Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Serikali moja, TAIFA MOJA, NCHI MOJA ndio inspiration ya WATANGANYIKA ndani ya muungano. Kwa upande wa Zanzibar hilo halikubaliki (abadan asilan), wala sipimi homa kwa kijanja. Kwa bahati mbaya au nzuri mfumo wa muungano hauwezi kubadilishwa kuwa mwengine wowote (achilia mbali wa TAIFA MOJA ; NCHI MOJA) bila ya mfumo huo unaopendekezwa kukubalika kwa WABIA (COUNTERPART) wa Muungano huu yaani ZANZIBAR - kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar, katiba ya Muungano na sheria za mikataba ya kimataifa - vyenginevyo tungekwishakuwa TAIFA MOJA NCHI MOJA tangu siku nyingi tu. Hivyo basi hata kama Watanganyika tutajipanga kwa mistari mirefu -urefu wa kutoka feri dar hadi tunduma- (upigaji kura wa wenzetu wa Kenya) kupiga kura ya TAIFA MOJA NCHI MOJA, ni buree tu labda kama yale madai ya UAMSHO kwamba Tanganyika yaitawala Zanzibar ni ya kweli.

What we forget is that the despite the appropriateness of Taifa moja Nchi moja notion, it can not be forcefully imposed to Zanzibaris.
 
huo ndo maana ya muungano..tatizo la wenzetu tumeshawapatia/wamejipa vielelezo vingi vya kujitambua kama taifa huru..ni kiasi cha wao kujitangaza kama nchi tu basi.. Hapo ndio ugumu wa kuwaambia tuunde serikali moja unapokuja kwani wameshaonja tamu ya madaraka mjj

No, tatizo sio la wenzetu.
" wenzetu tumeshawapatia vielelezo vya ...." hilo ndio tatizo lenu, mnadhani labda kutokana na wingi wa rasilimali zenu au wingi wa idadi ya watu wenu basi nyinyi mnahodhi madaraka ya kuamua mustaghbali wa zanzibar na watu wake kama vile mfanyavyo kwa maHOUSEGIRLS wenu na WAKE zenu


"kwani wameshaonja utamu wa madaraka ....." (hapa unamaanisha madaraka waliopewa/walioachiwa na Tanganyika - na hiyo ndio mentality wa watanganyika including our learned brothers and the like) UMEZALIWA LINI WEWE? KASOME UJUWE, UJIFUNZE UTAMBUE
 
lilikua ni wazo la cdm kuandika katiba ccm wakadandia hoja najua itawatoa roho na hili sakata la muungano, mmh liwalo na liwe.
 
Jumaane,
Mimi naona kwa sasa hivi Zanzibar ndiyo inayo colonize Tanganyika kwa sababu yenyewe inajitawala na bado inashare kwenye Muungano. Unasema Tanganyika can't force Muungano wanaoutaka wao na Zanzibar, Je huoni kwa kusema hivyo unataka Zanzibar ndiyo i force Muungano wanaoutaka wao na Tanganyika? Marekani ni muunganiko wa nchi zaidi 40 ambazo zilikuwa na mchanganyiko wa nchi ndogo na kubwa. Maskini na Tajiri lakini wameunda serikali moja. Kwa nini Serikali moja iwe nongwa kwa Tanganyika na Zanzibar? Je nini mantiki ya Muungano kama bado kila muungana ana serikali yake?

Hoja ya Serikali tatu ni hoja ya wanasiasa kujitengenezea nafasi za ulaji.

Nakala: Mzee Mwanakijiji.

TUMBIRI (PhD, University of HULL, United Kingdom),
tumbiri@jamiiforums.com


Hapo kwenye Red: Sisemi hivyo. Ukweli ni kwamba Muungano huu ni wa nchi mbili, TANGANYIKA NA ZANZIBAR sio wa nchi 52 kama Marekani. Kwa hivyo mfumo wowote tunaoutaka lazima ukubalike kwa watu wa pande zote mbili kwa ridhaa zao - wazanzibari kwa upande wao na watanganyika kwa umoja wao - Ndipo muungano utakuwa muungano. Sasa tulipofika: Muungano wa serikali mbili haukubaliki - haufai una kero luluki. Watanganyika hawataki serikali tatu - ni gharama kuziendesha. Wazanzibar hawataki serikali moja- hawataki kutawaliwa na kuwa mkoa wa tanganyika. Tufanyeje sasa? Ng'ombe avute gari au gari ivute ng'ombe?
 
Tudai serikali moja, nchi moja, taifa moja?

Tutafakari na haya:

Basi na tutafute mfumo ambao utaiondolea Zanzibar hofu hii ya kumezwa, bila kuibebesha Tanganyika mzigo wa kuendesha Serikalli mbili zenye uzito unaolingana.

Labda ni vizuri kukumbusha kwamba shabaha ya baadhi yetu ilikuwa nikuunganisha nchi za Afrika Mashariki ziwe nchi moja. Na wakati Zanzibar na Tanganyika zinaungana, Kenya, Uganda na Tanganyika zilikuwa katikati ya mazungurnzo ya kutafuta uwezekano, wa kuungana. Kama jambo hilo, lingetokea, nina hakika kabisa kwamba mfumo wa nchi mpya ambayo ingezaliwa ungelikuwa ni Shirikisho.

Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Mashariki zikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili - ya Zanzibar na ya Tanganyika - kuliko Tanzania yenye Serikali Mbili, ya Tanzania na ya Zanzibar.

Uk 11-12 link Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)

 
Je tumeshapata sababu ya kuimeza Zanzibar?

Je tumeshapata sababu ya kuanzisha ubeberu (ukoloni) mpya?

Je Shirikisho la Afrika la Mashariki la kisiasa( kuunganisha nchi za Afrika Mashariki) liko njiani kuja/ kuundwa?

Nani anaweza kutegua hiki kitendawili cha Mwalimu Nyerere?


Ni wakati muafaka kwa CCM kuona upepo unakoelekea na kufanya maamuzi magumu.
 
Nonda,
kuna kitu kimoja Wzn wameshindwa kukielewa. Wanadai mamlaka kamili 100%. Wakati huo huo wanadai kuwe na serikali 3 au mkataba. Kuwepo kwa vitu hivyo tayari kutaondoa asilimia 100 na kuirudisha chini. Zanzibar watakubali hilo? Kama hawakubali, mamlaka kamili wanayodai ni yapi yatakayowaacha na uhuru wa mamlaka kamili 100%

Ukishasema mamlaka kamili hapo tayari umeshaondoa uwezekano wa mkataba au serikali 3. Labda unieleweshe utakuwaje na mamlaka kamili halafu ukawa na mkataba au serikali 3?

Pili, kuna kitu kinaitwa serikali 3, nauliza kila siku na huwa ndio mwisho wa mjadala hasa kwa WZNZ. Serikali ya tatu ya muungano itashughulikia nini ili ihakikishe kuwa ZNZ inabaki na mamlaka kamili 100%. Na hiyo ya tatu inaendeshwaje kwa gharama ikiwa ZNZ yenye mamlaka kamili 100% ni mbia sawa na Tanganyika itakayokuwa na mamlaka kamili?

Tatu, katika mkataba unaongelewa kuna siri gani ya mkataba ambayo WZNZ hawataki kuiweka wazi? Nina maana mkataba ushughulikie mambo gani yenye faida kwa pande zote zikiwa wabia sawa?

Nne, kitu gani kinachowazuia kusema mnataka kuvunja muungano? Kwanini mnakimbilia serikali 3 au mkataba na si kuvunja bughudha hii ya muungano inayowanasabisha na wabantu ili hali ninyi ni waarabu? Kwanini msitamke LET Tanganyika GO! kama sisi tulivyo na uthubutu wa kusema LET ZNZ GO!

Nomba safari hii usikimbie, uwe na uthubutu wa kujibu. Ukikimbia utakuwa umepoteza uhalali wa kulizungumzia hili jambo kwasababu utakuwa sawa na yule kijana wa mtaani anayeimba mayenu na bolingo ambaye ukimuuliza maana yake hajui, lakini anaimba vema sana.
 
Maanakijiji acha ujanjaujanja,

Unachosema hapa hakina tofauti na wanachokifanya CUF aka UAMSHO,

SERIKALI MOJA + SERIKALI TATU NA MUUNGANO WA MKATABA HUKU SERIKALI ZA ZANZIBAR NA TANGANYIKA ZIKIWA NA MAMLAKA KAMILI = KUVUNJA MUUNGANO

Kuweni na uthubutu wa kusema yaliyomo moyoni na sio kutumia lugha za kiujanjaujanja. Thubutu kusema kuwa hautaki Muungano. Waambieni ukweli wafuasi wenu kuwa hamtaki Muungano uendelee kuwepo kuliko kuwadanganya wapiganie kisichoweza kupatikana.
 
Mumo wowote tunaoutaka lazima ukubalike kwa watu wa pande zote mbili kwa ridhaa zao - Wanzibari kwa upande wao na Watanganyika kwa umoja wao - Ndipo muungano utakuwa muungano. Sasa tulipofika: Muungano wa serikali mbili haukubaliki - haufai una kero luluki. Watanganyika hawataki serikali tatu - ni gharama kuziendesha. Wazanzibar hawataki serikali moja- hawataki kutawaliwa na kuwa mkoa wa tanganyika. Tufanyeje sasa? Ng'ombe avute gari au gari ivute ng'ombe?

Nyie ndiyo mnapotosha dhana ya Muungano. Ni vipi Zanzibar itakuwa Mkoa wa Tanganyika kwa mfumo wa serikali moja wakati Tanganyika na yenyewe itakuwa imekufa?

Ok Wanzibara hawataki serikali moja, swali langu linakuja nini mantiki ya Muungano kama bado kila nchi itakuwa na srikali yake. Huo utakuwa Muungano au Ushirikiano baina ya nchi mbili? Huwa nawashangaa sana Wanzinzibar Muungano hawautaki ila faida za Muungano wanataka! What's this Paradox?!

TUMBIRI (PhD, Hull University, HULL City - United Kingdom),
tumbiri@jamiiforums.com


 
Haya ndiyo matatizo ya kuwa waandishi habari wasiokuwa na miiko ya taaluma zao, wewe unataka kuwafundisha watanzania nini cha kusema? Kila mtanzania yupo huru kutoa mawazo yake huna haja ya kuwa mwalimu, nenda katoe mawazo yako binafsi kwenye tume usiwafundishe watanzania, wewe kama mfumo wa muungano uliopo haukufai huo ni mtazamo wako, acha watu wawe na uhuru wao wa mawazo.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Serikali 2 ni mzigo kuliko 3. tuna wabunge 352 kat yao 82 kutoka zenji, tunawalipa ambapo ikiwa serikali 3 tunaweza kuwa na bunge la watu 150 tanganyika, na shirikisho 30 (15 kila upande) Hii si mzigo.

Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

SAY NO TO SERIKALI TATU!!

Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
 
Nonda,
kuna kitu kimoja Wzn wameshindwa kukielewa. Wanadai mamlaka kamili 100%. Wakati huo huo wanadai kuwe na serikali 3 au mkataba. Kuwepo kwa vitu hivyo tayari kutaondoa asilimia 100 na kuirudisha chini. Zanzibar watakubali hilo? Kama hawakubali, mamlaka kamili wanayodai ni yapi yatakayowaacha na uhuru wa mamlaka kamili 100%

Ukishasema mamlaka kamili hapo tayari umeshaondoa uwezekano wa mkataba au serikali 3. Labda unieleweshe utakuwaje na mamlaka kamili halafu ukawa na mkataba au serikali 3?

Pili, kuna kitu kinaitwa serikali 3, nauliza kila siku na huwa ndio mwisho wa mjadala hasa kwa WZNZ. Serikali ya tatu ya muungano itashughulikia nini ili ihakikishe kuwa ZNZ inabaki na mamlaka kamili 100%. Na hiyo ya tatu inaendeshwaje kwa gharama ikiwa ZNZ yenye mamlaka kamili 100% ni mbia sawa na Tanganyika itakayokuwa na mamlaka kamili?

Tatu, katika mkataba unaongelewa kuna siri gani ya mkataba ambayo WZNZ hawataki kuiweka wazi? Nina maana mkataba ushughulikie mambo gani yenye faida kwa pande zote zikiwa wabia sawa?

Nne, kitu gani kinachowazuia kusema mnataka kuvunja muungano? Kwanini mnakimbilia serikali 3 au mkataba na si kuvunja bughudha hii ya muungano inayowanasabisha na wabantu ili hali ninyi ni waarabu? Kwanini msitamke LET Tanganyika GO! kama sisi tulivyo na uthubutu wa kusema LET ZNZ GO!

Nomba safari hii usikimbie, uwe na uthubutu wa kujibu. Ukikimbia utakuwa umepoteza uhalali wa kulizungumzia hili jambo kwasababu utakuwa sawa na yule kijana wa mtaani anayeimba mayenu na bolingo ambaye ukimuuliza maana yake hajui, lakini anaimba vema sana.

Nguruvi3
Nafikiri masuali yako mengi yanajibiwa na mwandishi wa hii makala.
Link Raia Mwema - Tusipoujadili muungano kwa makini, utavunjika II
 
Ndoto za alinacha.

Mdai kwani Zanzibar ni nchi yenu? nyie kwanza idaini Tanganyika, iko wapi?
 
Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

SAY NO TO SERIKALI TATU!!

Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!

MMkijiji acha kutafuna maneno...Kama ni mkweli usitafune maneno, SAY NO TO "MUUNGANO ,KATAA SERIKALI MBILI ,TATU, MOJA AU HATA NUSU SERIKALI" na uvunjwe yaishe. LET ZNZ GO!
 
Nini mawazo yako juu ya #post 88?
Nonda, ninachosema ni kuhusu mawazo ya Wazanzibar.
Joseph Mihangwa anaandika kama mwandishi tu na wala hawakilishi mawazo ya WZN.

Kama wewe mwenyewe huwezi kujibu maswali hayo basi huna uhalali wa kuongelea muungano kwasababu hujui unaongelea nini. Na hili si tatizo lako ni tatizo la WZNZ kuanzia Maalimu Seif Sharrfi Hamad Mshirazi hadi mwana uamsho.

Si Ahmed Rajab ambaye ameandika makala zapata 100 lakini hana chochote cha maana zaidi ya uzandiki.
Nasema uzandiki kwasababu hana solution isipokuwa kuwachochoea WZNZ.

Sasa amefanikiwa kuwapandisha munkari, lakini ametambua kuwa damu ya WZNZ itakapokuwa inahangaika mitaani atapata laana baada ya kusikia Watanganyika hawataki upuuzi wa serikali 3 au mkataba kwasababu hawafaidiki na lolote au chochote kutoka visiwani. Hapo ndipo anakuja na kioja cha serikali 3 au mkataba bila kueleza nini maana yake.

Nonda, nikupe ukweli wewe na WZNZ wote, hawa washirazi wanataka usultani kwasababu wanaunasaba nao ndiyo maana wanaandika kuwa ZNZ ina Washirazi wengi, na weusi ni watumwa tu hawana asili.

Kwa maana hiyo hawawaambi wazi serikali 3 za nini, mkataba wa nini. Siri ya washirazi ni kutaka mkataba au serikali 3 ili weusi watakapoona kunyanyasika wasipate tabu kurudi bara.

Washirazi wakioongozwa na maalimu wamefanikiwa ku-brain wash WZNZ na sasa wote wanaamini kuwa ZNZ ya mwaka 1963 ni bora kuliko ya 1964 na mapinduzi ni upuuzi.

Wamesha wasahaulisha kuwa wapo mabwana na Watwana.
Kurudi kwa ZNZ ya 1963 ni kutangaza utwana na hakika kama huna madevu, ngozi ya dhahabu na nywele za katani wewe utarudi kuwa kijakazi na mwosha vyoo vya washirazi.

Nonda, mmeshindwa kujibu maswali hapo juu mkae mkinya mkisubiri Jamsheed arudi.
Mumekariri makala za akina Ahmed Rajab bila kujua maudhui yake. Mnaimba nyimbo msizojua maana yake. Hamna uhalali wa kuongelea jambo la muungano hapa JF kwasababu hamjui mnataka nini na kwa nini.

Watanganyika, jiulizeni hivi kwanini hawa jamaa wamegeuka na kuacha hoja ya kuvunja muungano na sasa wanataka serikali 3 au mkataba?

Kwa taarifa hakuna chochote MZNZ anchomsaidia mtanganyika zaidi ya kuwa mnyonyaji wa kila kitu.
Watanganyika jiulizeni, hivi kwanini hawasemi serikali 3 za kushughulikia nini au mkataba wa nini wamebaki kuuma uma maneno? Hata kiongozi wao Maalimu Seif Mshirazi hana jibu sasa kuna siri gani?

LET TEHM GO! LET ZAN GO! We have nothing to lose



Wanachowaambia ni laana ya Nyerere na masikini mnaitikia tu.
 
Nonda, ninachosema ni kuhusu mawazo ya Wazanzibar.
Joseph Mihangwa anaandika kama mwandishi tu na wala hawakilishi mawazo ya WZN.

Pole sana Mkuu Nguruvi3

Ningependa kuazima maneno ya MziziMkavu, yanapatikana hapa https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-na-mustakbali-wa-muungano-3.html#post4401556
Kwa mfano wewe uwe ndio Rais wetu..
Kama hamna cha kuzungumza Siasa bora munyamaze kimya tu itakuwa ni jambo bora kunyamaza kuliko kuropoka ovyo tu pasipo kuwa na point Nguruvi3

Mkuu Nguvuri3 na wewe si uige ujasirimali wa MMJ utunge kitabu cha tamthilia au mashairi?
Umenifurahisha sana na masimulizi yako leo.

Sasa ndio huna mchango wowote au mawazo yoyote kuhusu hizo kauli za Mwalimu Nyerere, mwanzilishi wa Muungano zilizopo post#88?
 
Mwanakijiji, mimi nakubaliana na wewe kuwa tuvunje haina haja kujiwekea gharama zisizo kuwa za lazima. Ipigiwe kura ya maoni.
 
Back
Top Bottom