Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Ndugu wanajamvi wa MMU
Napenda kuleta muswada huu hapa kwa majadiliano.
Nimefuatilia kwa kiasi fulani kuhusu ufanisi wa hizi kozi zinazoitwa kitchen party na bag party na kugundua kuna upungufu fulani.
Kiini cha tatizo nimegundua kuwa ni kwa sababu kichen party (KP) zinaendeshwa na wanawake tu (wakufunzi), na hali kadhalika bag party (BP) zinakufunziwa na wanaume.
Kwa nini nasema ni tatizo? Mathalani katika KP msichana anaetarajiwa kuolewa anatakiwa apewe mafunzo ya aina mbili. Moja ni namna ya ku-handle tabia na matendo ya mumewe hata yakiwa sio mazuri, Mbili ni namna ya kumridhisha Mume wake. Sasa hapo kwa hilo la kwanza, ni sawa akielezwa na wanawake wenzake. Lakini hilo la pili (ambalo ndilo hupewa kipaumbele kwenye KP) ni vyema akaelezwa na wanaume. Kiukweli wanaume ndio wanaojua nini wanataka kutoka kwa wanawake (and vice versa). Hawa wanaojiita mama wa shuhuli, mambo mengi wanabuni na wanakosea. Wanaume (tena waliooa) ndio wanajua nini alikikosa kwa mkewe akakipata kwa nyumba ndogo. Wa mama wa shuhuli wanaongelea kukata viuno, kuvaa shanga, sijui kulala uchi, lakini hivyo ni vitu vidogo. Wababa wanajua ni wakati gani wanapenda mke awe mpole, au mkali, mbishi, au mtiifu, mcheshi, mtani au mkorofi, n.k.
Watu wanaweza wakasema ooh, hivyo vitu ataelezwa na mumewe huko ndani... Ukweli ni kuwa yapo mambo (tena mengi) ya kimapenzi ambayo mwanaume hawezi kumueleza live mkewe na akimweleza awe tayari kuhisiwa kuwa sio mwaminifu. Wanaume watamweleza mwanamke anayeolewa ni vipi wanapenda wachukuliweje au wahisiweje pale wanapofanya kitu kisichoridhisha kama kuchelewa kurudi nyumbani, au kupungua performance kitandani.
Nasisitiza tena kuwa wanaume wengi hawapendi tabia za kikondoo tu kwa mwanamke (upole, utii, unyenyekevu, wema), bali mara chache wanapenda kuona mke amekuwa mkali, mkorofi, mbishi, na mbabe lakini katika mazingira fulani tu machache.
Naamini pia hata kwenye BP tunapoenda kuwaambia wanaume wenzetu kuwa wafanye hivi, waishi vile.. tunapungukiwa kujua nini hasa ambacho wanawake zetu wanapenda ambacho hawawezi kutuambia direct. Yapo mambo fulani hivi hasa ya kitandani au yanayohusu ndugu ambayo wanawake hawawezi kuyasema direct kwa waume zao, otherwise wataonekana wahuni, waachoyo, wabinafsi nk.
Kwa experience ndogo niliyo nayo, nimegundua kuwa siku zote nilikuwa effective zaidi kuwashauri marafiki au ndugu zangu wa kike walipokuwa na matatizo na ndoa zao, kuliko nilipowashauri marafiki au ndgu wa kiume wenye matatizo na ndoa zao.
Ndugu wanajamvi, napenda kuwasilisha hoja,
Napenda kuleta muswada huu hapa kwa majadiliano.
Nimefuatilia kwa kiasi fulani kuhusu ufanisi wa hizi kozi zinazoitwa kitchen party na bag party na kugundua kuna upungufu fulani.
Kiini cha tatizo nimegundua kuwa ni kwa sababu kichen party (KP) zinaendeshwa na wanawake tu (wakufunzi), na hali kadhalika bag party (BP) zinakufunziwa na wanaume.
Kwa nini nasema ni tatizo? Mathalani katika KP msichana anaetarajiwa kuolewa anatakiwa apewe mafunzo ya aina mbili. Moja ni namna ya ku-handle tabia na matendo ya mumewe hata yakiwa sio mazuri, Mbili ni namna ya kumridhisha Mume wake. Sasa hapo kwa hilo la kwanza, ni sawa akielezwa na wanawake wenzake. Lakini hilo la pili (ambalo ndilo hupewa kipaumbele kwenye KP) ni vyema akaelezwa na wanaume. Kiukweli wanaume ndio wanaojua nini wanataka kutoka kwa wanawake (and vice versa). Hawa wanaojiita mama wa shuhuli, mambo mengi wanabuni na wanakosea. Wanaume (tena waliooa) ndio wanajua nini alikikosa kwa mkewe akakipata kwa nyumba ndogo. Wa mama wa shuhuli wanaongelea kukata viuno, kuvaa shanga, sijui kulala uchi, lakini hivyo ni vitu vidogo. Wababa wanajua ni wakati gani wanapenda mke awe mpole, au mkali, mbishi, au mtiifu, mcheshi, mtani au mkorofi, n.k.
Watu wanaweza wakasema ooh, hivyo vitu ataelezwa na mumewe huko ndani... Ukweli ni kuwa yapo mambo (tena mengi) ya kimapenzi ambayo mwanaume hawezi kumueleza live mkewe na akimweleza awe tayari kuhisiwa kuwa sio mwaminifu. Wanaume watamweleza mwanamke anayeolewa ni vipi wanapenda wachukuliweje au wahisiweje pale wanapofanya kitu kisichoridhisha kama kuchelewa kurudi nyumbani, au kupungua performance kitandani.
Nasisitiza tena kuwa wanaume wengi hawapendi tabia za kikondoo tu kwa mwanamke (upole, utii, unyenyekevu, wema), bali mara chache wanapenda kuona mke amekuwa mkali, mkorofi, mbishi, na mbabe lakini katika mazingira fulani tu machache.
Naamini pia hata kwenye BP tunapoenda kuwaambia wanaume wenzetu kuwa wafanye hivi, waishi vile.. tunapungukiwa kujua nini hasa ambacho wanawake zetu wanapenda ambacho hawawezi kutuambia direct. Yapo mambo fulani hivi hasa ya kitandani au yanayohusu ndugu ambayo wanawake hawawezi kuyasema direct kwa waume zao, otherwise wataonekana wahuni, waachoyo, wabinafsi nk.
Kwa experience ndogo niliyo nayo, nimegundua kuwa siku zote nilikuwa effective zaidi kuwashauri marafiki au ndugu zangu wa kike walipokuwa na matatizo na ndoa zao, kuliko nilipowashauri marafiki au ndgu wa kiume wenye matatizo na ndoa zao.
Ndugu wanajamvi, napenda kuwasilisha hoja,