MUUNDO wa Tume ya Kuratibu Kuandikwa kwa Katiba Mpya Uweje?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,462
39,928
Wengi tumetatizika na mapendekezo ya Muungo wa Tume ya Rais ya Kupitia Katiba kama inavyopendekezwa na Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba. Tuna tatizo jinsi Tume hiyo inavyoundwa, nguvu zake, majukumu yake n.k Baada ya kusoma zile kanuni za msingi za Kuelekea Katiba Mpya yawezekana kila mmoja wetu ana mawazo kuwa tunataka Katiba ambayo kweli itatokana na wananchi na siyo ya kuburuzwa na chama tawala au na serikali.

Binafsi ninayo mapendekezo yangu ya mchakato na muundo na nimefikia mbali kidogo lakini nami ninapata tatizo ambalo wengi tutakutana nalo. Tukizingatia kanuni zile tano za kuelekea Katiba Mpya:

a. Nani asimamie mchakato wa kuandika Katiba Mpya
b. Ateuliwa na nani
c. Asimamiwe na nani
d. Akamilishe vipi jukumu hilo

Kwa hiyo naomba mawazo yatanisaidia na mimi kurefine mawazo yangu kuhusu muundo ili niweze kuwashirikisha nanyi. Je Katiba Mpya tunayotaka mchakato wake uweje kulinganisha na ule uliopendekezwa na serikali? Mchakato ambao utaonesha kuwa wananchi ndio wanaoandika Katiba yao hasa na siyo kikundi cha watu wachache wateuliwa?
 
From my little understanding on it,

Napendekeza kuwepo tume ya watu from different groups e.g. wanataaluma, askaris, christians, muslims, wafungwa, vilema, wanasheria, wahandishi, waganga, NGO, vyama vya wafanyakazi, waajiri, wafanyabiashara wadogo wadogo, vyama vya siasa vyenye uwakilishi (ubunge, madiwani, nk kwa vile ambavyo ni rasmi. waelimishwe, wachaguane. wakishateua team basi ichague secretariet ndogo yenye watu wajuzi na wasomi kwenye hii fani. wapite kukusanya maoni, na riport yao ipelekwe kwenye timu then timu ipewe muda wa kurudi kwenye jumuiya zao ikiwezekana ile timu ndogo iende kwenye makundi kama hitaji fulani halikuzingatiwa na kutoa ufafanuzi. Wakikubaliana then ipelekwe kwa wananchi wote kwa voting. Before voting, kila mtu awe huru kuipigia kampeni kifungu fulani.

Napendekeza mchakato huu ndo utungiwe sheria na usizuiwe watu kuzungumza jambo fulani kwani katiba ya sasa itatumika mpaka hapo matokeo ya upigaji kura yatakapoisha.

Naomba kuwakilisha.
 
Iundwe tume huru ambayo jukumu lake ni kusimamia mchakato wa kuandika katiba mpya,iteuliwe na bunge kwa kupigiwa kura kuzingatia na sifa na vigezo vitakavyoonekana vinafaa...tume hii isimamiwe na Bunge!...Wakamilishe jukumu hili kwa kupitia kwa wananchi katika kada zote na kuchukua maoni na kero zao mbali mbali kabla hawajakaa na wanasheria na wanazuoni mbali mbali na kuweka sawa hili na lile kabla hawajaipeleka Bungeni na Bunge kuisoma wazi na baada ya kujiridhisha idurufiwe na kuanza kutumika!
 
From my little understanding on it,

Napendekeza kuwepo tume ya watu


Inaundwa na nani?

from different groups e.g. wanataaluma, askaris, christians, muslims, wafungwa, vilema, wanasheria, wahandishi, waganga, NGO, vyama vya wafanyakazi, waajiri, wafanyabiashara wadogo wadogo, vyama vya siasa vyenye uwakilishi (ubunge, madiwani, nk kwa vile ambavyo ni rasmi.

Huoni yaweza kuwa ni kubwa sana kama itajaribu kuwa "all inclusive"?

waelimishwe, wachaguane. wakishateua team basi ichague secretariet ndogo yenye watu wajuzi na wasomi kwenye hii fani. wapite kukusanya maoni, na riport yao ipelekwe kwenye timu then timu ipewe muda wa kurudi kwenye jumuiya zao ikiwezekana ile timu ndogo iende kwenye makundi kama hitaji fulani halikuzingatiwa na kutoa ufafanuzi. Wakikubaliana then ipelekwe kwa wananchi wote kwa voting. Before voting, kila mtu awe huru kuipigia kampeni kifungu fulani.

Nimekupata
 
Iundwe tume huru ambayo jukumu lake ni kusimamia mchakato wa kuandika katiba mpya,iteuliwe na bunge kwa kupigiwa kura kuzingatia na sifa na vigezo vitakavyoonekana vinafaa

Nani anaamua vigezo hivyo?

...tume hii isimamiwe na Bunge!...Wakamilishe jukumu hili kwa kupitia kwa wananchi katika kada zote na kuchukua maoni na kero zao mbali mbali kabla hawajakaa na wanasheria na wanazuoni mbali mbali na kuweka sawa hili na lile kabla hawajaipeleka Bungeni na Bunge kuisoma wazi na baada ya kujiridhisha idurufiwe na kuanza kutumika!

Inaonekana katika mfumo huu hakuna kura ya maoni?
 
So far as nijuavyo ni watu wachache sana wanaojua katiba inayotumika sasa...narecomend kusikiliza wanachi na kada zao kwamba wanafahamu nini juu ya katiba (tunayotaka kuibadili),ni wapi wanadhani paongezwe nini na wapi pasipoendana na wakati tuliopo...kwa wale wasiojua kabisa pawepo utaratibu wa kutoa elimu ya uraia kwa mfumo ambao utakua umerahisishwa ili kufikia wengi! Kwa kufanya hivi maoni ya watu (ambao ndio waathirika wa mwisho wa katiba) yatakua yametolewa!

Baada ya mchakato huu wa awali tume hii ambayo itaandika draft ya kwanza ambayo itarudishwa tenda kwa wananchi kujua maoni yao yamezingatiwa kiasi gani na kuonesha kazi waliyofanya tume ni kucompile pamoja mawazo yao(wananchi)
Tume hii itatakiwa kuwa na wataalamu mbalimbali chini ya consultation ya wanasheria ambao jukumu lao kubwa ni kutoa mwongozo wa nini kifanyike vipi na kwa namna gani bila kuathiri taratibu!
 
Wengi tumetatizika na mapendekezo ya Muungo wa Tume ya Rais ya Kupitia Katiba kama inavyopendekezwa na Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba. Tuna tatizo jinsi Tume hiyo inavyoundwa, nguvu zake, majukumu yake n.k Baada ya kusoma zile kanuni za msingi za Kuelekea Katiba Mpya yawezekana kila mmoja wetu ana mawazo kuwa tunataka Katiba ambayo kweli itatokana na wananchi na siyo ya kuburuzwa na chama tawala au na serikali.

Binafsi ninayo mapendekezo yangu ya mchakato na muundo na nimefikia mbali kidogo lakini nami ninapata tatizo ambalo wengi tutakutana nalo. Tukizingatia kanuni zile tano za kuelekea Katiba Mpya:

a. Nani asimamie mchakato wa kuandika Katiba Mpya
b. Ateuliwa na nani
c. Asimamiwe na nani
d. Akamilishe vipi jukumu hilo

Kwa hiyo naomba mawazo yatanisaidia na mimi kurefine mawazo yangu kuhusu muundo ili niweze kuwashirikisha nanyi. Je Katiba Mpya tunayotaka mchakato wake uweje kulinganisha na ule uliopendekezwa na serikali? Mchakato ambao utaonesha kuwa wananchi ndio wanaoandika Katiba yao hasa na siyo kikundi cha watu wachache wateuliwa?

nitajitahidi kujibu maswali yako mheshimiwa kama ifuatavyo lakini kabla ya kuyajibu
ningependa kukwambia kuwa hakuna katiba inayoweza kuandikwa na watu wote hilo ni lazima tulikubali isipokuwa wale wawakilishi wetu ndio watakaokuwa nguzo muhimu sana ktk kufikisha mawazo yetu halisi ktk kutengeneza katiba yetu.
a) tume maalum itakayoundwa na mkutano mkuu wa kitaifa utakaokutanisha makundi mengi kama si yote ya kijamii nchini. watanzania hao naamini watakuwa na busara ya kutosha ya kuchagua watu safi kwani wapo wengi na wanafaamika.
b) kama nilivyosema hapo awali wajumbe wa tume maalum ya katiba itachaguliwa na mkutano huo mkuu wa kitaifa ndio watasimamia kila kitu.
c) tume maalum ya katiba itatakiwa kuzingatia hadiju za rejea zitakazotolewa na mkutano mkuu wa kitaifa ambapo utakutana kila muda maalum uliopangwa kuona kama tume inakidhi maamuzi ya mkutano mkuu.
d) mawazo yote yakisha kukusanywa yapitiwe na kufanyiwa majumuisho na tume ya katiba na kupelekwa moja kwa moja ndani ya bunge maalum la katiba kwa ajili ya kupitishwa tu na siyo kubadilishwa ili kuyapa legal legitimacy na baada ya hapo yarudishwe kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni nchi nzima ili kuyapa political legitimacy yakipita basi ndio tunakuwa tumepata katiba kamili iliyotokana na wananchi. imetokea kwa wananchi wenyewe na imemalizwa na wananchi wenyewe.
swali lako linaonyesha kuwa na umoja lakini swala kama hili linahitaji maamuzi ya pamoja kwahiyo tume ndio kwa pamoja ifanye maamuzi na kama inakuwa na mwenyekiti basi achaguliwe na hiyo tume kwa ajili ya kusimamia hadiju za rejea tu na siyo kufanya maamuzi yoyote makubwa peke yake na pia tume iwe na uwezo wa kuweza kumuondoa endapo hatakidhi matakwa ya mkutano mkuu au akionyesha uwezo mdogo wa kutekeleza majukumu yake.
 
Tume iundwe na rais na ipitishwe na theluthi mbili ya wabunge waliochaguliwa na wananchi,sio walioteuliwa na vyama.
 
Ili kutoa uwanja mpana zaidi wa fursa kwa watu wote; huku mitaani tunapoishi kuwe na vikamati vidogo vidogo ambavyo vitaongozwa na wale wajumbe wa nyumba kumi. Mawazo yatapendekezwa na kujadiliwa halafu watateua mwakilishi mmoja au wawili ambao watapeleka hoja zao kwenye kamati ya serikali ya mtaa (hiyo kamati itaundwa na hao watu wawili wa kila mtaa na uongozi wa serikali ya mtaa).
Watajadili hoja na kuzitetea, zitakazokuwa na nguvu zitapelekwa kwenye kamati ya wilaya (kamati ya wilaya itaundwa na watu wawili kutoka serikali za mitaa na uongozi wa wilaya).
Baada ya kujadili hoja kwenye kamati ya wilaya na kuzipitisha zilizo na mashiko, watapendekezwa watu wawili watakaosimamia hoja hizo kwenye kamati/tume ya mkoa. Tume ya mkoa nayo itaundwa kwa utaratibu ule ule ila wanazuoni nao waongezeke katika tume ya mkoa.
Mapendekezo yote sasa katika kila mkoa yafikishwe mjengo kumalizia hatua zilizobaki.
 
Inaundwa na nani?

Serikali iwe na mswaada kama huu wenye uelekeo huo. Na kila taasisi ina viongozi na utaratibu wa kuchagua wawakilishi.

Huoni yaweza kuwa ni kubwa sana kama itajaribu kuwa "all inclusive"?

Kweli lakini tunahitaji uwakilishi, we can trim down kwa usema wale wenye lengo moja mfano wataalamu, NGO in one group, nk. Tunaweza kuja na approach nzuri ambayo kila mtu will be happy na aone kama ameshirikishwa. Tatizo ni wale wakulima wangu ambao hawana vyama au kitu kama hicho. Kwa kugundua ukubwa ndo maana nikapendekeza hio kamati ndogo yenye wataalamu.
 
Tume iundwe na rais na ipitishwe na theluthi mbili ya wabunge waliochaguliwa na wananchi,sio walioteuliwa na vyama.


Vigezo vya Rais kuteua wajumbe wa tume vinawekwa na nani? kwenye Bunge ambalo theluthi yake ni wabunge wa chama cha Rais kuna uwezekano gani wa kubadilisha wajumbe walioteuliwa na Rais?
 
Ili kutoa uwanja mpana zaidi wa fursa kwa watu wote; huku mitaani tunapoishi kuwe na vikamati vidogo vidogo ambavyo vitaongozwa na wale wajumbe wa nyumba kumi.

Nimelipenda wazo lako sana; isipokuwa kutumia wajumbe wa nyumba kumi kwani ni mfumo wa CCM huo. Labda hapa tuulize tuna mfumo gani katika ngazi za mitaa ambao unaweza kutumika?
 
Vigezo vya Rais kuteua wajumbe wa tume vinawekwa na nani? kwenye Bunge ambalo theluthi yake ni wabunge wa chama cha Rais kuna uwezekano gani wa kubadilisha wajumbe walioteuliwa na Rais?
Point hapa ni nani ateue au achague tume,it's almost impractical kuupa umma nguvu ya kuteua tume,umma haupo homogeneous na kama serikali haitachagua tume hakuna njia yoyote nyingine.....we should know that,vigezo atavitumia rais na bunge litakubali au kukataa.
juu ya composition ya bunge,you can't help it! 80% said no to multiparty system and 20yrs later 80% of parliament is CCM.For whatever reasons people don't really buy what "people" are selling,you ran on peoples power and you got it!Sorry if that was cold.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mimi nadhani Watanzania tunajipa kazi kubwa sana kufikiria vitu vikubwa hali katiba ni mwongozo wa kitaifa ukifuata dira ambayo sisi Watanzania tunataka kuijenga..
Kwanza kabisa swali la kujiuliza ni Taifa gani tunalotaka kulijenga..tupate dira ya kitaifa kinyume cha ile ya Ujamaa na kujiitegemea...
kwa hiyo tume itakayo chaguliwa ni lazima izingatie hilo kwanza, kisha utunzi wa katiba utakuwa ni mwongozo wa kufikia malengo hayo. Kwa hiyo washiriki wa tume hiyo wanatakiwa watu wenye uwezo mpana wa kutazama dira ya taifa badala ya itikadi, wanaojua tofauti ya vitu hivi na kisha wenye uwezo wa kutazama na kupokea mapendekezo yanayolenga sehemu muhimu za mageuzi ya kikatiba kuelekea new destination..

Binafsi nitapendekeza watu wenye uwezo na Uzalendo kwanza, watu walioweza kuona hitilafu na sii mapungufu kikatiba ktk muundo wa 1 Serikali, 2 Bunge na 3. Mahakama..
Hapa ndipo kuna madudu makubwa zaidi ukitazama madaraka makubwa ya rais, muundo wa serikali ambayo sidhani kama tunamhitaji Waziri mkuu ila rais wa jamhuri ya muungano mwenyewe kushika jukumu hilo baada ya kupunguziwa madaraka. na mwisho kama tuna wabunge madiwani na Halmashauri za miji hatuhitaji wakuu wa mikoa na wilaya laa sivyo haiwezekani basi wachaguliwe na wananchi na sii marais.
Ifikiriwe pia kuundwa kwa senate yenye uwakilishi wa kudumu ambayo ndiyo itawapitisha mawaziri, majaji, mkuu wa UWT, tume ya uchaguzi na vyombo vingine vyote vya kitaifa vinavyotakiwa kuwa huru..

Pili,
Watu ambao wanajua vyombo vya kitaifa ambavyo vinatakiwa kuwa huru na havifungamani na itikadi au chama chochote na uwakilishi wake ikiwa ni pamoja na mamlaka watakayo kabidhiwa kwa mapana na kikomo cha mamlaka hayo bila kuathiri majukumu yao ktk utendaji kazi..
Na jingine ni wawakilishi wa wananchi yaani wabunge na madiwani lazima wawe wakazi wa maeneo wanayowakilisha..

Tatu,
Mimi naamini kwamba hakuna Mtanzania asiyefahamu haki yake na inapotea wapi au haikulindwa vipi..
Hivyo wale watakaochaguliwa ni lazima waijue katiba ya sasa na vifungu vipi vimepokonya haki hiyo maana kutojitosheleza kunahitaji tu marekebisho..

Haki zote za kila Mtanzania zitokane kwa kuzingatia uzawa, maumbile, mila, desturi na tamaduni zetu,
Makosa ya katiba ya mwaka 1977 ikizingatiwa imani tofauti za dini na makabila ambazo ni endelevu na ibada muhimu kwa jamii wahusika bila kudhalilisha makabila au dini nyingine na zaidi ya hayo bila kuwahukumu au kuwatenga ktk jamii wasiofuata misingi ya kikabila au imani ya dini..

Sasa basi ktk mlolongo wa list ya mahitaji kama niliyoorodhesha hapo ndipo unatafuta wataalam, watu wenye uwezo wa kuifanya kazi hiyo na sii kuxhagua watu kwanza kabla hujajua unataka kujenga vitu gani..

Tusifanye makosa yetu ya kila siku kuwapa watu mamlaka ktk fani zisizokuwa ktk taaluma yao..hivyo basi tume itaundwa baada ya kuelewa tunataka kujenga kitu gani maana neno katiba tu halijitoshelezi
 
Nimelipenda wazo lako sana; isipokuwa kutumia wajumbe wa nyumba kumi kwani ni mfumo wa CCM huo. Labda hapa tuulize tuna mfumo gani katika ngazi za mitaa ambao unaweza kutumika?

mfumo wowote utakaotumika inabidi ueleweke mapema. Usiwe ni mfumo wa kuwaziba watu midomo au kuchakachua mawazo ya watu tangu awali, usiwe ni mfumo wa kutuchosha na kutuvunja nguvu.
Ila pia, hata hao wajumbe napendekeza waingie katika huo mfumo, katika suala zima la kuorganize watu wanaweza kufanikisha kwa namna moja au nyingine maana wao (wajumbe) ndio wapo karibu na watu wao.
 
MMM ahsante kwa post nzuri
Kwanza kabisa mambo ya muhimu kufahamu na kuzingatia ni haya yafuatayo:-

Jambo la Kwanza
: Tunatunga katiba ya karne ya 21 na zijazo na sio ya karne ya 20 au ya 21 peke yake. This means that we need the Contistitutional Review Committee to be be formed by people who will addressing national issues through the lenses of rational thinking.

We do not need people who are intellectually and political naïve and who have lost touch with the realities of governing the people based upon participatory democracy…Maana kuna mijitu ukiiambia ushiriki wa watu kwenye michakato ya maendeleo ya taifa inaona kama vile unataka kuinywesha Sulphuric Acid


Jambo la Pili:
Constitution of an independent country cannot be reviewed or written by one party (hata kama ni kwa kificho au kwa mgongo wa technical position zao)

Jambo la Tatu:
Hatuhitaji idadi ya watu kadhaa kwenye committee ila tunachohitaji ni uhakikisho wa uwakilishi wa makundi yote ya jamii katika kutunga mswaada wa katiba mpya.

Ninachojaribu kusema hapa ni kuwa, expression of diverse representation is key to a 21stC people-owned constitution so as to avoid having a constitution which speaks of a single group (monopoly by minority). Hatuhitaji katiba ya kudumisha fikra za kundi Fulani la watu waliojiandaa kufuga makucha kukwapua rasilimali na uthamani wa Mtanzania


Makundi yote key ni lazima yashiriki (Active Political parties, CSOs and FBOs/Religious Institutions). Ushiriki wao kwenye Tume ya mapendekezo unaweza kuwa wa namna mbili:

Nazo ni

Ushiriki wa Uwakilishi kwenye Tume
– Ushiriki wa makundi muhimu ya jamii kwenye Tume ya katiba kupitia muwakilishi wa kundi hilo. Huyu atakuwa ni muwakilishi wa interest za kundi husika kwenye jambo hilo

Ushiriki wa Mapendekezo kwenye Tume
– Sio lazima wote kubanana kwenye tume lakini kuna haja ya haya makundi to formulate and submit their own proposals to the committee for inclusion into a new constitution through their direct representative in the Review Committee…ambayo hii nayo ni njia nzuri sana kwao

SASA Kazi kubwa kwa bunge ni kuhakikisha tunaondokana na mapendekezo ya marekebisho ya katiba ya mwaka 61 au 77 bali ya karne tuliyonayo….Its chocking rais kuamua kuteua eti 10 bara 10 visiwani, that is naïve….



 
From my little understanding on it,

Napendekeza kuwepo tume ya watu from different groups e.g. wanataaluma, askaris, christians, muslims, wafungwa, vilema, wanasheria, wahandishi, waganga, NGO, vyama vya wafanyakazi, waajiri, wafanyabiashara wadogo wadogo, vyama vya siasa vyenye uwakilishi (ubunge, madiwani, nk kwa vile ambavyo ni rasmi. waelimishwe, wachaguane. wakishateua team basi ichague secretariet ndogo yenye watu wajuzi na wasomi kwenye hii fani. wapite kukusanya maoni, na riport yao ipelekwe kwenye timu then timu ipewe muda wa kurudi kwenye jumuiya zao ikiwezekana ile timu ndogo iende kwenye makundi kama hitaji fulani halikuzingatiwa na kutoa ufafanuzi. Wakikubaliana then ipelekwe kwa wananchi wote kwa voting. Before voting, kila mtu awe huru kuipigia kampeni kifungu fulani.

Napendekeza mchakato huu ndo utungiwe sheria na usizuiwe watu kuzungumza jambo fulani kwani katiba ya sasa itatumika mpaka hapo matokeo ya upigaji kura yatakapoisha.

Naomba kuwakilisha.

hiyo tume itakuwa na watu zaidi ya 200, sijui kazi itafanyika?
 
Kwa hali hii, inaonyesha watanzania hawana trust kwa serikali yao hata kidogo, sa sijui wamewapa dhamani ya nini? serikali imechaguliwa na wananchi, Rais, mawaziri ni wabunge wamechaguliwa na wananchi sasa sijui hiyo mistrust inatoka wapi? all in all hata kama tume haitateuliwa na Rais hao watu wataoteuliwa na wananchi will be trustable? hawataweza kuingiliwa kwa vyovyote vile? nani atawawezesha? will be answerable to whom? Mimi naona kazi ni kubwa no matter what serikali bado ina mkono katika kuundwa kwa hii katiba, haikwepeki. Vyovyote vile, maoni yakikusanywa, watz tuhabarishwe kila detail mswada ukitengenezwa kabla ya kupitishwa. Mimi binafsi sina imani na bunge kwa asilimia kubwa , they can do anything tukashangaa wamepitisha, hatuna sehemu ya kuaminika tz, kote kuna mapungufu yake, usafi wa moyo hakuna kabisa kwa watanzania.Labda tupeleke kanisani, LOL.
 
Point hapa ni nani ateue au achague tume,it's almost impractical kuupa umma nguvu ya kuteua tume,umma haupo homogeneous na kama serikali haitachagua tume hakuna njia yoyote nyingine.....we should know that,vigezo atavitumia rais na bunge litakubali au kukataa.

Zipo njia nyingine, ni kwamba hujazifikiria tu.

juu ya composition ya bunge,you can't help it! 80% said no to multiparty system and 20yrs later 80% of parliament is CCM. For whatever reasons people don't really buy what "people" are selling,you ran on peoples power and you got it!Sorry if that was cold.

mzee wengine tulishiriki huo mchakato uliosema 80 percent... haukuwa as transparent and participatory kama watu wengine wanavyodhania. Na ndio mchakato ambao unataka kurudiwa tena kwenye hili.
 
Tusifanye makosa yetu ya kila siku kuwapa watu mamlaka ktk fani zisizokuwa ktk taaluma yao..hivyo basi tume itaundwa baada ya kuelewa tunataka kujenga kitu gani maana neno katiba tu halijitoshelezi


Mzee Mkandara, nadhani hapa ndio kitu ambacho najaribu kukitafuta; tunafanyaje ili kujua tunataka kitu gani? Nani anaamua kukusanya maoni hayo na kwanini yeye na si wengine?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom