Muswada wa katiba mpya: CHADEMA wasitafute mchawi. Kosa lilikuwa ni kususia kuujadili bungeni.

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Binafsi nilikuwa nikiamini sana katika hoja nzito zilizokuwa zinatolewa na wabunge wa chadema mara kwa mara pale bungeni. Lakini kususia kujadili mjadala wa muswada tata wa katiba, kulikofanywa na wabunge hao kulitokana na jazba ya ghafla bila ya kufikiria madhara yatakayotokea mbele. Walikuwa na hoja nzito na sababu za msingi kuupinga mswaada huo ambapo watanzanzania kwa mamilioni wangepata somo kupitia kwao kwa hiyo hata kama ungepita kutokana na wingi wa wabunge wa CCM. Wangepata faida kubwa kwani mamilioni ya watanzania wangeona na kusikia pumba na mchele katika muswada huo. Naamini kwa uwezo wao mkubwa wa kujenga hoja. Kile walichokuwa wanakitetea kingekuwa na nguvu kuliko hali ya kutapa tapa iliyopo sasa. Mara nyingi hasira hasara, mpaka sasa sijafahamu sababu hasa ya kususia vikao vile. Kwa kususa kwao sasa kunawaghalimu watanzania walio wengi. Kwa hili hawawezi kukwepa lawama.
 
Binafsi nilikuwa nikiamini sana katika hoja nzito zilizokuwa zinatolewa na wabunge wa chadema mara kwa mara pale bungeni. Lakini kususia kujadili mjadala wa muswada tata wa katiba, kulikofanywa na wabunge hao kulitokana na jazba ya ghafla bila ya kufikiria madhara yatakayotokea mbele. Walikuwa na hoja nzito na sababu za msingi kuupinga mswaada huo ambapo watanzanzania kwa mamilioni wangepata somo kupitia kwao kwa hiyo hata kama ungepita kutokana na wingi wa wabunge wa CCM. Wangepata faida kubwa kwani mamilioni ya watanzania wangeona na kusikia pumba na mchele katika muswada huo. Naamini kwa uwezo wao mkubwa wa kujenga hoja. Kile walichokuwa wanakitetea kingekuwa na nguvu kuliko hali ya kutapa tapa iliyopo sasa. Mara nyingi hasira hasara, mpaka sasa sijafahamu sababu hasa ya kususia vikao vile. Kwa kususa kwao sasa kunawaghalimu watanzania walio wengi. Kwa hili hawawezi kukwepa lawama.
We subiri tu.... mwalimu Seif lazima tumpeleke jela kwa ufisadi anaofanya CUF. Unajaribu kupindisha hoja ili tumwache... Hatumwachi ngoooo lazima tumpeleke jela akanyee debe
 
@Jumakidogo, kama CHADEMA hawakutoka bungeni nina hakika sote tusingekuwa tunajadili huu muswada wa katiba hapa. Na sio kwenye hili jukwaa peke yake hata huko mitaani watu wa kawaida kabisa wanaongea kuhusu muswada wa katiba, na wengi wanaonekana kukubaliana na CHADEMA kuwa ni mbovu. Kuna miswada mingine imepitishwa bungeni pamoja na kwamba ni mibovu lakini imepita na hakuna mtu anaongea chochote huku uraini! Inabidi upime matokeo ya CHADEMA kutoka nje kwa upana zaidi.
 
Mangapi Mazuri wamejadili Bungeni yakakataliwa? Hili la Katiba ndo Mungu agewashushia Neema Wabunge wa CCM kupiga kura Kuupinga Mswaada kutokana na Chadema Kuujadili? Unakumbuka pendekezo la Sheria ya Mahakama la Lissu? Kwa mfumo wa Bunge hata Chadema wakikaa, kwenye issue nyeti hakuna anayewasikiliza..
Pili uliona walivyotukanwa wakati Maelezo ya Lissu yanajadiliwa, so ulitaka watu wazima wake pale kutukanwa? Kutoka ilikuwa ni Busara ya Hali ya juu
 
@Jumakidogo, kama CHADEMA hawakutoka bungeni nina hakika sote tusingekuwa tunajadili huu muswada wa katiba hapa. Na sio kwenye hili jukwaa peke yake hata huko mitaani watu wa kawaida kabisa wanaongea kuhusu muswada wa katiba, na wengi wanaonekana kukubaliana na CHADEMA kuwa ni mbovu. Kuna miswada mingine imepitishwa bungeni pamoja na kwamba ni mibovu lakini imepita na hakuna mtu anaongea chochote huku uraini! Inabidi upime matokeo ya CHADEMA kutoka nje kwa upana zaidi.

Siamini kama tukio lile lilikuwa limepangwa. Kulikuwa na makosa makubwa kwa spika yule mwanamke kukataa ule mwongozo. Lakini CDM hawakutulia. Mjadala unaendelea, lakini ni kwa sehemu finyu sana hasa kwa sisi tuishio mijini. Ningependa sana kama ngoma ile wangeanzia kuicheza palepale ndani ndipo mengine yafuate baadae.
 
umetumwa nini? mbona CUF walijadili na kupitisha lakini wameenda ikulu kurudia kitu kilekile au hilo hujaliona?
 
Magamba yakishaamua yameamua tu! Kwani PM Pinda alipolidanganya Bunge alifanywa nini? Kwa kweli yule mama ameharibu sana hadhi ya Bunge!
 
Hebu twende taratibu, tuwe wakweli kwa nafsi zetu na tuache kupotoshana. Unasema 'watanzania kwa mamilioni wangepata somo...!!' Mamilioni ambao hawakusikia, hawakuona, hawakusoma wala hawakuitafuta hotuba ya Lissu! Unataka kutuaminisha kuwa wangepata somo kama tu Chadema wasingetoka bungeni!! Ikiwa pamoja na Chadema kueleza mara kadhaa sababu za wao kutoka nje bado umekuwa mzito kuelewa, unataka usaidiweje?! Mtanzania yeyote mwenye nia njema anayetaka kujua sababu atatafuta hotuba ya Lissu au atatafuta msimamo wa wanasheria na wadau mbalimbali juu ya muswada huo ulivyo hovyo na jinsi sheria na kanuni zilivyopindishwa.
 
Hebu twende taratibu, tuwe wakweli kwa nafsi zetu na tuache kupotoshana. Unasema 'watanzania kwa mamilioni wangepata somo...!!' Mamilioni ambao hawakusikia, hawakuona, hawakusoma wala hawakuitafuta hotuba ya Lissu! Unataka kutuaminisha kuwa wangepata somo kama tu Chadema wasingetoka bungeni!! Ikiwa pamoja na Chadema kueleza mara kadhaa sababu za wao kutoka nje bado umekuwa mzito kuelewa, unataka usaidiweje?! Mtanzania yeyote mwenye nia njema anayetaka kujua sababu atatafuta hotuba ya Lissu au atatafuta msimamo wa wanasheria na wadau mbalimbali juu ya muswada huo ulivyo hovyo na jinsi sheria na kanuni zilivyopindishwa.

Nini kazi ya mbunge??
 
Hebu twende taratibu, tuwe wakweli kwa nafsi zetu na tuache kupotoshana. Unasema 'watanzania kwa mamilioni wangepata somo...!!' Mamilioni ambao hawakusikia, hawakuona, hawakusoma wala hawakuitafuta hotuba ya Lissu! Unataka kutuaminisha kuwa wangepata somo kama tu Chadema wasingetoka bungeni!! Ikiwa pamoja na Chadema kueleza mara kadhaa sababu za wao kutoka nje bado umekuwa mzito kuelewa, unataka usaidiweje?! Mtanzania yeyote mwenye nia njema anayetaka kujua sababu atatafuta hotuba ya Lissu au atatafuta msimamo wa wanasheria na wadau mbalimbali juu ya muswada huo ulivyo hovyo na jinsi sheria na kanuni zilivyopindishwa.

Kwa hiyo ulitaka lazima kile kilichoandikwa na Lissu ndo kikubaliwe. Nadhani unakumbuka nguvu ya hoja ya mbunge Manchali aliyebaki na kuchangia hoja ile. Wabunge wote wa CCM walikaa kimya. Chukulia kama wangechangia wengine zaidi ingekuwaje! Vyovyote vile kutoka haikuwa sahihi. Tusiwe watetezi wa kila kitu.
 
Kugonga meza na kuchambua maisha binafsi ya mh. Tundu Lisu!

Nafikiri ulikuwa una maanisha "Kukimbia na kutoka nje bunge kwa kuogopa kutetea hoja mfu au siyo"

Ili wananchi wasijue kwamba hawana hoja wanakimbia..halafu wanakwenda kubembeleza kuonana na rais?? oops
 
Kwa hiyo ulitaka lazima kile kilichoandikwa na Lissu ndo kikubaliwe. Nadhani unakumbuka nguvu ya hoja ya mbunge Manchali aliyebaki na kuchangia hoja ile. Wabunge wote wa CCM walikaa kimya. Chukulia kama wangechangia wengine zaidi ingekuwaje! Vyovyote vile kutoka haikuwa sahihi. Tusiwe watetezi wa kila kitu.
Kwa swali lako hilo hapo juu unataka kumaanisha kuwa hotuba aliyosoma Lissu siyo msimamo wa Chadema! kwa hiyo ungekubali michango ya wabunge wengine wa Chadema lakini siyo Lissu!!!
 
We subiri tu.... mwalimu Seif lazima tumpeleke jela kwa ufisadi anaofanya CUF. Unajaribu kupindisha hoja ili tumwache... Hatumwachi ngoooo lazima tumpeleke jela akanyee debe

@By Jumakidogo

Jumakidogo Ujuwe Maalim Seif sio Mzaramu wala Mnyamwezi kwa hio Muungano ukivunjika utampata vipi kumuhukumu wakati Tanganyika itakuwa nchi mbali na Zanzibar?
 
Back
Top Bottom