Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,196
- 25,516
Nianze kwa kuweka wazi hapa kuwa mimi si mwanachama wala mfuasi wa chama chochote cha siasa hapa nchini na kwingineko. Lakini, siwezi kukataa ukweli kutoka moyoni mwangu kuwa mimi ni muumini na mfuasi wa demokrasia safi na maendeleo ya nchi yetu.
Sichoki kuonyesha hayo kwa kupongeza kwangu;kukosoa kwangu na hata kushauri kwangu kwa Serikali yangu na vyama vya siasa. Nitaendelea kufanya hivyo kwa maslahi mapana ya taifa letu na ustawi wetu. Sitaacha!
Nimeiona na kuisikia 'clip' moja ya Cyprian Musiba inayotajwa kama kuujibu Waraka wa akina Kinana. Humo, Musiba anasikika akisema "kuwepo ndani ya CCM kunahitaji Ph.D ya unafiki". Kwangu mimi, bila hata kutumia ujuzi wa kisheria nilionao,hiyo ni kauli nzito na 'mbaya'.
CCM ni chama tawala. Ndicho chama kinachounda Serikali. Kinasemwa kama chama cha siasa hapa nchini chenye wanachama wengi zaidi ya vyama vyote vingine. Kuanzia Rais hadi viongozi wote wa kiserikali ni wanachama wa CCM. Wote hao wana Ph.D za unafiki?
Mdomo huponza kichwa. Hakika, Musiba amewatukana, kuwabagaza na kuwadhalilisha wanachama wote wa CCM ikiwa ni pamoja na viongozi wa kiserikali. Musiba anapaswa kudhibitiwa haraka.
Hana haki wala haja ya kudhalilisha chama tawala na wanachama wake wote kwa kusema kuwa wana Ph.D za unafiki. Asome kwanza maana ya unafiki kwenye Kamusi na kuwapima tena anaowazungumzia.Eti hiyo ndiyo sifa ya kuwa mwanachama wa CCM. Like seriously?
Sichoki kuonyesha hayo kwa kupongeza kwangu;kukosoa kwangu na hata kushauri kwangu kwa Serikali yangu na vyama vya siasa. Nitaendelea kufanya hivyo kwa maslahi mapana ya taifa letu na ustawi wetu. Sitaacha!
Nimeiona na kuisikia 'clip' moja ya Cyprian Musiba inayotajwa kama kuujibu Waraka wa akina Kinana. Humo, Musiba anasikika akisema "kuwepo ndani ya CCM kunahitaji Ph.D ya unafiki". Kwangu mimi, bila hata kutumia ujuzi wa kisheria nilionao,hiyo ni kauli nzito na 'mbaya'.
CCM ni chama tawala. Ndicho chama kinachounda Serikali. Kinasemwa kama chama cha siasa hapa nchini chenye wanachama wengi zaidi ya vyama vyote vingine. Kuanzia Rais hadi viongozi wote wa kiserikali ni wanachama wa CCM. Wote hao wana Ph.D za unafiki?
Mdomo huponza kichwa. Hakika, Musiba amewatukana, kuwabagaza na kuwadhalilisha wanachama wote wa CCM ikiwa ni pamoja na viongozi wa kiserikali. Musiba anapaswa kudhibitiwa haraka.
Hana haki wala haja ya kudhalilisha chama tawala na wanachama wake wote kwa kusema kuwa wana Ph.D za unafiki. Asome kwanza maana ya unafiki kwenye Kamusi na kuwapima tena anaowazungumzia.Eti hiyo ndiyo sifa ya kuwa mwanachama wa CCM. Like seriously?