Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Binafsi nilikuwa nikiamini sana katika hoja nzito zilizokuwa zinatolewa na wabunge wa chadema mara kwa mara pale bungeni. Lakini kususia kujadili mjadala wa muswada tata wa katiba, kulikofanywa na wabunge hao kulitokana na jazba ya ghafla bila ya kufikiria madhara yatakayotokea mbele. Walikuwa na hoja nzito na sababu za msingi kuupinga mswaada huo ambapo watanzanzania kwa mamilioni wangepata somo kupitia kwao kwa hiyo hata kama ungepita kutokana na wingi wa wabunge wa CCM. Wangepata faida kubwa kwani mamilioni ya watanzania wangeona na kusikia pumba na mchele katika muswada huo. Naamini kwa uwezo wao mkubwa wa kujenga hoja. Kile walichokuwa wanakitetea kingekuwa na nguvu kuliko hali ya kutapa tapa iliyopo sasa. Mara nyingi hasira hasara, mpaka sasa sijafahamu sababu hasa ya kususia vikao vile. Kwa kususa kwao sasa kunawaghalimu watanzania walio wengi. Kwa hili hawawezi kukwepa lawama.