Muswada wa maboresho ya utaratibu wa kitchen party/bag party

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
Ndugu wanajamvi wa MMU

Napenda kuleta muswada huu hapa kwa majadiliano.

Nimefuatilia kwa kiasi fulani kuhusu ufanisi wa hizi kozi zinazoitwa kitchen party na bag party na kugundua kuna upungufu fulani.

Kiini cha tatizo nimegundua kuwa ni kwa sababu kichen party (KP) zinaendeshwa na wanawake tu (wakufunzi), na hali kadhalika bag party (BP) zinakufunziwa na wanaume.

Kwa nini nasema ni tatizo? Mathalani katika KP msichana anaetarajiwa kuolewa anatakiwa apewe mafunzo ya aina mbili. Moja ni namna ya ku-handle tabia na matendo ya mumewe hata yakiwa sio mazuri, Mbili ni namna ya kumridhisha Mume wake. Sasa hapo kwa hilo la kwanza, ni sawa akielezwa na wanawake wenzake. Lakini hilo la pili (ambalo ndilo hupewa kipaumbele kwenye KP) ni vyema akaelezwa na wanaume. Kiukweli wanaume ndio wanaojua nini wanataka kutoka kwa wanawake (and vice versa). Hawa wanaojiita mama wa shuhuli, mambo mengi wanabuni na wanakosea. Wanaume (tena waliooa) ndio wanajua nini alikikosa kwa mkewe akakipata kwa nyumba ndogo. Wa mama wa shuhuli wanaongelea kukata viuno, kuvaa shanga, sijui kulala uchi, lakini hivyo ni vitu vidogo. Wababa wanajua ni wakati gani wanapenda mke awe mpole, au mkali, mbishi, au mtiifu, mcheshi, mtani au mkorofi, n.k.

Watu wanaweza wakasema ooh, hivyo vitu ataelezwa na mumewe huko ndani... Ukweli ni kuwa yapo mambo (tena mengi) ya kimapenzi ambayo mwanaume hawezi kumueleza live mkewe na akimweleza awe tayari kuhisiwa kuwa sio mwaminifu. Wanaume watamweleza mwanamke anayeolewa ni vipi wanapenda wachukuliweje au wahisiweje pale wanapofanya kitu kisichoridhisha kama kuchelewa kurudi nyumbani, au kupungua performance kitandani.

Nasisitiza tena kuwa wanaume wengi hawapendi tabia za kikondoo tu kwa mwanamke (upole, utii, unyenyekevu, wema), bali mara chache wanapenda kuona mke amekuwa mkali, mkorofi, mbishi, na mbabe lakini katika mazingira fulani tu machache.

Naamini pia hata kwenye BP tunapoenda kuwaambia wanaume wenzetu kuwa wafanye hivi, waishi vile.. tunapungukiwa kujua nini hasa ambacho wanawake zetu wanapenda ambacho hawawezi kutuambia direct. Yapo mambo fulani hivi hasa ya kitandani au yanayohusu ndugu ambayo wanawake hawawezi kuyasema direct kwa waume zao, otherwise wataonekana wahuni, waachoyo, wabinafsi nk.

Kwa experience ndogo niliyo nayo, nimegundua kuwa siku zote nilikuwa effective zaidi kuwashauri marafiki au ndugu zangu wa kike walipokuwa na matatizo na ndoa zao, kuliko nilipowashauri marafiki au ndgu wa kiume wenye matatizo na ndoa zao.

Ndugu wanajamvi, napenda kuwasilisha hoja,
 
Nikitumia JF kama mfano, ni kuwa migogoro mingi siku hizi ipo kwa wapenzi ambao hawajaoana. Madhara yake ni mengi, kuumizana nyoyo, mimba zisizotarajiwa, kufeli masomo, kuzorotesha kazi, vifo (kujiua/magonjwa), nk...

Je, mnadhani upo umuhimu wa kuanzishwa utaratibu wa elimu ya mapenzi kwa watu wanaotaka kuingia katika mahusiano hata kama sio ya kuoana?
 
Habari....
kutokana na wimbi la kuvunjika kwa ndoa..kwa siku za hivi karibuni...na lawama nyingi wakitupiwa wanawake..jambo ambalo nimegundua si sahihi...kutokana na uchunguzi wangu nimegundua vijana wengi wa kiume hawakujiandaa au kuandaliwa kabla ya kuingia kwenye ndoa...wanawake pekee ndio huandaliwa jambo ambalo halitoshi kuwafanya wadumu katika ndoa..hivyo kupelekea ndoa kuwa kama filamu za bongo movie..kwa kuwa mtoto wa kiume hakuandaliwa namna ya kuishi ndoani....kwa hiyo ingekuwa vyema kama vijana wa kiume nao wangeandaliwa kisaikolojia...kupitia mafunzo maalumu kabla ya kuingia ndoani....
NAWASILISHA..
 
hata wanawake wanaoandaliwa ni yaleyale tu. Haya makitchen paries hayana mantiki siku hizi
 
Ndugu wanajamvi wa MMU

Napenda kuleta muswada huu hapa kwa majadiliano.

Nimefuatilia kwa kiasi fulani kuhusu ufanisi wa hizi kozi zinazoitwa
kitchen party na bag party na kugundua kuna upungufu fulani.

Kiini cha tatizo nimegundua kuwa ni kwa sababu kichen party (KP)
zinaendeshwa na wanawake tu (wakufunzi), na hali kadhalika bag party
(BP) zinakufunziwa na wanaume.

Kwa nini nasema ni tatizo? Mathalani katika KP msichana anaetarajiwa
kuolewa anatakiwa apewe mafunzo ya aina mbili. Moja ni namna ya
ku-handle tabia na matendo ya mumewe hata yakiwa sio mazuri, Mbili ni
namna ya kumridhisha Mume wake. Sasa hapo kwa hilo la kwanza, ni sawa
akielezwa na wanawake wenzake. Lakini hilo la pili (ambalo ndilo hupewa
kipaumbele kwenye KP) ni vyema akaelezwa na wanaume. Kiukweli wanaume
ndio wanaojua nini wanataka kutoka kwa wanawake (and vice versa). Hawa
wanaojiita mama wa shuhuli, mambo mengi wanabuni na wanakosea. Wanaume
(tena waliooa) ndio wanajua nini alikikosa kwa mkewe akakipata kwa
nyumba ndogo. Wa mama wa shuhuli wanaongelea kukata viuno, kuvaa shanga,
sijui kulala uchi, lakini hivyo ni vitu vidogo. Wababa wanajua ni
wakati gani wanapenda mke awe mpole, au mkali, mbishi, au mtiifu,
mcheshi, mtani au mkorofi, n.k.

Watu wanaweza wakasema ooh, hivyo vitu ataelezwa na mumewe huko ndani...
Ukweli ni kuwa yapo mambo (tena mengi) ya kimapenzi ambayo mwanaume
hawezi kumueleza live mkewe na akimweleza awe tayari kuhisiwa kuwa sio
mwaminifu. Wanaume watamweleza mwanamke anayeolewa ni vipi wanapenda
wachukuliweje au wahisiweje pale wanapofanya kitu kisichoridhisha kama
kuchelewa kurudi nyumbani, au kupungua performance kitandani.

Nasisitiza tena kuwa wanaume wengi hawapendi tabia za kikondoo tu kwa
mwanamke (upole, utii, unyenyekevu, wema), bali mara chache wanapenda
kuona mke amekuwa mkali, mkorofi, mbishi, na mbabe lakini katika
mazingira fulani tu machache.

Naamini pia hata kwenye BP tunapoenda kuwaambia wanaume wenzetu kuwa
wafanye hivi, waishi vile.. tunapungukiwa kujua nini hasa ambacho
wanawake zetu wanapenda ambacho hawawezi kutuambia direct. Yapo mambo
fulani hivi hasa ya kitandani au yanayohusu ndugu ambayo wanawake
hawawezi kuyasema direct kwa waume zao, otherwise wataonekana wahuni,
waachoyo, wabinafsi nk.

Kwa experience ndogo niliyo nayo, nimegundua kuwa siku zote nilikuwa
effective zaidi kuwashauri marafiki au ndugu zangu wa kike walipokuwa na
matatizo na ndoa zao, kuliko nilipowashauri marafiki au ndgu wa kiume
wenye matatizo na ndoa zao.

Ndugu wanajamvi, napenda kuwasilisha hoja,

kp haina maana siku izi mtu anaolewa wakati ameishazaa.mc mmoja alituvunja mbavu alisema...jaman eeeee tukajibu semaaa bibie' mm leosina kazi kubwa maana mtalajiwa kaishazaa so nitaongelea usafi tuuuuu. tulicheka mbaya
 
kp haina maana siku izi mtu anaolewa wakati ameishazaa.mc mmoja alituvunja mbavu alisema...jaman eeeee tukajibu semaaa bibie' mm leosina kazi kubwa maana mtalajiwa kaishazaa so nitaongelea usafi tuuuuu. tulicheka mbaya

Hahahaa...
 
Kitchen Party siku hiz ni kwa ajili ya kutafuta vyombo tuu...Huwezi kufundishwa mbele ya watu kibaooo, tena kwa sherehe halafu ukaelewa.....!
 
ni wastage ya resources za kupeleka watoto shule.!! hamna la maana huko maana wahudhuriaji wenyewe ni nyumba ndogo za watu, michepuko etc. Watafundisha nini?
 
Back
Top Bottom