Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,495
- 9,275
Mkuu wa wilaya ya Musoma, Vicent Naano ametoa wiki moja kwa wananchi wa kijiji Kakisheri kata ya Nyakatende wilaya ya Musoma Vijijini wanaojihusisha na matukio ya kishirikina kuacha vitendo hivyo haraka na endapo vitandelea basi atafunga shule na kuwahamisha walimu wa Shule ya Msingi Kambarage.
Shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na matukio yasiyo ya kawaida ikiwemo walimu kuingiliwa kimwili nyakati za usiku, kulazwa nje na wanafunzi kudondoka ovyo na kupiga kelele.
DC Naano ametoa maagizo hayo baada ya kutokea kwa tukio la wanafunzi wa darasa la saba katika shule hiyo kuanguka na kupiga kelele, kukuta chakula aina ya makande kikiwa kimewekwa chooni hali iliyowalazimu walimu, wazazi na wanafunzi kupiga kura ili kubaini anayefanya matukio hayo kwa imani ya kishirikina.
IPP
Shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na matukio yasiyo ya kawaida ikiwemo walimu kuingiliwa kimwili nyakati za usiku, kulazwa nje na wanafunzi kudondoka ovyo na kupiga kelele.
DC Naano ametoa maagizo hayo baada ya kutokea kwa tukio la wanafunzi wa darasa la saba katika shule hiyo kuanguka na kupiga kelele, kukuta chakula aina ya makande kikiwa kimewekwa chooni hali iliyowalazimu walimu, wazazi na wanafunzi kupiga kura ili kubaini anayefanya matukio hayo kwa imani ya kishirikina.
IPP