Musukuma: Wabunge wa chadema leteni muswaada bungeni.

GRAMAA

JF-Expert Member
Nov 1, 2014
1,155
3,398
Musukuma amewataka wabunge wa chadema wapeleke muswaada bungeni wa kisheria utakaotoa nafasi ya watuhumiwa kama kinambowe kutokuwekwa ndani.

Msukuma amesema kilichowaweka ndani kina mbowe ni sheria walizozipitisha wenyewe bungeni.

Hivyo amewataka wabunge wapeleke mswaada bungeni utakaowalinda viongozi wa kisiasa wasiwekwe mahabusu hovyo.

Wao kama CCM wapo tayari kuunga mkono mswaada huo.

Source: star TV ajenda 2020
 
MISWADA INGEKUWA HAITAFSIRIWI KISWAHILI PALE BUNGENI WATU KAMA MUSUKUMA WANGEKUA MABUBU:D:D:D
 
Kwa hiyo una maananisha nn? Sheria ni za kutumika kwa nchi ya waswahili halafu ziwe kwa lugha ya trump tupu! Wapinzani leteni hoja zenye mashiko basi sio hizi dharau nyepesinyepesi
Wanachotaka Upinzani ni kuwa kibaka kama kaua hata la saba hakufika hukumu inasomwa kiingereza mahakama kuu au rufaa !!!!! Kibaka katulia haambulii hata Moja linalosemwa.Sheria iko kiingereza kumsomea mswahili kesi kiingereza asiyejua hata neno Moja la kiswahili ndio Upinzani wanataka.Kuhusu Upinzani serikali iombwe na bunge itangaze siku maalumu ya kuutangaza Upinzani kama janga la kitaifa na bendera ya taifa ipepee nusu mlingoti.Naomba mheshimiwa Msukuma atoe hoja binafsi bungeni kwa niaba yangu kama mbunge wangu.
 
Walete na muswaada wa kutaka makaburi yote kufufuliwa.watz tujue wa kina Nani hasa wamekuwa wakiitafuna nchi
 
Musukuma amewataka wabunge wa chadema wapeleke muswaada bungeni wa kisheria utakaotoa nafasi ya watuhumiwa kama kinambowe kutokuwekwa ndani.

Msukuma amesema kilichowaweka ndani kina mbowe ni sheria walizozipitisha wenyewe bungeni.

Hivyo amewataka wabunge wapeleke mswaada bungeni utakaowalinda viongozi wa kisiasa wasiwekwe mahabusu hovyo.

Wao kama CCM wapo tayari kuunga mkono mswaada huo.

Source: star TV ajenda 2020

Kwa nini yeye asipeleke huo mswada? Kama lengo ni kuwalinda viongozi wa kisiasa wasiwekwe maabusu hovyo, kwani CCM haina viongozi wa kisiasa? Au wanaolengwa ni viongozi wa vyama pinzani tu?
 
Musukuma amewataka wabunge wa chadema wapeleke muswaada bungeni wa kisheria utakaotoa nafasi ya watuhumiwa kama kinambowe kutokuwekwa ndani.

Msukuma amesema kilichowaweka ndani kina mbowe ni sheria walizozipitisha wenyewe bungeni.

Hivyo amewataka wabunge wapeleke mswaada bungeni utakaowalinda viongozi wa kisiasa wasiwekwe mahabusu hovyo.

Wao kama CCM wapo tayari kuunga mkono mswaada huo.

Source: star TV ajenda 2020
Awambie na CCM wapeleke Muswaada wa waliokopa Benki na kushindwa kulipa kama Yeye Nyumba zao zisiuzwe ahaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom