Magazetini
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 588
- 1,698
Mussa Zungu: Dunia ina matatizo makubwa, bei za bidhaa zimepanda huko zinapotengenezwa na kwakuwa zinapotengenezwa huko, zikija kwetu zinapanda vilevile.
Kwahiyo kupanda kwa bidhaa hizi sio suala la Tanzania, limetengenezwa na watanzania au limetengenezwa na Serikali ya Tanzania, ni suala ambalo limejitokeza kwa matatizo ya kiulimwengu ambayo yapo na hasa vita ya nchi hizi mbili kati ya Ukraine na Urusi.
Tutegemee mengi magumu yatakuja, kikubwa ni kumuomba Mwenyezi Mungu atunusuru na adha hii, amalize vita hii na dunia na nchi yetu irudi katika hali ya kawaida.
Mimi hivi karibuni nilikuwa Ufaransa, mkate sasa hivi huruhusiwi kununua kama zamani, mwisho ni mikate miwili, mkate umepanda kutoka euro moja sasa unauzwa euro nne, mafuta ya kupikia kutoka euro 2 mpaka 8, petroli euro 1.6 mpaka 7, hiyo ni Ulaya.
Kwahiyo kupanda kwa bidhaa hizi sio suala la Tanzania, limetengenezwa na watanzania au limetengenezwa na Serikali ya Tanzania, ni suala ambalo limejitokeza kwa matatizo ya kiulimwengu ambayo yapo na hasa vita ya nchi hizi mbili kati ya Ukraine na Urusi.
Tutegemee mengi magumu yatakuja, kikubwa ni kumuomba Mwenyezi Mungu atunusuru na adha hii, amalize vita hii na dunia na nchi yetu irudi katika hali ya kawaida.
Mimi hivi karibuni nilikuwa Ufaransa, mkate sasa hivi huruhusiwi kununua kama zamani, mwisho ni mikate miwili, mkate umepanda kutoka euro moja sasa unauzwa euro nne, mafuta ya kupikia kutoka euro 2 mpaka 8, petroli euro 1.6 mpaka 7, hiyo ni Ulaya.