Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,495
- 9,275
Kwa mara nyingine tena Rais Yoweri Museveni ameishutumu kampuni kubwa ya teknolojia ya mawasiliano Facebook kwa kuwa na upendeleo dhidi ya chama tawala cha Uganda na wafuasi wake.
Matandao huo wa kijamii ulifunga akaunti kadhaa zenye uhusiano na chama cha National Resistance Movement (NRM) siku kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi Januari, ikizituhumu kuhusika katika uratibu wa mienendo isiyo ya kuaminika katika jaribio la kushawishi mdahalo wa umma kabla ya uchaguzi huo.
Wakati huo Bw Museveni aliishutumuFacebook kwa "majivuno " na akatangaza kupigwa marufuku kwa mtandao huo. Hadi sasa mtandao huo haupatikani nchini Uganda isipokuwa kwa kutumia mtandao wa) Virtual Private Network (VPN
Katika mkutano wa Jumapili na "waathiriwa wa Facebook" – Wajumbe wa NRM ambao akaunti zao zilifungwa-rais aliwaambia wako vyema bila mtandao huo.
"Tangu Facebook iondoke, mliwahi kusikia kuna uhaba wa sukari mjini? Hamna nguo ? Facebook itaongea lakini tutasonga, wao sio Mungu ,"Bw Museveni alisema.
Aliongeza kuwa: ‘’Hii ndio sababu katika baahdi ya nchi hawaruhusiwi, je wanafanya kazi Uchina? Tuachane na hayo, kile nilichosikia ni kwamba Mungu yupo kila mahali, kila mahali na anafahamu kila kitu. Sijawahi kusikia kwamba Facebook iko katika kitengo hicho."
BBC
Matandao huo wa kijamii ulifunga akaunti kadhaa zenye uhusiano na chama cha National Resistance Movement (NRM) siku kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi Januari, ikizituhumu kuhusika katika uratibu wa mienendo isiyo ya kuaminika katika jaribio la kushawishi mdahalo wa umma kabla ya uchaguzi huo.
Wakati huo Bw Museveni aliishutumuFacebook kwa "majivuno " na akatangaza kupigwa marufuku kwa mtandao huo. Hadi sasa mtandao huo haupatikani nchini Uganda isipokuwa kwa kutumia mtandao wa) Virtual Private Network (VPN
Katika mkutano wa Jumapili na "waathiriwa wa Facebook" – Wajumbe wa NRM ambao akaunti zao zilifungwa-rais aliwaambia wako vyema bila mtandao huo.
"Tangu Facebook iondoke, mliwahi kusikia kuna uhaba wa sukari mjini? Hamna nguo ? Facebook itaongea lakini tutasonga, wao sio Mungu ,"Bw Museveni alisema.
Aliongeza kuwa: ‘’Hii ndio sababu katika baahdi ya nchi hawaruhusiwi, je wanafanya kazi Uchina? Tuachane na hayo, kile nilichosikia ni kwamba Mungu yupo kila mahali, kila mahali na anafahamu kila kitu. Sijawahi kusikia kwamba Facebook iko katika kitengo hicho."
BBC