Muongozo na ushauri kwa wanafunzi waliopokea matokeo ya kidato cha nne 2018

Casuist

JF-Expert Member
Jul 23, 2014
1,179
2,940
Habari wakuu,

Kuna wadogo zetu wamepata matokeo yao ya kidato cha nne leo. Ni ngwe muhimu sana kwenye maisha yao, kwa sababu ndio inayotoa upepo awe nani baadae kitaaluma kwa uchaguzi anaofanya sasa japo kwa baadhi wanaweza kuwa na wigo mpana wa kuchagua tena baadae.

Hapa jukwaani kuna wengi ambao walipita huko na wana uzoefu wa matokeo tofauti, iwe ya kufaulu, wastani au kufeli na jinsi gani walijikwamua kutoka kwenye hali yaliyokuwa nao wakati husika.

Kwa pamoja naamini tunaweza kuwapa mwanga hawa wadogo zetu wapunguze idadi ya makosa yanayotokana na kutokuwa na ufahamu ama kukata tamaa kwa kupata matokeo hafifu. Kwa heshima ningependa kuwaita wanajamvi wote katika kufikisha lengo la mada hii.

Karibuni!

Swala la kwanza kama mzazi/mlezi muulize mwanao anapenda kwenda A level au anapenda kwenda chuo?maana kuna wazazi wengine wanalazimisha watoto wao kwenda A level ilihali mtoto hataki kwenda huko ,anataka kwenda chuo!

Akikujibu chuo, muulize anapenda kusomea mambo gani,kutoka moyoni akujibu anavyofeel!

Then,mpeleke akasomee anachotaka!

Faida yake

Kutokana na kuwepo kwa wimbi la ukosefu wa ajira ,itamsaidia kufanya kitu akipendacho,hali itakayompelekea aweze kujiajiri!

Mfano,akisema anataka kuwa mwalimu mpeleke,kwani huko atasoma kwa bidii na kuelewa mambo hivyo itamsaidia kufanya chochote juu ya field yake kwa sababu utakuwa na uelewa wa kutosha! Kuliko kumpeleka kusoma kwa kuangalia kuajiriwa hali itakayomfanya asome akifikiria kuajiriwa hivyo atakariri kuliko kuelewa (hii itamcost sana)

Akisema A level

Kuna baadhi ya wazazi hawapendi wanao waende A level,wanataka waende diploma baada ya form iv,tafadhali kama mwanao anapenda A level,mpeleke A level...,hii itamsaidia kusoma kwa bidii kwa sababu hili ndilo limekua chaguo lake!

Mwisho napenda kuwakumbusha wale wazazi ambao watoto wao wanataka kwenda chuo ,waombe kwani dirisha la maombi litafunguliwa Siku si nyingi kwa ajili ya march intake 2019

Nitaendelea kuelezea wanafunzi ambao wamepata matokeo ambayo hawakuyatarajia wafanye Nini ili kuwepo kwenye njia sahihi!

🤝🤝🤝🤝🤝🤝🤝🤝

Blogger boy
 
Kufaulu ama kufeli yote ni mipango ya Mungu kikubwa tu nikutokufa moyo, mie nina diploma ya local government administration ni mwajiriwa ktk moja ya halmashauri hapa nchini, matokeo yangu ya kidato cha nne ya kwanza sikufanya vizuri niliambulia 4 ya 29, nikarisit kwakuwa nilikuwa naamini kuwa ili ufanikiwe lazima upitie advance level hivyo nika risit tena kilicho nikuta sitakuja kaa nisahau kwa niliambulia D 2 tuu,

Ndipo nilipojiunga na Chuo cha serikali za mitaa kilichopo Dodoma nikaanza certificate nilipomaliza mwaka mmoja nikaajiriwa , diploma yangu nimemaliza nikiwa kwenye system, kwahiyo maisha muda mwingine ni techniques tuu, hujafanikiwa kufanya vizuri umepata D zako nne tafuta chuo chochote kilichosajiliwa nenda kasome kozi inayoajirika, au unayoweza kujiajiri.
 
Waliofaulu wanatakiwa wachukue tahasusi nzuri ambayo aitegemei matokeo ya o level Kwenda chuo kikuu. Wale wa science watafakali tcu wanataka ngapi form 6 uende chuo sio c 3 olevel uende pcb chuo ndo kwa heri
 
Hivi unamsaidiaje kijana alieyapata div 4 ya 26 mwenye C Mbili na D zote. Anaweza kwenda form 5 kwa matokeo hayo? Kama hawezi kuna mbadala gani ukizingatia umri huo bado ni mdogo.

Ni changamoto sana kwa wazazi na walezi ambao matokeo hayajawa mazuri.
 
Aiise nichangamoto ila kufeli mtihani sio kufeli maisha .
Anaweza kuingia kwenye uzalishaji kama unaona kitabu unapoteza muda.
Kilimo bado kinalipa

Biashara ndogo ndogo kuelekea biashara kuwa Ufundi

Uwakala hasa kwenye mabasi inalipa kwa Elimu yako akiwa na Basi zako 3 umeula
Uvuvi

Ufugaji hasa nguruwe na kuku , Ng'ombe hawalipi kwa utawala huu
Usindikaji vyakula binadamu & mifugo
 
Aiise nichangamoto ila kufeli mtihani sio kufeli maisha .
Anaweza kuingia kwenye uzalishaji kama unaona kitabu unapoteza muda.
Kilimo bado kinalipa
Biashara ndogo ndogo kuelekea biashara kuwa
Ufundi
Uwakala hasa kwenye mabasi inalipa kwa Elimu yako akiwa na Basi zako 3 umeula
Uvuvi
Ufugaji hasa nguruwe na kuku , Ng'ombe hawalipi kwa utawala huu
Usindikaji vyakula binadamu & mifugo
Acha kudanganya watu wewe kilimo hakilipi Tanzania
 
Habari zenu wanaJF

Kuna thread niliwahi kuandika mwaka jana iliyokuwa inasema NALIAMSHA DUDE LA NECTA TAREHE 30 OKTOBA
Leo nimewaletea mrejesho huu
Literature In English D
Geography F
History B
Civics D

NB
Hilo somo la Literature In English lilisajiliwa kimakosa pale Posta ya Temeke tarehe 28.02.2017 badala ya kuandika English Language wameniandikia Literature In English.
Je naweza kujiunga kidato cha 5 mwaka huu na shule gani itaweza kunipokea?

Nina C ya Kiswahili niliyoipata miaka ya nyuma kabla ya kuwa Private Candidate.
 
Habari zenu wanaJF

Kuna thread niliwahi kuandika mwaka jana iliyokuwa inasema NALIAMSHA DUDE LA NECTA TAREHE 30 OKTOBA
Leo nimewaletea mrejesho huu
Literature In English D
Geography F
History B
Civics D

NB
Hilo somo la Literature In English lilisajiliwa kimakosa pale Posta ya Temeke tarehe 28.02.2017 badala ya kuandika English Language wameniandikia Literature In English.
Je naweza kujiunga kidato cha 5 mwaka huu na shule gani itaweza kunipokea?

Nina C ya Kiswahili niliyoipata miaka ya nyuma kabla ya kuwa Private Candidate.
mkuu unapataje Geography F wkt ni somo simple hata usiposoma unafaulu
 
Hivi unamsaidiaje kijana alieyapata div 4 ya 26 mwenye C Mbili na D zote. Anaweza kwenda form 5 kwa matokeo hayo? Kama hawezi kuna mbadala gani ukizingatia umri huo bado ni mdogo.

Ni changamoto sana kwa wazazi na walezi ambao matokeo hayajawa mazuri.
si ajarbu kureseat atafute credit moja changamoto iko wapi hapo??
 
Back
Top Bottom