Mutahabwa: Kutokuwapo kwa upendo kati ya Mwanafunzi na Mwalimu wa Hisabati huchangia Wanafunzi kufeli

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
KAMISHNA wa Elimu, Dk. Lyabwene Mutahabwa, ametaja sababu za wanafunzi kufanya vibaya somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ikiwamo mazingira ya ufundishaji kutokuwa rafiki na wezeshi.

Sababu nyingine, amesema ni kutokuwapo kwa upendo kati ya mwanafunzi na mwalimu wa somo hilo, hali inayoweka uwoga wa kulielewa somo hilo.

Alibainisha hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa miongozo minne ya kufundishia elimu ya stadi za maisha kwa kuzingatia afya ya uzazi, Virusi vya Ukimwi (VVU), jinsia na kuhusiana kwa heshima kwa walimu wa shule za msingi na sekondari, iliyoandaliwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

"Mlisikia juzi matokeo ya kidato cha nne katika somo la Hisabati yalikuwa si mazuri. Nimefuatilia katika baadhi ya shule nimekuta hivi, mwalimu akitoa hesabu 10 anakuwa na mzigo wa fimbo, mwanafunzi atakayekosa hesabu tano atachapwa viboko vitano, akikosa hesabu tatu atachapwa fimbo tatu. Yaani unapigwa fimbo kulingana na idadi ya hesabu ulizokosa,” alisema.

Dk. Mutahabwa alisema endapo kuna mwalimu mwenye dhana kwamba anapofundisha akitumia fimbo inasaidia kumjaza akili mwanafunzi, atakuwa anajidanganya na kwamba ualimu hauko hivyo.

Aliwashauri walimu wanaofundisha somo la Hisabati kuwa na ushirikiano, upendo na kuwa tayari wakati wote kuwasaidia wanafunzi. Alisema kwa kufanya hivyo, wanafunzi wengi watafaulu somo hilo.

Alibainisha kwamba utafiti umeonyesha kuwa ili mwanafunzi azingatie masomo ya mwalimu anayemfundisha, ni lazima kuwapo na upendo na heshima kati yao ili miaka ijayo mwanafunzi huyo atamani kuwa mwalimu.

“Utafiti umeonyesha kwamba ili mwanafunzi azingatie masomo yake la kwanza ni lazima akupende wewe unayemfundisha. Yaani uwe mfano wa kuigwa kwa wanafunzi, atamani unavyovaa, atamani unavyohusiana na wengine ofisini na jamii,” alisema.

Dk. Mutahabwa alisema endapo mwanafunzi atampenda mwalimu anayemfundisha, atalipenda pia somo husika analofundishwa na kulisoma mara kwa mara.


IppMedia
 
Ni kweli anayosema mchambuzi mimi nilisoma shule ya bweni mwl wangu wa hisabati kidato cha kwanza alikuwa hapendi warokole mi nilikuwa miongoni kwanza alikuwa hanichagui hata nikinyosha mkono zaidi atasema eti mirokole kazi Julia lia na kupiga kelele . Somo la hisabati linahitaji upendo wa juu kuliko masomo mengine mwl amfundishe technique mbalimbali za kugundua swali Upendo ni muhimu sana sana naunga hoja.
 
Ni kweli anachosema lakini shida bado ipo tu kwa mazingira yetu haya. Mimi ni mwalimu wa hesabu,nimejaribu hata kutoa zawadi za madaftari na fedha taslimu lakini bado hazizai matunda. Ila nilipochapa mboko kusema kweli mwaka huo nilipata watoto kadhaa waliofanya vizuri somo langu.
Kwa hiyo mimi nafikiri,mboko inaweza kutumika kama alternative pale ambapo njia ya kwanza na ya pili zimefeli
 
KAMISHNA wa Elimu, Dk. Lyabwene Mutahabwa, ametaja sababu za wanafunzi kufanya vibaya somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ikiwamo mazingira ya ufundishaji kutokuwa rafiki na wezeshi.

Sababu nyingine, amesema ni kutokuwapo kwa upendo kati ya mwanafunzi na mwalimu wa somo hilo, hali inayoweka uwoga wa kulielewa somo hilo.

Alibainisha hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa miongozo minne ya kufundishia elimu ya stadi za maisha kwa kuzingatia afya ya uzazi, Virusi vya Ukimwi (VVU), jinsia na kuhusiana kwa heshima kwa walimu wa shule za msingi na sekondari, iliyoandaliwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

"Mlisikia juzi matokeo ya kidato cha nne katika somo la Hisabati yalikuwa si mazuri. Nimefuatilia katika baadhi ya shule nimekuta hivi, mwalimu akitoa hesabu 10 anakuwa na mzigo wa fimbo, mwanafunzi atakayekosa hesabu tano atachapwa viboko vitano, akikosa hesabu tatu atachapwa fimbo tatu. Yaani unapigwa fimbo kulingana na idadi ya hesabu ulizokosa,” alisema.

Dk. Mutahabwa alisema endapo kuna mwalimu mwenye dhana kwamba anapofundisha akitumia fimbo inasaidia kumjaza akili mwanafunzi, atakuwa anajidanganya na kwamba ualimu hauko hivyo.

Aliwashauri walimu wanaofundisha somo la Hisabati kuwa na ushirikiano, upendo na kuwa tayari wakati wote kuwasaidia wanafunzi. Alisema kwa kufanya hivyo, wanafunzi wengi watafaulu somo hilo.

Alibainisha kwamba utafiti umeonyesha kuwa ili mwanafunzi azingatie masomo ya mwalimu anayemfundisha, ni lazima kuwapo na upendo na heshima kati yao ili miaka ijayo mwanafunzi huyo atamani kuwa mwalimu.

“Utafiti umeonyesha kwamba ili mwanafunzi azingatie masomo yake la kwanza ni lazima akupende wewe unayemfundisha. Yaani uwe mfano wa kuigwa kwa wanafunzi, atamani unavyovaa, atamani unavyohusiana na wengine ofisini na jamii,” alisema.

Dk. Mutahabwa alisema endapo mwanafunzi atampenda mwalimu anayemfundisha, atalipenda pia somo husika analofundishwa na kulisoma mara kwa mara.


IppMedia
Hizo ni hisia zake na majibu ya kisiasa, si matokeo ya utafiti. Ni matokeo ya chanzo ambacho anakwepa kutaja. Sababu kubwa ni msingi mbovu wanao pata watoto kwa somo hilo. Tangu msingi walimu wa somo hilo hawaandaliwi vya kutosha. Walimu hawatoshi, matokeo ni uchache wa vipindi kwa watoto. Wanafunzi ni wengi darasani nalo ni kutomwezesha mwl kutoa majaribio na kazi za nyumbani mara kwa mara. Siasa nayo inachukua muda wa watoto kusoma na kuwashindisha barabarani kuwapokea viongozi.
 
Ni kweli anachosema lakini shida bado ipo tu kwa mazingira yetu haya. Mimi ni mwalimu wa hesabu,nimejaribu hata kutoa zawadi za madaftari na fedha taslimu lakini bado hazizai matunda. Ila nilipochapa mboko kusema kweli mwaka huo nilipata watoto kadhaa waliofanya vizuri somo langu.
Kwa hiyo mimi nafikiri,mboko inaweza kutumika kama alternative pale ambapo njia ya kwanza na ya pili zimefeli
Fundisha, acha mboko. Wengi wa walimu wa hesabu hawaijui hesabu, hawana muda kujifunza kujikumbusha. Siri kubwa ya kujua hesabu ni kucheza nazo. Ni kawaida Mwl wa hesabu kwenye vikundi vya kijamii kutumia calculator kujua makusanyo ya michango ya wanachama wawili. Table za kuzidisha kichwani hazimo.
 
Fundisha, acha mboko. Wengi wa walimu wa hesabu hawaijui hesabu, hawana muda kujifunza kujikumbusha. Siri kubwa ya kujua hesabu ni kucheza nazo. Ni kawaida Mwl wa hesabu kwenye vikundi vya kijamii kutumia calculator kujua makusanyo ya michango ya wanachama wawili. Table za kuzidisha kichwani hazimo.
Hivi na Physics ingekua ni lazima Kwa wote wanapofikia kidato Cha tatu ngekua na maoni gani?
 
KAMISHNA wa Elimu, Dk. Lyabwene Mutahabwa, ametaja sababu za wanafunzi kufanya vibaya somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ikiwamo mazingira ya ufundishaji kutokuwa rafiki na wezeshi.

Sababu nyingine, amesema ni kutokuwapo kwa upendo kati ya mwanafunzi na mwalimu wa somo hilo, hali inayoweka uwoga wa kulielewa somo hilo.

Alibainisha hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa miongozo minne ya kufundishia elimu ya stadi za maisha kwa kuzingatia afya ya uzazi, Virusi vya Ukimwi (VVU), jinsia na kuhusiana kwa heshima kwa walimu wa shule za msingi na sekondari, iliyoandaliwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

"Mlisikia juzi matokeo ya kidato cha nne katika somo la Hisabati yalikuwa si mazuri. Nimefuatilia katika baadhi ya shule nimekuta hivi, mwalimu akitoa hesabu 10 anakuwa na mzigo wa fimbo, mwanafunzi atakayekosa hesabu tano atachapwa viboko vitano, akikosa hesabu tatu atachapwa fimbo tatu. Yaani unapigwa fimbo kulingana na idadi ya hesabu ulizokosa,” alisema.

Dk. Mutahabwa alisema endapo kuna mwalimu mwenye dhana kwamba anapofundisha akitumia fimbo inasaidia kumjaza akili mwanafunzi, atakuwa anajidanganya na kwamba ualimu hauko hivyo.

Aliwashauri walimu wanaofundisha somo la Hisabati kuwa na ushirikiano, upendo na kuwa tayari wakati wote kuwasaidia wanafunzi. Alisema kwa kufanya hivyo, wanafunzi wengi watafaulu somo hilo.

Alibainisha kwamba utafiti umeonyesha kuwa ili mwanafunzi azingatie masomo ya mwalimu anayemfundisha, ni lazima kuwapo na upendo na heshima kati yao ili miaka ijayo mwanafunzi huyo atamani kuwa mwalimu.

“Utafiti umeonyesha kwamba ili mwanafunzi azingatie masomo yake la kwanza ni lazima akupende wewe unayemfundisha. Yaani uwe mfano wa kuigwa kwa wanafunzi, atamani unavyovaa, atamani unavyohusiana na wengine ofisini na jamii,” alisema.

Dk. Mutahabwa alisema endapo mwanafunzi atampenda mwalimu anayemfundisha, atalipenda pia somo husika analofundishwa na kulisoma mara kwa mara.


IppMedia
Wanafunzi wengi Hawapendi kuumiza vichwa (kuvishughulish) ndiyo maana Hawapendi hesabu, niliona hao waliomaliza kidato Cha 4 mwaka 2021 wakiingia na scientific calculator kwenye mitihani, Sasa ilikuwaje 89%wakafeli mtihani?
 
St Francis wenyewe watu kibao wanna wani za 7,8,9 na hawana A za Hisabati.
 
Hatari naona zaidi vyuoni.

Kwa sasa ma'ticha' wakiume wa vyuo wanachukua tahadhari kubwa kukaa karibu na wanafunzi wa kike. Kwa sababu wametuhumiwa mno kwa masuala ya kutoa maksi kwa kujua rangi za nguo ndani za wanafunzi hao.

Hata kwenye kusimamia miradi maalumu ya kukamilisha masomo yao ya chuo, wanafunzi wa kike wakati mwingine wanakosa nafasi ya kusimamiwa na ticha mzuri wa kiume kwenye mada yake aliyoichagua ya kufanya mradi maalumu (special project).

Hizi mada maalumu zinahitaji ukaribu sana kati ya ticha na mwanafunzi. Wakati mwingine ticha na mwanafunzi wanalazimika kukaa maabara mpaka saa 4 usiku wakifuatilia "experiment" ya mradi maalumu. Na hii ni hasa pale ticha anapotaka mwanafunzi apate takwimu sahihi za kuweza kutoa pepa. Katika mazingira haya ticha ambaye hapendi kuwa na makando kando ...lazima amteme mwanafunzi wa kike hata kama mwanafunzi wa kike anauwezo mkubwa.

Kwa hiyo si suala la hesabu tu kwa mwalimu kuwa karibu na mwanafunzi bali kuna mambo mengi yanaathiri uwezekano wa mwanafunzi kupata elimu sahihi katika mazingira sahihi.
 
Hatari naona zaidi vyuoni.

Kwa sasa ma'ticha' wakiume wa vyuo wanachukua tahadhari kubwa kukaa karibu na wanafunzi wa kike. Kwa sababu wametuhumiwa mno kwa masuala ya kutoa maksi kwa kujua rangi za nguo ndani za wanafunzi hao.

Hata kwenye kusimamia miradi maalumu ya kukamilisha masomo yao ya chuo, wanafunzi wa kike wakati mwingine wanakosa nafasi ya kusimamiwa na ticha mzuri wa kiume kwenye mada yake aliyoichagua ya kufanya mradi maalumu (special project).

Hizi mada maalumu zinahitaji ukaribu sana kati ya ticha na mwanafunzi. Wakati mwingine ticha na mwanafunzi wanalazimika kukaa maabara mpaka saa 4 usiku wakifuatilia "experiment" ya mradi maalumu. Na hii ni hasa pale ticha anapotaka mwanafunzi apate takwimu sahihi za kuweza kutoa pepa. Katika mazingira haya ticha ambaye hapendi kuwa na makando kando ...lazima amteme mwanafunzi wa kike hata kama mwanafunzi wa kike anauwezo mkubwa.

Kwa hiyo si suala la hesabu tu kwa mwalimu kuwa karibu na mwanafunzi bali kuna mambo mengi yanaathiri uwezekano wa mwanafunzi kupata elimu sahihi katika mazingira sahihi.
Point
 
Back
Top Bottom