateja walitaka mafisadi washitakiwe na hili la muafaka lifikie mwisho na wote walitarajia kufikia mwisho ,ili wapate nguvu kuipiga jeki bajeti ya Tanzania ,Je mwelekeo wao au mtazamo wao utakuwa ule ule wa kuipiga jeki Bajeti ya Tanzania.

Mwalimu Julius alitwambia tufunge mkaja kwa muda wa miezi kumi na nane sasa Muungwana nae ajitayarishe kuwafahamisha wananchi ni muda gani tutahitajika kufunga mkaja na CU hawajaanza kutia tifu.
Hivi muwafaka maana yake nini. Kwa sababu unataka kuwaridhisha wafadhali wakupe chao ndio uwaambie wale unaotaka waafikiane , afikianeni, japo hawajafikia satuwa ya kuafikiana? Ubaotaka waafikiane wako kule Zanzibar. kuna pande mbili. Kwa nini unataka kusikiliza ya upande mmoja tu na kutaka yaafikiwe, hutaki kuwasikiliza wa upande wa pili na hoja na sababu zao. Sasa CCM -Zanzibar (viongozi na wafuasi wao) wakiwa wadau wakuu katika maafikiano hayo unataka wasielze kile wanachikitaka na kukiamini ili kufikia maafikiano ya kweli. Hiyo demokrasia na utawala bora uko wapi hapo?
Haya washurutishe, walazimishe waburuze tuone kama utakuwa nao huo muwafaka wa kweli wakati wao ndio wadau wakuu, hata pale wafadhili watakapokupigia makofi na kukupa hicho unachokitegemea kutoka kwao?
 
Hivi muwafaka maana yake nini. Kwa sababu unataka kuwaridhisha wafadhali wakupe chao ndio uwaambie wale unaotaka waafikiane , afikianeni, japo hawajafikia satuwa ya kuafikiana? Ubaotaka waafikiane wako kule Zanzibar. kuna pande mbili. Kwa nini unataka kusikiliza ya upande mmoja tu na kutaka yaafikiwe, hutaki kuwasikiliza wa upande wa pili na hoja na sababu zao. Sasa CCM -Zanzibar (viongozi na wafuasi wao) wakiwa wadau wakuu katika maafikiano hayo unataka wasielze kile wanachikitaka na kukiamini ili kufikia maafikiano ya kweli. Hiyo demokrasia na utawala bora uko wapi hapo?
Haya washurutishe, walazimishe waburuze tuone kama utakuwa nao huo muwafaka wa kweli wakati wao ndio wadau wakuu, hata pale wafadhili watakapokupigia makofi na kukupa hicho unachokitegemea kutoka kwao?

Hii ni kama nimeshaiona katika zaidi ya thread tatu - kama ni hoja tumeisikia.
 
Unapoteza muda na shy ? Inasemekana ni mtoto wa nje ya ndoa na sasa ana laana kwa kuwa kapatikana katika kitanda cha haramu.Majuzi nimeona Lunyungu kamksema nikadhani ni utani mie nikafuatilia naambiwa mbali ya hilo shy ana u mental kidogo .Lakini pia ni mlamba miguu wa majamaa na anajitangazia kwamba yeye ana close ties na usalama kwamba yeye ni informer and he is waorking on damaging Jambo Forum .Ukweli ni mwingi hapa kutokana na maandiko yake .Si akili ya kawaida hii .

Ni kweli kabisa maana inaonekana shy yupo hapa kwa ajiri ya Jambo forums. Waliposema aliwauza wana jambo si kutilia maanani maana nilijua maneno, lakini sasa i can see the man anyejiita researcher wakati hawezi kutofautisha fact na unazi wa kisiasa
 
Ni kweli kabisa maana inaonekana shy yupo hapa kwa ajiri ya Jambo forums. Waliposema aliwauza wana jambo si kutilia maanani maana nilijua maneno, lakini sasa i can see the man anyejiita researcher wakati hawezi kutofautisha fact na unzi wa kisiasa

Shy ni kweli alishirikiana na polisi kuwauza wana JF! Polisi wenyewe wamemtosa baada ya kumuona jamaa amezidi kujipendekeza na wanamsema waziwazi. Achaneni naye huyo ni bonge la snitch na hafai kabisa hata kuwa memba hapa (maoni yangu binafsi)
 
Back
Top Bottom