Muongozo wa kununua vifaa vinavyotumia processor za intel

Hivi ukitumia laptop yenye core 2duo inakuwa na kasi au
Computer nyingi tunazonunua huwa zinatumia processor za intel au amd, lakini ni intel ambaye ametawala sana kushinda amd kwenye computer zetu. Leo nimeamua niandike uzi huu kuhusu hizi processor za intel na namna ya kuzichagua ili kuwasaidia watu wanapotaka kununua laptop/desktop mpya wafanye maamuzi sahihi.
Processor ni nini?
Labda utakuwa unajiuliza kwa nini ukitaka kununua laptop mpya unatakiwa uangalie processor? Nini cha muhimu kuhusu hii processor?
-Kwa lugha rahisi processor ni kifaa ndani ya computer yako kinachobeba maagizo ya program za computer. Maagizo hayo yanaweza kuwa ya kimahesabu, kimantiki, maagizo yanayoingia kwenye computer na yanayotoka.
-jinsi processor inavyokuwa na speed kubwa ndio jinsi maagizo yatakavyofanywa haraka na ndio jinsi program za computer zitakavyofanya kazi upesi.
processor_01.jpg

Familia ya processor za intel
Intel wana processor za aina nyingi na ni ngumu kuzitaja kwa pamoja, ila wameturahisishia kwa kuzipanga processor zao kwenye familia. Na hii ndio familia yao.
1. Atom processor- processor hizi hutumika kwenye vimini laptop na tablet ni ndogo kiumbo ndio maana hata vifaa vyake ni vidogo, processor hizi hazina nguvu sana na vifaa vyake hukaa sana na chaji.
2. Celeron processor- Haina tofauti sana na atom ila hii ina afadhali kidogo. Inatumika kwenye vifaa vikubwa kuliko atom kama vile laptop kubwa na desktop
3. Pentium- hii ina speed kuliko celeron na atom pia inatumika kwenye vifaa vikubwa.
4. Core 2 duo- hii ni maarufu kwa perfomance yake ya multitasking, inauwezo wakufanya mambo mengi kwa wakati mmoja ila nyingi ni za kizamani.
5. Core i3- hii ni processor latest za intel ni dual core lakini core zake zina perfomance kubwa na pia inakuwa na thread 2 kwenye kila core, ni nzuri kwa wanaotaka perfomance kubwa kwa bei rahisi.
6. Core i5- ya laptop ni dualcore na ya desktop ni quadcore isiyokuwa na thread, software nyingi kubwa duniani zimekuwa optimized kutumia core kama za i5, ni nzuri sana kwa watu wanaotumia software zinazodemand perfomance lakini hawafanyi multitasking.
7.Core i7- hii inakuwa na quadcore processor na thread 8 kwenye desktop na pia inaweza kuwa dualcore kwenye laptop. Hii ndio processor nzuri zaidi kwa watu wa kawaida na inafanya multitasking hata kama software zinademand sana.
8. Xeon- hii ndio processor yenye speed zaidi kwenye processor za intel lakini imekuwa designed kufanya kazi kwenye computer kubwa kama vile server. Unapohost website processor kama hii ndio inayoprocess webpages.
Generation ya processor(muhimu)
Ni muhimu sana kujua processor inatokea generation ipi kuna processor zenye i7 ya 2010 ambazo zipo slow vibaya mno, na pia kuna uwezekano i3 kuipita i7 kwenye perfomance kama zinatoka generation tofauti. Hivyo eneo hili inabidi uwe makini kuepuka kuuziwa mbuzi kwenye gunia. Hivyo unaponunua laptop/desktop ni lazima ujue ipo generation gani la sivyo upo hatarini na hivi ndio namna ya kujua.
- Processor yenye namba inayoanziwa na elfu nne ni fourth generation(4xxx)
Mfano Intel i3-4130.
- Processor yenye namba inayoanziwa na elfu tatu ni third generation (3xxx)
Mfano i3-3130.
- Processor inayoanziwa na elfu mbili ni second generation(2xxx)
Mfano i3-2140
Sishauri kabisa kununua processor ya first generation, mtu unatakiwa atleast ununue ya second generation na pia bei inatakiwa iwe ndogo kwa hii second compare na third/fourth.
Processor ndogo kama atom na celeron zina generation zake ambazo ni
-clover trail
-bay trail
Processor za zamani za atom zilikuwa mbaya sana na zipo slow ila baytrail ikaja kuzipa nguvu na kuzifanya ziwe na perfomance kubwa, hivyo kama unataka kifaa cha atom/celeron make sure processor yake iwe inatoka generation ya baytrail.
Herufi za mbele ya processor(muhimu)
Kama umechunguza mbele ya processor kunakuwa na herufi mbali mbali hizi pia ni muhimu sana kuzijua kwani usipozizingatia unaweza kujuta.
Mfano processor inaweza kuitwa i5-4000m au i5-4000u au i5-4000y je nini kinatofautisha hizi processor?
1. Herufi kwenye processor za desktop.
Bila herufi – hii inakuwa na speed halisi ya processor mfano i7-4770
K- herufi hii inamaanisha processor ipo unlocked na unaweza kui over clock na kuongeza speeed. Processor yenye 3.5ghz unaweza kui overclock ikafika 4ghz. Jina lake linakuwa mfumo huu i7-4770K. ni nzuri sana kwa wanaocheza magame na kufanya rendering.
R- herufi hii inamaanisha processor hii ni ndogo sana na inaweza kutumika kwenye videsktop vyenye umbo dogo hali ya kuwa ina graphic kubwa kama iris pro. Jina lake linakuwa mfumo huu i7-4770R hii ni nzuri kwa wale wenye ofisi ambazo ni safi hawataki mawaya mengi na desktop kubwa kukaa kwenye meza. angalia picha hapo chini uone desktop ndogo.
brix1_s.gif

S- herufi hii inamaanisha hiyo proceesor wame optimize perfomance mara nyingi wanai underclock kuzuia processor kupata joto sana. Mfano i7-4770 ina 3.4ghz lakini i7-4770S ina 3.1ghz tu, ina maana hapa wamepunguza 300mhz kutoka stock kuja S.
T- herufi hii inamaanisha processor inatumia power ndogo, kwa wale wenzangu wanaotumia luku kama unataka desktop isiokula umeme basi hii ndio yenyewe ila perfomance nayo itapungua kidogo. Mfano wa jina ni i7-4770T
2. Herufi mbele ya processor za laptop(mobile)
Tumeshaona herufi mbele ya desktop, sasa hivi tuangalie herufi mbele ya processor za laptop ambazo pia zinaweza kutumika kwenye home theatre pc (htpc) au wengine wanaita mini desktop.
M- herufi hii inamaanisha hio processor ni mobile, ndio herufi common kwenye processor za laptop mfano i5-4000M
U- herufi hii inamaanisha processor ya laptop inatumia power ndogo hizi processor zinatumika sana kwenye vilaptop vyembamba (ultrabook). Kwa sababu zinakaa na chaji kutokana na kutumia power ndogo, perfomance yake nayo pia ni ndogo. Mfano i5 4250U
Y- hii ni ultra low power yaani inakula umeme mdogo kushinda hata U lakini vile vile perfomance inazidi kushuka nayo mfano i7-4610Y
HQ- herufi hii inamaanisha high perfomance, zinauzwa bei ghali sana na power yake inashindana na desktop. Usije ukajaribu kuieka kwenye mapaja laptop ya design hii maana zinashika moto upesi sana kutokana na quality ya processor. Ni nzuri kwa wale wanaopenda kucheza game, kutumia software kubwa wakiwa kitandani. Mfano ni i7-4700HQ
MQ- herufi hii inamaanisha hio procesor ni quad core. Kama umesoma vizuri juu i5 na i7 za desktop ni quadcore lakini za laptop ni dualcore, hivi processor hii inamaanisha unaweza tumia quadcore kwenye laptop yako kama unataka mfano i7-4900MQ
MX- herufi hii inamaanisha ni xtreme edition, processor hii unaweza kui over clock kama vile K series ya desktop na ina perfomance kubwa sanaaa, ila kuwa makini na mapaja tu.
Mfano i7-4940MX
Huu ndio muongozo wa kununua processor za intel, kama kuna sehemu hujapaelewa unaweza kuuliza nitaelezea zaidi.
 
Inategemea na unachokifanya
Unapendekeza laptop au desktop zipi ?
Nataka run hii software hapa chini kwajili ya rendering

Lumion recommends the following minimum requirements:

OS: Windows XP, Vista, 7, 8 (32- and 64-bit) and DirectX 9.0c or later
System memory: 3 GB
Graphics card: NVIDIA GeForce GTS 450 or ATI/AMD Radeon HD 4890, with at least 1 GB dedicated memory (not shared system memory)
 
Unapendekeza laptop au desktop zipi ?
Nataka run hii software hapa chini kwajili ya rendering

Lumion recommends the following minimum requirements:

OS: Windows XP, Vista, 7, 8 (32- and 64-bit) and DirectX 9.0c or later
System memory: 3 GB
Graphics card: NVIDIA GeForce GTS 450 or ATI/AMD Radeon HD 4890, with at least 1 GB dedicated memory (not shared system memory)
Mbona hakuna cpu?
 
Nimezitoa kwenye website kama zilivyo, anyway nimeambatanisha screenshot
View attachment 1144707

Ebu pendekeza desktop ambazo naweza pata kwa budget ya 300K to 500K

Laptop zipi zitafaa kwa hii software
Mkuu hio software ni demanding Sana. Kwa hio budget huwezi kupata Kila kitu. Graphics minimum ni passmark 2000, in maana ukikosa kabisa ni GT 1030 chini ya Hapo haitarun na recommended ni passmark point 8000 Ina maana Hapo ni gtx 1060 maana hadi 1050ti Ina point 6000.

Kutoka kwa 8th gen desktop za 7th na 6th gen zimeshuka Sana Bei, nimenunua i5 6500 desktop kwa laki 4 tu na nimeziona za 7th gen kwa laki 5 (i5 7500)

Ushauri wangu Kama utapata ya 7th gen yenye ram 8GB ama zaidi nunua, ila Kama Zina 4GB ram nunua 6th gen, kwenye 6th gen utaweza tumia ram za DDR3 ama DDR4 (tegemea na motherboard), hizi ram za DDR3 zinapatikana kirahisi kwa Bei nafuu hapa Tanzania, hivyo itakuwa rahisi ku Upgrade.

Ukipata 6th gen kwa laki 4, utai upgrade taratibu, inakuwa na slot 4 za ram moja wanakuwekea na tatu uta upgrade mwenyewe taratibu.

Weakness za hizi desktop ni power supply Ndogo hivyo itakulimit Sana kwenye graphics, utaweza tumia Nvidia 750ti, 1030 ama amd rx 550.

Graphics itabidi uweke mwenyewe baadae.

Kuhusu laptop hadi 940mx/940m hazifiki passmark 2000 hivyo itaku cost kuanzia 1m hivi.

Laptop ya rahisi ambayo inakidhi baadhi ya vigezo ni Lenovo IdeaPad 330s yenye Ryzen 5 2500u na yenyewe inauzwa dola 400 huko ughaibuni. Mpaka ije huku inazidi milioni.
 
Pia mkuu Soma hapa kuhusu graphics hio Ndogo ipo limited kwenye majengo madogo tu, majengo makubwa Kama viwanja vya mipira ama miji inataka passmark 10k level za kina 1080 na Titan.
 
Pia mkuu Soma hapa kuhusu graphics hio Ndogo ipo limited kwenye majengo madogo tu, majengo makubwa Kama viwanja vya mipira ama miji inataka passmark 10k level za kina 1080 na Titan.
Ok mkuu shukrani kwa maelezo mazuri
 
Ina maana pia kulingana na generation. Mabadriko kwa upande wa Gpu ni makubwa kuliko CPU?
 
Ina maana pia kulingana na generation. Mabadriko kwa upande wa Gpu ni makubwa kuliko CPU?
Ndio mkuu na siku zote kwa same generation i3/i5/i7 zinakuwa na GPU moja. Hivyo GPU ya i3 5005u ni sawa na i5 5200u au i7 5500u, ndio maana unaona japo i3 inapitwa performance ila GPU ipo vizuri.
 
Chief naomba niangalzie hii Dell
Processor akeView attachment 1182874
Processor yake inaitwa core M mkuu, na Hapo ameandika generation ya Saba.

Ila M3 6Y30 Kama alivyoandika yeye Ni generation ya 6 na sio Saba. Ingekuwa gen ya 7 ingekuwa m3 7y30

Ila nimeicheki online hio model Ina 7th generation, hivyo kimoja wapo Hapo juu amekosea, Ni vyema kabla hujanunua ukahakiki mwenyewe specification Hawa Jamaa hawaaminiki.

Kuhusu laptop yenyewe sababu Ina core m Ina maana itakula umeme kidogo Sana, core m inakula umeme kidogo Kushinda hata taa ya kawaida ya nyumbani just 4W tu.

Hivyo Kama unataka laptop yenye umbo Dogo na inayokaa na chaji, hio Ni laptop sahihi.

Kama unataka laptop yenye nguvu na ya kucheza games na kufanya kazi nzito achana nayo, tafuta laptop ya 8th gen, gape la performance baina ya 8th na 7th gen Ni kubwa Sana.
 
Processor yake inaitwa core M mkuu, na Hapo ameandika generation ya Saba.

Ila M3 6Y30 Kama alivyoandika yeye Ni generation ya 6 na sio Saba. Ingekuwa gen ya 7 ingekuwa m3 7y30

Ila nimeicheki online hio model Ina 7th generation, hivyo kimoja wapo Hapo juu amekosea, Ni vyema kabla hujanunua ukahakiki mwenyewe specification Hawa Jamaa hawaaminiki.

Kuhusu laptop yenyewe sababu Ina core m Ina maana itakula umeme kidogo Sana, core m inakula umeme kidogo Kushinda hata taa ya kawaida ya nyumbani just 4W tu.

Hivyo Kama unataka laptop yenye umbo Dogo na inayokaa na chaji, hio Ni laptop sahihi.

Kama unataka laptop yenye nguvu na ya kucheza games na kufanya kazi nzito achana nayo, tafuta laptop ya 8th gen, gape la performance baina ya 8th na 7th gen Ni kubwa Sana.
Nmeona insta jamaa wanaziuza....ila bei za kule siziamini mana pc ina specs kubwa afu bei chee
 
Back
Top Bottom