Mkwawe
JF-Expert Member
- Jun 10, 2016
- 2,344
- 4,167
Watanzania mara nyingi tumekuwa tukiimbiwa wimbo wakuwa wazalendo na viongozi katika masuala mbalimbali, na miongoni mwa hao viongozi na mara nyingi rais wetu ndo amekuwa mstari wa mbele katika kuuimba wimbo wa uzalendo.
Patric Mfugale mbali ya kwamba ni mwenyekiti mtendaji wa sekta ya mabarabara ila pia amepewa heshima kubwa ya kuenziwa kwa daraja la pale TAZARA kupewa jina lake na hii imetokana na Mh. Rais kutuambia kuwa Mfugale ni mzalendo aliyetukuka kwenye hii nchi yetu kwa ameyanya mengi ila "wajanja" walikuwa wanamfifisha.
Mfano mwingine ni yule mzee aliyetorosha ndege kutoka Kenya kuirudisha Tanzania na mifano mingine ambayo wengi wetu tunaikumbuk qmbqyo Mh. Rais alishawahi kuitoa
Sasa katika kipindi ambacho watu hatujatarajia akatokea MZALENDO mwingine wa KWELI, Profesa (Nadhani sio Pro-pesa) Mussa Assad (SIMBA) ambaye ameyafanya makubwa sana kwenye nchi hii kwa hiki kipindi kupitia taaluma yake na majukumu ambayo anatakiwa kufanya. Bahati nzuri sekta nyingi zimeguswa ikiwepo sekta ya wakubwa wenyewe wa nchi.
katika hili ndo nataka kuona Rais wetu mpendwa achukue maamuzi atatuaminisha kuwa na yeye ni mzalendo wa kweli kwa imma kutomsumbua Assad au kulinda na kumpigania kwa ajili ya maslahi mapana ya nchi yetu dhidi ya watu na taasisi DHAIFU
Patric Mfugale mbali ya kwamba ni mwenyekiti mtendaji wa sekta ya mabarabara ila pia amepewa heshima kubwa ya kuenziwa kwa daraja la pale TAZARA kupewa jina lake na hii imetokana na Mh. Rais kutuambia kuwa Mfugale ni mzalendo aliyetukuka kwenye hii nchi yetu kwa ameyanya mengi ila "wajanja" walikuwa wanamfifisha.
Mfano mwingine ni yule mzee aliyetorosha ndege kutoka Kenya kuirudisha Tanzania na mifano mingine ambayo wengi wetu tunaikumbuk qmbqyo Mh. Rais alishawahi kuitoa
Sasa katika kipindi ambacho watu hatujatarajia akatokea MZALENDO mwingine wa KWELI, Profesa (Nadhani sio Pro-pesa) Mussa Assad (SIMBA) ambaye ameyafanya makubwa sana kwenye nchi hii kwa hiki kipindi kupitia taaluma yake na majukumu ambayo anatakiwa kufanya. Bahati nzuri sekta nyingi zimeguswa ikiwepo sekta ya wakubwa wenyewe wa nchi.
katika hili ndo nataka kuona Rais wetu mpendwa achukue maamuzi atatuaminisha kuwa na yeye ni mzalendo wa kweli kwa imma kutomsumbua Assad au kulinda na kumpigania kwa ajili ya maslahi mapana ya nchi yetu dhidi ya watu na taasisi DHAIFU