Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
Polisi mkoani Mara inamshikilia mkazi wa kijiji cha Rugasha Bukoba Vijijini, Marco Saidi (68) kwa tuhuma za kuwalewesha abiria kwenye mabasi yanayofanya safari zake kati ya Mwanza-Musoma na kuwaibia.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Longinus Tibushubwamu amesema kuwa mtuhumiwa huyo amekamatwa katika kituo cha mabasi wilayani Bunda mkoani Mara baada ya kumywesha abiria mmoja.
Kamanda Tibishubwamu amesema kuwa mtu huyo anadaiwa kuwalisha na kuwanywesha abiria dawa za kienyeji zinazojulikana kwa jina la khabharagata kutoka nchini Congo kwa lengo la kuwalewesha abiria na kuwaibia mali zao.
Amesema mtu huyo akishirikiana na watu wengine watano (bado hawajakamtwa) wamekuwa wakiwanywesha abiria dawa hizo kwa kuziweka kwenye maji au soda na kupaka kwenye biskuti au pipi kisha kuwapa abiria ambao baada ya kunywa ujikuta wamelewa na kupoteza fahamu.
"Walikuwa wanaweka kwenye kinywaji au anapaka kwenye shati lake eneo la mkononi kisha anasubiri abiria akishakaa yeye anapitisha mkono kama anafungua au kufunga dirisha wakati huo mkono wake anauelekeza kwenye pua ya abiria hivyo abiria anajikuta amevuta hewa baada ya hapo mtu analewa na kupoteza fahamu au anakupa pipi ama biskuti ukila unalewa kisha anaiba na kushuka kabla hajagundulika" amesema.
Mwananchi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Longinus Tibushubwamu amesema kuwa mtuhumiwa huyo amekamatwa katika kituo cha mabasi wilayani Bunda mkoani Mara baada ya kumywesha abiria mmoja.
Kamanda Tibishubwamu amesema kuwa mtu huyo anadaiwa kuwalisha na kuwanywesha abiria dawa za kienyeji zinazojulikana kwa jina la khabharagata kutoka nchini Congo kwa lengo la kuwalewesha abiria na kuwaibia mali zao.
Amesema mtu huyo akishirikiana na watu wengine watano (bado hawajakamtwa) wamekuwa wakiwanywesha abiria dawa hizo kwa kuziweka kwenye maji au soda na kupaka kwenye biskuti au pipi kisha kuwapa abiria ambao baada ya kunywa ujikuta wamelewa na kupoteza fahamu.
"Walikuwa wanaweka kwenye kinywaji au anapaka kwenye shati lake eneo la mkononi kisha anasubiri abiria akishakaa yeye anapitisha mkono kama anafungua au kufunga dirisha wakati huo mkono wake anauelekeza kwenye pua ya abiria hivyo abiria anajikuta amevuta hewa baada ya hapo mtu analewa na kupoteza fahamu au anakupa pipi ama biskuti ukila unalewa kisha anaiba na kushuka kabla hajagundulika" amesema.
Mwananchi