Muswada kuhusu usajili wa Biashara na Kampuni. Watu wenye miaka 70 kuruhusiwa kuwa Wakurugenzi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Kuhusu Sheria ya Mawakili, alisema inalenga kuanzisha Kamati za Maadili za Mawakili kwa ngazi ya mkoa ili kurahisisha upatikanaji wa haki.

“Pia, kumwezesha mwananchi anayemlalamikia wakili kwa ukiukaji wa maadili kushughulikia tatizo lake katika ngazi ya mkoa bila ya uhitaji wa kusafiri kuifuata kamati ya maadili katika ngazi ya taifa," alisema.

Kwenye Sheria ya Usajili wa Vizazi na Vifo, muswada huo unapendekeza ubadilishanaji wa taarifa za usajili wa matukio muhimu baina ya taasisi moja na nyingine.

Kuhusu Sheria ya Majina ya Biashara, muswada unapendekeza majina ya biashara yanayosajiliwa yawe ni ya wale tu wanaokidhi vigezo vya kusajiliwa kwa madhumuni mahsusi.

Pia inapendekezwa kuongeza adhabu ya faini ili kuhakikisha adhabu inayotolewa na sheria inaendana na wakati na hivyo kuzuia utendaji wa makosa.

Katika Sheria ya Kampuni, muswada unapendekeza kuhakikisha watu wenye sifa ya kusajili kampuni ni wale tu wenye sifa na watapaswa kuwasilisha taarifa zao binafsi.

Pia, unapendekeza kuweka katazo au zuio la kusajili kampuni kwa watu waliowahi kutiwa hatiani au ambao taarifa zao zimetolewa na mamlaka husika kuwa mwombaji wamekuwa wakijihusisha na makosa yanayohusiana na utakatishaji fedha, ufadhili wa ugaidi, biashara ya binadamu, biashara ya dawa za kulevya au makosa mengine yanayohusiana nayo.

Inapendekezwa katika muswada huo kuruhusu watu wenye umri wa zaidi ya miaka 70 kuteuliwa kuwa wakurugenzi wa kampuni.

Kwenye Sheria ya Mahakama za Migogoro ya Ardhi, inapendekezwa kubadilisha muhula wa kushikilia nafasi kwa wenyeviti wa mabaraza ya ardhi na nyumba ya wilaya.

Muswada huo unapendekeza kufanya marekebisho katika Sheria ya Mahakama za Mahakimu ili kuwaondoa wazee washauri wa mahakama katika mahakama za mwanzo kwa kuwa mahakama hizo sasa zinasimamiwa na mahakimu wakazi wenye weledi wa sheria na hivyo kuongeza kasi ya utoaji haki kwa wakati.
 
Kuna ulazima gani wa kumteua mtu mwenye umri wa miaka 70 na kuendelea kuwa Mkurugenzi wa Kampuni?

Kwanini hatuheshimu umri wa kustaafu na pia kuupumzisha mwili? Sas vijana wenye weledi na wenye mawazo mapya watapata wapi nafasi ya kuonesha vipaji vyao iwapo tutaendelea kuwakumbatia wazee?
 
Kuna ulazima gani wa kumteua mtu mwenye umri wa miaka 70 na kuendelea kuwa Mkurugenzi wa Kampuni?

Kwanini hatuheshimu umri wa kustaafu na pia kuupumzisha mwili? Sas vijana wenye weledi na wenye mawazo mapya watapata wapi nafasi ya kuonesha vipaji vyao iwapo tutaendelea kuwakumbatia wazee?
Yanayozungumziwa ni makampuni binafsi au ya kiserikali?
Inapendekezwa katika muswada huo kuruhusu watu wenye umri wa zaidi ya miaka 70 kuteuliwa kuwa wakurugenzi wa kampuni.
 
Sidhani kuna kampuni ya umma ina mkurugenzi mwenye umri wa zaidi ya miaka 65. Sasa kama sheria ilikuwa inazuia makampuni binafsi kuwa na wakurugenzi wenye umri wa zaidi ya miaka 70, basi ilikuwa sheria ya hovyo.
 
Kumbe walikuwa wanakatazwa ? Kampuni binafsi ni ya watu binafsi na mambo yao binafsi so long as hawaathiri jamii.

Hayo mengine ya kusajili na kuongeza faini n.k. ni muendelezo ule ule wa kufanya ufanyaji kazi Tanzania kuwa mgumu hususan wakati huu ambapo biashara nyingi bado changa, hakuna ajira na tunamwambia kila kiumbe awe mwekezaji / ajiajiri, sasa sijui ajira hizo zinajumuisha na kuwa kibaka?

Hawa watu akili yao ipo kwenye ukusanyaji tu.
 
Kuna ulazima gani wa kumteua mtu mwenye umri wa miaka 70 na kuendelea kuwa Mkurugenzi wa Kampuni?

Kwanini hatuheshimu umri wa kustaafu na pia kuupumzisha mwili? Sas vijana wenye weledi na wenye mawazo mapya watapata wapi nafasi ya kuonesha vipaji vyao iwapo tutaendelea kuwakumbatia wazee?
Ujana usikutishe, nawe utafika huko. Wakurugenzi ni wa makampuni binafsi acha mapovu
 
Kuna ulazima gani wa kumteua mtu mwenye umri wa miaka 70 na kuendelea kuwa Mkurugenzi wa Kampuni?

Kwanini hatuheshimu umri wa kustaafu na pia kuupumzisha mwili? Sas vijana wenye weledi na wenye mawazo mapya watapata wapi nafasi ya kuonesha vipaji vyao iwapo tutaendelea kuwakumbatia wazee?
Nchi ngumu sana hii ,siku ya kiama nadhani tutafutiwa dhambi
 
Kuna ulazima gani wa kumteua mtu mwenye umri wa miaka 70 na kuendelea kuwa Mkurugenzi wa Kampuni?

Kwanini hatuheshimu umri wa kustaafu na pia kuupumzisha mwili? Sas vijana wenye weledi na wenye mawazo mapya watapata wapi nafasi ya kuonesha vipaji vyao iwapo tutaendelea kuwakumbatia wazee?
Kuwa mkurugenzi wa kampuni (director) haimaanishi ni lazima ushiriki kwenye management ya kampuni on a daily basis,

Huwa kwa structure ya kampuni one among the directors ndio anakuwa na mamlaka ya kuiendesha kampuni kwa kufanya maamuzi ya kuiendesha kwa shughuli zake za kila siku (Managing Director).

So huyo mkurugenzi mwenye 70 years anaweza tumika tu kwenye vikao vya bodi na kwenye maamuzi makubwa yanayohitaji consent ya directors wote.
 
Back
Top Bottom