abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
[h=1][/h]Written by makame silima // 26/06/2011 // Habari // No comments
Muungano upo lakini Tanganyika imeshakufa kwa jina la Tanzania.
[caption id="attachment_31252" align="aligncenter" width="405" caption="Mbunge wa Chwaka Yahya Issa"]
Mbunge wa Chwaka (CCM), Yahya Kassim Issa, amesema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, umechangia kuwarudisha nyuma kimaendeleo Wazanzibari.Yahya alisema hayo alipokuwa akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ujao wa fedha wa mwaka 2011/2012.
Kisiwe kile mimi nasema Wallaahi, Wallaahi kama si Muungano kisiwa kile siye nasema tungekuwa mbali, miye nakwambieni. Msitudanganye, alisema Yahya.
Aliongeza: Hata nchi hii misaada iliyopata kama tungekuwa tunajitegemea unafikiri tungekuwa wapi? Na nchi zote zinakwenda wapi? Sisi tulikuwa na bendera yetu kimataifa, tuache mambo haya. Hatuwezi kuitupa nchi leo sisi tukasema tumeipoteza. Hatukubali suala hili. Na sisi ndio wa kusema wenye umri huu kwa sababu hamna humu wa kusema.
Alisema kitu, ambacho amekibaini ni kwamba, kuna watu hawapendezwi kwa Zanzibar kuitwa nchi kwani vitabu vingi vya serikali, kwenye machapisho yake, sehemu ya mikoa vimeichapisha Zanzibar katika orodha ya mikoa.
Mtoto leo kizazi kinachokuja atakujafahamu nini? Lipi analokuja lielewa? Hili ni kosa tunalofanya. Wakubwa kaeni mfahamiane na kwamba Zanzibar kuihesabu kama mkoa sisi hatutaki. Sisi hatutaki, alisema Yahya.
Alisema kati ya hoja tisa kuhusu kero za Muungano zilizojadiliwa chini ya uenyekiti wa Ofisi ya Makamu wa Rais, hoja mbili tu ndizo zilizopata maamuzi na kuonya kuwa jambo hilo linaweza kusababisha mgogoro kati ya pande mbili za Muungano.
Yahya alisema iwapo serikali inataka usalama nchini na Muungano uweze kudumu na kuimarika, basi inapasa iwaelimishe vijana juu ya Muungano.
Alisema serikali imetoa takwimu za vikao vilivyofanyika kwa lengo la kufahamiana, undugu na urafiki kati ya pande mbili za Muungano kwamba vimefikia 75, lakini imeshindwa kueleza ni vikao vingapi vya kujadili kero za Muungano, ambazo ndizo zinazotesa wananchi, vimekwishafanyika.
Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, alisema serikali inaogopa kutoa maamuzi ili kuliletea taifa maendeleo, ambayo yanawezekana kupatikana.
Katika mchango wake, Lowassa alisifia amani iliyopo nchini na mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru wa nchi, ikiwamo ujenzi wa reli ya Tazara na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) na kusema mambo hayo Watanzania wanajua na dunia pia inajua.
Alisema mafanikio hayo yanatokana na kazi nzuri iliyofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM na serikali yake kwa kuthubutu, hivyo akashauri juhudi hizo ziendelezwe, kwani iwapo serikali itanuia inaweza.
CHANZO: NIPASHE
Muungano upo lakini Tanganyika imeshakufa kwa jina la Tanzania.
[caption id="attachment_31252" align="aligncenter" width="405" caption="Mbunge wa Chwaka Yahya Issa"]
Mbunge wa Chwaka (CCM), Yahya Kassim Issa, amesema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, umechangia kuwarudisha nyuma kimaendeleo Wazanzibari.Yahya alisema hayo alipokuwa akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ujao wa fedha wa mwaka 2011/2012.
Kisiwe kile mimi nasema Wallaahi, Wallaahi kama si Muungano kisiwa kile siye nasema tungekuwa mbali, miye nakwambieni. Msitudanganye, alisema Yahya.
Aliongeza: Hata nchi hii misaada iliyopata kama tungekuwa tunajitegemea unafikiri tungekuwa wapi? Na nchi zote zinakwenda wapi? Sisi tulikuwa na bendera yetu kimataifa, tuache mambo haya. Hatuwezi kuitupa nchi leo sisi tukasema tumeipoteza. Hatukubali suala hili. Na sisi ndio wa kusema wenye umri huu kwa sababu hamna humu wa kusema.
Alisema kitu, ambacho amekibaini ni kwamba, kuna watu hawapendezwi kwa Zanzibar kuitwa nchi kwani vitabu vingi vya serikali, kwenye machapisho yake, sehemu ya mikoa vimeichapisha Zanzibar katika orodha ya mikoa.
Mtoto leo kizazi kinachokuja atakujafahamu nini? Lipi analokuja lielewa? Hili ni kosa tunalofanya. Wakubwa kaeni mfahamiane na kwamba Zanzibar kuihesabu kama mkoa sisi hatutaki. Sisi hatutaki, alisema Yahya.
Alisema kati ya hoja tisa kuhusu kero za Muungano zilizojadiliwa chini ya uenyekiti wa Ofisi ya Makamu wa Rais, hoja mbili tu ndizo zilizopata maamuzi na kuonya kuwa jambo hilo linaweza kusababisha mgogoro kati ya pande mbili za Muungano.
Yahya alisema iwapo serikali inataka usalama nchini na Muungano uweze kudumu na kuimarika, basi inapasa iwaelimishe vijana juu ya Muungano.
Alisema serikali imetoa takwimu za vikao vilivyofanyika kwa lengo la kufahamiana, undugu na urafiki kati ya pande mbili za Muungano kwamba vimefikia 75, lakini imeshindwa kueleza ni vikao vingapi vya kujadili kero za Muungano, ambazo ndizo zinazotesa wananchi, vimekwishafanyika.
Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, alisema serikali inaogopa kutoa maamuzi ili kuliletea taifa maendeleo, ambayo yanawezekana kupatikana.
Katika mchango wake, Lowassa alisifia amani iliyopo nchini na mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru wa nchi, ikiwamo ujenzi wa reli ya Tazara na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) na kusema mambo hayo Watanzania wanajua na dunia pia inajua.
Alisema mafanikio hayo yanatokana na kazi nzuri iliyofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM na serikali yake kwa kuthubutu, hivyo akashauri juhudi hizo ziendelezwe, kwani iwapo serikali itanuia inaweza.
CHANZO: NIPASHE