Naomba ushauri juu hili la viboko mashuleni. Kumekuwepo na kasumba imejitokeza katika shule za sekondari wilaya ya kyela. Walimu wanapiga wanafunzi kama vile sio binadamu.
Mwanafunzi kupigwa fimbo hadi hamsini kwa wakati mmoja, tena maeneo tofauti tofauti. Kama mikononi, mgogoni, miguuni, matakoni ndio usiseme.
Kuna shule kama za sekondari Bojonde, Ngonga Masukila, hizo ni mifano tu ya shule nilizo na uthibitisho Nazo. Ila kwa taarifa zilizopo ni kwamba hii kasumba imeambukiza shule nyingi za wilaya ya kyela.
Athari zilizoanza kujitokeza ni kwamba wanafunzi wanaacha shule kisa kuogopa mijeledi ambayo haina kiasi. Ni mifano ya wanafunzi watatu katika shule ya sekondari Bujonde walioacha shule, (majina nitayahifadhi).
Athari nyingine ni kwamba sio kuwa nidhamu inatengezwa ila woga ndio uliotengezwa kwa wanafunzi. Hakuna mwanafunzi anayesema "mwalimu flani anafundisha vizuri" zaidi ya walimu kushindana idadi ya viboko anavyopiga wanafunzi.
Waziri wa elimu na wadau wa elimu liangalieni hili suala katika wiliya ya kyela. Kwa sababu moja, halijengi nidhamu kwa wanafunzi ila woga, Pili, haliongezi ufaulu kwa wanafunzi kwa sababu walimu hawafundishi afu wanapiga sana viboko.
Mfano wiki iliyopita shule ya Bujonde wa form one wamefanya test ya civics lakini hawajawahi fundishwa, wanafunzi wakapata zero wameambulia viboko zaidi ya ishirini kwa kila mmoja.
Ninaomba sana maana wanafunzi wameanza kutokupenda shule na kufikia kuacha shule. Maana wanaona shule sio sehemu ya kujifunza ila ni sehemu ya mateso.
Mwanafunzi kupigwa fimbo hadi hamsini kwa wakati mmoja, tena maeneo tofauti tofauti. Kama mikononi, mgogoni, miguuni, matakoni ndio usiseme.
Kuna shule kama za sekondari Bojonde, Ngonga Masukila, hizo ni mifano tu ya shule nilizo na uthibitisho Nazo. Ila kwa taarifa zilizopo ni kwamba hii kasumba imeambukiza shule nyingi za wilaya ya kyela.
Athari zilizoanza kujitokeza ni kwamba wanafunzi wanaacha shule kisa kuogopa mijeledi ambayo haina kiasi. Ni mifano ya wanafunzi watatu katika shule ya sekondari Bujonde walioacha shule, (majina nitayahifadhi).
Athari nyingine ni kwamba sio kuwa nidhamu inatengezwa ila woga ndio uliotengezwa kwa wanafunzi. Hakuna mwanafunzi anayesema "mwalimu flani anafundisha vizuri" zaidi ya walimu kushindana idadi ya viboko anavyopiga wanafunzi.
Waziri wa elimu na wadau wa elimu liangalieni hili suala katika wiliya ya kyela. Kwa sababu moja, halijengi nidhamu kwa wanafunzi ila woga, Pili, haliongezi ufaulu kwa wanafunzi kwa sababu walimu hawafundishi afu wanapiga sana viboko.
Mfano wiki iliyopita shule ya Bujonde wa form one wamefanya test ya civics lakini hawajawahi fundishwa, wanafunzi wakapata zero wameambulia viboko zaidi ya ishirini kwa kila mmoja.
Ninaomba sana maana wanafunzi wameanza kutokupenda shule na kufikia kuacha shule. Maana wanaona shule sio sehemu ya kujifunza ila ni sehemu ya mateso.