Muuaji Mwenye Barakoa

Story Room

Member
Nov 27, 2020
56
147
Sultan Uwezo
🇹🇿 +255

Mchungaji Rodney alisimamisha gari lake kando ya mto senegal na kisha akashuka chini taratibu akijikagua suruali yake ya kadeti ya kaki ambayo ilikuwa imechafuka sana.

Iliitazama kwa muda akajaribu kuipukuta lile vumbi lakini hakuweza hivyo aliamua kuachana nayo na kuelekea mtoni ambako kwa mbali kulikuwa na watoto waliokuwa wakiogelea.

"Yaani ningeipata furaha kama ya hawa watoto japo kwa dakika moja tu ningefarijika sana aisee lakini kila siku matatizo tu kwangu kwanini?"

Alijisemesha akiketi kwenye jiwe lililokuwa kando ya maji na kuanza kuyachezea maji kwa mikono yake.

Na kwa kumuangalia ni dhahiri alikuwa na jambo kichwani linalomsumbua.

" Hivi kwanini Bartholomew haupatikani? Na kwanini ulinifanganya kuwa umeshaziweka hela kwenye akaunti? Mbona nashindwa kupata majibu ya moja kwa moja mimi Rodney?" Alivua miwani yake na kuanza kuitazama.

Aliketi pale kwa dakika kadhaa kisha aliona aondoke zake hivyo alianza kuufuata mto ule mpaka walipokuwa wale watoto waliokuwa wakiogelea na baada ya kuwafikia alitoa simu yake mfukoni na kuanza kuwapiga picha, tendo lile kiasi fulani lilimsahulisha na kilichotokea kwani alionekana kukifurahia sana mpaka pale simu ilipoita.

"Mke wangu kipenzi." Aliita baada ya kupokea.

"Uko wapi mume wangu?" Mke wake alimuuliza.

"Niko nje ya mji kidogo najaribu kuutafuta utulivu wa akili mke wangu vipi kuna tatizo huko?" Alimuuliza.

"Hapana si kawaida yako mpaka muda huu hata kunipigia simu?"

"Kichwa hakiko vizuri nisamehe mke wangu dakika chache nitakuwa hapo." Alimjibu akiitazama saa hakika muda ulikuwa umesogea hivyo alipandisha kimlima kutoka kule mtoni mpaka alipolifikia gari lake aliwasha na kuondoka. Kijua kikiwa kinazama Mchungaji Rodney aliwasili nyumbani.

" Piiii pipiii...... " Alipiga honi afunguliwe geti. Mlinzi alichungulia kupitia mlango mdogo na baada ya kujua ni mwajiri wake haraka alifungua geti. Baada ya kupaki gari alimwita mlinzi kwa kumpigia honi.

"Ndani kuna nani?"

"Kwa sasa hakuna mtu, mama katoka muda huu kasema anarudi muda si mrefu."

"Okay kaendelee na kazi."

"Sawa bosi."

Mchungaji Rodney alishuka kwenye gari na kuingia ndani ambako aliongoza moja kwa moja chumbani kwake huko alifungua kabati lenye biblia akaichukua moja na kurudi nayo sehemu ambayo huitumia kusali na hapo alipiga magoti na kuanza kusali.

Lakini wakati hayo yote yakifanyika mke wake alikuwa katulia kwenye gari lake ambalo alikuwa amelipaki kwenye uchochoro wa kuja nyumbani kwake huku macho yake yakiwa kwenye laptop yake akifuatilia kila tukio lililokuwa likifanywa na mume wake.

"Hivi nje ya huyu Bartholomew ni nani mwingine alikiona kichupa?" Mchungaji alikuwa akiongea peke baada ya kuinuka kutoka kwenye eneo la sala.

"Hivi kwanini hiki kichupa kimemchanganya sana huyu mwanaharamu? Ni cha nini?" Mke wake akiwa kakishika alijiuliza maswali ambayo majibu yake hakuwa nayo, aliifunga laptop na kisha aliondoka lile eneo kurudi nyumbani kwake.

"Mke wangu ulikuwa wapi?"
Mchungaji alimuuliza mke wake.

"Nilikuwa dukani kuna vitu vilikuwa vimepungua ndani nikaona nisisubiri kesho wakati muda huu nina nafasi."
"Sawa sawa mke wangu." Alimjibu akifungua friji.

"Hivi mume wangu una nini maana siku kadhaa hizi sikuelewi vizuri ni kama kuna jambo linakusibu lakini hautaki kuliweka wazi."

"Ni uchovu tu mke wangu unafikiri kuna lolote basi hakuna." Mchungaji alimjibu akinywa maji.

"Sawa mume wangu wacha nikaoge."

Alimuaga na kuingia chumbani. Akiwa chumbani Catherine alitoa simu yake na kumpigia mtu ambaye hakujulikana mara moja wana uhusiano gani naye.

"Nisikilize Jumbe, huyu mpuuzi keshaanza kuchanganyikiwa na huu ni mwanzo tu, sasa cha kufanya ninahitaji umuandae huyo mpuuzi alfajiri na mapema tunakwenda kuimaliza kazi yetu."

"Itakuwaje bosi hawezi kukushtukia kweli?" Jumbe alimuuliza.

"Hiyo kazi niachie mimi wewe fanya kama nilivyokueleza sawa?"

"Sawa bosi." Jumbe alimjibu. Na kisha Catherine akakata simu na kuiweka pembeni akaoga na baada ya kumaliza alitoka na kumkuta mume wake akiwa anapitia nyaraka kadhaa.

"Mume wangu..!" Catherine alimwita mume wake.

"Naam mke wangu." Aliitika Mchungaji.

"Nilikuwa naomba ruhusa kesho niende kijijini nikaione mifugo yetu kama ujuavyo majukumu ya hapa na pale yamesababisha kukosa muda wa kutembelea mashamba na mifugo na ukizingatia vifaranga ndiyo vina majuma mawili tu."

" Mungu wangu unajua mke wangu akili haikuwepo kabisa upande huo yaani toka Bartholomew aingilie mambo yangu nimechanganyikiwa sana. Ningependa tuongozane ila wewe nenda kaangalie inaendeleaje mimi ngoja nimalizie majukumu yangu na kama nikimaliza mapema nitakufuata mke wangu, ulikuwa unategemea kuwa huko kwa siku ngapi?" Mchungaji alimuuliza mke wake Catherine.

" Kama nikikuta iko vizuri sitakaa sana labda siku mbili hivi ila ikiwa tofauti hapo nitakupigia simu kuomba siku nyingine zaidi za kuihudumia." Alimjibu huku akimng'ong'a kisogoni.

" Wala usijali mke wangu kumbe itabidi nimtaarifu mzee Daud akupokee na pia uongozi wa kanisa utatakiwa kujulishwa juu ya uwepo wako au unaonaje?" Mchungaji alishauri.

" Hapana Mchungaji mimi nafikiri usiwataarifu kwani kwa kufanya hivyo watanipokea kwa ukubwa wangu kitu ambacho kitanifanya nishindwe kushughulikia shamba langu. Wewe usiwaambie kitu chochote waje washangae niko kijijini." Catherine alimjibu mume wake kile ambacho alikifikiria.

"Hakuna tatizo mke wangu kama umeona iwe hivyo sawa ila tu tahadhari ni muhimu ukifika toa taarifa ili wajue uwepo wako."

"Sawa mume wangu wala usiwe na wasiwasi juu yangu nitakwenda salama na nitarudi salama tu lakini kuna kitu umeongea hapa sijakielewa vizuri."

"Kipi mke wangu?" Mchungaji aliachia ile karatasi na kumgeukia mke wake.

"Umesema Bartholomew sijui kafanyaje?"

"Aaahh huyo achana naye mke wangu kuna pesa nilimkabidhi apeleke benki lakini cha ajabu akaunti bado haijapokea hela yoyote ile mpaka sasa na kinachotuchanganya akili hapatikani hewani wala kwake yaani sijui itakuwaje na ukizingatia tulimuamini tu kwenye nafasi hiyo ya uhasibu hajasomea kokote kule, na hatujui Wahisani wetu wakilijua hili itakuwaje?" Alimjibu akijifuta jasho usoni.

" Mhh yaani jambo kubwa kiasi hicho unakaa nalo tu bila kunishirikisha Mchungaji? Au hatuaminiani?" Catherine alimtupia lawama Mchungaji.

" Hapana siyo hivyo mke wangu kumbuka si suala langu peke yangu linahusu kanisa hivyo baada ya kikao cha kwanza cha Bodi walishauri tulifanye kimya kimya hata wake zetu tusiwape taarifa na ndicho kilichofanywa siyo kwamba sikuamini mke wangu kipenzi." Mchungaji alijitetea mbele ya mke wake ambaye alionekana kukerwa na jambo hili.

" Sawa mume wangu lakini ninachokuomba jaribu kumpelekeza mke wake anaweza kujua chochote kwenye hili au hata kueleza mume wake kaenda wapi."

" Nashukuru mke wangu kwa ushauri nitaufanyia kazi kesho asubuhi kabla ya kuanza pilika zangu." Alimjibu akifunika dokumenti zake na kisha kumfuata mke wake kitandani.

JE NINI KITAENDELEA?

KARIBUNI KATIKA SEHEMU YA PILI YA HADITHI HII.

PicsArt_11-08-01.31.34.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

***

Ndani ya msitu mnene ulio kwenye mlima Casamance ambao unapatikana kilometa zipatazo 425 kutoka katikati ya jiji la Dakar kwenye jumba chakavu ambalo lilikuwa likimilikiwa na kampuni ya Utalii ya 'Go safaris' na baada ya kufilisika ililitelekeza jumba hilo likibaki kumilikiwa na popo pamoja na buibui wa kutosha. Lakini leo kulikuwa na wakazi wapya kabisa ambao walikuja na kuweka makazi hapa kwa lengo maalum.

"Bosi huyo kafika." Kiongozi wao aliwaambia wenzake. Na walipoangalia nje kupitia dirishani waliweza kuliona gari likiingia hapo kwa kasi na baada ya kulipaki nyuma ya jengo hilo ambako kulikuwa na maegesho ya magari,alishuka haraka na kufunga milango kisha akaongoza ndani ambako alikaribishwa na wenyeji wake.

"Karibu bosi kwenye makazi yetu mapya kabisa." Aliongea Jumbe.
"Asante Jumbe mnaendeleaje lakini?" Catherine alimuuliza.

"Tunashukuru tunaendelea vizuri japo mtu wako alianza kusumbua baada ya kuzinduka ikabidi tumpige sindano nyingine ya usingizi."
"Ni muda gani umepita toka mumdunge hiyo sindano?" Catherine aliuliza.

"Yamepita masaa matatu na inaisha nguvu baada ya masaa manne tuna saa moja mbele." Jumbe alijibu.
Catherine aliongoza mpaka kwenye chumba walichomhifadhi Bartholomew na kumtaka Jumbe amfungue pingu za miguuni abakie na za mikononi tu.

"Abakie na za mikononi tu kuelekea kwenye pumzi yake ya mwisho."

"Sawa Bosi." Alijibu Jumbe na kuanza kuzikata. Kisha yeye Catherine alitoka mle kwenye chumba cha giza na kuingia kwenye chumba chake alichokuwa kaandaliwa. Mle ndani aliitoa laptop yake na kuiwasha kisha akaifungua 'connect app' ambayo huitumia kunasa mawasiliano ya mume wake Mchungaji Rodney. Lakini ni kama alihisi kitu hivyo alitoka haraka nje na kumfuata Jumbe aliyekuwa kwenye kile chumba cha giza.

"Jumbe tunahitaji mtaalamu wa tarakilishi kuna vitu navihitaji."

"Kuhusu hilo ondoa shaka kuna dogo nitamcheki kesho baada ya hili tukio." Alimjibu.

"Kuwa makini asije kuwa kimeo nadhani unajua ni watu gani tunafanya nao kazi hapa." Naelewa Bosi.

"Kingine, ulikutana na uongozi wa kitongoji hiki kuwapa taarifa ya uwepo wetu?"

"Ndiyo nilishakamilisha na nilichowamaliza ni baada ya kujitambulisha kama Kampuni ya Usafirishaji watalii ya 'Eagle Tours' na huwezi amini mwenyekiti kafurahi sana kwa sisi kuwa kwenye majengo haya." Jumbe alimjibu Catherine.
"Kwanini?"

"Anasema wahalifu wengi walikuwa wakijificha hapa."

"Inatakiwa tufanye shughuli zetu kama leseni inavyosema nyuma ya pazia tunafanya yetu."
"Ondoa shaka mkuu katika hili."
"Sasa niitie vijana wako wote niongee nao muda huu."

"Sawa mkuu." Jumbe alijibu na kutoka nje ambako aliwaita vijana wake wote ambao walikuja na kuongea na mtu ambaye sura yake hawakuiona kutokana na vazi ambalo alivalia, Catherine aliongea nao kwa kirefu sana juu ya wao kuwa pale na majukumu yao na mwisho kabisa alisisitiza.

"Kwa ambaye hayuko tayari kufanya kazi nasi apite mbele tuachanane naye kwa amani hapa tunahitaji waliojitoa kwa dhati." Baada ya kauli ile ya Catherine kuna vijana wawili walipita mbele kuashiria kuwa hawako tayari kufanya kazi walizozisikia kwa bosi wao huyo.
" Jumbe nilikwambia nini si unaona sasa kumbe ukurutu ulikuwa bado miilini mwetu." Aliongea hayo na kuinuka kitini na kuwafuata vijana wale ambao alianza kuwashambulia kwa kichapo na baada ya kuona anapoteza muda alichomoa bastola na kuwamiminia risasi kama mvua zilizowapeleka chini.

" Kawatupeni kwenye mtoni muda huu na kama kuna wengine wanataka kuacha kazi wapite mbele." Aliongea hayo akiondoka pale na kurudi chumbani kwake na kuwaacha vijana wake wakiitoa ile miili ya wenzao ambao walikuwa maiti tayari.

"Mama Jennifer tafadhali wataarifu wazee wa baraza kuwa kesho tukutane asubuhi na mapema kujadili huu upotevu wa hizi milioni mia moja pamoja na mengine." Ulikuwa ni ujumbe ambao Mchungaji aliutuma kwa mama Jennifer ambaye ni katibu wa Kanisa. Catherine baada ya kuusoma ujumbe huu kupitia laptop yake alitabasamu sana na kujipa ushindi.

" My husband, baba Mchungaji nakuonea mpaka huruma nikifikiria namna nitakavyokunyofoa roho yako, kwa sasa sina haraka sana kwani naanzia matawi kwanza kisha shina litakuwa la mwisho." Bado haijafahamika ni kwanini Catherine anayafanya haya maana yeye ndiye aliyemteka Bartholomew na kumpora fedha zote na sasa plani yake ni kumuua kwa sababu ameshamtambua na yeye tageti yake ni kuitunza siri hii.

Akiwa anataka kuizima laptop yake mara kuna ujumbe uliingia kwenye namba ya mume wake Mchungaji Rodney kutoka kwa mama Jennifer haraka akausoma.

"Baba Mchungaji hivi mama kaenda wapi? Maana si kawaida yake kumaliza masaa zaidi ya mawili bila kutupigia wanakikundi?" Alikaa vizuri kusubiri mume wake atajibu nini baada ya kuusoma ujumbe huo.

"Kaelekea nje ya mji kuangalia miradi yetu maana ni muda mrefu hatukupata muda wa kuendelea huko na kama ujuavyo mifugo inataka uangalifu wa karibu, na mtandao kule ni tatizo mpaka apandishe kwenye kimlima fulani hivi ndiyo mtandao ukamate."
Majibu ya mume wake yalimfurahisha sana akajikuta anapiga ngumi hewani ya ushindi, mara kuna ujumbe uliingia tena kwenye simu ya mume wake baba Mchungaji Rodney.

" Hivi kuna kitu gani anakitaka huyu mwanakondoo?" Catherine alijikuta akijiuliza hili swali huku akiiangalia simu ambayo ilimuonesha kuwa ilikuwa ni saa saba ya usiku.

"Wha......t??"Alijikuta akiuliza kwa lugha ya kigeni baada ya kuusoma ujumbe alioutuma mama Jennifer kwa Mchungaji.

" Naomba kesho tuonane kwangu au sehemu yoyote ile kuna kitu nahitaji kukueleza juu ya mkeo kuhusu usalama hapa kwangu ni wa kutosha maana mume wangu kasafiri leo kuelekea nchini Afrika ya Kusini kufuata mali ghafi za kiwandani." Catherine hakutaka kusubiri majibu kutoka kwa mama Jennifer alichokifanya aliizima laptop na kuingia kuoga bafuni kuoga tena maana alihisi joto mwilini mwake na aliporejea alijitupa kitandani huku kichwani kwake jina la mama Jennifer lilikuwa likizunguka.

"Nitamuonesha mimi ni nani huyu Mwanakondoo." Catherine aliongea hayo akijifunika shuka vizuri.

Kukiwa kumetulia vizuri giza limetanda kiasi cha kutokuona mbele labda mpaka kwa msaada wa mwanga wa taa yoyote. Catherine aliamka na kutoka nje akiwa kwenye vazi lake huwa akilivaa tu hili ujue kuna roho ya mtu inakwenda kubebwa.

"Jumbe nitolee pikipiki nje ya geti fasta." Alimuagiza Jumbe ambaye ni kama alitaka kuuliza swali maana alipoiangalia saa yake ilikuwa ni saa nane kasoro kama dakika kumi na nne.

"Jumbe sihitaji swali fanya kama nilivyokwambia unanichelewesha ujue." Catherine aliona amfokee labda atamuelewa. Jumbe aliingia kwenye jumba linalohifadhi mashine tofauti tofauti na kuitoa pikipiki aina ya Honda Sky B690 na kuiwasha akiwa anajiandaa kuitoa nje Catherine alimfuata na kumvuta kisha yeye akapanda na kumpigia honi mlinzi aliyefungua geti kumruhusu atoke. Mlinzi baada ya kuona bosi wao katokomea gizani kwa spidi ya ajabu alifunga geti na kumfuata Jumbe pale chini alipokuwa kaangukia.

"Kapteni kuna nini mbona bosi kaondoka ghafla bila hata kuogopa hili giza ambalo muda wowote linamwaga maji?"
"Pemba acha maswali umesahau ulichoambiwa muda mfupi uliopita? Labda nikuulize swali ndugu yangu kuna mwezi hujalipwa mshahara?" Jumbe alimtupia swali Pemba ambaye ni mlinzi.

"Nalipwa Kapteni." Alimjibu
"Kwa hiyo?"
"Nisamehe Kapteni wacha nikupe kampani uinuke asije rudi akakukuta hapa chini na kukupitia." Jumbe hakujibu chochote zaidi ya kutabasamu tu. Umbali kutoka Casamance mpaka Dakar ni zaidi ya kilometa 400 huku muda unaotumika kwa magari ya kawaida ni masaa sita lakini Catherine alilenga kutumia maswali matatu tu kwenda na kurudi ili walau saa kumi na moja alfajiri awe amesharejea kijijini.

***

"Hodi, hodi, hodi mama Jennifer..." Catherine alikuwa mlangoni akibisha hodi kwa sauti ya kiume.
"Nani mwenzangu?" Mama Jennifer aliuliza kwa sauti ya mashaka.

"Ni mimi Mchungaji Rodney." Catherine alimjibu kwa sauti ya maigizo.

"Mchungaji Rodney? Mbona usiku hivi kuna usalama kweli?" Mama Jennifer aliuliza akiufungua mlango. Lakini kabla hajafanya chochote alijikuta akivutwa nje na kumchoma visu vitatu mfululizo vya kifua na kisha alimtupa chini huku kisu kikiwa kifuani na kuondoka zake haraka kabla wazurulaji hawajaona hilo tukio, na kwa kuwa mitaa ile anaifahamu vizuri haikuwa shida kwake kutembea mwendo autakao kurudi Casamance.

Ndani ya saa moja alikuwa ameuacha mji wa Dakar na tayari miji kadhaa iliyo katikati ya Dakar na Casamance iliweza kumshuhudia Catherine akikata mitaa lakini alipoingia kwenye mji wa Kanel alikutana kizuizi, hapa alichanganyikiwa kwani alipopita awali hakikuwepo.

"Shiiiit kuna nini tena hapa?" Alijiuliza Catherine akipunguza mwendo baada ya askari wa doria kumpiga mkono.

Kwa mavazi aliyokuwa kayavaa kuanzia kichwani mpaka miguuni ilikuwa ngumu kwa mtu yeyote kumtambua vizuri hivyo alisimama na kumsubiri huyo askari amfikie, alichokifanya alishuka na kuegemea pikipiki akiweka mikono yake sawa huku macho yake yakiwa yanalichunguza lile eneo lina watu wangapi.

"Vipi unatoka wapi muda huu? Unaweza kunionesha utambulisho wako tafadhali?" Alimuuliza huku akimsogelea karibu.

"Samahani kama nitakuwa nimekosea nisamehe, naomba kukujua maana siku hizi Wasanii wamekuwa wengi." Catherine alimjibu.
"Acha ujuaji wewe mavazi yangu tu ni utambulisho tosha, tekeleza agizo langu."

Catherine alimtazama askari huyo vizuri na baada ya kugundua kibanda cha mapumziko kiko mbali kidogo na pale walipo aliona hakuna cha kupoteza alichokifanya aliingiza mkono mfukoni mwake kama vile alikuwa akitoa vitambulisho vyake. Askari huyo akiwa kajisahau alikutana na kisu cha kifuani kilichomfanya atake kupiga kelele lakini Catherine alimuwahi na kumziba mdomo kisha

Akakichomoa na kukishindilia tena kifuani,alikichomoa na kukifuta damu kwa kutumia kombati la huyo askari akakirudisha sehemu yake na kuondoka zake. Masaa mawili baadaye akawa ndani ya ngome yake na tayari ilikuwa ni saa kumi na moja alifajiri, alimshukuru Mungu kabla ya kushuka kwenye pikipiki baada ya kuondoka salama na kurudi salama kisha akamwita Jumbe aiingize pikipiki sehemu yake na yeye akaingia ndani ambako moja kwa moja alielekea bafuni kuoga na kuyafua mavazi yake yaliyokuwa na matone ya damu alipomaliza kuoga na kuyaosha mavazi yake kwa staili ya kufuta maeneo yaliyokuwa na damu aliyatundika mahali pake na kuchukua Barakoa yake akaibusu na kuiweka kabatini kisha akalifunga na kuitoa funguo ambayo aliiweka nyuma ya kabati lile kulikokuwa na kisehemu cha kuhifadhia hiyo funguo kisha akaketi kitandani na kuanza kupaka mafuta taratibu kwa staili ya kuukanda mwili kutokana na uchovu aliokuwa nao.

"Kama nawaona vile watakavyohaha kumtafuta muuaji wa watu watatu kwenye maeneo tofauti na miji tofauti. Sipati picha pale baba Mchungaji atakapokutana na maiti ya kondoo wake aliyeongea naye masaa kadhaa." Aliongea haya macho yake yakiwa kwenye simu ya mama Jennifer ilikuwa kitandani.

Baada ya kubadilisha mavazi yake alitoka na kumtaka Jumbe amuandae mtu wake akaimalize kazi yake.
" Fanya haraka Jumbe kunapambazuka sasa tusije shindwa kutekeleza jukumu letu."

"Kila kitu kiko sawa tulikuwa tunakusubiri wewe tu." Alimjibu.

"Mwambie mlinzi afungue geti haraka." Alimuagiza akiingia kwenye gari ambalo lilimpakia Bartholomew.
"Mnataka kuni...kunifanya nini mbo... na si..si..sina kosa lolote?" Bartholomew aliuliza baada ya kuzinduka.
"Mmh kumbe uko macho?" Catherine alimuuliza.

"Wewe si mama Mchungaji?" Bartholomew alimuuliza.

"Hata nikisema ndiyo itasaidia nini Bartholomew?" Catherine alimuuliza akiwasha gari baada ya Jumbe kuingia.
"Kama kuna......." Kabla hajamalizia sentensi yake alikutana na ngumi ya uso kutoka kwa Jumbe iliyomfanya ashindwe kuongea na kujikuta akitoa mlio wa kugugumia maumivu.

"Unatakiwa kutulia kimya na kusubiri utakachoamriwa kukifanya siyo unatupigia mikelele yako hapa." Jumbe alimwambia Bartholomew kwa sauti nzito na ya kukwaruza.

JE, NI NINI KITATOKEA KATIKA KITIMUTIMU HIKI?

TUUNGANE KATIKA SEHEMU INAYOFUATA TUPATE KUJUA MBIVU NA MBICHI.

PicsArt_11-08-01.31.04.jpg
 
Sultan Uwezo
🇹🇿+255

***

"Bwana Yesu asifiwe Baba Mchungaji!!" Upande wa pili wa simu uliongea baada ya Mchungaji Rodney kupokea simu.

"Amina mzee Lusoka, mmeamkaje?" Mchungaji aliuliza.

"Tumeamka salama lakini kuna tatizo mtaani kwetu." Mzee Lukosa alimjibu

"Kuna tatizo? Tatizo gani hilo?"
"Mama Jennifer kauawa kikatili hapa kwake." Mzee Lukosa alimjibu.

"Unasemaje mzee Lukosa?" Mchungaji aliuliza kwa mshangao.
"Ndiyo hivyo Mchungaji hatuko naye mama yetu sijui nini kimemsibu?" Mzee Lukosa alimjibu.

"Huwezi amini mzee wangu jana kanipigia simu akiwa na furaha tele na pia aliomba kuonana na mimi leo hii sijui alitaka kuniambia nini mama Jennifer?" Mchungaji Rodney alishangazwa na taarifa ile kutoka kwa mzee Lusoka.

"OK naungana nanyi muda si mrefu wacha nijiandae."

"Sawa baba Mchungaji." Mzee Lusoka alimjibu Mchungaji na kuikata simu.
Upande wa Mchungaji taarifa ile ilikuwa pasua kichwa ukizingatia alikuwa ni mtu wake wa sirini kwa muda mrefu sana wakuwa kwenye mahusiano haya ambayo hakuna mtu kutoka nje aliyeweza kuyashtukia kutokana na mbinu waliyokuwa wakiitumia haikutoa mwanya kwa jamii inayowazunguka kujua hili. Na hata mtoto huyu aitwaye Jennifer ni wa Mchungaji Rodney kitu ambacho hata Otago Mathew ambaye ni Mume wa mama Jennifer hajui akijuacho yeye Jennifer ni mtoto wake.

"Ni nani aliyefanya unyama huu kipenzi changu? Kwanini umeondoka na kumuacha mwanangu mikononi mwa adui yangu huoni umeninyang'anya haki yangu?"

Mchungaji aliendelea kulia akiwa mbele ya kioo kama vile kampoteza mke wake halisi kumbe alikuwa mchepuko tu, akiwa anabubujikwa machozi kama mtoto simu yake iliita akaichukua na kuitega sikioni

" Habari ya asubuhi mume wangu." Alikuwa ni mke wake Bi Catherine akimtakia hali kama ilivyo kawaida yake kwa mume wake.

"Nzuri mke wangu, Bwana Yesu asifiwe." Alimjibu akilifuata taulo kabatini.

"Amina mume wangu vipi mbona sauti inatoka kama vile una mafua?" Catherine alimuuliza mume wake baada ya kumsikia akiongea kama vile ana mafua.

"Hapana mke wangu nimepata mshtuko kwa simu niliyopokea muda mfupi uliopita....." Kabla hajamaliza kuongea alikatishwa.

"Mshituko? Kuna nini baba Mchungaji?" Ilibidi aulize kutaka kujua ni kitu gani hicho.

"Ni mama Jennifer." Akatulia kwanza.

"Mama Jennifer kafanya nini tena?" Catherine alimuuliza Mchungaji.
"Kauawa kikatili na watu wasiofahamika pale pale nyumbani kwake kwa mujibu wa mzee Lusoka." Mchungaji alimjibu mke wake.

"Hapana mume wangu siyo kweli, nasema siyo kweli... Mama Jennifer awe kafariki? Kwanini? Na kwanini wamuue? Aaghhh mume wangu ndani ya masaa kadhaa nitakuwa hapo." Alionekana kushtushwa na taarifa hii ya mauaji ya mama Jennifer kama vile hajui chochote kile.

" Sawa mke wangu lakini kuwa makini ukiwa unaendesha ajali haipigi hodi."Mchungaji alimjibu.

" Nimekuelewa mume wangu nitakuwa makini." Catherine alimjibu mume wake na kukata simu baada ya kuiweka simu pembeni aliendelea kujiandaa na kila kitu kilipokuwa tayari Mchungaji Rodney alitoka na kuingia kwenye gari lake aina ya BMW Kentucky nyekundu na kuondoka kuelekea msibani. Na ndani ya dakika kama kumi na saba hivi Mchungaji Rodney aliwasili nyumbani kwa Otago Mathew, umati uliokuwa nyumbani hapo haukuwa wa kawaida kiasi kwamba ili uweze kuingia ndani ilibidi kujipenyeza kwa tabu sana lakini kwa Mchungaji haikuwa hivyo kwani lile gari lake linafahamika sana alipoteremka tu mtu wa mapokezi alifika na kumuongoza Mchungaji sehemu ambayo iliandaliwa kwa ajili yao.

"Karibu Mchungaji." Kijana huyo alimkaribisha.

"Asante kijana wangu, poleni na kilichotokea." Mchungaji Rodney alimjibu baada ya kumtazama kwanza kijana huyo aliyefika kumchukua.

"Asante Mchungaji ni kama ulivyosikia." Kijana huyo alimjibu wakipenya kuingia ndani.

Baada ya kuingia ndani Mchungaji aliongozwa mpaka kwenye kiti ambacho alikuwa kawekea na kuketi. Pale ndani kulikuwa na watu maarufu tu huku wengine wakiwa nje kwenye maeneo ambayo ualitengwa.

"Baba Mchungaji karibu sana, dada yetu mpendwa Agnes Jahokwa katuachia majonzi na wala hakutaka kusubiri aagane nasi wapendwa wake." Mzee Lukosa alivunja ukimya uliokuwa umetanda mahali pale huku nje pamoja na chumba walichokuwa wameketi wakina mama vilio vilikuwa vimetawala.

" Bwana Yesu asifiwe ndugu zangu." Mchungaji alisimama.
" Amina." Walijibu.

" Ndugu zangu nashindwa hata nianzie wapi kwenye hili najikuta mwili wote unanitetemeka hakika Agnes kajua kutuliza, lakini niongee tu kwamba hatuko naye kimwili kama hivi lakini kiroho tuko naye na siku hizi ambazo tunaziona kama ni za majonzi tunatakiwa tuzitumie kumuombea ndugu yetu kwa Mungu mwenzetu katangulia njia hii ni yetu sote. Sijui kama tumeelewana ndugu zangu?" Mchungaji aliongea kwa kirefu na kisha alihitimisha kwa kuuliza.

" Amina, amina baba Mchungaji."Walijibu. Mchungaji alimfuata mume wa marehemu bwana Otago Mathew pale alipokuwa kaketi na kumkumbatia.

" Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu mtumishi."

" Amina baba Mchungaji nashukuru sana ndiyo hivyo mama Jennifer kaniacha hakunipigia hata simu aliamua kwenda kimya......" Alishindwa kuendelea akaanza kulia.

"Pole sana rafiki yangu najua kidonda hiki kitachukua muda mrefu kupona lakini naomba nikutie moyo kuwa haijalishi kaondokaje tunachotakiwa kuamini ni kwamba ametangulia mbele za haki na kazi yake Mungu haina makosa." Mchungaji alimwambia.

"Nashukuru Mchungaji wangu nitakuwa imara kwa kipindi hiki." Otago alimjibu.

"Amina, naomba kuuliza kidogo k....." Kabla hajauliza swali lake Mchungaji Rodney aliingia Afisa Upelelezi ambaye alifanya kila mmoja mle ndani kutulia bila shaka walitaka kujua kuna kipi walichokibaini kwenye mwili wa marehemu.

"Poleni sana ndugu zangu kwa msiba huu wa mpendwa wetu Agnes Jahokwa." Alianza Afisa Upelelezi.
"Tunashukuru kiongozi." Alimjibu mzee Lusoka.

"Baada ya kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu tumebaini kuwa muuaji hakufanya kitu chochote kile zaidi ya kumvamia na kumchoma visu viwili vya kifuani.

Lakini kinachotushangaza ni kwamba namna alivyouawa marehemu hapa ndivyo walivyouawa marehemu wengine watatu kutoka maeneo tofauti ya mji huu ambapo kwenye mpaka wa Dakar na Casamance ameuawa Askari wetu aliyekuwa doria na kule Casamance kumekutwa miili miwili mmoja umekutwa msituni na mwingine umekutwa mtoni. Na miili yote imechomwa visu viwili kifuani hivi hivi na mkono uliotumika ni wa kushoto kwa miili yote... " Kabla hajaendelea Mchungaji alimkatisha Ofisa huyu jeshi la Polisi.

" Afande samahani unasema kuna maiti nyingine tena?"
" Ndiyo baba Mchungaji na kitu kilichotuacha mdomo wazi ni muda wa mauaji, maiti zote zimeuawa ndani ya usiku wa kuamkia leo ndani ya masaa mawili mpaka manne hivi." Afisa Upelelezi huyu alimjibu.

"Mungu wangu kwanini iwe hivyo?" Mzee Lukosa aliuliza kwa mshangao.
"Ndugu zangu naomba niwaache muendelee na taratibu za mazishi ya mpendwa wetu ni kwanini yamefanyika haya tuachieni sisi na majibu yatatolewa Upelelezi ukikamilika."

"Tunashukuru Afande kwa taarifa hiyo na Mungu awaongoze kwenye Upelelezi wenu." Mzee Lukosa alimjibu Afisa Upelelezi huyo D O. Shaidour na baada ya hapo aliwaaga na kutoka.

"..... Ifuatayo ni Habari kwa ufupi kutoka County Radio ikisomwa nami Leila Othman... Miongoni mwa taarifa tutakazokuletea hapo baadaye ni pamoja na watu wanne akiwemo Askari wa Doria kutoka geti la 'Livingstone Hill', wawili kutoka eneo la Casamance na mmoja kutoka Dakar ambaye ndiye mwanamke pekee... Pamoja na mengine mengi ungana nami itakapofika saa saba kamili mchana na nikutakie mchana mwema. Asante..." Kila mmoja aliyekuwa akiangalia Televisheni alimtolea mwenzake macho kama vile alitaka kumwambia kitu lakini alishindwa na hivyo kusababisha kimya kutawala kwa muda.

" Ndugu zangu mtakumbuka kabla ya tukio la kuuawa kwa mama Jennifer kuna kijana wetu alipotea mpaka leo hajapatikana asije kuwa miongoni mwa hao wengine?" Mzee mmoja ambaye muda wote alikuwa kimya akitafuna karanga aliongea jambo lililozua mzozo.

"Kwa upande wangu sina uhakika huyo Bartholomew si aliondoka na hela za kanisa je yuko zake mji mwingine akila jasho la wengine?" Mama mmoja ambaye ni mfanyabiashara pale mtaani kwa wakina Otago alimjibu yule mzee bila shaka yoyote.

"Ni kweli lakini tusubiri taarifa yenyewe tutajua tu hakuna haja ya kulumbana hapa ndugu zangu."Mzee Lukosa alishauri kusubiri mpaka watakapopata taarifa kamili isiyo na maswali. Suala la kupotea kwa Bartholomew pamoja na matukio ya kuuawa kikatili kwa watu hawa wanne akiwemo mama Jennifer liliendelea kuwa agenda kubwa katika msiba huu kila mmoja aliongea lake, kuna wengine waliosema inawezekana mama Jennifer alikuwa ni mmoja wa watu walioshirikiana na Bartholomew kwenye upotevu wa fedha za kanisa na ndiyo maana wameamua kumuua ili kufuta ushahidi na wapo waliosema kuwa muuaji wa mama Jennifer na Bartholomew yuko ndani ya Kanisa hili la 'JESUS OUR KING' kutokana na waumini wawili kutoka kwenye kanisa hili kuuawa ndani kipindi kifupi.

"Jamani mimi bado naamini kaka Bartholomew hajafa anaweza kuwa Ulaya anatumia mamilioni aliyotoroka nayo, yaani ndiyo naamini mbele ya dollar hakuna mlokole kwa namna alivyo Bartholomew unaweza kuamini ndiye mtuhumiwa wa upotevu huu?" Kijana mmoja alimwambia mwenzake wakati taratibu za kuuaga mwili wa mama Jennifer ziliendelea pale nyumbani kwake.

" James achana na masuala usiyokuwa na uhakika nayo, huwezi kujua ni nini kilimkuta kaka Bartholomew?" Jacob alimsihi.

" Aaahh na wewe si ni wale wale tu."

James alimjibu Jacob na kuondoka eneo lile na kusogea karibu na pale walipokuwa wameketi viongozi wa mtaa pamoja na baadhi ya viongozi wa dini.

Wakati zoezi la kuuaga mwili wa marehemu likielekea ukingoni aliwasili mama Mchungaji na kukaribishwa vijana waliokuwa wameandaliwa kwa zoezi hili.

"Karibu mama Mchungaji." Mmoja wa vijana hao alimkaribisha.

"Asante vijana wangu poleni na msiba wa mpendwa wetu."

"Tunashukuru mama." Walimjibu wakimuongoza mpaka walipokuwa wameketi wakina mama na kwa kuwa walikuwa wakimalizia kuuaga mwili naye aliunganisha moja kwa moja kuuaga kwanza kabla ya kuketi na baada ya kumaliza ndiyo aliketi na kuwasalimu wafiwa pamoja na wote waliokuwa pale.

"Poleni sana ndugu zangu."
"Asante mama Mchungaji ndugu yetu kaumalima mwendo." Alimjibu dada yake marehemu.

"Ni kweli lakini inauma sana kwa alichofanyiwa...." Catherine alianza kulia kuonesha kuguswa sana na msiba ule, kitendo kile kiliwafanya wakina waliokuwa pale kumuinua Catherine aliyekuwa akigalagala chini na kumuingiza ndani na kupisha shughuli za maziko kuendelea.

HII NI SEHEMU YA TATU TU MPENZI MSOMAJI, JIANDAE KWA SEHEMU YA NNE YA KIGONGO HIKI KIKUBWA NI KUENDELEA KUOMBA MUNGU INTERNET ISIKUTANE NA KIKWAZO KITAKACHOSABABISHA TUSHINDWE KUSONGA MBELE.

PicsArt_11-08-01.31.34.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

Baada ya kuingizwa kwenye chumba hiki ambacho kilikuwa na baadhi ya Waombolezaji Catherine aliinuka na kuingia chooni, huko aliitoa simu yake na kumtafuta kijana wake Jumbe ambaye alitaka kumpa ujumbe fulani.

"Naam Bosi." Jumbe aliitika.
"Nimeshafika msibani mdogo wangu lakini mambo si mambo taarifa za mizoga yetu ziko kila kona na tayari serikali imeanza kufuatilia hivyo kuwa makini na hao madogo na kama kutakuwa na yeyote atakayeuza ramani mmalize."

"Nimekupata Bosi wangu na hata hivyo nilitaka kukucheki kwa hewa ni baada ya kuziona hizi taarifa mtandaoni.." Jumbe alimjibu.
"Ulitaka kusema nini jeshi langu?" Catherine alimuuliza.

"Nilitaka kukwambia ni kwanini tusimfuatilie huyu Afisa Upelelezi kumpunguza kasi?" Jumbe alimjibu.
"Siko sehemu nzuri Jumbe nitakucheki baadaye kidogo."

"Sawa Bosi." Kisha Catherine alikata simu na kutoka nje.
"Samahani mama wameanza kuzika?" Catherine alimuuliza mama mmoja wa makamo ambaye alimkuta pale sebuleni na wengine hakuwakuta.

"Ndiyo mwanangu, na muda huu Mchungaji anamalizia neno." Mama huyu alimjibu na kumfanya Catherine kutoka nje kuungana na wafiwa wengine katika kumsindikiza mpendwa wao Agnes Jahokwa ambaye alikuwa maarufu kwa jina la mama Jennifer. Akiwa pale nje pamoja na majonzi ya kuigiza aliyokuwa nayo aliweza kumuangalia kila aliyemtilia shaka mahali pale.

Na baada ya kuweka shada la maua aliungana na mume wake Mchungaji Rodney ambaye wana siku kadhaa hawajaonana.
"Pole na msiba baba Mchungaji.." Alimpa pole Mchungaji aliyekuwa akifuta jasho baada ya kuendesha ibada ya mazishi.

"Amina mke wangu huu ni wetu sote kikubwa tuendelee kumuombea kwa Mungu tu."
"Ni kweli kabisa mume wangu dada wa watu hakuwa na makuu na mtu yoyote ila ndiyo hivyo tuseme nini sisi." Catherine alimjibu mume wake akiwa kamshika mkono. Taratibu zote zilipokamilika watu wote walirejea sehemu zao kusubiri taratibu nyingine kutoka kwa wanafamilia kwani alizikwa ndani viunga vya nyumba yao hapo hapo.

" Bwana Yesu asifiwe mama Mchungaji." Mzee Lukosa alimsalimu mama Mchungaji aliyekuwa kiti cha pembeni ya Mchungaji.
"Amina mzee wangu, pole na msiba."

"Mwanangu ya Dunia haya kikubwa ni kumuombea tu ndugu yetu ili apate pumziko la milele." Mzee Lukosa alimjibu.
"Amina baba." Catherine alimjibu.

Wakati mazungumzo kati ya mzee Lusoka na mama Mchungaji Bi Catherine yakiendelea Mchungaji aliombwa kutoa neno la kuwatia moyo wafiwa, alifanya hivyo na kisha alimfuata Otago Matthew na kumkumbatia kisha binti Jennifer ambaye kiuhalisia ni mtoto wake.
"Binti yangu kuwa imara katika kipindi hiki cha maombolezo." Wakati akitoa maneno haya alitokwa na machozi kitu kilichomshangaza mke wake akamfuata na kumshika bega.

"Mume wangu ndiyo nini sasa jaribu kujikaza basi." Alimnong'oneza sikioni na kumuondoa mahali hapo na kumpeleka mpaka kwenye gari kisha akarudi ndani kuwaaga wafiwa wakiwemo Otago Mathew pamoja na binti yake Jennifer kisha akarejea kwenye gari na wakaondoka kurejea nyumbani.

" Naomba unisamehe kwa kilichotokea pale nilijikuta nikishindwa kuzuia hisia zangu baada ya kumuona binti Jennifer katika umri ule akienda kuishi bila wazazi." Mchungaji alimwambia mke wake.

"Nilijua hilo mume wangu na ndiyo maana nikaona nikuondoe pale si unajua tena nilihofia usije anza kulia kwa sauti si ninakufahamu." Alimjibu mke wake.

"Nashukuru kwa kunielewa mke wangu. Ngoja nimwambie Oketh alete gari nyumbani."
"Sawa baba." Catherine alimjibu macho yakiwa mbele kuhakikisha usalama unakuwepo barabarani.

"Oketh naomba uniletee gari nyumbani tafadhali." Mchungaji alimwambia kijana wake huyu ambaye humtumia kwenye shughuli zake mbalimbali.

"Sawa Mchungaji naleta sasa hivi, funguo?" Oketh alimuuliza.
"Oohh my God!! Samahani Oketh utaifuata akili sijui ilikuwa ikiwaza nini?" Alimjibu.

"Basi nakuja sasa hivi kuichukua." Alijibiwa kisha alikata simu macho yakiwa kwa mke wake ambaye akili yake ilikuwa kwenye usukani. Waliwasili nyumbani huku nyumba ikiwa kimya kama vile hakuna mtu wakati mlinzi muda wote yupo na hii ilikuja mara baada ya Mchungaji kuingia ndani kupitia mlango wa dharura na kuikuta nyumba iko kimya sana hakujali alichofanya akaliendea lango na kulifungua kisha Catherine akaingiza gari.

"Adoyee kaenda wapi mpaka asisikie honi zote hizi?" Catherine alimuuliza Mchungaji.

"Kwa akili yake anaweza kuwa kalala humo bandani mwake." Mchungaji alimjibu akivua koti lake na kumkabidhi mke wake Catherine ambaye hakutaka kuishia hapo akaona aende kumuangalia kwenye banda lake kama yumo ndani.

"Hee makubwa! Adoyee unafanya nini? Yaani una...." Kabla hajamalizia neno lake alisukumwa na kuanguka chini na kupoteza fahamu mara baada ya kuangukia mguu wa meza.

"Umefanya nini sasa?" Adoyee alimuuliza mpenzi wake aliyekuwa akitokomea nje na kumuachia tatizo mwenzake. Alijaribu kumfukuzia lakini alijikuta akiishia getini baada ya kumkosa na kurejea haraka mle ndani kumuokoa mke wa bosi wake.

"Kuna nini Adoyee mbona unakwenda huku mara kule kulikoni?" Mchungaji alimuuliza baada ya kuona hatulii mara huku mara kule.
"Mchungaji ma...ma maana...ma yaani nas....nasema mama humo ndani (akionesha kidole) kaanguka."

"Unasemaje Adoyee?" Mchungaji alimuuliza swali akishuka ngazi kuliendea banda.

"Ni kweli bosi kaanguka." Adoyee alimjibu lakini Mchungaji alimpita na kuingia ndani na kumkuta mke wake akiwa kapoteza fahamu lakini akiwa hana jeraha lolote mwilini mwake haraka Mchungaji alimuinua na kumbeba.

"Unashangaa nini uvute mlango vizuri nipite."Alimwambia Adoyee aliyekuwa kaduwaa asijue afanye lipi muda huo.

Aliingia naye ndani na kuanza kumpa huduma ya kwanza katika sehemu mbalimbali za mwili wake na baada ya kumaliza alimlaza kwenye zulia pale sebuleni kisha yeye akaingia chumba cha maombi na kuanza kumuombea mke wake akiamini mke wake kaingiwa na pepo. Akiwa ndani ya chumba cha maombi huku sebuleni mke wake alizinduka na kuketi huku mkono wake wa kulia akiupitisha sehemu ya sikio ambayo ndiyo iliangukia kwenye mguu wa meza akihisi alipata mchubuko lakini hakuweza kuona hata tone la damu kwenye vidole vyake, hakutaka kusubiri alisimama na kuingia chumbani ambako alipitiliza kwenye kioo ili kuhakikisha kama hana mchubuko wowote.

"Adoyee unacheza na akili yangu, yaani malaya wako anisukume mimi? Ananijua mimi vizuri?" Alitabasamu mbele ya kioo lakini tabasamu lake halikuwa halisi lilikuwa lenye hasira na bila shaka lilimhusu Adoyee na mpenzi wake aliyekimbia.

"Mungu mkubwa! Umezinduka mke wangu?" Mchungaji alitokwa na maneno hayo baada ya kumkuta mke wake katulia mbele ya kioo.
"Amina mume wangu niko sawa." Alimjibu akigeuka na kumkumbatia mume wake.
"Nini kilitokea?" Alimuuliza.

"Wakati nimeingia kumuangalia Adoyee mle bandani kabla sijafanya chochote nilipatwa na kizunguzungu kilichonipeleka chini na kupoteza fahamu." Catherine alimdanganya mume wake na kuuficha ukweli.

"Pepo wabaya wapite mbali na makazi yetu." Mchungaji alimwambia mke wake akiwa anamuongoza kitandani.
"Samahani mume wangu naomba maji ya kunywa." Baada kuketi kitandani alimuomba maji ya kunywa mume wake.

"Dakika sifuri." Mchungaji alimjibu na kutoka mbio kuelekea sebuleni kuchukua maji. Akiwa kabaki peke mle ndani alichukua simu yake na kuanza kupitia namba fulani.

"Mke wangu maji haya hapa." Mchungaji alifika na kumkabidhi maji.

"Asante baba." Alishukuru huku akiiweka kando simu yake pembeni.

"Ukimaliza kunywa unatakiwa kupumzika mke wangu." Mchungaji alimshauri mke wake ambaye hakupingana naye alimkubalia.
"Hali ni tete bosi." Ujumbe mfupi uliingia kwenye simu ya Catherine wakati huo alikuwa sebuleni kuweka glasi na aliporejea alikutana na ujumbe huo ambao ulimchanganya sana kabla hajaujibu alitoka nje kumuangalia mume wake alipo na kama bahati walikutana mlangoni.

" Samahani mke wangu wacha nitoke mara moja naona Oketh anachelewa wacha niifuate mwenyewe." Mchungaji alimwambia mke wake ambaye kwake ilikuwa ni taarifa njema japo alionesha kama kuchukizwa na taarifa hiyo ya mume wake.

"Mume wangu si umpigie ujue yupo wapi kuliko kuondoka wakati unajua ni muda hatujakuwa pamoja."

"Usijali mke wangu nakuja narejea muda si mrefu hata mimi nina hamu ya kukaa na wewe mke wangu." Mchungaji alimjibu mke wake akiwa kamkumbatia huku mke wake akimng'ong'a kisogo.

"Basi nenda kipenzi lakini usichukue muda mrefu nakusubiri." Alimjibu mume wake akimbusu shavuni.
"Niamini mke wangu." Mchungaji alimjibu akitoka. Hapo hapo Catherine aliifuata simu yake na moja kwa moja akampigia Jumbe ili kujua kuna kitu gani kimetokea.

"Enhh hebu nijuze kulikoni Jumbe?" Aliuliza baada ya Jumbe kuipokea simu yake.

"Muda huu tuko porini tunamkimbiza kijana mmoja sijui katokea wapi alikuwa akipiga picha kambi yetu." Jumbe alimjibu.
"Unasemaje Jumbe? Imekuwaje mpaka mtu anaifikia kambi yetu na kuanza kufanya yake? Haujua mpaka sasa muuaji anatafutwa na jeshi la polisi? Hakikisheni huyo pimbi anapatikana akiwa mzima au mfu umenielewa?" Catherine alivurugwa na taarifa ya Jumbe akajikuta jasho linamtiririka mwili mzima akiwa anajifuta lile la usoni akatoka nje mpaka alipokuwa mlinzi wao ambaye dakika kadhaa zilizopita alimsababishia majanga. Adoyee alipomuona tu akajua kumekucha haraka akainuka kwenye kiti na kusimama kama askari wa jeshi la Adroph Hitler.

"Karibu bosi..." Alimkaribisha.
"Nifuate." Hakuongea kitu kingine zaidi ya kumtaka amfuate ndani. Adoyee hakuwa na pingamizi zaidi ya kutii oda ya bosi wake, walipofika ndani Catherine bila aibu alimvutia chumba cha kulala wageni na kuufunga mlango na funguo kuiweka mfukoni kisha akamgeukia.

"Nakuona kidume cha mbegu kinacholima kila shamba lillilo mbele yake." Aliongea akivua kikoti chake cheusi na kukitupa chini.
Hali ile ilianza kumtisha Adoyee kwani hakuwa kukutana nayo hata siku moja kwa bosi hivyo alianza kurudi nyuma.

"Naomba unisamehe bosi yule mwanamke alinilazimisha lakini mimi nilimkatalia haki ya Mungu tena." Aliongea akipitisha alama ya kidole shingoni kwake.

"Kumbe ulilazimishwa eee basi nataka ufanye kama ulivyomfanyia huyo malaya wako sawa?"

"Bosi naanzaje kufanya hivyo kwako naomba unipe adhabu nyingine lakini siyo hiyo..." Aliendelea kujitetea mbele ya mwanamke aliyekuwa hacheki wala kutabasamu.

"Hautaki si ndiyo..." Catherine alimuuliza Adoyee huku kibao kikitua kwenye paji la uso lililompeleka chini na hapo hapo alimfuata juu akiwa hanavaa vazi lolote zaidi ya ile traki tu huku kisu kikiwa mkononi na kumuwekea shingoni.

"Nisikilize wewe mtoto wa pori, mimi huwa siguswi mwili wangu na wanaharamu lakini wewe na huyo mshenzi wako mmeamua kufanya hivyo, sasa basi ninachokufanyia muda huu hutokuja kusahau maishani mwako."

"Bo...bo...bosi nimekosa naomba unisamehe lililotokea halitajirudia tena nakuapia bosi wangu." Alijitetea.
"Huna la kunishawishi Adoyee kifo ndiyo salama yako.."

"Bosi naomba usiniue nyumbani wananitegemea nikifa wataishi maisha magumu sana naomba unipe adhabu nyingine..." Adoyee alijitetea huku tayari shingo yake ikiwa imeanza kutiririsha damu.

"Nimekuelewa (akikitoa kisu shingoni) nakuachia kwa sharti moja tu unanisikia?" Catherine alimuuliza akimvuta shati sehemu ya shingo.

"Nimekusikia bosi wangu." Alimjibu akiwa kamtolea macho.

"Vizuri simama." Alimtaka asimame huku yeye akichungulia nje kupitia dirishani.
"Nisikilize Adoyee nimekusamehe lakini ninakutaka kufanya kazi ambayo nitakueleza muda si mrefu."
"Niko tayari mama."

Adoyee alimjibu huku akiiangalia suruali yake ambayo ilikuwa imelowana kwa mkojo.

"Haya nenda lindoni haraka kabla sijapiga kelele za kubakwa sasa hivi." Adoyee alitoka mbio baada ya kusikia atapigiwa kelele za kubaka, na muda huo huo simu ya Catherine iliita akaifuata na kuipokea.

"Nahitaji kusikia taarifa zenye tabasamu Jumbe."
"Bosi tayari tumemshamdaka tunaye mikononi mwetu."

"Vizuri muwekeni chumba cha mateso mpaka nitakapokuja kumshughulikia." Catherine alimjibu.
" Sawa bosi." Jumbe alimjibu. Na Catherine hakuwa na maelezo mengine ya ziada zaidi ya kuikata simu. Alijikagua na kugundua alikuwa kifua wazi hivyo aliinuka na kuingia chumbani kwake kwa ajili ya kuoga na kubadili mavazi mengine.

JE, NINI KITATOKEA?

UNGANA NA MTUNZI NA MWANDISHI WA HADITHI HII UPATE KUJUA SONGOMBINGO LA MCHUNGAJI RODNEY NA MKEWE BI CATHERINE.
 
Sultan Uwezo
+255

***

Mchungaji alichukua gari na kuelekea mji uitwao Thies ambako anaishi mtaalamu wake ambaye alimkabidhi dawa aliyoipoteza na baada ya kuwasili alimkuta mtoto wa mganga huyo akifua nguo.

"Karibu Mjomba." Binti huyo alimkaribisha Mchungaji.

"Asante Seynabou, baba yuko wapi?" Alimjibu akifungua buti.

"Baba yuko kilinge cha porini kuna watu anawashughulikia." Seynabou alimjibu akimsogelea kupokea mizigo ambayo Mchungaji aliitoa kwenye buti. Mchungaji aliangaza macho yake eneo lile na kuona gari ndogo aina ya Citroën ya blue ikiwa imepaki karibu na banda la mbuzi.

" Huyo anayemshughulikia ndiyo mwenye hilo gari?" Aliuliza.
"Ndiyo Mjomba, nikamwite?" Seynabou alimuuliza.

"Hapana Seynabou wewe ingiza hiyo mizigo ndani wacha mimi nimfuate huko huko aliko."

"Sawa." Seynabou alimjibu akianza kubeba mizigo. Mchungaji alimuacha Seynabou na kuelekea aliko mzee Alioune. Lakini kichwa chake kilikuwa na mashaka kutokana na masharti ambayo alimpa ya kuhakikisha hiyo dawa haiguswi na mtu yeyote yule zaidi yake yeye na sasa alikuwa hajui kama imeshikwa na mtu au imepotea tu hapo alibaki njiapanda, alifika kwenye kilinge cha mzee Alioune lakini ajabu hakuweza kumkuta na hata baada ya kuchungulia mle ndani hakuona mtu.

"Ndiyo nini sasa mbona hakuna mtu?" Mchungaji Rodney alijiuliza.

"Baba Mchungaji karibu ndani, nilimtoa mteja wangu mara moja." Sauti ya mzee Alioune ilitokea nyuma yake na kumfanya Mchungaji ashtuke.

"Mazingira yalianza kunitisha mzee wangu maana nimehakikishiwa na mjomba wangu Seynabou kuwa uko huku sasa nafika nakutana na kilinge kikinitazama tu, na ghafla unatokea nyuma yangu." Mchungaji alimjibu akigeuka.

"Usiniambie hiki ninachokiona usoni kwako Rodney?" Mzee Alioune alimwambia Mchungaji akiwa anaingia ndani.

"Yaani sijui nianzie wapi mzee wangu lakini ukweli ndiyo huo kwani kile kichupa nilisahau kukitoa kwenye mkoba uliokuwa na hela zilizopotea naomba msaada wako tafadhali." Mchungaji alimjibu mzee Alioune akipiga magoti.

"Pole sana kijana wangu kwani nikiangalia hapa nakiona kimeshikwa na mtu mmoja hatari sana na huyu ndiyo alifanikisha uporaji wa hela za kanisa.."
"Unamuona? Ni nani? Vipi hajazitumia hela za watu? Vipi kuhusu dawa?" Mchungaji aliuliza maswali mengi kiasi cha kumfanya mzee Alioune abaki kumkodolea macho tu.

"Nisikilize kijana wangu, huyu mtu hajatumia hata mia na nikimuangalia hapa anapanga mipango mibaya juu yako." Mzee Alioune alimueleza.

"Nifanye kitu gani ili nimthibiti mtu huyu?" Mchungaji alimuuliza.

"Huna la kufanya kwa sasa kwani mtu huyu ni miongoni mwa wahanga wa matukio yako ya kuwaua wale waumini uliokuwa ukiwatumia kwenye miujiza yako na nikiangalia hapa hayuko mbali na malango yako." Mzee Alioune aliendelea kumtisha Mchungaji.
"Ni mhanga wa mauaji yangu? Kivipi?" Alimuuliza.

"Ndiyo ulimuua mama yake na amekuja kulipiza kisasi na ndiye anayehusika na mauaji ya watu wanne wa hivi karibuni..." Kabla hajaendelea Mchungaji alimkatisha.

"Ndiyo mhusika? Na hao watu nahusika nao vipi mimi na vifo vyao?" Mchungaji alizidi kuuliza huku kitambaa kikiwa hakikauki usoni.
"Ilikuwa hivi baada ya kumteka kijana wako uliyempa hela alikwenda kumficha mafichoni huko inaonekana walipishana kauli ndiyo akamuua mmoja wa vijana wake kisha kijana wenu Bartholomew msiba wa askari ulitoa wakati akirudi mafichoni kutoka kumuua mzazi mwenzako.. "

" Nani mama Jennifer?" Mchungaji alijikuta akiuliza swali hili baada ya kuambiwa kitu alichokuwa hakijui kabisa.

" Huyo huyo, na hivi tunavyoongea tayari anamshikilia askari mmoja ambaye aliyabaini makazi yao huko porini nafikiri muda wowote wanamuua."Mzee Alioune aliendelea kutiririka kama vile yeye ndiye mhusika wa matukio yote yaliyotokea.

" Mzee wangu naomba unisaidie kumbaini mtu huyu ni nani maana kama haya yote umeyabaini itakuwa siyo kazi kumtambua muuaji wetu."

" Kijana wangu siyo rahisi kama unavyosema huyu mtu ni hatari kwani haonekani vizuri hapa ninachokiona ni kivuli tu lakini nipe muda niendelee kumfuatilia japo najua itakuwa ngumu kwa sababu kile kichupa kiko mikononi mwake yeye kikimsaidia pasipo yeye kujua kama kina msaada kwenye shughuli zake."

" Kwa hiyo unataka kusema kuwa huwezi kunipa dawa nyingine? Si unajua tena wiki ijayo nina mkutano mkubwa wa Injili ambao nitatakiwa kufanya miujiza mikubwa ambayo itanifanya kuandikwa kwenye magazeti yote makubwa pamoja na vyombo vikubwa vya habari ndani na nje ya nchi yetu na hapa ndipo ndoto yangu ya kuwa Mchungaji Tajiri itatimia." Mchungaji alifunguka zaidi kwa mzee Alioune.

" Kijana wangu hakuna dawa yenye uwezo mkubwa tena kama ambayo nilikupa na kila kitu kitaharibika kwa sababu masharti yamevunjwa hivyo lolote baya linaweza kukupata Mchungaji." Mzee Alioune alimwambia ukweli Mchungaji ambao yeye hakutaka kuusikiliza.

"Acha uswahili mzee nadhani akili yangu siyo ngeni hata kidogo, sasa dawa nyingine unanipa au hunipi?" Mchungaji alishavurugwa alimuuliza mzee Alioune akiwa kamuwekea bastola kichwani.

"Mchungaji Rodney wewe si mtu wa kuongea kwa bastola hebu itoe kichwani kwangu itaniua ujue? Kama ni dawa nakupa usijali." Mzee Alioune aliongea akianza kushikashika vibuyu vyake pamoja na vichupa vya dawa.

"Fanya haraka mzee kabla sijausambaratisha ubongo wako." Mchungaji aliongea. Mzee Alioune alichanganya dawa zake na kuziweka ndani ya kichupa kimoja cha kijani na kumkabidhi.

"Asante mzee nakupa siku mbili tu uwe umemjua huyo mtu kabla hajatekeleza alichopanga."

"Sawa kijana wangu." Mzee Alioune alimjibu akiwa kaitolea macho ile bastola ambayo Mchungaji aliitoa kichwani kwake na kuiweka sehemu yake na kuondoka. Taarifa ya mauaji ya Bartholomew yalianza kuzunguka kichwani kwake kwani ilikuwa tofauti na vile ambavyo alikuwa akiamini yeye na waumini wengine kuwa Bartholomew aliingiwa na tamaa akatoroka nazo.

"Okay tufanye ni kweli Bartholomew kauawa nitaanza vipi kuwaelezea waumini mpaka waniamini? Mungu wangu au nikae kimya tu." Alijisemesha mwenyewe akiwa anaingia kwenye gari.

"Na huyu mtu ambaye nilimuua mama yake ni nani? Mbona kwenye lile kundi wanawake walikuwa ni wawili tu ambao ni Oliver na Sara, sasa kati ya hawa ni yupi?" Aliendelea kukuna kichwa pale nyuma ya usukani bila kujali kuna nani alikuwa akimuangalia.

"Mjomba mbona unaongea peke yako au hujamkuta baba?" Seynabou alimuuliza baada ya kumsogelea lakini cha ajabu hakumjibu aliwasha gari na kuondoka na kumuacha Seynabou kakodoa macho asijue kapatwa na nini mjomba wake. Njia nzima aliyafikiria maneno aliyoambiwa na mganga wake mzee Alioune na zaidi ilikuwa ni kwa huyu mtu ambaye anafanya mauaji kila kona.

"Natakiwa nimpate huyu mtu kabla hajafanya chochote kingine kibaya, lakini tatizo muuaji ni nani?" Ni swali ambalo Mchungaji Rodney alizidi kujiuliza. Na wakati yeye akiwa anachanja mbuga kurejea nyumbani mke wake Bi Catherine alikuwa katulia kitandani macho yakiwa kwenye laptop akimfuatilia pasipo yeye kulielewa hilo na hata baada ya kuwasili nyumbani alimkuta mke wake akiwa anaandaa chakula mezani.

"Mume wangu vipi ulipata dharura? Maana ulisema utalifuata gari na kurejea lakini yamepita masaa kadhaa." Catherine alimuuliza Mchungaji.

"Ni kweli mke wangu niliona kabla sijarudi nyumbani wacha nikawatembelee wafiwa pamoja na mke wa Bartholomew si unajua mapito anayoyapitia kwa sasa toka mume wake apotee?" Mchungaji aliamua kumdanganya mke wake.

"Namuonea huruma sana binti wa watu, bado mdogo lakini tayari kakutana mtihani mkubwa usioendana na umri wake. Lakini kuna muda nahisi wale wanawasiliana vizuri tu na unaweza kukuta mke wake kabaki hapa kwa sababu maalum ya kuangalia kanisa linafanya nini kwenye hili la upotevu wa fedha."

" Mke wangu naomba tusifikirie kwa sura hiyo na kama ndivyo ilivyo tutajua tu si unajua Mungu huwa hamfichi mnafiki?"
" Ndiyo lakini nilichokisema ni kile ambacho kinaisokota nafsi yangu." Catherine alimjibu huku akimpa ishara mume wake ya kuketi mezani kwa chakula.

" Bwana Yesu asifiwe Baba Mchungaji, tumepata taarifa zinazomhusu kijana wetu Bartholomew." Ujumbe uliingia kwenye simu ya Mchungaji, baada ya kuusoma aliamua kumpigia mtuma ujumbe.

"Unasema kuwa kuna taarifa za Bartholomew? Na wewe ni nani?" Mchungaji alimuuliza.

"Mimi ni nani si muhimu kwa sasa unachotakiwa kukijua ni kuwa kijana na muumini wako aitwaye Bartholomew ni miongoni mwa waliouawa hivi karibuni. Ukiwa kama mlezi wake kiroho nimeona nikujuze." Simu ilikatwa na kitendo hicho kilimfanya Mchungaji aitafute hiyo namba inamilikiwa na nani aliishiwa nguvu baada ya kuiona ni 'private' hapo alishusha pumzi ndefu macho yakiwa kwa mke wake.

" Kuna usalama mume wangu?" Catherine alimuuliza.
" Yaani ni majanga tu."Alimjibu akinawa kuahirisha kula chakula.

" Majanga?"
" Bartholomew ni miongoni mwa waliouawa mke wangu nq ninachojiuliza muuaji ni nani? Na kwanini mpiga simu hajataka nimtambue?"

" Hajataka umtambue? Angekupigia simu? Si kagua usajili wake." Catherine alimjibu mume wake ambaye alishavurugwa.
"Catherine mke wangu nitaangaliaje wakati kaificha?" Alimjibu akiinuka.

"Kuna kitu hapo mume unatakiwa kuwa makini."

"Nahisi huyu ndiye muuaji na ndiye anayefuatilia nyayo zangu." Alilopoka Mchungaji akichukua koti lake na kuufuata mlango.
Catherine alimtazama mume wake ambaye tayari alishachanganyikiwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa mtu asiyemjua.

"Vipi kazi yangu tayari?" Catherine alimuuliza Jumbe huku macho yakiwa bado dirishani kuhakikisha hakuna mtu anayemfuatilia.
"Ndiyo bosi nimeshamtumia ujumbe Mchungaji kwa kutumia simu ya mkulima mmoja hapa lakini nikiifanyia utundu fulani hivi." Jumbe alimjibu.

"Vizuri naona sindano imemuingia maana kaondoka anaongea peke yake, ila cha kufanya Jumbe naomba mzamishie kisu kifuani huyo panya na mtupeni mtoni kisha anzeni safari usiku kuelekea nilikowaambia hapo si mahali salama tena Jumbe. Mimi nataka nimfuate mganga wa Mchungaji."

"Unataka umrudishie dawa?" Jumbe alimuuliza Catherine.

"Hapana hii siwezi kuirudisha bali nataka nikamuingize kwenye orodha yangu." Catherine alimjibu Jumbe na hakutaka kusubiri chochote alikata simu na kutoka mle ndani.

"Adoyee unaikumbuka ahadi yetu?" Catherine alimuuliza mlinzi wao.
"Naikumbuka bosi wangu." Adoyee alimjibu Catherine.

"Okay, mimi natoka kazi yako ni kuitunza siri yangu tu ambayo sikwambii ila utaijua mwenyewe na nikigundua umenigeuka nitakufanya kitu mbaya sana, umenielewa Adoyee?"

"Niamini Bosi katika hili siwezi kukugeuka." Alijibu.
"Vizuri tunaanza leo."

"Sawa Bosi." Adoyee alimjibu Catherine ambaye aliitika kwa kichwa na kurudi ndani ambako hakuchukua muda mrefu alitoka na kuingia kwenye gari lake na kutoka.

JE, NINI KITAENDELEA TENA?

USICHOKE KUUNGANA NA KIRANJA WAKO MTUNZI NA MWANDISHI WA HADITHI HII TUWEZE KUYAJUA YAJAYO.
 
Sultan Uwezo
+255

***

Mchungaji alichukua gari na kuelekea mji uitwao Thies ambako anaishi mtaalamu wake ambaye alimkabidhi dawa aliyoipoteza na baada ya kuwasili alimkuta mtoto wa mganga huyo akifua nguo.

"Karibu Mjomba." Binti huyo alimkaribisha Mchungaji.

"Asante Seynabou, baba yuko wapi?" Alimjibu akifungua buti.

"Baba yuko kilinge cha porini kuna watu anawashughulikia." Seynabou alimjibu akimsogelea kupokea mizigo ambayo Mchungaji aliitoa kwenye buti. Mchungaji aliangaza macho yake eneo lile na kuona gari ndogo aina ya Citroën ya blue ikiwa imepaki karibu na banda la mbuzi.

" Huyo anayemshughulikia ndiyo mwenye hilo gari?" Aliuliza.
"Ndiyo Mjomba, nikamwite?" Seynabou alimuuliza.
"Hapana Seynabou wewe ingiza hiyo mizigo ndani wacha mimi nimfuate huko huko aliko."

"Sawa." Seynabou alimjibu akianza kubeba mizigo. Mchungaji alimuacha Seynabou na kuelekea aliko mzee Alioune. Lakini kichwa chake kilikuwa na mashaka kutokana na masharti ambayo alimpa ya kuhakikisha hiyo dawa haiguswi na mtu yeyote yule zaidi yake yeye na sasa alikuwa hajui kama imeshikwa na mtu au imepotea tu hapo alibaki njiapanda, alifika kwenye kilinge cha mzee Alioune lakini ajabu hakuweza kumkuta na hata baada ya kuchungulia mle ndani hakuona mtu.

"Ndiyo nini sasa mbona hakuna mtu?" Mchungaji Rodney alijiuliza.
"Baba Mchungaji karibu ndani, nilimtoa mteja wangu mara moja." Sauti ya mzee Alioune ilitokea nyuma yake na kumfanya Mchungaji ashtuke.

"Mazingira yalianza kunitisha mzee wangu maana nimehakikishiwa na mjomba wangu Seynabou kuwa uko huku sasa nafika nakutana na kilinge kikinitazama tu, na ghafla unatokea nyuma yangu." Mchungaji alimjibu akigeuka.

"Usiniambie hiki ninachokiona usoni kwako Rodney?" Mzee Alioune alimwambia Mchungaji akiwa anaingia ndani.

"Yaani sijui nianzie wapi mzee wangu lakini ukweli ndiyo huo kwani kile kichupa nilisahau kukitoa kwenye mkoba uliokuwa na hela zilizopotea naomba msaada wako tafadhali." Mchungaji alimjibu mzee Alioune akipiga magoti.

"Pole sana kijana wangu kwani nikiangalia hapa nakiona kimeshikwa na mtu mmoja hatari sana na huyu ndiyo alifanikisha uporaji wa hela za kanisa.."

"Unamuona? Ni nani? Vipi hajazitumia hela za watu? Vipi kuhusu dawa?" Mchungaji aliuliza maswali mengi kiasi cha kumfanya mzee Alioune abaki kumkodolea macho tu.

"Nisikilize kijana wangu, huyu mtu hajatumia hata mia na nikimuangalia hapa anapanga mipango mibaya juu yako." Mzee Alioune alimueleza.

"Nifanye kitu gani ili nimthibiti mtu huyu?" Mchungaji alimuuliza.

"Huna la kufanya kwa sasa kwani mtu huyu ni miongoni mwa wahanga wa matukio yako ya kuwaua wale waumini uliokuwa ukiwatumia kwenye miujiza yako na nikiangalia hapa hayuko mbali na malango yako." Mzee Alioune aliendelea kumtisha Mchungaji.

"Ni mhanga wa mauaji yangu? Kivipi?" Alimuuliza.

"Ndiyo ulimuua mama yake na amekuja kulipiza kisasi na ndiye anayehusika na mauaji ya watu wanne wa hivi karibuni..." Kabla hajaendelea Mchungaji alimkatisha.

"Ndiyo mhusika? Na hao watu nahusika nao vipi mimi na vifo vyao?" Mchungaji alizidi kuuliza huku kitambaa kikiwa hakikauki usoni.
"Ilikuwa hivi baada ya kumteka kijana wako uliyempa hela alikwenda kumficha mafichoni huko inaonekana walipishana kauli ndiyo akamuua mmoja wa vijana wake kisha kijana wenu Bartholomew msiba wa askari ulitoa wakati akirudi mafichoni kutoka kumuua mzazi mwenzako.. "

" Nani mama Jennifer?" Mchungaji alijikuta akiuliza swali hili baada ya kuambiwa kitu alichokuwa hakijui kabisa.

" Huyo huyo, na hivi tunavyoongea tayari anamshikilia askari mmoja ambaye aliyabaini makazi yao huko porini nafikiri muda wowote wanamuua."Mzee Alioune aliendelea kutiririka kama vile yeye ndiye mhusika wa matukio yote yaliyotokea.

" Mzee wangu naomba unisaidie kumbaini mtu huyu ni nani maana kama haya yote umeyabaini itakuwa siyo kazi kumtambua muuaji wetu."

" Kijana wangu siyo rahisi kama unavyosema huyu mtu ni hatari kwani haonekani vizuri hapa ninachokiona ni kivuli tu lakini nipe muda niendelee kumfuatilia japo najua itakuwa ngumu kwa sababu kile kichupa kiko mikononi mwake yeye kikimsaidia pasipo yeye kujua kama kina msaada kwenye shughuli zake."

" Kwa hiyo unataka kusema kuwa huwezi kunipa dawa nyingine? Si unajua tena wiki ijayo nina mkutano mkubwa wa Injili ambao nitatakiwa kufanya miujiza mikubwa ambayo itanifanya kuandikwa kwenye magazeti yote makubwa pamoja na vyombo vikubwa vya habari ndani na nje ya nchi yetu na hapa ndipo ndoto yangu ya kuwa Mchungaji Tajiri itatimia." Mchungaji alifunguka zaidi kwa mzee Alioune.

" Kijana wangu hakuna dawa yenye uwezo mkubwa tena kama ambayo nilikupa na kila kitu kitaharibika kwa sababu masharti yamevunjwa hivyo lolote baya linaweza kukupata Mchungaji." Mzee Alioune alimwambia ukweli Mchungaji ambao yeye hakutaka kuusikiliza.

"Acha uswahili mzee nadhani akili yangu siyo ngeni hata kidogo, sasa dawa nyingine unanipa au hunipi?" Mchungaji alishavurugwa alimuuliza mzee Alioune akiwa kamuwekea bastola kichwani.

"Mchungaji Rodney wewe si mtu wa kuongea kwa bastola hebu itoe kichwani kwangu itaniua ujue? Kama ni dawa nakupa usijali." Mzee Alioune aliongea akianza kushikashika vibuyu vyake pamoja na vichupa vya dawa.

"Fanya haraka mzee kabla sijausambaratisha ubongo wako." Mchungaji aliongea. Mzee Alioune alichanganya dawa zake na kuziweka ndani ya kichupa kimoja cha kijani na kumkabidhi.

"Asante mzee nakupa siku mbili tu uwe umemjua huyo mtu kabla hajatekeleza alichopanga."

"Sawa kijana wangu." Mzee Alioune alimjibu akiwa kaitolea macho ile bastola ambayo Mchungaji aliitoa kichwani kwake na kuiweka sehemu yake na kuondoka. Taarifa ya mauaji ya Bartholomew yalianza kuzunguka kichwani kwake kwani ilikuwa tofauti na vile ambavyo alikuwa akiamini yeye na waumini wengine kuwa Bartholomew aliingiwa na tamaa akatoroka nazo.

"Okay tufanye ni kweli Bartholomew kauawa nitaanza vipi kuwaelezea waumini mpaka waniamini? Mungu wangu au nikae kimya tu." Alijisemesha mwenyewe akiwa anaingia kwenye gari.

"Na huyu mtu ambaye nilimuua mama yake ni nani? Mbona kwenye lile kundi wanawake walikuwa ni wawili tu ambao ni Oliver na Sara, sasa kati ya hawa ni yupi?" Aliendelea kukuna kichwa pale nyuma ya usukani bila kujali kuna nani alikuwa akimuangalia.

"Mjomba mbona unaongea peke yako au hujamkuta baba?" Seynabou alimuuliza baada ya kumsogelea lakini cha ajabu hakumjibu aliwasha gari na kuondoka na kumuacha Seynabou kakodoa macho asijue kapatwa na nini mjomba wake. Njia nzima aliyafikiria maneno aliyoambiwa na mganga wake mzee Alioune na zaidi ilikuwa ni kwa huyu mtu ambaye anafanya mauaji kila kona.

"Natakiwa nimpate huyu mtu kabla hajafanya chochote kingine kibaya, lakini tatizo muuaji ni nani?" Ni swali ambalo Mchungaji Rodney alizidi kujiuliza. Na wakati yeye akiwa anachanja mbuga kurejea nyumbani mke wake Bi Catherine alikuwa katulia kitandani macho yakiwa kwenye laptop akimfuatilia pasipo yeye kulielewa hilo na hata baada ya kuwasili nyumbani alimkuta mke wake akiwa anaandaa chakula mezani.

"Mume wangu vipi ulipata dharura? Maana ulisema utalifuata gari na kurejea lakini yamepita masaa kadhaa." Catherine alimuuliza Mchungaji.

"Ni kweli mke wangu niliona kabla sijarudi nyumbani wacha nikawatembelee wafiwa pamoja na mke wa Bartholomew si unajua mapito anayoyapitia kwa sasa toka mume wake apotee?" Mchungaji aliamua kumdanganya mke wake.

"Namuonea huruma sana binti wa watu, bado mdogo lakini tayari kakutana mtihani mkubwa usioendana na umri wake. Lakini kuna muda nahisi wale wanawasiliana vizuri tu na unaweza kukuta mke wake kabaki hapa kwa sababu maalum ya kuangalia kanisa linafanya nini kwenye hili la upotevu wa fedha."

" Mke wangu naomba tusifikirie kwa sura hiyo na kama ndivyo ilivyo tutajua tu si unajua Mungu huwa hamfichi mnafiki?"

" Ndiyo lakini nilichokisema ni kile ambacho kinaisokota nafsi yangu." Catherine alimjibu huku akimpa ishara mume wake ya kuketi mezani kwa chakula.

" Bwana Yesu asifiwe Baba Mchungaji, tumepata taarifa zinazomhusu kijana wetu Bartholomew." Ujumbe uliingia kwenye simu ya Mchungaji, baada ya kuusoma aliamua kumpigia mtuma ujumbe.

"Unasema kuwa kuna taarifa za Bartholomew? Na wewe ni nani?" Mchungaji alimuuliza.

"Mimi ni nani si muhimu kwa sasa unachotakiwa kukijua ni kuwa kijana na muumini wako aitwaye Bartholomew ni miongoni mwa waliouawa hivi karibuni. Ukiwa kama mlezi wake kiroho nimeona nikujuze." Simu ilikatwa na kitendo hicho kilimfanya Mchungaji aitafute hiyo namba inamilikiwa na nani aliishiwa nguvu baada ya kuiona ni 'private' hapo alishusha pumzi ndefu macho yakiwa kwa mke wake.

" Kuna usalama mume wangu?" Catherine alimuuliza.
" Yaani ni majanga tu."Alimjibu akinawa kuahirisha kula chakula.
" Majanga?"
" Bartholomew ni miongoni mwa waliouawa mke wangu nq ninachojiuliza muuaji ni nani? Na kwanini mpiga simu hajataka nimtambue?"
" Hajataka umtambue? Angekupigia simu? Si kagua usajili wake." Catherine alimjibu mume wake ambaye alishavurugwa.

"Catherine mke wangu nitaangaliaje wakati kaificha?" Alimjibu akiinuka.
"Kuna kitu hapo mume unatakiwa kuwa makini."

"Nahisi huyu ndiye muuaji na ndiye anayefuatilia nyayo zangu." Alilopoka Mchungaji akichukua koti lake na kuufuata mlango.
Catherine alimtazama mume wake ambaye tayari alishachanganyikiwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa mtu asiyemjua.

"Vipi kazi yangu tayari?" Catherine alimuuliza Jumbe huku macho yakiwa bado dirishani kuhakikisha hakuna mtu anayemfuatilia.
"Ndiyo bosi nimeshamtumia ujumbe Mchungaji kwa kutumia simu ya mkulima mmoja hapa lakini nikiifanyia utundu fulani hivi." Jumbe alimjibu.

"Vizuri naona sindano imemuingia maana kaondoka anaongea peke yake, ila cha kufanya Jumbe naomba mzamishie kisu kifuani huyo panya na mtupeni mtoni kisha anzeni safari usiku kuelekea nilikowaambia hapo si mahali salama tena Jumbe. Mimi nataka nimfuate mganga wa Mchungaji."

"Unataka umrudishie dawa?" Jumbe alimuuliza Catherine.

"Hapana hii siwezi kuirudisha bali nataka nikamuingize kwenye orodha yangu." Catherine alimjibu Jumbe na hakutaka kusubiri chochote alikata simu na kutoka mle ndani.

"Adoyee unaikumbuka ahadi yetu?" Catherine alimuuliza mlinzi wao.
"Naikumbuka bosi wangu." Adoyee alimjibu Catherine.
"Okay, mimi natoka kazi yako ni kuitunza siri yangu tu ambayo sikwambii ila utaijua mwenyewe na nikigundua umenigeuka nitakufanya kitu mbaya sana, umenielewa Adoyee?"

"Niamini Bosi katika hili siwezi kukugeuka." Alijibu.
"Vizuri tunaanza leo."
"Sawa Bosi." Adoyee alimjibu Catherine ambaye aliitika kwa kichwa na kurudi ndani ambako hakuchukua muda mrefu alitoka na kuingia kwenye gari lake na kutoka.

JE, NINI KITAENDELEA TENA?

USICHOKE KUUNGANA NA KIRANJA WAKO MTUNZI NA MWANDISHI WA HADITHI HII TUWEZE KUYAJUA YAJAYO.

PicsArt_11-08-01.31.04.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

***

Kikao cha Viongozi wa Kanisa la JESUS OUR KING (JOK) linaloongozwa na Mchungaji Rodney kiliendelea kwenye chumba maalum kujadili upotevu wa fedha zilizotolewa na Wahisani Kanisani hapo ambazo mpaka sasa hesabu yake haijulikani vizuri huku wengine wakidai ni shilingi milioni mia moja na wengine wakidai ni chini ya hapo. Kikao hiki cha siri pia kilikuwa kikijadili utekwaji wa kijana wa fedha Bartholomew ambaye taarifa zinadai ni marehemu, mjadala ulikuwa ni nani aliye nyuma ya haya yote.
"Wajumbe wenzangu mimi nina mashaka na watu wawili hapa, katika hili kwanza naomba radhi kama nitakuwa kinyume kimaadili mtu wa kwanza ni Baba yangu Mchungaji Rodney na wa pili ni ofisi ya fedha chini ya mzee wetu Magugu, kwanini hofu yangu nimeielekeza kwa watu hawa ndugu zangu? Ni kwa sababu wao ndiyo waliopokea fedha hizo siku ile kutoka Umoja wa Watu wa Tanzania waishio hapa Senegal kiasi cha shilingi milioni mia Nne lakini mtakumbuka tuliambiwa ni shilingi milioni mia moja tu hamuoni kuna mchezo hapa tunachezewa? Na huyu kijana wetu Bartholomew inawezekana kuna siri alikuwa nayo ndiyo maana waliamua kummaliza. Narudia tena kama nimewakwaza mnisamehe lakini nimeongea kilicho moyoni mwangu. Asanteni!" Aliketi chini Isaya Daniel mwakilishi wa vijana kwenye kikao hicho.
" Ndugu zangu tuendelee na kikao chetu tupunguze minong'ono kama kuna jambo jingine nyosha mkono uongee, sawa ndugu zangu?" Mwenyekiti wa kikao hiki Dr. Brown Lutasya aliwataka wajumbe kutulia ili kikao kiendelee.
"Ndiyo mzee Lukosa unaweza kuongea." Mwenyekiti Dr. Brown Lutasya alimsimamisha mzee Lukosa.
"Asante Mwenyekiti kwa nafasi hii niliyoipata, kwanza kabisa nianze kwa kupinga kilichozungumzwa na Mjumbe mwenzangu bwana Isaya Daniel ni ngumu kuwashushia lawama waliotajwa wakiongozwa na Mchungaji wetu, ninachokiomba hapa mimi tuunde tume ya kufuatilia suala hili hatuwezi kujua inawezekana akawepo mtu ndani yetu anayefanya haya kwa matakwa yake mwenyewe na kutuvuruga ili tupoteane kumbukeni Kanisa letu limepokea mamilioni mangapi kwa ajili ya huduma na zilifanya kazi yake kwanini leo hivi vimilioni vichache vizue sintofahamu na kuwachafua viongozi wetu? Tulitafakari hili kwanza ndipo tufanye maamuzi." Mzee Lukosa alikaa baada ya kumaliza kuzungumza.
" Asante mjumbe kwa maoni yako, kuna mwingine?" Mwenyekiti aliuliza, lakini hakuna aliyenyoosha mkono na badala yake minong'ono iliendelea chini kwa chini kitu kilichomshtua Mchungaji. Hivyo akaona anyooshe mkono kuomba nafasi ya kuongea dukuduku lililo moyoni mwake.
" Ndugu zangu wajumbe mi...... "Lakini kabla hajamaliza kuongea wajumbe wote walisimama na kutoka nje ikiwa ishara mbaya juu yake kitu kilichomfanya mwenyekiti kumpa ishara ya kuketi chini Mchungaji baada ya kuona wamebakia wenyewe tu na mzee Lusoka huku viti vikiwazodoa baada ya waliokuwa wamekalia kutoka nje.
"Ina maana wajumbe wote wameungana na Isaya Daniel kunishutumu mimi kuwa nahusika na upotevu wa fedha hizi pamoja na mauaji yaliyotokea?" Mchungaji Rodney aliwauliza mle ndani.
"Picha ndivyo inavyosema baba Mchungaji tuna kazi ya ziada ya kufanya katika hili." Mwenyekiti Dr. Brown Lutasya alimjibu.
"Hali hii ni ya hatari sana na tusipokuwa makini tunaweza kulisambaratisha kanisa letu wazee wenzangu." Mzee Lukosa alimwambia mwenyekiti baada ya kumuona Mchungaji akitoka kwa ghadhabu na kuwaacha peke yao.
"Lakini mzee Lusoka unasemaje katika hili tukiacha majungu?" Mwenyekiti alimuuliza mzee Lusoka aliyekuwa akijifuta jasho wakitoka nje.
"Daktari unataka kusemaje na wewe? Ina maana nawe uko upande wa waliotoka nje?" Alimuuliza.
"Sijamaanisha hivyo mzee Lusoka lakini nilitaka tuliangalie hili kwa mapana yake." Mwenyekiti alijikuta peke yake huku mzee Lusoka akitoka kasi.
"Mwaka huu sijui itakavyokuwa." Mwenyekiti aliongeza mwendo mpaka nje ambako hakukuwa na mtu yoyote zaidi ya mzee lu aliyekuwa akiongea na simu kitu kilichomfanya Dr. Brown Lutasya kutulia kwanza kusikiliza mzee Lusoka anaongea nini na anaongea na nani.
"Nitakupigia baadaye kijana wangu ngoja nitafute utulivu." Mzee Lukosa alimaliza kwa kuongea hayo baada ya kumuona Daktari Brown akiwa kwenye gari lake akimfuatilia. Hali ilikuwa mbaya kwa siku hiyo kwani kila mjumbe alitoka akiwa na shaka lake huku kila mmoja akionesha hofu yake kwa Mchungaji Rodney ambaye muda huu alikuwa njiani kuelekea kwa mganga wake mzee Alioune ambaye kamtumia kwa muda mrefu kwenye mambo yake ya gizani ambayo ni kinyume na imani yake. Na baada ya kikao kuvunjika Mchungaji alitambua kuwa mtu pekee aliye nyuma yake ni mzee Lusoka na wengine wote wakimpa shutuma,suala hili lilimchanganya sana kiasi cha kumfanya kurudi kwa mganga wake ambaye anaamini anaweza kuwatuliza waumini wake pamoja na wajumbe wote ambao wanaamini yeye ndiye anahusika na kila kitu. Baada ya kufika nyumbani kwa mzee Alioune alipaki gari lake vizuri na kushuka na moja kwa moja alielekea kilingeni baada ya kukuta nyumba iko kimya sana. Alipofika Kilingeni alikuta hakuko vizuri kila kitu kilikuwa kimevurugwa huku madawa yakiwa yamemwagwa na kukifanya chumba kile kuwa na harufu nzito iliyosababishwa na madawa yaliyomwagwa mle ndani.
"Mhh nini kimetokea hapa? Mbona madawa yamemwagwa kiasi hiki?" Mchungaji Rodney alijiuliza maswali haya kutokana na hali aliyoikuta. Wakati akitoka nje aliiona michirizi ya damu ikiwa mlangoni na kuelekea vichakani ambako aliona aifuatilie ilikoelekea.
"Mungu wangu ni macho yangu au naota?" Alijiuliza baada ya kukutana na mwili wa mzee Alioune ukiwa chini umetapakaa damu. Alitaka kukimbia lakini mara alikiona kikaratasi kikiwa kwenye kisu kilichokuwa mkononi mwa mzee Alioune.
"Sasa mbona kisu chenye damu kimeshikwa na yeye mwenyewe? Ina maana kajiua mwenyewe?" Mchungaji alijiuliza maswali akiinama kuchukua kikaratasi kile kilichotapakaa damu lakini kikiwa na maandishi yanayosomeka vizuri kabisa.
"Huu ni mwanzo tu, safari hii itaishia kwako Mchungaji. Pokea salamu zangu. Kamfuate mtoto wa mganga wako nyuma ya nyumba yao." Baada ya kuusoma ujumbe huu Mchungaji alijikuta akikuna kichwa chake kwa hofu.
"Ina maana muuaji huyu bado anatembea na mimi kama kivuli?" Mchungaji alijiuliza akiuacha mwili wa mzee Alioune na kutoka mbio kuelekea nyumbani kwa mzee Alioune kumuangalia mtoto wa mzee huyu aitwaye Seynabou akiwa hajui nini kafanyiwa.
"Mhh mmhhh......." Alimkuta Seynabou akiwa kafungwa kitambaa usoni na kamba kwenye miguu yake na mikono yake na kufungiwa kwenye mti. Haraka sana Mchungaji alimfungua kamba na kitambaa ili kutaka kujua nini kimewakuta.
"Kumetokea nini Seynabou?" Mchungaji alimuuliza akimalizia kumfungua kamba za miguuni.
"Unauliza? Au unajifanyisha ili nijue wewe ni mtu safi?" Seynabou alimuuliza Mchungaji huku akitaka kukimbia.
"Seynabou una maanisha nini kusema hivyo? Unataka kusema mimi najua hili?" Alimuuliza.
"Mjomba niisikilize vizuri hapa, kuna mtu ambaye sura yake ilikuwa ndani ya Barakoa na kunikamata na kuanza kunipiga mangumi ya tumbo akinitaka nimuoneshe baba aliko, na kutokana na maumivu ambayo niliyapata kwa kichapo kile ilibidi nimuoneshe aliko baba alinifunga na kuniacha hapa lakini baada ya dakika kama kumi hivi alirejea akiwa anacheka sana na kuniambia kuwa kazi aliyotumwa na wewe ameimaliza hivyo nikifanikiwa kujifungua kamba nitaikuta maiti ya baba Kilingeni. Sasa unataka kuongea nini hebu niache kwanza." Seynabou alimaliza kumfafanulia Mchungaji na kuondoka mbio kuelekea Kilingeni kumuangalia baba yake kama kweli kauawa. Mchungaji hakuwa na la kufanya zaidi ya kumfuata anakoelekea ili kutaka kumueleza ukweli Seynabou ambaye anaamini muuaji wa baba yake katumwa na yeye.
"Muuaji huyu anayeficha sura yake ni nani? Na kwanini afanye hivi? Ina maana mauaji ya mama yake ambaye simkumbuki ndiyo yalipiwe kisasi kwa staili hii?" Mchungaji alijiuliza akiwa njiani kumfuata Seynabou, lakini mara alifunga breki na kuamua kugeuka kurudi kwenye gari.
" Hata nikimwambia ukweli atanielewa? Na kama akielewa nitampeleka wapi na huko nitamweleza mke wangu huyu ni nani? Si atajua ni mtoto wangu? Potelea mbali wacha niondoke eneo hili kabla makubwa hayajanifika maana siwezi kujua muuaji huyu kaandaa mtego gani kwangu."Mchungaji alijiuliza maswali akiwa anaingia kwenye gari. Alifunga mlango akawasha gari na kutimua vumbi.
Breki ya kwanza ilikuwa nyumbani kwa mzee Lusoka ambako alimkuta akimsaidia mke wake kuifanyia usafi bustani yao.
"Baba Mchungaji mbona hivyo kulikoni? Kwema utokako?" Mzee Lukosa alimuuliza baada ya kulishuhudia gari likifunga breki kana kwamba mtu alikuwa akikimbizwa vile.
"Si kwema mzee wangu." Mchungaji alimjibu.
"Bwana asifiwe baba Mchungaji!" Mke wa mzee Lusoka alimwamkia.
"Shemeji samahani siko sawa tafadhali." Mchungaji alijikuta akimjibu hivyo mama wa watu.
"Samahani mke wangu tupishe mara moja." Mzee Lukosa alimtaka mke wake awapishe waongee kidogo.
"Sawa mume wangu, wacha nikaandae chochote jikoni."
"Itakuwa vizuri mke wangu." Alimjibu mke wake akimfuata Mchungaji ambaye alitangulia kwenye gari naye akapanda.
"Enhh kuna jipya?" Mzee Lukosa hakutaka kusubiri alimtwanga swali akifunga mlango wa gari.
"Mzee wangu hali inazidi kuwa mbaya."
"Kivipi Mchungaji mbona unanitisha?" Mzee Lukosa alimuuliza.
"Tulivyoachana pale kanisani mimi moja kwa moja nikamfuata mzee Alioune atufanyie mambo ili kanisani litulie."Mchungaji alianza kumsimulia mzee Lusoka.
" Karekebisha tayari?"
" Si bora ingekuwa hivyo mzee wangu, huwezi amini mzee Alioune kauawa na muuaji yule yule anayenifuatilia mimi na mbaya zaidi kamwambia mtoto wa mganga kuwa mimi ndiye niliyemtuma amuue mzee wake." Mchungaji alimjibu.
"Makubwa! Ndiyo kasema hivyo? Na vipi kuhusu huyo mtoto hajamfanyia kitu chochote kibaya?"
"Hapana zaidi ya kumfunga kitambaa cheusi usoni na kumfunga kamba za mikono na miguu." Mchungaji alimjibu mzee Lusoka.
"Mhh si bure kuna jambo hapo tena si dogo kijana wangu na tusipokuwa makini majina yetu yanakwenda kubadilika muda si mrefu." Mzee Lukosa alianza kuogopa baada ya kuambiwa hayo na Mchungaji.
"Na nilivyomuuliza yukoje kasema hakubahatika kumuona sura yake kwani alivalia Barakoa usoni."
"Yuko wapi huyo mtoto?" Mzee Lukosa alimuuliza Mchungaji.
"Baada ya kuniambia mimi ndiye niliyeagiza kuuawa kwa baba yake sikuona sababu ya kuendelea kukaa pale nilitimua mbio."
"Ulikosea washa gari turudi tukaongee naye kwa mara nyingine kuna maswali nahitaji kumuuliza." Mchungaji hakuwa na la kubisha zaidi ya kuwasha gari na kuondoka.

JE, KITENDAWILI HIKI KITATEGULIWA NA NANI?

USIACHE KUWEKA BANDO LA KUTOSHA ILI UWE MMOJA WA WAFAIDI WA HADITHI HII YENYE WINGI WA VISA.
 
Sultan Uwezo
🇹🇿+255

Mchungaji Rodney aliendesha gari kama kichaa vile hakujali ubovu wa barabara kuelekea kijijini kule kwenye makazi ya mganga wao ambaye kwa sasa ni marehemu mzee Alioune. Ilikuwa kila akipunguza mwendo mzee Lusoka anamhimiza aongeze mwendo hivyo ikawa kama wimbo wa Taifa vile. Walipolikaribia daraja la mto Nongi ambalo ukilivuka tu unakuwa umeyakaribia makazi ya wakina Seynabou walikutana na kizuizi, mti mkubwa wa mbuyu ulikuwa umeangukia barabarani na kuifanya kutoruhusu magari kupita hivyo moja kwa moja ikawawia vigumu kupita na gari wakateremka na kuanza kutembea kwa miguu.

"Mchungaji hivi huu mbuyu umeangushwa na nini?" Mzee Lukosa alimuuliza.
"Mimacho imenitoka hapa kuangaza chanzo cha mti huu kuanguka na si kuanguka tu bali kuangukia barabarani lakini sioni kitu." Mchungaji alimjibu mzee Lusoka huku akiukagua vizuri ule mbuyu.
"Mchungaji hebu angalia pale.." Mzee Lukosa alimtaka Mchungaji aangalie alikokuwa akimuonesha.
"Kuna nini mzee?" Mchungaji alimuuliza.
"Huu mti haujakatika kwa upepo wala nini bali kuna mchezo mchafu hapa hebu angalia hapa."
"Kweli mzee Lusoka hii ni alama ya mashine ya kukatia miti, inavyoonekana mkataji aliitumia mashine na kutokana na ukubwa wa mti alipofika katikati ulimalizikia wenyewe." Mchungaji alimuunga mkono mzee Lusoka baada ya kuona mikato ya mashine.
"Ni kweli kabisa Mchungaji lakini hebu tuachane na huu mti ambao hatuwezi kuufanya chochote hebu tukiwahi kilichotuleta huwezi jua labda huyu muuaji ndiye aliyefanya hivi." Mzee Lukosa alimtaka Mchungaji waondoke pale na hakuwa na pingamizi lolote zaidi ya kuondoka na kuliacha gari pale pale.
" Mungu wangu! Nani kafanya haya tena?" Mchungaji aliuliza walipowasili nyumbani kwa mzee Alioune na kukuta nyumba zikimalizikia kuteketea kwa moto. Mchungaji alipigwa na butwaa kiasi cha kushindwa kumjibu mzee Lusoka ambaye alikuwa macho yalikuwa kwenye kikaratasi kilichokuwa kimebandikwa kwenye mti karibu na walipokuwa wamesimama.
"Zamu ya nani?" Mzee Lukosa alijiuliza baada ya kukisoma kikaratasi kilichokuwa kimeandikwa hivi ; 'NIMEMALIZA HAPA INAFUATA ZAMU YAKO WEWE.' Alimsogelea Mchungaji na kumgusa begani kisha kumuonesha kile kikaratasi, Mchungaji baada ya kukisoma alimgeukia mzee Lusoka.
" Zamu ya nani hiyo mzee wangu?" Mchungaji alimuuliza mzee Lusoka.
"Labda wewe Mchungaji si ulisema kuwa muuaji anakuwinda?" Mzee Lukosa alimjibu.
"Unasemaje?" Mchungaji alimuuliza mzee Lusoka akiwa kamtolea macho.
"Tusigombane hapa Mchungaji kinachotakiwa kufanywa hapa ni kuondoka eneo hili huku tukitafakari ni wapi aliko mtoto wa watu kauawa au katekwa?" Mzee Lukosa alimjibu.
"Unaongea sana mzee wangu hebu twenzetu bwana." Mchungaji alimwambia mzee Lusoka akivua koti lake. Walitoka mbio mpaka kwenye gari na kuingia ndani yake kisha kuondoka kasi kurudi mjini.
"Mchungaji unajua kuna kitu bado najiuliza hapa juu ya haya matukio.." Mzee Lukosa alimwambia Mchungaji.
"Kitu gani mzee wangu? Mbona hutulii?" Mchungaji alimjibu kwa ukali.
"Si kwa ubaya kijana wangu, bado naumiza kichwa huyu muuaji kwanini akuweke kwenye tageti zake wewe? Na ni tukio gani ambalo umewahi kulifanya huko nyuma ambalo ndiyo linaanza kukutafuna?" Mzee Lukosa alimuuliza. Mchungaji Rodney badala ya kujibu swali la mzee Lusoka alisimamisha gari na kumpa ishara ya kushuka kitu kilichomshtua.
" Una maanisha nini?" Mzee Lukosa alimuuliza tena Mchungaji ambaye hakumjibu kitu zaidi kuendelea kukazia katika ishara yake ya kumtaka ashuke chini. Mzee Lukosa hakuwa na jinsi zaidi ya kuteremka garini japo ilikuwa ni porini bado. Mchungaji alipandisha vioo vya gari lake na kuliondoa kwa kasi na kupelekea vumbi jingi kutimka huku macho yake yakiwa kwenye 'site mirror' akijaribu kumtazama mzee Lusoka ambaye hakuweza kumuona vizuri kutokana na vumbi lile.
"Potelea mbali hayo maswali yako iulize miti ikujibu mtu gani usiyekuwa na simile hata kidogo kazi kukera tu." Alijisemesha mwenyewe huku tabasamu likichukua nafasi usoni kwake akiamini amemkomoa mzee Lusoka. Na baada ya saa moja hivi aliwasili nyumbani kwake na baada ya kupaki gari sehemu yake alirejea kulifunga geti lililokuwa wazi.
" Huyu bwege sijui kaenda wapi na giza hili?" Alijiuliza Mchungaji.
Alipohakikisha kuwa kalifunga vizuri geti alikifuata kibanda ambacho Adoyee hujipumzisha na kuhifadhi vitu vyake mbalimbali lakini alikutana na mlango ukiwa umefungwa huku funguo imening'ia.
" Kuna nini?" Mchungaji alijiuliza swali akilikagua kufuli. Lakini wakati akiondoka pale lindoni macho yake yaliweza kuona mwanga wa kwenye maua hivyo akaona aufuate kutaka kujua kuna nini na baada ya kufika aliikuta tochi ambayo hutumiwa na mlinzi wake Adoyee ikiwa pale chini huku ikiendelea kuwaka na pembeni yake kukiwa na shati lililokuwa limevaliwa na Adoyee asubuhi likiwa limetapakaa damu.
"Ina maana muuaji huyu ameshapafahamu nyumbani kwangu?" Alijiuliza akiitoa simu yake mfukoni. Alikagua namba fulani kisha akaipiga.
"Samahani, namba unayopiga haipatikani hivyo jaribu njia nyingine kumfikia mhusika." Yalikuwa ni maneno kutoka kwenye kampuni ya mawasiliano ambayo alipiga kuashiria namba hiyo haikuwa hewani hali hiyo ilimtisha Mchungaji Rodney, aliipiga tena namba ile lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote.
" Mke wangu uko wapi mama?" Mchungaji alijiuliza swali huku akiondoka eneo lile na mkono mwingine ukiwa umekamata tochi na lile shati. Aliingia ndani na kuiweka tochi mezani huku lile shati akilirushia kwenye kona ya sebule na kuelekea chumbani moja kwa moja. Lakini hakuweza kumuona mke wake zaidi ya kikaratasi kilichokuwa kitandani na pembeni yake kukiwa na kalamu iliyotumiwa kuandika ujumbe huo.
"USIFANYE CHOCHOTE KILE ZAIDI YA KUSUBIRI SIMU YANGU KESHO ASUBUHI KWA MAELEKEZO KINYUME CHAKE KICHWA CHAKO HALALI YANGU." Baada ya kuusoma ujumbe ule aliishiwa nguvu na kujikuta akienda chini na kuketi kwa kukosa nguvu.
"Ina maana mke wangu na mlinzi wametekwa na Kimburu huyu? Okay hakuna tabu wacha nitulie tu lakini si kwamba nimekuogopa nimeamua tu." Mchungaji alijisemesha mwenyewe akijitahidi kusimama kuona kama yuko fiti.

Aliposimama alirejea sebuleni na kwenda kwenye friji ambako alichukua maji na kunywa kama vile kaambiwa akiyamaliza haraka atapata zawadi kwani ndani ya dakika mbili kopo lilikuwa tupu pamoja na ubaridi wake. Kisha alirudi kwenye kiti na kuketi huku kichwa kikimuwasha asijue afanye nini kwa wakati huo kuna muda aliishika simu na kulitafuta jina la mzee Lusoka lakini alisita kumpigia kutokana na kilichotokea kule porini muda mfupi uliopita, hapo hapo akapata wazo la kumpigia simu mzee Kitesa ambaye pia ni mmoja wa viongozi wakubwa wa Kanisa lao la JESUS OUR KING (JOK) Stesheni ya Tanzania katika mkoa wa Mbeya na kwa bahati nzuri simu iliita.
"Asante Yesu ipo hewani." Mchungaji alijisemesha mwenyewe baada ya simu ya mzee Kitesa kuita.
"Daktari Sylvester Kitesa anaongea, naongea na nani tafadhali?" Alianza baada ya kupokea simu.
"Bwana asifiwe mzee wangu!" Mchungaji Rodney alimjibu.
"Ameeen mtumishi nani mwenzangu?" Mzee Kitesa aliuliza bila shaka ni baada ya kuona namba ngeni.
"Ni kijana wako Mchungaji Rodney kutoka Dakar Senegal." Alijitambulisha.
"Ooh My God!! Rodney mbona unapotea hivyo? Angalia sasa mpaka umeingia kwenye orodha ya watu ambao niliyafutilia mbali majina yao kwenye simu yangu siku ya jana." Mzee Kitesa alifurahi sana kulisikia jina la Mchungaji Rodney muda huo.
"Nisamehe bure mzee wangu maana nikisema ni majukumu itakuwa ni kusingizia tu itoshe kusema naomba unisamehe." Mchungaji aliomba radhi.
"Nimekusamehe kijana wangu kuwa na amani vipi wanasemaje Wasenegali?"
"Mhh huku hawana usemi mzee wangu zaidi ya majanga tu...."
"Majanga? Kivipi Rodney?" Mzee Kitesa alimkatisha na kumuuliza.

UNAFIKIRI NI MAJANGA GANI HAYO?

USIKOSE KUSOMA SEHEMU YA NANE UPATE KUUFAIDI UHONDO HUU USIOKWARUZA KOONI LAKINI UNAOSABABISHA MAPIGO YA MOYO KWENDA KASI.

PicsArt_11-08-01.31.04.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

Mchungaji Rodney aliendesha gari kama kichaa vile hakujali ubovu wa barabara kuelekea kijijini kule kwenye makazi ya mganga wao ambaye kwa sasa ni marehemu mzee Alioune. Ilikuwa kila akipunguza mwendo mzee Lusoka anamhimiza aongeze mwendo hivyo ikawa kama wimbo wa Taifa vile. Walipolikaribia daraja la mto Nongi ambalo ukilivuka tu unakuwa umeyakaribia makazi ya wakina Seynabou walikutana na kizuizi, mti mkubwa wa mbuyu ulikuwa umeangukia barabarani na kuifanya kutoruhusu magari kupita hivyo moja kwa moja ikawawia vigumu kupita na gari wakateremka na kuanza kutembea kwa miguu.

"Mchungaji hivi huu mbuyu umeangushwa na nini?" Mzee Lukosa alimuuliza.
"Mimacho imenitoka hapa kuangaza chanzo cha mti huu kuanguka na si kuanguka tu bali kuangukia barabarani lakini sioni kitu." Mchungaji alimjibu mzee Lusoka huku akiukagua vizuri ule mbuyu.
"Mchungaji hebu angalia pale.." Mzee Lukosa alimtaka Mchungaji aangalie alikokuwa akimuonesha.
"Kuna nini mzee?" Mchungaji alimuuliza.
"Huu mti haujakatika kwa upepo wala nini bali kuna mchezo mchafu hapa hebu angalia hapa."
"Kweli mzee Lusoka hii ni alama ya mashine ya kukatia miti, inavyoonekana mkataji aliitumia mashine na kutokana na ukubwa wa mti alipofika katikati ulimalizikia wenyewe." Mchungaji alimuunga mkono mzee Lusoka baada ya kuona mikato ya mashine.
"Ni kweli kabisa Mchungaji lakini hebu tuachane na huu mti ambao hatuwezi kuufanya chochote hebu tukiwahi kilichotuleta huwezi jua labda huyu muuaji ndiye aliyefanya hivi." Mzee Lukosa alimtaka Mchungaji waondoke pale na hakuwa na pingamizi lolote zaidi ya kuondoka na kuliacha gari pale pale.
" Mungu wangu! Nani kafanya haya tena?" Mchungaji aliuliza walipowasili nyumbani kwa mzee Alioune na kukuta nyumba zikimalizikia kuteketea kwa moto. Mchungaji alipigwa na butwaa kiasi cha kushindwa kumjibu mzee Lusoka ambaye alikuwa macho yalikuwa kwenye kikaratasi kilichokuwa kimebandikwa kwenye mti karibu na walipokuwa wamesimama.
"Zamu ya nani?" Mzee Lukosa alijiuliza baada ya kukisoma kikaratasi kilichokuwa kimeandikwa hivi ; 'NIMEMALIZA HAPA INAFUATA ZAMU YAKO WEWE.' Alimsogelea Mchungaji na kumgusa begani kisha kumuonesha kile kikaratasi, Mchungaji baada ya kukisoma alimgeukia mzee Lusoka.
" Zamu ya nani hiyo mzee wangu?" Mchungaji alimuuliza mzee Lusoka.
"Labda wewe Mchungaji si ulisema kuwa muuaji anakuwinda?" Mzee Lukosa alimjibu.
"Unasemaje?" Mchungaji alimuuliza mzee Lusoka akiwa kamtolea macho.
"Tusigombane hapa Mchungaji kinachotakiwa kufanywa hapa ni kuondoka eneo hili huku tukitafakari ni wapi aliko mtoto wa watu kauawa au katekwa?" Mzee Lukosa alimjibu.
"Unaongea sana mzee wangu hebu twenzetu bwana." Mchungaji alimwambia mzee Lusoka akivua koti lake. Walitoka mbio mpaka kwenye gari na kuingia ndani yake kisha kuondoka kasi kurudi mjini.
"Mchungaji unajua kuna kitu bado najiuliza hapa juu ya haya matukio.." Mzee Lukosa alimwambia Mchungaji.
"Kitu gani mzee wangu? Mbona hutulii?" Mchungaji alimjibu kwa ukali.
"Si kwa ubaya kijana wangu, bado naumiza kichwa huyu muuaji kwanini akuweke kwenye tageti zake wewe? Na ni tukio gani ambalo umewahi kulifanya huko nyuma ambalo ndiyo linaanza kukutafuna?" Mzee Lukosa alimuuliza. Mchungaji Rodney badala ya kujibu swali la mzee Lusoka alisimamisha gari na kumpa ishara ya kushuka kitu kilichomshtua.
" Una maanisha nini?" Mzee Lukosa alimuuliza tena Mchungaji ambaye hakumjibu kitu zaidi kuendelea kukazia katika ishara yake ya kumtaka ashuke chini. Mzee Lukosa hakuwa na jinsi zaidi ya kuteremka garini japo ilikuwa ni porini bado. Mchungaji alipandisha vioo vya gari lake na kuliondoa kwa kasi na kupelekea vumbi jingi kutimka huku macho yake yakiwa kwenye 'site mirror' akijaribu kumtazama mzee Lusoka ambaye hakuweza kumuona vizuri kutokana na vumbi lile.
"Potelea mbali hayo maswali yako iulize miti ikujibu mtu gani usiyekuwa na simile hata kidogo kazi kukera tu." Alijisemesha mwenyewe huku tabasamu likichukua nafasi usoni kwake akiamini amemkomoa mzee Lusoka. Na baada ya saa moja hivi aliwasili nyumbani kwake na baada ya kupaki gari sehemu yake alirejea kulifunga geti lililokuwa wazi.
" Huyu bwege sijui kaenda wapi na giza hili?" Alijiuliza Mchungaji.
Alipohakikisha kuwa kalifunga vizuri geti alikifuata kibanda ambacho Adoyee hujipumzisha na kuhifadhi vitu vyake mbalimbali lakini alikutana na mlango ukiwa umefungwa huku funguo imening'ia.
" Kuna nini?" Mchungaji alijiuliza swali akilikagua kufuli. Lakini wakati akiondoka pale lindoni macho yake yaliweza kuona mwanga wa kwenye maua hivyo akaona aufuate kutaka kujua kuna nini na baada ya kufika aliikuta tochi ambayo hutumiwa na mlinzi wake Adoyee ikiwa pale chini huku ikiendelea kuwaka na pembeni yake kukiwa na shati lililokuwa limevaliwa na Adoyee asubuhi likiwa limetapakaa damu.
"Ina maana muuaji huyu ameshapafahamu nyumbani kwangu?" Alijiuliza akiitoa simu yake mfukoni. Alikagua namba fulani kisha akaipiga.
"Samahani, namba unayopiga haipatikani hivyo jaribu njia nyingine kumfikia mhusika." Yalikuwa ni maneno kutoka kwenye kampuni ya mawasiliano ambayo alipiga kuashiria namba hiyo haikuwa hewani hali hiyo ilimtisha Mchungaji Rodney, aliipiga tena namba ile lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote.
" Mke wangu uko wapi mama?" Mchungaji alijiuliza swali huku akiondoka eneo lile na mkono mwingine ukiwa umekamata tochi na lile shati. Aliingia ndani na kuiweka tochi mezani huku lile shati akilirushia kwenye kona ya sebule na kuelekea chumbani moja kwa moja. Lakini hakuweza kumuona mke wake zaidi ya kikaratasi kilichokuwa kitandani na pembeni yake kukiwa na kalamu iliyotumiwa kuandika ujumbe huo.
"USIFANYE CHOCHOTE KILE ZAIDI YA KUSUBIRI SIMU YANGU KESHO ASUBUHI KWA MAELEKEZO KINYUME CHAKE KICHWA CHAKO HALALI YANGU." Baada ya kuusoma ujumbe ule aliishiwa nguvu na kujikuta akienda chini na kuketi kwa kukosa nguvu.
"Ina maana mke wangu na mlinzi wametekwa na Kimburu huyu? Okay hakuna tabu wacha nitulie tu lakini si kwamba nimekuogopa nimeamua tu." Mchungaji alijisemesha mwenyewe akijitahidi kusimama kuona kama yuko fiti.

Aliposimama alirejea sebuleni na kwenda kwenye friji ambako alichukua maji na kunywa kama vile kaambiwa akiyamaliza haraka atapata zawadi kwani ndani ya dakika mbili kopo lilikuwa tupu pamoja na ubaridi wake. Kisha alirudi kwenye kiti na kuketi huku kichwa kikimuwasha asijue afanye nini kwa wakati huo kuna muda aliishika simu na kulitafuta jina la mzee Lusoka lakini alisita kumpigia kutokana na kilichotokea kule porini muda mfupi uliopita, hapo hapo akapata wazo la kumpigia simu mzee Kitesa ambaye pia ni mmoja wa viongozi wakubwa wa Kanisa lao la JESUS OUR KING (JOK) Stesheni ya Tanzania katika mkoa wa Mbeya na kwa bahati nzuri simu iliita.
"Asante Yesu ipo hewani." Mchungaji alijisemesha mwenyewe baada ya simu ya mzee Kitesa kuita.
"Daktari Sylvester Kitesa anaongea, naongea na nani tafadhali?" Alianza baada ya kupokea simu.
"Bwana asifiwe mzee wangu!" Mchungaji Rodney alimjibu.
"Ameeen mtumishi nani mwenzangu?" Mzee Kitesa aliuliza bila shaka ni baada ya kuona namba ngeni.
"Ni kijana wako Mchungaji Rodney kutoka Dakar Senegal." Alijitambulisha.
"Ooh My God!! Rodney mbona unapotea hivyo? Angalia sasa mpaka umeingia kwenye orodha ya watu ambao niliyafutilia mbali majina yao kwenye simu yangu siku ya jana." Mzee Kitesa alifurahi sana kulisikia jina la Mchungaji Rodney muda huo.
"Nisamehe bure mzee wangu maana nikisema ni majukumu itakuwa ni kusingizia tu itoshe kusema naomba unisamehe." Mchungaji aliomba radhi.
"Nimekusamehe kijana wangu kuwa na amani vipi wanasemaje Wasenegali?"
"Mhh huku hawana usemi mzee wangu zaidi ya majanga tu...."
"Majanga? Kivipi Rodney?" Mzee Kitesa alimkatisha na kumuuliza.

UNAFIKIRI NI MAJANGA GANI HAYO?

USIKOSE KUSOMA SEHEMU YA NANE UPATE KUUFAIDI UHONDO HUU USIOKWARUZA KOONI LAKINI UNAOSABABISHA MAPIGO YA MOYO KWENDA KASI.

View attachment 1640801
Mbona sehemu ya 07 mara 08
sehemu ya kwanza ipo wapi?!
Au
Ni style mpya Chief.......!!!!!
 
Sultan Uwezo
+255

"Ndiyo mzee wangu na si majanga tu bali ni tetemeko na hofu juu yake na hapa ninapoongea na wewe sijui kama kesho nitaiona." Mchungaji aliendelea kumpa presha mzee Kitesa.
"Hebu acha kupindisha maneno kuwa wazi Mchungaji." Mzee Kitesa alimtaka Mchungaji Rodney kueleza kinachomkabili pasipo kumficha.
"Mzee wangu hivi karibuni nimekuwa nikitishiwa maisha na mtu nisiyemfahamu na tayari keshaua waumini wangu zaidi ya watatu kama hilo halitoshi alihusika na kumteka Bwana fedha wetu Bartholomew ikiwa ni pamoja na kupora kiasi chote cha fedha kilichotumwa na Taasisi rafiki kutoka Ng'ambo na kama haitoshi leo hii mke wangu na mlinzi sijawakuta hapa nyumbani nimekutana na ujumbe tu wa vitisho juu yangu." Mchungaji Rodney alimsimulia mzee Kitesa kila kitu ya yaliyotokea.
" Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa mkeo pamoja na mlinzi wako wametekwa au kuuawa?"
" Naweza kusema ndiyo au hapana labda niisubiri simu yao kwanza maana wameniambia nisifanye chochote japo nimekwenda kinyume nao sijui itakuwaje baada ya mazungumzo haya." Mchungaji alimjibu.
" Mtegemee Mungu kwa kila jambo maana yeye ndiye mleta majibu, hebu kata simu kwanza kuna mtu nataka kuongea naye nafikiri kesho asubuhi tuwasiliane kijana wangu." Mzee Kitesa alimtia moyo Mchungaji Rodney na kisha Mchungaji alifanya kama alivyoambiwa, alichukua begi lake dogo lililokuwa kwenye kiti kisha aliifuata 'Main switch' na kuzima umeme kwa nyumba nzima na kuondoka zake kwa miguu akiyaacha magari mle ndani.

***

Baada ya safari ndefu hatimaye mama Mchungaji Bi Catherine, Seynabou na Adoyee waliwasili ndani mji wa Saint Louis ulioko kaskazini magharibi mwa Pwani ya Senegal na moja kwa moja walifikia kwenye jumba fulani hivi chakavu kwa muonekano wa nje lakini kwa ndani kulikuwa tofauti kabisa kwani kulisheheni kila kitu cha thamani kinachopatikana kwenye majengo mengine ya kifahari. Jengo hili linalokadiliwa kujengwa miaka ya 1897 na lilikuwa likitumiwa na wavuvi wa kifaransa mpaka pale walipoamua kulitelekeza na kurejea kwao baada ya kutokea mapigano kati ya wavuvi wa Kifaransa pamoja na wavuvi wazawa ambao waliamini kuwa wavuvi hawa wageni walipoka ajira zao na kuwafanya kuwa watumwa wao mpaka pale walipoamua kushikamana pamoja na kuwasambaratisha mnamo mwaka 1932 ambapo jengo hili lilikuja kuchukuliwa na serikali ambayo iliwakabidhi watoa tiba za asili ambao wanaendelea kulitumia mpaka sasa lakini likiwa chini ya Tabibu maarufu na tishio wa Tiba za asili kwa ukanda wote wa Jangwa la Sahara Mzee Malick Bolenge.
"Kabla hamjafanya chochote wajukuu zangu naweni nyuso zenu kwa maji yaliyo kwenye hivyo vyungu." Ilikuwa ni sauti ya mzee Malick Bolenge akiwapa maagizo wageni wake walioingia mahali pale mida ya usiku wa saa nne.
"Tayari babu." Catherine alimjibu baada ya kufanya kama alivyowaagiza.
"Vizuri sasa acheni hapo mizigo yenu kisha nifuateni."
"Sawa babu." Catherine aliyekuwa mwenyeji wa maeneo yale alimjibu mzee Malick Bolenge. Walimfuata mpaka ndani na wakati haya yote yanafanyika Adoyee alionekana kuogopa sana tofauti na Seynabou aliyekuwa mtulivu muda wote akifuatilia maagizo yalivyokuwa yakitaka wafanye.
"Kuna baridi kali sana dada Catherine." Seynabou alimwambia Catherine baada ya kuanza kuonja baridi lililokuwa likipuliza kama vile limefunguliwa sehemu kwa makusudi.
"Hali hii ni ya kawaida sana kwa eneo hili ukizingatia kuwa tuko kwenye ncha ya mto senegal pamoja na uso wa bahari ya Atlantiki hivyo kulifanya kuwa na hali ya kipekee zaidi, japo kuna majira hali hubadilika na kuwa ya joto sana." Catherine alimjibu Seynabou.
" Karibuni sana wageni wangu nimewasubiri sana toka uliponijulisha kuwa uko njiani." Mzee Malick Bolenge aliwakaribisha sebuleni na kuwataka waketi vitini.
" Pole sana mzee wangu lakini si unajua mapito yetu yalikuwa ni ya kusubiri giza tu jua likichomoza tu ilikuwa ni lazima tulikwepe kwa kuingia kwenye mapango."
" Poleni sana kikubwa mmefika salama mengine ni changamoto tu."
"Ni kweli kabisa mzee wangu." Catherine alimjibu mzee Malick.
Baada ya Catherine kueleza kilichompeleka pale kwake mzee Malick Bolenge aliwataka waoge ili kupata nguvu wakati chakula kikiandaliwa kwa ajili yao. Huyu mzee Malick Bolenge ni kaka wa marehemu mama yake Catherine japo yeye kulingana na shughuli zake uganga alitengana na ndugu zake kufuata maagizo ya mizimu. Kila kitu kilipokuwa tayari ikiwa ni pamoja na chakula mzee Malick Bolenge alipata wasaa wa kuzungumza na Catherine.
"Mhh kulikoni mwanangu mwenyewe?" Alianza.
"Mjomba kilichonileta hapa nyumbani ni kutaka kuweka mambo yangu sawa." Catherine alimwambia Mjomba wake.
"Lakini nikikuangalia wewe na watu ulioongozana nao nahisi kuna tatizo hivi?"
"Ni kweli kuna tatizo lakini wacha niwaoneshe sehemu za kulala wageni wangu maana wamechoka sana." Catherine aliona ampotezee kwanza mzee Malick Bolenge.
"Okay sawa fanya hivyo." Alimjibu. Catherine aliinuka na kutoka kuelekea walikokuwa wakina Adoyee.
"Poleni kwa kunisubiri."
"Tulijua ndiyo tunalala hapa hapa kama unavyomuona Adoyee hapo anakoroma tu kama gari lililotumika kwenye vita ya kwanza ya dunia." Seynabou alimjibu.
"Hapana bwana si unajua tena ni muda mrefu sijakutana na mjomba wangu lakini kila kitu kiko sawa hebu muamshe nikamuoneshe malalo yake." Seynabou alimuamsha Adoyee kisha akapelekwa kwenye chumba ambacho kiliandaliwa kwa ajili yake na baada ya kumuonesha alirudi na kumuambia Seynabou amfuate. Waliingia kwenye chumba kilichokuwa karibu zaidi na sebule.
" Karibu mdogo wangu hapa ndiyo tutalala mimi na wewe." Catherine alimwambia Seynabou.
"Asante dada." Alimjibu akijitupa kitandani.
"Lakini kuna jambo tunatakiwa tutete usiku huu huu ili ikiwezekana kesho tuanze utekelezaji."
"Lipi hilo dada?" Seynabou alimuuliza.
"Kama tulivyoongea huko nyuma mimi na wewe ni wahanga wa Mchungaji Rodney pamoja na kundi lake na kilichonifurahisha zaidi ni kuwa tayari kulipa kisasi."
"Kuhusu hilo niko tayari hata muda huu haiwezekani mama yangu apotee katika mazingira yenye utata kama yale huku baba yangu hata sura yake tu siikumbuki, inauma sana." Seynabou aliongea ya moyoni huku machozi yakimtoka.
"Seynabou inaonekana una mengi ambayo bado hujaniambia, ina maana huyu mzee Alioune hakuwa baba yako?" Catherine aliuliza.
"Dada naomba tulale kisha siku ya kesho tuitumie kujuana zaidi."
"Bila shaka, kumbe weka mambo sawa wacha nikamuage mjomba ananisubiri bandani mwake."
"Sawa dada." Seynabou alimjibu na Catherine alitoka.

Hakumkuta mzee Malick Bolenge pale alipomuacha hivyo alirejea chumbani kwa ajili ya kuutafuta usingizi ukizingatia kuwa ana siku kama tatu hajapata usingizi wa kutosha kutokana na heka heka za hapa na pale. Akiwa chumbani kwao kabla ya kulala aliichukua laptop yake na kuiwasha ili kuangalia kinachoendelea kwa mume wake Mchungaji Rodney kwa kutumia App maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kufuatilia nyendo za Mchungaji huyu na hata kama asipokuwa hewani akiiunganisha tu na mtandao kila kitu kitaingia kuanzia jumbe alizotuma na kupokea Mchungaji pia simu alizopiga na kupokea zitakuwa zimerekodiwa hivyo kazi yake itakuwa na kusikiliza na kusoma, kama alivyokuwa ametegemea ndivyo ilivyokuwa kwani alipoifungua tu aliweza kuuona ujumbe ambao alimwambia kijana wake Jumbe amtumie baada ya kuusoma alitabasamu kisha akakifungua kisanduku cha sauti na kuanza kuyasikiliza mazungumzo yote yaliyofanywa kati ya Mchungaji na mzee Kitesa. Hapa ilibidi achunguze kiunganishi cha namba hii ili kujua mtu huyu ni kutoka nchi gani na ndipo alipoikuta ni +255 hapo hapo akaichukua simu yake na kufungua 'app' ya 'codes' za nchi mbalimbali ili kuibaini.
"Tanzania? Inapatikana kanda gani ya Afrika? Na kwanini alimpigia mtu huyu?" Catherine alijiuliza akiifungua 'Google map'.
"Baba Mchungaji kwa sasa wewe ni kivuli changu huwezi kunikwepa hata kidogo." Catherine aliongea huku akiurusha mkono wake mmoja juu kama ishara ya ushindi. Aliifunga laptop yake na kuiweka kwenye begi lake kisha akampigia simu Jumbe muda huo huo hakutaka kusubiri mpaka kesho.
" Naam Bosi." Jumbe aliitika baada ya kupokea simu.
" Ni hivi Jumbe, huyu panya kaanza kufanya mawasiliano na mtu kutoka nchi inayoitwa Tanzania bila shaka kuna jambo hapa."
"Tunafanyaje bosi?" Jumbe alimuuliza.
"Najua mpaka kesho nitakuwa nimepata jibu, kingine naomba wale vijana ambao nilikwambia kuwa nina mashaka nao waulie mbali kabla hawajauza ramani yetu kisha miili yao hakikisha inakwenda kutupwa nje ya Kanisa la JESUS OUR KING la Mchungaji Rodney na baada ya hapo wewe na wenzako mtaondoka eneo hilo kuelekea sehemu nitakayowaelekeza."
"Kama ulivyoagiza bosi nitafanya." Jumbe alimjibu Catherine ambaye alikata simu na kujilaza.

JE NI NINI KITATOKEA KATIKA KITIMUTIMU HIKI?

TAFADHALI UNGANA NAMI KATIKA SEHEMU INAYOFUATA TUJUE NINI KILICHOJIRI KATIKA SONGOMBINGO HILI.

PicsArt_11-08-01.31.34.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

****

Baada ya dakika kadhaa aliwasili Kanisani kwake akitumia usafiri wa Bajaj ambao aliukodi na baada ya kumlipa mwenye Bajaj hiyo alichukua mkoba wake na kuelekea getini ambako alibonyeza kengele.
"Nani?" Mlinzi aliuliza.
"Fungua geti Davis."
Alipoisikia sauti hiyo mlinzi huyo haraka sana alifungua geti dogo na kuchungulia nje.
"Karibu baba Mchungaji." Alimkaribisha.
"Asante Davis, habari ya kazi?"
"Ni nzuri tu bosi vipi kwema utokako maana sioni gari hapa nje." Davis alimuuliza Mchungaji ambaye kwa muda huo alihisi maswali yale yanamchelewesha tu.
"Usiwe na wasiwasi Davis kila kitu kiko sawa nimekuja hapa kuna kazi maalum na sitapenda kupokea mgeni muda huu mpaka kesho, sawa!" Alimwambia akimpiga begani.
"Nimekuelewa Mchungaji, halafu mzee Lusoka alikuja hapa kama masaa kadhaa nyuma akakuuliza."
"Ukamwambiaje?" Mchungaji alimuuliza baada ya kulisikia jina hilo.
"Nilimwambia haujafika akaondoka." Davis alimjibu.
"Vizuri endelea na kazi yako fanya kama nilivyokueleza."
"Sawa Mchungaji." Davis alimjibu na wakati huo Mchungaji aliachana na mlinzi huyo na kuelekea ofisini.
"Nilikuonya usifanye chochote kile lakini naona umevuka mipaka mpaka nchi ya Tanzania, unafikiri utaondoka mbele ya macho yangu yenye uwezo wa kuangalia kila kona ya Dunia? Nafikiri ndani ya masaa machache utakipata kilichowapata Catherine pamoja Adoyee mlinzi wako." Ulikuwa ni ujumbe ambao uliingia kwenye simu ya Mchungaji wakati akiketi kitandani kwenye chumba kilicho ndani ya ofisi yake. Alipousoma ujumbe ule aliishusha pumzi ndefu kama vile aliutua mzigo mzito mgongoni mwake. Na baada ya kutafakari kwa muda ikabidi aipige ile namba iliyotuma ujumbe ule ili aweze kumtambua adui yake ambaye kila kukicha ni vitisho tu. Maajabu aliyokutana nayo Mchungaji kiasi cha kumfanya kutabasamu na halikuwa la furaha bali la hasira kutokana na namba ile kutopatikana na ilikuwa ni namba mficho hivyo ikawa ni ngumu kumpata.
"Ni nani huyu ambaye kila hatua yangu yuko nyuma yangu?" Mchungaji Rodney alijiuliza. Na katika kuwaza zaidi akaijiwa na wazo la kumpigia simu mzee Lusoka ambaye mchana walikwaruzana, hivyo aliipiga namba ya mzee huyo lakini wakati inaita alitupa macho yake kwenye saa ya ukutani ndipo aliposhangaa kuona ni saa nane usiku haraka sana akakata simu na kuizima kabisa.
"Ndiyo nimefanya nini usiku wote huu kwenye majumba ya watu na masimu." Aliwaza haya akiwa analivuta blanket.

Kulikucha japo hali ya hewa haikuwa nzuri sana kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha kiasi cha kusababisha utokaji kuwa mgumu kuelekea makazini. Kwa upande wa wakulima kwao ilikuwa ni furaha kubwa hasa ukizingatia mvua ilikuwa ina muda mrefu haijanyesha hivyo muda huu kila mmoja alikuwa shambani kwake wa kupanda alikuwa akipanda na wale wa kulima ilikuwa hivyo hivyo ilmradi tu siku isiende bure.
Wakati hayo yakienda hivyo nje ya geti la kanisa kulikuwa na mtu ambaye alikuwa akigonga geti kama vile ana ugomvi nalo na wala hakujali mvua hii iliyokuwa ikiendelea kunyesha. Kelele za geti hili zilimuamsha Mchungaji kule ndani na kuchungulia nje kupitia dirishani ambapo alikuwa kasimama akiangalia kuna nini.
"Hivi huyu Davis kakumbwa na nini yaani hayo makelele hayasikii?" Mchungaji alijiuliza akiendelea kuchungulia pale dirishani, lakini kijasho kilimshuka baada ya kumuona Davis akilifungua geti na kabla hajachungulia nje kulikoni alimshuhudia Davis akisukumwa na kuanguka chini na hapo hapo aliingia mama fulani ambaye anamfahamu vizuri kutoka nyumba kama ya nne hivi.
"Mhh huyu si mama Sharon?" Mchungaji alijiuliza.
"Mchungaji, Mchungajiiiiii kama uko ndani naomba utoke huku nje kuna tatizooo......" Mama Sharon alisikika kiasi cha kumshtua Mchungaji.
"Tatizoooo? Tatizo gani hilo?" Alijiuliza akitoka kumsikiliza mama Sharon.
"Enheeee afadhali nimekuona baba Mchungaji njoo uone huku nje." Mama Sharon aliongea akimkamata mkono Mchungaji na kuanza kumvuta kuelekea nje. Mlinzi baada ya kuona kitendo kile cha kuvutwa bosi wake akainuka kutoka pale chini na kuwafuata nyuma.
"Mama Sharon kuna nini naona unanipelekesha tu bila kuongea chochote kwani kuna nini dada yangu?" Mchungaji Rodney aliona aulize tu ili ajue kuna nini.
"Utajua huku huku baba Mchungaji." Mama Sharon alimjibu kwa kifupi. Baada ya kufika nyuma ya ukuta wa kanisa palipo na dampo la taka Mchungaji hakuamini macho yake kwa alichokutana nacho.
"Hicho ndicho nilitaka kukuonesha baba Mchungaji, nimeikuta miili hiyo mitatu kama inavyoonekana hapo wakati nimekuja kutupa taka." Mama Sharon alitoa ufafanuzi kuhusu ile miili ya marehemu iliyokutwa pale jalalani ikiwa ndani ya fuko moja la nailoni angavu.
" Ni nani kafanya mauaji haya na kuja kuitelekeza hapa?" Mchungaji alijiuliza wakati mama Sharon akiondoka eneo lile.
"Mchungaji ni wakina nani hawa?" Davis alimuuliza Mchungaji wakati akiipekua simu yake.
"Wala sifahamu chochote wacha nitoe taarifa Polisi wao ndiyo watajua kipi ni kipi." Mchungaji alimjibu mlinzi huku simu ikiwa tayari sikioni.
"Ndiyo Afande ni hapa kwenye Jalala letu la taka." Baada ya kutoa maelezo hayo Mchungaji alitulia kidogo kusikiliza na ndipo alihitimisha kwa kumjibu.
"Nawasubiri Afande bila shaka."
Alipoitoa simu sikioni macho yake yalibaki kwenye kioo.
"Kama ambavyo nilikujulisha jana kuwa ifikapo leo nitakupa maelekezo nadhani kuna ujumbe umeupokea hapo ufanyie kazi lakini jua kwamba taarifa hizi zikifika kwenye vyombo vya sheria utatujua." Ulisema ujumbe huo. Alipomaliza tu kuusoma ujumbe huo alimwita Davis kwa ishara ya mkono.
" Naam Bosi." Aliitika mlinzi.
" Utabakia hapa mpaka pale Askari watakapofika kuchukua hii miili."
"Sawa bosi." Davis alimjibu. Mchungaji aliondoka pale jalalani na kuelekea ofisini kwake.
"Hapa usalama wangu ni kutoroka tu." Alijisemesha Mchungaji.

SORRY KUMETOKEA TATIZO KIDOGO NDIYO MAANA UMEIPATA FUPI LAKINI USIJALI TUKUTANE KESHO KATIKA SEHEMU YA KUMI TUWEZE KUMTAFUTA MUUAJI HUYU MWENYE BARAKOA PAMOJA.

PicsArt_11-08-01.31.34.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

****

Baada ya dakika kadhaa aliwasili Kanisani kwake akitumia usafiri wa Bajaj ambao aliukodi na baada ya kumlipa mwenye Bajaj hiyo alichukua mkoba wake na kuelekea getini ambako alibonyeza kengele.

"Nani?" Mlinzi aliuliza.
"Fungua geti Davis."
Alipoisikia sauti hiyo mlinzi huyo haraka sana alifungua geti dogo na kuchungulia nje.
"Karibu baba Mchungaji." Alimkaribisha.
"Asante Davis, habari ya kazi?"
"Ni nzuri tu bosi vipi kwema utokako maana sioni gari hapa nje." Davis alimuuliza Mchungaji ambaye kwa muda huo alihisi maswali yale yanamchelewesha tu.

"Usiwe na wasiwasi Davis kila kitu kiko sawa nimekuja hapa kuna kazi maalum na sitapenda kupokea mgeni muda huu mpaka kesho, sawa!" Alimwambia akimpiga begani.
"Nimekuelewa Mchungaji, halafu mzee Lusoka alikuja hapa kama masaa kadhaa nyuma akakuuliza."
"Ukamwambiaje?" Mchungaji alimuuliza baada ya kulisikia jina hilo.
"Nilimwambia haujafika akaondoka." Davis alimjibu.

"Vizuri endelea na kazi yako fanya kama nilivyokueleza."
"Sawa Mchungaji." Davis alimjibu na wakati huo Mchungaji aliachana na mlinzi huyo na kuelekea ofisini.
"Nilikuonya usifanye chochote kile lakini naona umevuka mipaka mpaka nchi ya Tanzania, unafikiri utaondoka mbele ya macho yangu yenye uwezo wa kuangalia kila kona ya Dunia? Nafikiri ndani ya masaa machache utakipata kilichowapata Catherine pamoja Adoyee mlinzi wako." Ulikuwa ni ujumbe ambao uliingia kwenye simu ya Mchungaji wakati akiketi kitandani kwenye chumba kilicho ndani ya ofisi yake.

Alipousoma ujumbe ule aliishusha pumzi ndefu kama vile aliutua mzigo mzito mgongoni mwake. Na baada ya kutafakari kwa muda ikabidi aipige ile namba iliyotuma ujumbe ule ili aweze kumtambua adui yake ambaye kila kukicha ni vitisho tu. Maajabu aliyokutana nayo Mchungaji kiasi cha kumfanya kutabasamu na halikuwa la furaha bali la hasira kutokana na namba ile kutopatikana na ilikuwa ni namba mficho hivyo ikawa ni ngumu kumpata.

"Ni nani huyu ambaye kila hatua yangu yuko nyuma yangu?" Mchungaji Rodney alijiuliza. Na katika kuwaza zaidi akaijiwa na wazo la kumpigia simu mzee Lusoka ambaye mchana walikwaruzana, hivyo aliipiga namba ya mzee huyo lakini wakati inaita alitupa macho yake kwenye saa ya ukutani ndipo aliposhangaa kuona ni saa nane usiku haraka sana akakata simu na kuizima kabisa.
"Ndiyo nimefanya nini usiku wote huu kwenye majumba ya watu na masimu." Aliwaza haya akiwa analivuta blanket.

Kulikucha japo hali ya hewa haikuwa nzuri sana kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha kiasi cha kusababisha utokaji kuwa mgumu kuelekea makazini. Kwa upande wa wakulima kwao ilikuwa ni furaha kubwa hasa ukizingatia mvua ilikuwa ina muda mrefu haijanyesha hivyo muda huu kila mmoja alikuwa shambani kwake wa kupanda alikuwa akipanda na wale wa kulima ilikuwa hivyo hivyo ilmradi tu siku isiende bure.

Wakati hayo yakienda hivyo nje ya geti la kanisa kulikuwa na mtu ambaye alikuwa akigonga geti kama vile ana ugomvi nalo na wala hakujali mvua hii iliyokuwa ikiendelea kunyesha. Kelele za geti hili zilimuamsha Mchungaji kule ndani na kuchungulia nje kupitia dirishani ambapo alikuwa kasimama akiangalia kuna nini.
"Hivi huyu Davis kakumbwa na nini yaani hayo makelele hayasikii?" Mchungaji alijiuliza akiendelea kuchungulia pale dirishani, lakini kijasho kilimshuka baada ya kumuona Davis akilifungua geti na kabla hajachungulia nje kulikoni alimshuhudia Davis akisukumwa na kuanguka chini na hapo hapo aliingia mama fulani ambaye anamfahamu vizuri kutoka nyumba kama ya nne hivi.

"Mhh huyu si mama Sharon?" Mchungaji alijiuliza.
"Mchungaji, Mchungajiiiiii kama uko ndani naomba utoke huku nje kuna tatizooo......" Mama Sharon alisikika kiasi cha kumshtua Mchungaji.
"Tatizoooo? Tatizo gani hilo?" Alijiuliza akitoka kumsikiliza mama Sharon.
"Enheeee afadhali nimekuona baba Mchungaji njoo uone huku nje." Mama Sharon aliongea akimkamata mkono Mchungaji na kuanza kumvuta kuelekea nje. Mlinzi baada ya kuona kitendo kile cha kuvutwa bosi wake akainuka kutoka pale chini na kuwafuata nyuma.

"Mama Sharon kuna nini naona unanipelekesha tu bila kuongea chochote kwani kuna nini dada yangu?" Mchungaji Rodney aliona aulize tu ili ajue kuna nini.
"Utajua huku huku baba Mchungaji." Mama Sharon alimjibu kwa kifupi. Baada ya kufika nyuma ya ukuta wa kanisa palipo na dampo la taka Mchungaji hakuamini macho yake kwa alichokutana nacho.
"Hicho ndicho nilitaka kukuonesha baba Mchungaji, nimeikuta miili hiyo mitatu kama inavyoonekana hapo wakati nimekuja kutupa taka." Mama Sharon alitoa ufafanuzi kuhusu ile miili ya marehemu iliyokutwa pale jalalani ikiwa ndani ya fuko moja la nailoni angavu.
" Ni nani kafanya mauaji haya na kuja kuitelekeza hapa?" Mchungaji alijiuliza wakati mama Sharon akiondoka eneo lile.
"Mchungaji ni wakina nani hawa?" Davis alimuuliza Mchungaji wakati akiipekua simu yake.

"Wala sifahamu chochote wacha nitoe taarifa Polisi wao ndiyo watajua kipi ni kipi." Mchungaji alimjibu mlinzi huku simu ikiwa tayari sikioni.
"Ndiyo Afande ni hapa kwenye Jalala letu la taka." Baada ya kutoa maelezo hayo Mchungaji alitulia kidogo kusikiliza na ndipo alihitimisha kwa kumjibu.
"Nawasubiri Afande bila shaka."
Alipoitoa simu sikioni macho yake yalibaki kwenye kioo.

"Kama ambavyo nilikujulisha jana kuwa ifikapo leo nitakupa maelekezo nadhani kuna ujumbe umeupokea hapo ufanyie kazi lakini jua kwamba taarifa hizi zikifika kwenye vyombo vya sheria utatujua." Ulisema ujumbe huo. Alipomaliza tu kuusoma ujumbe huo alimwita Davis kwa ishara ya mkono.

" Naam Bosi." Aliitika mlinzi.
" Utabakia hapa mpaka pale Askari watakapofika kuchukua hii miili."
"Sawa bosi." Davis alimjibu. Mchungaji aliondoka pale jalalani na kuelekea ofisini kwake.
"Hapa usalama wangu ni kutoroka tu." Alijisemesha Mchungaji.

SORRY KUMETOKEA TATIZO KIDOGO NDIYO MAANA UMEIPATA FUPI LAKINI USIJALI TUKUTANE KESHO KATIKA SEHEMU YA KUMI TUWEZE KUMTAFUTA MUUAJI HUYU MWENYE BARAKOA PAMOJA.

PicsArt_11-08-01.31.04.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

***

Catherine aliamka asubuhi na mapema na kutoka nje ya lile jengo akiwa kavalia mavazi yake ya michezo bila shaka alikuwa akielekea kufanya mazoezi ufukweni. Akijua kuwa amewahi sana kufika mazoezini alistaajabu kumkuta Adoyee akiwa sambamba na mzee Malick Bolenge wakiwa wamelowa kwa jasho.
"Ndiyo kusema wameamka usiku sana?" Catherine alijiuliza mwenyewe.
"Kumbe na wewe ni muumini wa mazoezi ee hatukuona sababu ya kuwaamsha tulihisi mtakuwa mmechoka sana." Mzee Malick Bolenge alimuuliza.
"Sawa tu Mjomba mmeshinda." Catherine alimjibu mjomba wake huku akimpita kwa spidi ndogo ya mbio.
"Usichukie mjomba, ukifanya hivyo asubuhi yangu itaanza vibaya."
"Wala hajakusikia." Adoyee alimwambia mzee Malick Bolenge aliyekuwa kaelekeza macho yake kwenye uelekeo wa Catherine.
"Kasikia sana ila tu kaamua kukaa kimya na hii ndiyo ilikuwa tabia ya mama yake hajaacha kitu. Achana naye wacha mimi nikaoge kuna sehemu natakiwa kuelekea."

"Sawa mzee." Adoyee alimjibu. Wakati huo huo alikuja Seynabou na kuungana na Catherine ambaye mwili wake ulikuwa umeshapata moto. Walifanya mazoezi yao kwa muda wa masaa mawili hivi kisha Seynabou na Catherine wakaona waingie kuogelea huku Adoyee akiwaacha na kurudi nyumbani.
"Madam nikuulize swali?" Seynabou alimuuliza Catherine.
"Uliza tu mdogo wangu."
"Hivi unafahamu kuogelea?" Alimuuliza.
"Kiukweli Seynabou mimi siyo fundi sana wa kuyakata maji lakini kiasi chake vipi kuhusu wewe?" Alimjibu na kumgeuzia swali naye.
"Mimi tena? Hapa ni maji marefu madam naweza kuogelea hapa mpaka ng'ambo ya bahari." Alimjibu na kuanza kucheka na bila shaka alijua amedanganya.

"Nahisi baridi ishakuanza mdogo tuondoke maana si kwa kamba uliyonifunga yaani wewe uyakate maji haya ya bahari mpaka ng'ambo kweli? Hebu tuondoke zetu huyo Shetani wako wa uongo asijetokea bure hapa ukazidi kunipiga vitasa vya uongo bure."
"Huamini au nianze?" Seynabou alimjibu.

"Hapana bwana mimi sina nguvu za kumbeba mtu aliyeshiba vikombe vya majichumvi." Majibu ya Catherine yaliwafanya waanze kucheka na wakati huo walikuwa wakikimbia taratibu kurejea nyumbani.

"Bosi kifungua kinywa kiko tayari mezani." Adoyee alimpa taarifa hiyo Catherine.
"Mhh mapema hivi, ni nani kaiandaa?" Seynabou alishangaa.

"Seynabou mbona washangaa nimeiandaa mwenyewe hapa au kuna ubaya?" Adoyee alimjibu.
"Haujakosea hata kidogo Adoyee tunashukuru, ngoja tujiweke sawa kwanza kisha tujumuike mezani." Catherine alimjibu.
"Sawa bosi." Adoyee aliitika na kurudi sebuleni. Catherine alipoingia chumbani kitu cha kwanza kikawa ni kuiwasha simu yake pamoja na laptop kama utaratibu wake ulivyo kila siku.

"Maskini!" Aliongea kwa sauti mara baada ya kukutana meseji nyingi za Jumbe zilizomkosa hewani.
"Kuna nini Madam?" Seynabou aliuliza.

"Si kubwa sana mdogo wangu ni Jumbe kapiga simu nyingi sana wakati simu ikiwa 'off' sijui kuna nini?" Alimjibu huku akiipiga namba ya Jumbe.
"Naam Bosi." Jumbe aliitika baada ya kupokea simu.
"Kwema Jumbe."

"Huku ni kwema bosi kwa kuwa ile shughuli nimeimaliza masaa kadhaa nyuma na muda huu tuko ndani ya msitu mmoja hapa tunapumzika kidogo kabla ya kuendelea na safari."

"Poleni sana, na wale washirika wetu umeongea nao juu ya kuyafuata magari yao?" Aliuliza.
"Muda mrefu sana na hivi tunavyoongea inawezekana hata 'plate numbers' washazibadilisha." Jumbe alimjibu.
"Vizuri, sasa ndani ya saa moja hivi nitakuwa hapo kuwachukua."

"Hapana bosi usihangaike sisi tutafika tu kuna mzee mmoja tumekutana naye hapa ana gari lake aina 'land lover' kakubali kutupa lifti na yeye katuomba tumsaidie kupakia magunia ya viazi mviringo alivyokuja kununua huku porini ambako ni wazalishaji wa zao hilo." Jumbe alimtoa hofu Catherine.

" Sawa Jumbe lakini kuweni makini msimuamini kila mtu mbele ya macho yenu." Aliwatahadharisha.
" Nimekuelewa mkuu wangu." Jumbe alimjibu. Catherine aliikata simu na kuiweka kitandani kisha macho yake yakahamia kwenye 'special app' na kufungua kisanduku cha simu ambazo ziliingia kwa Mchungaji haikuchukua muda kuondoka kwani alikutana na simu chache zisizo na maana hivyo akafungua kisanduku cha ujumbe mfupi nako hakupata anachokihitaji hapo aliondoka kwenye 'app' hiyo na kuingia kwenye 'unknown call' akaingiza namba ya Mchungaji na kuipiga.

"Shiiiit......!" Alijisemesha.
Seynabou aligeuka kumtazama bosi wake alitamani kuuliza kitu lakini aliona wacha akae kimya.
"Hauwezi kunikimbia mimi Rodney subiri uone." Catherine aliongea akiizima laptop.
"Vipi wewe tayari?" Alimuuliza Seynabou.

"Hapa nakusubiri wewe tu." Seynabou alimjibu.
"Okay wacha nifanye haraka mdogo wangu." Alimjibu akiinuka pale kitandani. Baada ya kuulainisha mwili wake kwa mafuta na vipodozi mbalimbali kama ilivyo kawaida kwa Wanawake na kutupia tracksuit yake ya rangi ya blue alitoka mle chumbani akiwa sambamba na Seynabou ambaye muda wote alikuwa kama mlinzi wake kwani hakubanduka mpaka pale Catherine alipokamilisha yale aliyokuwa akiyafanya.

"Adoyee mfuate Mjombe tushiriki pamoja kifungua kinywa." Catherine alimwambia Adoyee ambaye alikuwa bize kwenye simu yake.
"Bosi, mjomba kaondoka kasema amepata dharura kasema atarejea baadaye kidogo kuna mtu anakwenda kuonana naye."
"Mbona kaondoka kimya kimya hivyo?"

"Hakutaka kuwasumbueni na ndiyo maana akaniachia maagizo mimi." Adoyee alimjibu.
"Okay basi tufungue kinywa kisha tufanye moja ya shughuli iliyotuleta hapa Saint Louis."
"Sawa bosi." Adoyee alijibu.

"Seynabou umesikia nilichosema? Maana naona macho yamefia kwenye simu." Alimgeukia Seynabou.
"Macho ndiyo yalikuwa kwenye simu lakini kila kitu nimekisikia dada." Seynabou alimjibu.

Walijisevia kifungua kinywa na kuanza kupata huku mazungumzo ya hapa na pale yakiendelea na kwa kuziangalia nyuso zao walionekana kuwa furaha sana utafikiri wameishi pamoja muda mrefu.

" Bosi hivi unafikiri mchezo tuliomfanyia baba Mchungaji hautashtukiwa kweli?" Adoyee alimuuliza Catherine.
"Jamani si tumalize kwanza kula angalia sasa tunatemeana mate." Seynabou alimwambia Adoyee ambaye wakati akiongea alitokwa na vimate.

"Umeshinda basi siongei tena mimi." Adoyee alimjibu na kuinuka kisha akaondoka pale sebuleni.
"Kwa hiyo ndiyo kusema umezira au?" Catherine alimuuliza lakini hakupata jibu lolote kutoka kwa Adoyee.
"Seynabou umeshamkwaza mwenzako sasa." Catherine alimwambia Seynabou.

"Namshangaa sana anakuwa na vitabia vya kike kike sasa kilichomfanya azile hapo ni kipi kama siyo umama huo?"

"Mtajuana wenyewe bwana wacha mimi nijaze tumbo kwanza." Catherine aliongea akiongeza vipande vya nanasi kwenye sahani yake. Lakini wakati akichukua kipande kimoja cha nanasi simu ya mezani iliita ambayo toka wafike hapo wamekuwa wakiitumia kufanya mawasiliano na wakina Jumbe ambao wako njiani kuungana nao hapo Saint Louis hivyo kumfanya Catherine amwambie Seynabou akaipokee,naye akafanya kama alivyoelekezwa na bosi wake.

"Naongea na nani tafadhali?" Seynabou aliuliza baada ya kuuinua mkonge wa simu na kuiweka sikioni.

"Hapa ni ndani ya kijiji cha Omuega vijana wako tumewateka hivyo kama utakuwa tayari kuwapata wakiwa hai fuata masharti yetu." Upande wa pili uliongea kitu ambacho kilimfanya Seynabou asite kidogo kuongea chochote mpaka pale alipoweka kiganja chake kwenye simu na kuwasiliana kwanza na bosi wake juu ya kilichotokea.

" Unahitaji kitu gani kutoka kwetu?" Catherine aliingilia mazungumzo baada ya kuona ishara anazompa Seynabou haelewi.
"Simu itakayokuja muda si mrefu itakuwa na maelezo ambayo utatakiwa kuyafanyia kazi ndani ya saa moja kinyume na hapo hutotusahau maishani mwako." Kisha simu ilikatwa.

"Buushiiiiit ndiyo nini sasa au Jumbe kanichezea mchezo?" Catherine alipiga kelele.
"Kwanini afanye hivyo bosi wanaweza kuwa wametekwa kweli." Seynabou alipingana na kile alichoongea Catherine.
"Hapana mdogo wangu kuna kitu hakiko sawa hapa nilimwambia Jumbe tukawafuate lakini akakataa sasa yako wapi kama siyo kuunguza picha huku?"

"Tunahitaji kiasi cha paundi milioni moja ndipo tuwaachie na ukiwa tayari tujulishe mchana kupitia link hiyo hapo chini ili tukujulishe mahali kwa kuziweka." Upande wa pili uliongea baada ya Catherine kuipokea simu kwa mara ya pili.
"Paundi milioni moja?" Catherine aliuliza akiwa kaushika mdomo wake.
"Nimemaliza kazi kwako."Upande wa pili ulikata simu.

" Huu ni mchezo nimeamini haiwezekani nasema haiwezekaniiii!!!!!!!" Catherine alipiga kelele huku akiuachia mkonge wa simu kitu kilichomtoa chumbani kwake Adoyee kuja kuangalia kulikoni.
" Nini kimetokea bosi?" Adoyee aliuliza.

" Hivi mnafikiri zaidi ya shilingi bilioni tatu nitazipata wapi kwa muda huu?"Catherine aliuliza akijitupa kitini.
" Ni nani anahitaji kiasi hicho cha fedha?" Adoyee alimuuliza bosi wake.

" Kuwa mpole basi Adoyee huoni bosi hayuko sawa?" Seynabou alimuuliza Adoyee ambaye hakujua kinachoendelea sebuleni pale. Catherine alitoka nje ambako alizunguka nje ya nyumba huko alitulia kwa muda macho yakiwa baharini kuangalia muonekano bahari na shughuli mbalimbali zilizokuwa ziliendelea na bila kufanya vile ilikuwa ni kuutafuta utulivu juu ya kilichotokea dakika chache zilizopita. Akiwa pale nje alipata wazo la kumpigia simu mjomba wake mzee Malick Bolenge kutaka kumjulisha kilichotokea. Aliitoa simu yake mfukoni na kuitafuta namba ya mjomba wake kisha alimpigia.

"Nimetoka mara moja Mjomba wangu kuna sehemu nimekuja mara moja kuonana na mtu mmoja muhimu sana." Mzee Malick alianza baada ya kuipokea simu ya Catherine.

"Mjomba bwana sijakupigia kwa ajili ya hilo!" Catherine alimjibu.
"Kuna nini tena?" Mzee Malick Bolenge akamuuliza baada ya kubaini kajichanganya.
"Wageni wangu wametekwa na watekaji wanahitaji kiasi cha paundi milioni moja..."

"Paundi milioni? Zote hizo? Mjomba tutazitoa wapi sasa?" Mzee Malick Bolenge alimuuliza maswali mfululizo.
"Na ndiyo maana nimekupigia simu ili tushauriane na wanazihitaji fedha hizo leo hii hii Mjomba." Catherine alifafanua.
"Pole Mjomba suala hili si dogo hata kidogo."

"Asante Mjomba wangu." Catherine alimjibu.
"Hebu jiandaeni muda huu mje kwenye Hotel moja iitwayo TRAVIS MARK HOTEL." Mzee Malick alimwambia Catherine.
"Iko mji gani hiyo hotel Mjomba?" Catherine aliuliza.

"Iko nje kidogo ya mji huu wa Saint Louis tumieni gari ya kukodi mkimuelekeza tu dereva atawafikisha." Mzee Malick Bolenge alimuelekeza Catherine.

"Nimekuelewa Mjomba, tunakuja sasa hivi." Catherine alimjibu na kukata simu kwani hakutaka hata kusubiri neno lolote kutoka kwa Mjomba wake kisha alirudi ndani akiwa na furaha kiasi tofauti na mwanzo.

"Adoyee, Seynabou jiandaeni tunatoka mara moja." Aliwaambia akiingia chumbani.
Wakina Seynabou walishindwa hata kumuuliza chochote kwani alikuwa juu juu.
"Umemuelewa bosi Seynabou?" Adoyee alimuuliza Seynabou.

"Wala sijamuelewa maana namshangaa karejea akiwa na tabasamu usoni." Seynabou alimjibu.
"Mhh nenda kajiandae tusije mkwaza bosi wetu." Adoyee alimwambia Seynabou akiingia chumbani kwake.
"Mimi sina cha kubadili hivi hivi imetosha ninyi kajiandaeni nawasubiri." Seynabou alimjibu Adoyee. Ndani ya dakika kama kumi hivi Catherine alitoka akiwa ndani ya gauni refu jekundu huku mtandio mweupe ukikifunika kichwa na macho hakuyaacha hivi hivi aliyavisha miwani mikubwa myeusi mguuni akiwa kavalia raba nyeusi zenye soli nyembamba hakika alipendeza sana.

"Mhh umependeza sana bosi wangu wacha nikupokee mkoba kwa ulivyopendeza mkoba haukufai hata kidogo." Seynabou alimsifia Catherine ambaye hakumjibu kitu zaidi ya kutabasamu na kumkabidhi mkoba wake.

"Adoyee unavaa mavazi gani hayo muda wote huu?" Catherine alimtania.
"Niko tayari Madam." Alimjibu akitoka. Kisha walitoka mpaka nje ambako waliisimamisha taxi iliyokuwa ikipita.
"Samahani kaka tunaelekea TRAVIS MARK HOTEL kiasi gani?" Catherine aliuliza.

"Samahani dada hii siyo taxi lakini naweza kuwasaidia tu maana na mimi naelekea huko huko." Dereva yule aliongea akishuka kuwafungulia milango.

"Tunashukuru sana kaka kwa msaada wako." Catherine alimjibu akipanda siti ya mbele.
"Ingieni waungwana tuondoke." Dereva aliwaambia wakina Adoyee waliokuwa bado hawajapanda kwenye gari.
"Ubarikiwe kaka." Seynabou alimshukuru dereva huyu aliyejitolea kuwasaidia mpaka TRAVIS MARK HOTEL ambayo kwa hapa Saint Louis ndiyo hotel ya kifahari na ambayo hutembelewa na watu wa Mataifa mbalimbali.

"Msaada nilioutoa dada yangu kila mmoja angeweza kuufanya tu hivyo naombeni msinishukuru sana kiasi cha kupitiliza ndugu zangu." Dereva huyu aliwaambia wakina Catherine.

"Haya bwana tumeelewa." Catherine alimjibu huku akiiangalia simu yake.
" Ninyi ni wenyeji wa jiji hili?" Dereva aliwauliza.
" Mmhh ndiyo sisi ni wenyeji japo shughuli zetu huwa tunazifanyia nje ya nchi." Alijibu Catherine huku macho yake yakimkagua vizuri dereva huyu.
" Waoo kumbe na ninyi ni kama mimi tu."
"Kivipi?" Catherine alimuuliza.

"Naitwa Gidion Michael ni mfanyabiashara maarufu hapa nchini Senegal lakini makazi yangu yakiwa nchini Morocco na hapa mjini kwenu nimetua jana tu na nimefikia TRAVIS MARK HOTEL hivyo kukutana nanyi ni bonge la kampani. Kama hamtojali ningependa kuungana nanyi ukizingatia leo pale kuna Bonge la Show kutoka kwa Msanii mmoja maarufu sana kutoka nchini Tanzania anaitwa Diamond Platnumz." Gidion alijitambulisha kwa kirefu.

" Wee kaka acha uongo Mungu anakuona wewe, huyo Diamond unayemzungumzia ni yupi? Huyu huyu ninayemfahamu mimi au kuna mwingine?" Seynabou hakukubaliana na maneno ya Gidion.
" Dada yangu elewa kuna Diamond Platnumz mmoja tu Barani Afrika kama huamini tulia tukifika ndiyo unihukumu mambo yakiwa tofauti." Gidion alimjibu.

" Labda ngoja tufike." Seynabou alikubali kwa shingo upande.
" Kwani wewe Seynabou huyo sijui Platnumz unamfahamu?" Catherine alimuuliza Seynabou.
" Simfahamu kwa kumuona 'live' bali huwa namuona kwenye Televisheni tu." Seynabou alimjibu.

"Basi leo ndiyo siku yako ya kumuona macho kwa macho Nyota kutoka Afrika Mashariki." Gidion alikandamizia zaidi na muda wote huo Adoyee alikuwa bize na muziki 'earphones' zikiwa masikioni hasikii chochote kile kinachoendelea.

BILA SHAKA TUMESAFIRI PAMOJA MSOMAJI WANGU BILA TATIZO LOLOTE WALA KIKWAZO KUTOKEA, JE NI NINI KITATOKEA HUKO TRAVIS MARK HOTEL?

UNGANA NAMI KATIKA SEHEMU INAYOFUATA UPATE KUJUA NI NANI MASTER PLAN WAKO.

PicsArt_11-08-01.31.04.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

"Tumeshafika tayari hapa ndiyo TRAVIS MARK HOTEL." Gidion Michael aliwaambia wakina Catherine.

"Oohh kumbe ndiyo hapa eee?" Catherine aliuliza.

"Ndiyo dada." Gidion alimjibu Catherine akipaki gari lake ndani ya maegesho ya Hotel ya TRAVIS MARK HOTEL.

"Tunashukuru sana kwa msaada wako na Mungu akubariki." Catherine alimshukuru Gidion.

"Usijali dada yangu kwa sasa ninyi ni zangu na hii hapa ni kadi yangu yenye mawasiliano yote." Gidion

Alimkabidhi kadi Catherine ambaye ni alishashuka chini macho yakiwa kwa watu wanaoingia na kutoka ndani ya Hotel hiyo.

"Okay Gidion tutawasiliana, tungependa kuambatana nawe lakini kuna mtu tumekuja kumuona hapa." Catherine alimjibu akiwapa ishara wakina Adoyee wamfuate.

"Bila shaka ndugu zangu." Gidion alimjibu Catherine akiziweka sawa 'site mirror' za gari lake huku wakina Catherine wakipanda ngazi kuelekea ndani ya Hoteli.

"Mjomba ndiyo tunaingia hapa Hotelini." Catherine alimwambia mjomba wake baada ya kumpigia simu na kuipokea.

"Mkifika hapo mapokezi msiondoke nakuja sasa hivi." Mzee Malick Bolenge alimuelekeza Catherine.
"Ndiyo tuko hapa mapokezi."

Catherine alimjibu mjomba wake.
"Dakika sifuri niko hapo mjomba wangu." Mzee Malick alimjibu na kukata simu. Hata dakika nne hazikuisha mzee Malick Bolenge alifika pale mapokezi na kukutana nao.

"Nifuateni huku." Mzee Malick aliwaambia wakina Catherine wamfuate na baada ya kuingia kwenye chumba kimoja ambacho kiko ghorofa ya tatu mzee Malick aliwaeleza kitu ambacho Catherine hakukitarajia hata chembe na kisha alitaka kujua zaidi ya kutekwa kwa wakina Jumbe.

"Catherine hii ni Hotel yangu japo wengi hawajui hicho na hii ndiyo ofisi yangu ambayo huwa naitumia kufanya mambo yangu mengi ya kibiashara lakini nikiwa kama mteja na..."

"Subiri kwanza Mjomba unataka kusema hili Hotel ni lako au umeamua tu kunipandisha presha?" Catherine alimuuliza mjomba wake.

"Mjomba, Mjomba hivi toka lini nikakudanganya? Hii ni Hotel yetu na labda tu nikwambie hii ni moja ya vitega uchumi vyangu lukuki vilivyo hapa nchini Senegal kwa muda huu tuachane na hili kwanza tuzungumzie uliloniambia." Mzee Malick Bolenge alimjibu Catherine huku akiiweka simu sikioni.

" Njoo ofisini kwangu mara moja." Aliongea na simu kisha akaikata na kumgeukia Catherine.

" Ndiyo Mjomba nakusikiliza."

"Kama nilivyokuambia Mjomba watu wangu wametekwa huko porini na watekaji wanataka paundi milioni moja na wanazihitaji leo hii hii mchana hapa kichwa kinaniuma Mjomba sijui nitazitoa wapi hizo hela kwa masaa machache hivi." Catherine alimweleza Mjomba wake kila kitu juu ya kilichotokea.

" Mhh ilikuwaje mpaka wakatekwa?" Mzee Malick alimuuliza Catherine.
" Yaani Mjomba sijui nikujibu vipi swali lako maana hata mimi naumiza kichwa hivyo hivyo."

" Naam Bosi." Alikuja mmoja wa wahudumu wa ile Hotel.

"Wahudumie wageni wangu hapa." Mzee Malick aliagiza.

"Karibuni niwahudumie tafadhali."
"Mimi nitakula baadaye niombe maji tu ya baridi." Catherine alimjibu.

"Mimi naomba Wali mkavu ulioungwa nazi pamoja na juisi ya nanasi." Adoyee aliagiza menyu yake.

"Kwa upande wangu mimi niletee kuku nusu na Coca Cola ya baridi usisahau na pilipili eee."

"Vinakuja mara moja." Mhudumu alijibu na kuondoka.

Baada ya mhudumu wa Hotel kuondoka Catherine alimgeukia mjomba wake.

"Wewe ni kiboko yaani mjengo kama huu hakuna anayejua? Au nilibaki mimi tu kujua?" Alimuuliza.

"Tena una bahati Mjomba hakuna anayejua zaidi yako na rafiki zako hawa mpaka nimefanya hivi mjue nimewaamini sana hivyo hakikisheni kila mlichokisikia hapa kinabaki hapa hapa." Mzee Malick alitoa tahadhari.

"Kuhusu hilo ondoa shaka Mjomba wangu na kuwahusu hawa nikutoe wasiwasi hawana tabia za kimbea ni watu makini sana." Catherine
alimuondoa wasiwasi mjomba wake juu ya kuvuja kwa siri zake.

"Okay nimekuelewa mjomba wangu sasa juu ya hili la watekaji naomba nikuahidi kuwa vijana wako wote tutawaokoa na hao watekaji hawataambulia hata shilingi mbovu."

"Kweli Mjomba?" Catherine alimuuliza Mjomba.
"Kweli ndiyo au hauamini?"
"Nakuamini mjomba na ndiyo maana niko hapa."

Mhudumu alikuja akiwa menyu yote aliyoagizwa na wakina Seynabou.
"Karibuni mfurahie huduma zetu kutoka hapa TRAVIS MARK HOTEL ambapo siku zote tunasema 'Tuko Tayari kukuhudumia mteja wetu' muda wowote."

" Tunashukuru sana dada." Alimjibu Adoyee kwa niaba ya wenzake.
" Rachel utaniletea Kande zangu kama ziko tayari."

" Sawa bosi." Mhudumu alijibu na kutoka zake.

" Namba yao kama uliikamata wapigie ukiwaambia kuwa uko tayari kutoa kiasi hicho cha fedha ili tujue plani yao ni ipi."

"Walinitajia ninayo hapa wacha niwapigie." Catherine alimjibu huku akiinuka na kuelekea dirishani simu ikiwa tayari sikioni. Lakini wakati akiwa anaisikilizia simu ipokelewe upande wa pili Catherine kuna kitu aliweza kukiona kule chini akamwita Mjomba wake na kumuonesha kitu.

" Yule mtu pale chini ni nani? Na unaweza ukawa unamfahamu?" Alimuuliza.

"Nani Gidion? Kwa nchi hii ya Senegal ni nani asiyemjua huyo kwa utajiri alionao?" Mzee Malick alimjibu.
"Ana hela ndefu eee?" Catherine alimuuliza tena.

"Hebu ongea na hao kwanza huyo mwingine huko chini achana naye muda ni mali." Mzee Malick alimsisitiza baada ya kuona Catherine anataka kuchanganya masuala.

"Sawa Mjomba lakini huyu mtu nina mashaka naye sana unajua nini?" Catherine alimuuliza Mjomba wake.

"Hata mimi nina mashaka naye pia si unakumbuka alituambia kuwa ndani ya Hotel hii kutakuwa na Onesho kubwa la Muziki kutoka kwa msanii maarufu ambaye kila nchi ingejivunia kuwa naye lakini toka tumeingia humu hotelini hata shangwe lenyewe sijalisikia." Seynabou aliongeza baada ya kusogea pale dirishani na kumuona Gidion.

" Kuna onesho hapa? Onesho gani hilo na ni la msanii gani huyo?" Mzee Malick Bolenge aliuliza baada ya kupata habari ambayo si ya kweli ukizingatia Hotel yake haijawahi kujishughulisha na maonesho ya aina yoyote ile toka ainunue Hotel hiyo kutoka kwa mfanyabiashara maarufu kutoka nchini Kenya aitwaye Onyango Keuthi ambaye alifanya hivyo baada ya kufilisika na kuamua kurejea nchini kwao kujipanga na kuanza upya.

"Ndiyo, na alisema kuwa ni la Mwanamuziki aitwaye Diamond Platnumz kutoka nchini Tanzania sasa ukiwa kama mmiliki wa Hotel hii mbona unashangaa?" Catherine alimuuliza Mjomba wake.

"Mjomba nashangaa ndiyo sababu hii Hotel kama mlivyoiona wenyewe haijawahi kufanya shughuli hizo labda huko mbeleni lakini siyo kwa sasa.

Adoyee nenda kule chini kwa kupitia mlango wa nyuma ambao mhudumu wa mapokezi atakuonesha mfuatilie Gidion tujue anatafuta nini halafu na wewe Mjomba watu wako wanasemaje?"

" Kiukweli hawapokei simu labda watapiga wenyewe wacha tuwasubiri kidogo."

"Hakuna haja ya kusubiri wacha tucheze nao mchezo mzuri ambao hawatausahau maishani mwao, nifuateni huku." Mzee Malick aliwaambia wamfuate huku Adoyee akiwa tayari nje ya Hotel akimfuatilia Gidion ambaye alikuwa bize akiongea na simu huku mkononi akiwa na chupa kubwa ya maji. Waliingia mpaka kwenye chumba ambacho kilikuwa na Kompyuta nyingi sana huku vijana wawili waliowakuta mle wakiwa bize nazo inawezekana hawa walikuwa wataalam wa hizo Kompyuta.

"Vijana wangu kwanza poleni na kazi, itafuteni namba fulani kwenye 'Mark finder' mara moja." Mzee Malick alitoa maagizo akiketi kwenye kiti ambacho kilionekana dhahiri huwa hakikaliwi na yeyote zaidi yake kwa namna kilivyokuwa tofauti na vingine.

"Tunaiomba hiyo namba mkuu." Mmoja wa wale vijana aliiomba.
"Catherine wapatie ile ya maumbwa pori."

"Sawa Mjomba." Catherine alimjibu akimsogelea huyo kijana ili amkabidhi hiyo namba.

***

"Samahani binti." Mchungaji alimuita mhudumu wa ndege aliyekuwa akipita karibu yake.

"Karibu Bosi kwa huduma." Mhudumu huyo alimkaribisha.
"Naomba uniletee juisi ya limao tafadhali." Mchungaji aliagiza.
"Umeipata Bosi wangu si unajua kwetu mteja ni Mfalme japo hana Miliki." Mhudumu alimjibu akielekea kufuata.

"Hii ni kali ya mwaka yaani leo hii nakwenda kuishi ugenini? Kisa huyu muuaji muoga asiyejitokeza hadharani?" Mchungaji alijisemesha mwenyewe na muda huo ndege hiyo ilikuwa juu ya anga la nchi ya mzee Magufuli, kiongozi aliyejipatia Umaarufu hivi karibuni baada ya kufanya maamuzi magumu ya kuwataka Watanzania kuendelea na shughuli za uzalishaji Mali pasipo kuliogopa gonjwa hatari la COVID-19 linalo isumbua dunia baada ya kuua mamilioni ya watu.

Akiwa anasubiri juisi yake aliyomuagiza mhudumu wa ndege mara kuna ujumbe ukaingia kwenye simu yake, hivyo akaufungua na kuusoma.

"Mchungaji Rodney unatafutwa na jeshi la Ulinzi la hapa Senegal kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya watu kadhaa ambao asilimia kubwa ni waumini wa kanisa lako la JESUS OUR KING.

Kwa kukukumbusha tu nafikiri unawakumbuka wafuatao; Kijana wako Bartholomew, mama Jennifer mke wa Otago Mathew, Askari wa Doria mpaka wa Casamance, vijana wawili waliouawa huko Casamance mmoja akiwa ni 'Inspector' wa Jeshi la Polisi na kama haitoshi kuna watu wawili hawajulikani walipo mpaka sasa ambao ni Mama Mchungaji 'Catherine' na mlinzi wenu 'Adoyee' na hujaripoti kituo chochote cha Polisi pia kuna tetesi za kuuawa kwa rafiki yako Mganga wa Tiba za Asili mzee Alioune huku mtoto wake hajulikani aliko mpaka sasa, matukio haya yote yanaunganishwa pamoja kutokana na kupotea na kuuawa kwa Waumini wako miaka zaidi ya kumi na mbili iliyopita. Na vipi kuhusu miili ya vijana watatu iliyokutwa Kanisani kwako ni nani anayehusika?

KULIKONI TANZANIA TENA MCHUNGAJI RODNEY? JE UNAFIKIRI UJUMBE HUO UMETUMWA NA NANI?

TUKUTANE NDANI YA SEHEMU YA KUMI NA MOJA YA KIGONGO HIKI CHA MUUAJI MWENYE BARAKOA TUPATE MAJIBU YA MASWALI YETU.

PicsArt_11-08-01.31.34.jpg
 
Sultan Uwezo
+255

Ni ujumbe ulioingia kwenye simu yake na kumfanya Mchungaji kutokwa na jasho mfululizo huku macho yakirudia mara mbili mbili kuusoma ujumbe huo. Na hata alipokuja yule mhudumu kumletea juisi aliyoagiza hakuweza kumuona hata kidogo.
" Karibu mheshimiwa." Alikaribishwa.
"Unasemaje?" Aliuliza kwa kufoka.
"Nimekuletea juisi yako bosi." Yule mhudumu alijibu.
"Oohh sorry binti, nashukuru sana." Alimjibu akiichukua ile glasi na kuikata yote kisha akairudisha ile glasi kwenye trei, tukio lile lilimshangaza sana yule mhudumu.
"Unanidai shilingi ngapi?" Alimuuliza.
"Hapana hiyo ni moja ya huduma zetu ndani ya SERENGETI AIRWAYS." Mhudumu alimjibu huku akiwa bado anamshangaa Mchungaji Rodney.
"Okay kazi njema." Mchungaji alimuondoa kijanja mhudumu.
"Asante, lakini ni kama kuna tatizo hivi, naweza kukusaidia?" Alimuuliza kabla ya kuondoka.
"Nikiwa na tatizo nitakuiteni binti sawa?" Mchungaji alimjibu.
"Sawa Bosi." Mhudumu alimjibu na kuondoka.
"Ni nani aliyeutuma ujumbe huu Mungu wangu mbona majanga yananiandana kiasi hiki?" Mchungaji alijiuliza maswali huku akijitahidi kulitafuta jina la mtuma 'Email' hiyo ambayo haikuwa na jina wala anuani ya mtumaji.
"Abiria wetu awali ya yote nipende kumshukuru Mungu mwingi wa Rehema kwa kutufikisha salama na pili niwashukuru ninyi Wafalme wetu kwa kulichagua Shirika letu la SERENGETI AIRWAYS kuwa chombo chenu cha Usafiri. Tunashukuru sana na Karibuni tena wakati mwingine. NAWAOMBENI FUNGENI MIKANDA NDEGE INAJIANDAA KUSHUKA, ASANTENI." Ilikuwa ni sauti Nyororo ya Mhudumu wa kike wa ndege hiyo ndiyo iliyomtoa Mchungaji kutoka kwenye lindi la mawazo.
" Shabashi!! Ndiyo kusema tumeshawasili jijini Dar Es Salaam - Tanzania?" Alijiuliza Mchungaji.
" Ndiyo tumeshafika tayari." Bibi aliyekuwa karibu yake alimjibu.
"Hee ina maana nimeongea kwa sauti mpaka huyu bibi anijibu." Alijiuliza Mchungaji baada ya kuona bibi aliyekuwa siti ya jirani yake akimjibu wakati yeye hakumbuki kama aliongea kwa sauti. Baada ya ndege kusimama alimshukuru Mungu wake kwa kumfikisha salama safari yake kisha aliungana na abiria wenzake kushuka. Alipochukua mizigo yake alitoka eneo lile la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akivuta begi lake huku macho yake yakiwa huku na kule kuona kama anaweza kumuona mwenyeji wake Daktari Sylvester Kitesa lakini hakuweza kumuona hivyo akaendelea kuvuta begi lake mpaka pale alipoweza kumuona mtu akimpungia mkono, alimtazama kwa muda mtu huyo aliyekuwa mbali kidogo na alipokuwa yeye hivyo aliona isiwe shida akaitoa simu yake na kumpigia.
"Vuka ng'ambo ya pili hapa ninapokupungia mkono Mchungaji." Daktari Sylvester Kitesa alimwelekeza baada ya kupokea simu.
"Sawa mzee."Mchungaji alimjibu huku akiangalia huku na kule kabla ya kuvuka na kama bahati vile alimuona akiwa karibu zaidi na gari aina ya Prado 2500LX ya mwaka 2020. Hivyo alivuka haraka huku sura yake ikiwa imepambwa na tabasamu na hii ni baada ya kumuona mwenyeji wake.
"Karibu Tanzania kijana wangu." Daktari Sylvester Kitesa alimkaribisha Mchungaji Rodney akimpokea begi.
"Nashukuru sana mzee wangu, nafurahi kuwa ndani ya nchi yenye historia ya kipekee duniani." Mchungaji alimjibu.
"Hii ndiyo nchi ya mzee wetu mpendwa rafiki wa wanyonge lakini pia mwenye hofu ya Mungu Mheshimiwa John Pombe Magufuli." Mzee Kitesa aliendelea kumtamanisha Mchungaji Rodney.
"Najiona niko Ulimwengu mwingine kabisa mzee wangu, yaani huko nyumbani mpaka kwenye Ndege nikiwa nakuja huku pua zetu na midomo ni mwendo wa Barakoa tu lakini cha ajabu toka nashuka kwenye Ndege mpaka hapa tulipo sijamuona mtu yeyote akiwa na Barakoa kaivaa. Ninachojiuliza hii Tanzania iko Ulimwengu gani maana nchi zote zilizo Duniani zinapambana na gonjwa hili la Covid-19 huku maelfu kwa maelfu wakiendelea kupoteza maisha."
" Kwanza kabisa niwape pole kwa yanayoendelea nchini kwenu katika kufanikisha mapambano dhidi ya Covid-19 pia na yote yaliyoikumba familia yako pamoja na Kanisa kwa ujumla wake." Daktari Sylvester Kitesa alimpa pole.
"Hatujapoa mzee wangu vita vinaendelea lakini yote kwa yote tumemkabidhi Mwenyezi Mungu." Mchungaji Rodney alimjibu. Mazungumzo yalikuwa yakiendelea kati yao huku gari likiwa linakata mitaa kutoka nje ya uwanja wa Ndege. Walipofika nje ya jengo moja refu hivi lililokuwa limeandikwa TROPICANA PLAZA mzee Kitesa alisimamisha gari kisha akamgeukia Mchungaji Rodney. "Sasa kijana wangu nisubiri mara moja nimchukue Mchungaji Tumaini Kalulanzi humu ndani." Mchungaji Rodney aliliangalia jengo hilo lililokuwa na ghorofa kama kumi na tatu kisha akamjibu Daktari Sylvester Kitesa.
"Sawa mzee wangu."
Macho ya Mchungaji Rodney yalikuwa kwa Daktari Sylvester Kitesa aliyekuwa akipanda ngazi kuelekea ndani ya jengo hilo. Akiwa kwenye tafakari mara simu yake iliita akaichukua na kuipokea.
"Bwana Yesu asifiwe Mchungaji." Upande wa pili wa simu ulianza na salamu.
"Amina mzee Lusoka, kwema huko?" Mchungaji alimjibu na kumuuliza.
"Kwema? Yaani unauliza kabisa Mchungaji wangu kana kwamba hujui kilichotokea huku?" Aliuliza mzee Lusoka.
"Mzee wangu unafahamu vizuri ninavyokuheshimu na si hivyo tu bali kwa umoja wetu tumefanya mengi sana lakini siku za hivi karibuni umekuwa kikwazo kwangu kwa hilo sipendi kabisa, ninachokitaka kwa sasa ni amani tu na si vinginevyo." Mchungaji alimfungukia mzee Lusoka
" Mchungaji samahani sijakupigia simu kwa ajili ya hilo." Mzee Lusoka alimkatisha.
" Enhh nakusikiliza." Mchungaji aliongea.
"Inspekta wa Jeshi la Polisi akiwa kaongozana na viongozi wengine wa Kiserikali akiwemo Mwenyekiti wa Mtaa huu wamefika kwa mahojiano juu ya tukio la miili iliyokutwa jalalani kwetu hivyo wameniomba nikuite maana Inspekta kakupigia simu mara kadhaa haupatikani." Mzee Lusoka alimjibu kwa kutoa taarifa hiyo.
" Si muwaambie kuwa hata sisi tumeikuta hapo hapo!!" Mchungaji Rodney alimjibu kisha aliikata simu na kuizima kabisa.
" Wanautani na mimi hawa yaani nijitokeze kwa suala kama hili naumwa? Na hata ningekuwa mzima bado nisingekwenda huko." Mchungaji alijisemesha mwenyewe. Na muda huo huo mzee Kitesa akiwa na Mchungaji Tumaini Kalulanzi walifika na kuingia garini.
"Tulikutelekeza Mchungaji?" Mzee Sylvester Kitesa alimuuliza akikaa vizuri kitini.
"Hapana baba."
"Bwana Yesu asifiwe Mtumishi." Mchungaji Tumaini Kalulanzi alimsalimu Mchungaji Rodney.
"Amina kiongozi, poleni na Majukumu." Mchungaji Rodney alimjibu.

Baada ya hapo waliondoka huku nyuma ya usukani akiwa Mchungaji Tumaini Kalulanzi ambaye naye ni Mchungaji wa Kanisa hilo la JESUS OUR KING mkoani Morogoro. Na hata hilo gari ni mali yake Daktari Kitesa alilitumia tu mara baada ya Mchungaji Rodney kumtaarifu kuwa yuko ndani ya Tanzania hivyo aliona aazime.
"Mchungaji tulikuwa na kikao cha kazi ndani ya jiji la Dar es Salaam kwa lengo la kutanua huduma nchini Tanzania. Ni baada ya kuona mikoa ambayo tumeifikia inafanya vizuri hivyo tukaona tuyafanyie kazi maombi ya Wasikilizaji wetu ambao wameomba tufikishe huduma mikoani mwao." Mzee Kitesa alimfafanulia.
" Ina maana mahubiri yenu huyatoa kwa njia ya redio?" Mchungaji Rodney aliuliza.
" Ndiyo na si hivyo tu tuliamua kuitumia mitandao ya kijamii kufikisha huduma zetu ikiwa ni pamoja na mtandao wa Facebook, Twitter, YouTube bila kusahau Instagram ambako kuna kundi kubwa la vijana na kwa kupitia hizo 'platforms' tumeweza kufanya vizuri na ndiyo maana tulikuwa jijini Dar es Salaam ndani ya Ukumbi wa TROPICANA PLAZA." Daktari Sylvester Kitesa alimjibu.
" Hongereni sana kwa hilo natamani hata kwetu lingefanyika hili."
" Hamjachelewa muda bado mnao kikubwa ni mikakati tu Mchungaji." Mchungaji Tumaini Kalulanzi aliongeza.
" Tutakuwa Morogoro kwa muda wa siku mbili kisha tutaelekea jijini Mbeya." Daktari Sylvester Kitesa alimwambia Mchungaji ambaye mawazo yalimsonga mara baada ya kupokea ujumbe wa Mwenyekiti wa Bodi kanisani kwake Dr Brown Lutasya uliosomeka kama ifuatavyo : " Mchungaji unasubiriwa hapa na viongozi kutoka Serikalini wanataka kuongea na wewe juu ya mauaji yasiyoisha hapa Kanisani. Hivyo fanya haraka kiongozi." Ujumbe huu uliingia mara baada ya kuiwasha simu yake ambayo aliizima muda mfupi uliopita.

JE NI NINI KITATOKEA KATIKA KITIMUTIMU HIKI?

TAFADHALI UNGANA NAMI KATIKA SEHEMU INAYOFUATA TUJUE NINI KILICHOJIRI.

1607534661335.jpg
 
MUUAJI MWENYE BARAKOA - 13
Sultan Uwezo
+255

"Hili balaa mbona naandamwa na mikosi kiasi hiki lakini? Kwamba niwaambie ukweli kuwa nimeondoka nchini? Hapana hiyo ni ngumu kwangu." Mchungaji Rodney aliendelea kuwaza wakati wenyeji wake wakijadili yale waliyoazimia kikaoni. Safari iliendelea na muda huo walikuwa wakikaribia kuingia mkoani Morogoro.
" Mtumishi unaouona mbele ni mkoa wetu wa Morogoro ambao una historia kubwa sana ndani ya bara letu la Afrika." Mchungaji Tumaini Kalulanzi alimuonesha mgeni wao aliyekuwa ndani ya dimbwi la mawazo.
"Panaonekana pazuri sana." Mchungaji Rodney alimjibu.
"Ni mji mzuri kwa siku hizi mbili utauona uzuri wake wewe mwenyewe."
"Nitashukuru sana kaka." Mchungaji alimjibu. Na muda huo walikuwa wakiingia ndani ya jengo lililoko ndani ya Kanisa kubwa lenye maandishi makubwa yaliyoandikwa JESUS OUR KING (JOK) na gari lilikwenda na kusimama sehemu ambayo ina magari mengine mawili madogo na kusimama.
" Karibuni sana Viongozi." Mchungaji Tumaini Kalulanzi aliwakaribisha wageni wake.
"Tunashukuru sana Mtumishi." Mzee Sylvester Kitesa alimjibu huku akimpa ishara ya kuteremka Mchungaji Rodney. Walishuka na kulakiwa na mama Mchungaji Bi Silvia Kalulanzi.
"Karibuni sana."
"Asante shemeji." Mchungaji Rodney alimjibu macho yakiwa kwenye mazingira.
"Kaka hongera sana kwa kunogesha mazingira yako ya Kanisa na nyumbani pia." Hakuacha kumsifia mwenyeji wake.
"Nashukuru sana ndugu yangu si unajua tena majukumu yetu?" Alimjibu. Na wakati huo huo mzee Sylvester Kitesa alikuwa akiongea na simu.

***

Mmoja wa wale vijana alipoichukua ile namba alikwenda kuiingiza kwenye system na kufanya kama bosi wao mzee Malick alivyowaelekeza. Lakini wakati yule kijana akianza kutafuta eneo inakopatikana hiyo namba mara simu yake ilipata ujumbe mfupi uliomfanya yule kijana aukague hasa baada ya kuliona jina la mtumaji. "NI VIJANA WETU HIVYO TAFUTA UONGO WENYE MATUMAINI KWAO." Alipomaliza kuusoma alimgeukia mzee Malick Bolenge na kumpiga ukope kisha akaiweka mfukoni simu yake na kuendelea na shughuli ambayo alishaianza huku ikiwa ni nyepesi zaidi hasa baada ya kupewa muongozo na bosi wake. Wakati huo Catherine alikuwa bize kwenye simu akiwa hana wasiwasi na wenyeji wake ukizingatia mzee Malick Bolenge ni mjomba wake wa damu na si wa mkopo. Na baada ya kumaliza kile ambacho alikuwa akikifanya alimfuata Mjomba wake alipokuwa kaketi kisha naye alivuta kiti kilichokuwa karibu na kuketi.
"Mjomba tunaweza kuongea?" Catherine alimuuliza mjomba wake.
"Bila shaka tunaweza." Mzee Malick alimjibu.
"Nashukuru mjomba wangu, unajua nini hatujapata muda wa kuongea maana toka tumefika ni pilika tu." Catherine alimwambia mjomba wake.
"Ni kweli kabisa lakini bado tuna muda wa kufanya hivyo mjomba wangu." Alimjibu
"Haswaa...." Lakini kabla hajaendelea kuna ujumbe uliingia kwenye simu yake na kuusoma.
"Huyu Gidion si wa kawaida kwani ni kama kashtukia hivi, kaondoka haraka." Alipomaliza kuusoma alimjibu.
"Kama umemuona jaribu kumfuatilia mpaka tumfahamu ni nani." Alipoutuma aliiweka mfukoni simu yake na kusogea karibu na Mjomba wake.
"Unafuatiliwa mpige chenga huyo Kima kisha mvizie na kumkausha damu yake." Mzee Malick akiwa bize kumalizia kuandika ujumbe wake hakumuona Catherine aliyefika na kuusoma ujumbe ule uliompa mashaka na baada ya kubaini hajaonwa na mjomba wake alirudi nyuma kidogo kisha akainuka na kumfuata kijana aliyemkabishi ile namba.
" Kaka yangu kuna uwezekano wa kubaini eneo walipo?" Alimuuliza.
"Mpaka sasa sijapata signo yoyote ile labda wacha niendelee kuitafuta." Kijana huyo alimjibu. Majibu ya kijana huyu yalimpa mashaka kidogo kiasi cha kuanza kumtilia mashaka mjomba wake.
"Ok sawa jitahidi mdogo wangu ni muhimu sana." Catherine alimjibu.
"Mjomba nakuja mara moja." Catherine alimwambia mjomba wake baada ya kumkuta akiwa katulia akichezea vidole vyake.
"Sawa mjomba." Mzee Malick alimjibu. Hivyo Catherine aliinuka na kuondoka kuelekea viliko vyoo vya ile ofisi ambako aliingia na alipoufunga mlango vizuri aliitoa simu yake na kwenda sehemu ya ujumbe mfupi huko alimuandikia 'text' Adoyee.
"Geuka haraka sana hali si shwari achana naye huyo rudi tuangalie namna ya kujinasua mtegoni." Hakutaka kusubiri majibu aliifuata koki ya bomba la maji na kuyafungulia kwa nguvu huku mkono ukiwa kwenye hayo maji ya baridi.
" Inawezekana huu mchezo ni wa mjomba ee? Na ndiyo maana asubuhi tu mtu katuacha nyumbani kumbe alikuwa na lake jambo, nitamnasa tu we ngoja tu." Catherine alijiuliza maswali yaliyomchanganya kichwa baada ya kubaini kuwa anaishi na mtu mwenye nia ovu juu yao. Kabla hajatoka mle chooni alimpigia Seynabou simu ili kumpa tahadhari.
" Uko wapi wewe?" Catherine alimuuliza Seynabou.
" Naongea na simu hapa nje vipi nije?" Alimuuliza.
"Naomba unisikilize mdogo wangu, huku ndani si shwari hivyo usirudi wasiliana na Adoyee mjue namna ya kujinasua mtegoni mimi kwa sasa nimenasa sijui kama nitatoka salama kwenye huu mtego." Wakati Seynabou akitaka kumuuliza swali Catherine alishakata simu baada ya kuhisi minyatio nje ya choo, aliizima simu na kuiweka kwenye mfuko wa ndani ya tracksuit yake badala ya kwenye kipochi chake kisha akaufungua mlango na kutoka nje ambapo moja kwa moja alirudi na kumkuta Mjomba wake akiwa anajadiliana jambo na vijana wake, Hivyo hakutaka kuwaingilia alivuta kiti na kuketi huku masikio akiwa kayategesha kiaina kunasa wanachoteta pale lakini hakuweza kusikia chochote.
"Mjomba uko poa?" Mzee Malick alimuuliza Catherine.
"Niko sawa kabisa Mjomba kwanini umeuliza hivyo?" Catherine aliuliza.
"Nimeona umechukua muda mrefu chooni nikapata wasiwasi kidogo." Alimjibu.
"Hapana Mjomba wangu mazingira ya kule yalinifanya niweze kufanya mambo yangu mengine kwa utulivu kabisa si unajua tena wanasema mazingira mazuri ya chooni humfanya mtu kupata utulivu wa akili ambao hupelekea kuanza kupanga mikakati bila shaka yoyote." Catherine alimjibu mjomba wake.
" Hilo hata mimi niliwahi kulisikia lakini bado sijaukubali hata kidogo." Mjomba wake aliongeza.
" Mimi ni shuhuda mzuri katika hili kwani mambo yangu mengi yamefanyika katika mazingira haya ya maliwatoni na matokeo chanya nimeyaona." Catherine aliitetea hoja yake akiinuka kuwafuata vijana aliowakabidhi ile namba.
" Vipi hamjafanikiwa bado?" Aliwauliza.
" Tumefanikiwa kunasa sehemu ambayo mpigaji alikuwa kama saa moja na nusu lililopita, angalia hapa kwenye doti hii ya kijani." Kijana yule alimjibu.
"Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa wanaweza kuwa karibu na hili eneo?" Catherine alimuuliza swali kijana huyu huku akiwa makini kumfuatilia machoni kama ana kiashiria chochote cha hatari.
"Nahisi hivyo dada japo sina uhakika maana signo imepotea kabisa." Alimjibu.
"Na ninachoweza kushauri hapa ni kulifuatilia eneo hili maana sina uhakika kama wameondoka haraka hivyo ikiwa hawajui kama tunawaguatilia huku." Kijana mwingine alichangia wazo lake.
"Ngoja niwasiliane na Mjomba kwanza tujue la kufanya." Catherine alimjibu akimfuata mjomba wake aliyekuwa akiongea na mmoja wa wafanyakazi wa ile Hotel.
"Samahani Mjomba hii ndiyo mida yenye ya kuwasiliana na watekaji tunafanyaje?" Catherine aliwakatisha na kuuliza swali.
"Si umeiona ile signo ya saa moja nyuma?" Mzee Malick alimuuliza.
"Nimeiona."
"Nimeshaagiza dereva alete gari yangu ya kazi ili tuelekee huko maana ni eneo la kilometa zaidi ya arobaini na saba kama zilivyoonekana kwenye king'amuzi chetu." Mzee Malick alimjibu.
"Sawa Mjomba lakini tunakwenda kufanya nini ilhali sina kiasi cha fedha wanachokitaka hao watekaji." Catherine alikubaliana naye lakini akaonesha shaka yake.
"Ondoa shaka mjomba hao watekaji hawataamini kwani tunakwenda kuwakomboa mateka bila kutoa hata kumi moja, cha kufanya waambie vijana wako wajiandae kwa safari." Mzee Malick alimpa jibu ambalo lilimfanya atabasamu, si kwamba alilifurahia hili bali alikuwa akimhadaa mjomba wake asimshtukie kwenye mpango wake alioupanga. Baada ya majadiliano mzee Malick Bolenge alimwambia Catherine amsubiri nje ili amalizie maongezi na mfanyakazi wake ndipo waianze safari, Catherine alikubali na kutoka nje ya ile ofisi ya mjomba wake kuwaacha wamalizie mipango yao lakini pale nje alikutana na mazingira ambayo yalimfanya ahisi hatari kwani walikuwa ni vijana watatu waliokuwa wamevalia miwani ya rangi nyeusi huku t-shirt zao zikiwa za rangi ya blue zenye maandishi meupe yaliyosomeka 'SULTAN UWEZO' suruali zao za jinsi zikiwa nyeusi na chini wakiwa ndani ya buti nyeusi zenye asili ya Marekani. Watu hawa wenye miili iliyojengeka vizuri kimazoezi walikuwa karibu zaidi na mlango wa ofisi ya mjomba wake.
"Ohooo mambo yamekuwa mambo hapa, nisipokuwa makini nalamba mchanga." Catherine aliwaza akiwatazama watu wale. Wakati bado anaendelea kuwashangaa watu wale pale nje Mjomba wake alitoka na kumtaka waondoke.
"Sawa mjomba." Catherine alimjibu mjomba wake huku macho yakiwa kwa wale vijana.

JE UNAFIKIRI NINI KINAKWENDA KUTOKEA?

KAA KARIBU NAMI TUENDELEE KUIFUATILIA HADITHI HII MPAKA MWISHO.
1607534661335.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom