Muundo wa maswali ya kuchagua jibu sahihi kwa mtihani wa darasa la saba utazamwe,upya

stella halimoja

New Member
Dec 14, 2013
4
1
Waliobadili muundo wa mtihani wa taifa wa kuhitimu elimu ya msingi kuwa wa maswali ya kuchagua jibu sahihi tu,ndio wanaosababisha leo hii wanafunzi wengi wanafaulu kuendelea na elimu ya sekondari ikiwa hawajui kusoma,aina hii ya maswali inasaidia kufanikisha sera za kisiasa na kuua elimu yetu,na inapotokea kunahitajika kufanyika mabadiliko kama haya,inapaswa wadau hasa wa ngazi husika ya elimu kushirikishwa kwa hatua zote,kwani sasa ukiwauliza walimu wa s/msingi nini hasa lengo la kuondolewa aina zote za maswali ktk mtihani huo hawajui chochote
 
Mim nadhani huu ni mpango madhubuti wa watawala kudumaza elimu' ili kizazi kijacho kisijitambue' hivyo waendelee kurithishana madaraka maana watoto zao hawasomi huko!
 
Waliobadili muundo wa mtihani wa taifa wa kuhitimu elimu ya msingi kuwa wa maswali ya kuchagua jibu sahihi tu,ndio wanaosababisha leo hii wanafunzi wengi wanafaulu kuendelea na elimu ya sekondari ikiwa hawajui kusoma,aina hii ya maswali inasaidia kufanikisha sera za kisiasa na kuua elimu yetu,na inapotokea kunahitajika kufanyika mabadiliko kama haya,inapaswa wadau hasa wa ngazi husika ya elimu kushirikishwa kwa hatua zote,kwani sasa ukiwauliza walimu wa s/msingi nini hasa lengo la kuondolewa aina zote za maswali ktk mtihani huo hawajui chochote,mtaala wa elimu ya msingi unapimwa kwa kuzingatia maeneo tofauti tofauti ikiwepo kupima uwezo wa maarifa aliyoyapata mwanafunzi kwa miaka yote 7,uwezo wa kutofautisha mambo,uwezo wa kujieleza,kutumia maarifa aliyoyapata...n.k,iweje leo hadi mtihani wa hesabu achague jibu sahihi?tuache kutafuta unafuu utakaoleta madhara makubwa kwa taifa,ndio maana kukawepo aina tofautitofauti za maswali
 
serikali sikivu ya chama cha mapinduzi italishughulikia hili ...
 
Back
Top Bottom