mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,075
- 4,111
Mwenyekiti wa CCM Geita na mbunge wa Geita Vijijini, Mh. Joseph Kasheku almaarufu kama King Musukuma tajiri wa Geita, amekishukia CHADEMA pamoja na Edward Lowassa.
Musukuma anasema KIDAMPA kama Lema hawezi kumshambulia Lowassa, kama wana uwezo wamfukuze kwenye chama.
Mimi nakuomba mzee Lowassa, hatua ulioinza ni nzuri, huku ndio kwenu. Hilo genge la wahuni hutoliweza. Rudi ukaombe radhi kwenye chama chako ambacho kitakuzika kwa heshima.
Lowassa kwenda kwenye lile genge la wahuni ilikuwa ni hasira tu, lakini halisi watu wenye maana tuko huku, ni busara tu arudi.
Rais wetu ana busara na hekima, sio kila mtu wa kumkaribisha. Wewe huwezi kumkaribisha mtu kama MBOWE, mnaenda kuzungumzia nini? Ataenda kuzungumzia nyanya zake zimeng'olewa na DC. Sio suala la kitaifa, ni binafsi.
Musukuma amesema upinzani wa kweli ni kukubaliana na yanayotendwa na mwengine na kama chama kilichoko madarakani kimefanya nzuri, uungwana ni kwenda kupongeza ila hofu kwa wahusika ni kuwa Lowassa anakimbia.
Ameendelea kusema mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe asiishie kufurahisha watu kwenye redio na mitandao ya kijamii, atoe kauli naye aone kama mwenye mbwa anaweza kung'atwa na mbwa wake mwenyewe kwani Lowassa ndio mwenye chama.