MUONGOZO: Mambo ya kuzingatia unaponunua gari lililotumika ndani ya Tanzania

BREVIS imetulia sana barabarani kwa safari ndefu hasa ukiwa una mwendo (zaidi ya 100 kph, tatizo tochi/faini) pia zinabugia mafuta mithili ya PRADO. Xtrail jiandae kwa kukusanya namba za mafundi magari angalau 10.

Ko X trail ni kimeo yaani
 
Ko X trail ni kimeo yaani
Mimi mtu akiniambia xtrail ni kimeo sikubali. yupo mtu ninayemfahamu anaitumia huu mwaka wa nne na route zake ni arusha tanga. ukweli watu hatujui kuzitunza. rejeta wanatia maji, oil siyo iliyokuwa prescribed na manufacturer lazima ife.
 
Mimi mtu akiniambia xtrail ni kimeo sikubali. yupo mtu ninayemfahamu anaitumia huu mwaka wa nne na route zake ni arusha tanga. ukweli watu hatujui kuzitunza. rejeta wanatia maji, oil siyo iliyokuwa prescribed na manufacturer lazima ife.
Xtrail vs RAV 4 je?
 
wabongo hawajui magari. Wengi wananunua kisa eti plate number. Hawaangali mileage ya gari,ubora hapana ilimradi inaonekana vizuri nje.

hawa madalali ni kuwapiga marufuku.
 
Sorry kama nitakuwa nje ya mada, endapo nikiwa na 4M ninaweza kuagiza Vitz Japan? Au itabidi ninunue tu used za hapa TZ?
 
Ni bora nitoboke mfuko ila mimi huwa sipendi vitu used... huwa napenda sana kumenya karatasi ya vitu vipya tu... usafiri wangu ni daladala ila gari yangu ya kwanza lazima ni zame showroom ni menye mwenyewe....

Yote kwa yote pongezi kwa kutujuza! Safi
 
Aisee asante sana kwa ushauri wako muruwa yaani huwezi amini wiki hii yote natafuta gari lakini kwa style niliyoiona ya madalali ni usanii mtupu,huu uzi wako ni kama umeniona mimi jinsi ninavyotafuta gari bila mafanikio

Mungu akubariki
 
Mkuu RRONDO Mungu akubariki sana kwa huu Uzi, mi natafuta Harrier old model, vipi unanishauri nini na labda bei zake kwa hapa TZ inaendaje? Thanks in advance
 
Baada ya kusikia watu wengi 'wakiumizwa' na 'kupigwa' wakiwa kwenye harakati za kutafuta usafiri uliotumika nchini, nimeona sio mbaya nikitoa ushauri ni jinsi gani unaweza kuepuka majanga kwenye zoezi hilo.

Naandika kama mnunuzi au muuzaji wa aina hio ya magari, kwahio siegemei upande wowote na ninachokiandika hapa sio sheria naweza kuwa sahihi au nisiwe sahihi ila ni imani yangu lipo litakalosaidia baadhi ya watu.

Njia muhimu za kufuata ili kupata gari unalotaka ni kama ifuatavyo:

1. Fanya utafiti mdogo juu ya gari unalolitaka: Uliza ujue gari unalolitaka linauzwa kiasi gani[makadirio]. Ukiweza kujua bei ya showroom au ukiagiza mwenyewe Japan halafu linganisha na bei utakayopewa hapa. Hili ni muhimu kwa sababu nimeshuhudia watu wananunua magari yaliyotumika Tanzania kwa bei ambayo ukiagiza mwenyewe unalipata kutoka japan au ukiongeza kidogo tu unapata la showroom.

2. Usiwe na haraka: Usiwe na haraka kabisa kwenye kutafuta gari. Utaletewa kila aina ya gari na usipokuwa makini utanunua gari bovu. Angalia taratibu angalau magari matano tofauti kwenye chaguo lako ndipo uamue, madalali watakusumbua ili mradi tu wapate cha juu.

3. Epuka madalali: Kama unaweza epuka madalali. Tafuta gari kwa kuuliza watu ulio karibu nao, ndugu jamaa na marafiki au unaofanya nao kazi au biashara. Hii ni nzuri chochote kikitokea una pa kuanzia. Madalali wengi hawajali maslahi yako wala ya muuzaji cha muhimu kwao ni cha juu tu. Gari la 4m dalali atakuuzia 5-6m.

4. Tafuta Fundi: Ukilipenda gari lolote tafuta fundi akusaidie kulikagua, hata kama una ujuzi(idea) na magari kuna vitu hutaviona ila fundi atakusaidia. Kuwa makini kuna mafundi huwa wanabonyezwa wakufiche hitilafu halafu baadae wanarudi kupewa chao ukishauziwa kanyaboya.

5. Epuka gari lililopigwa rangi: Epuka gari iliopigwa rangi siku chache kabla ya kuwekwa sokoni, wazoefu wanajua gari za aina hio ndio umuhimu wa fundi unapokuja. Gari inaweza kuwa imegongwa hivyo imenyooshwa na wanakuzuga kwa rangi inayong'aa. Siku hizi rangi hata 200,000 unapiga gari nzima ila ukinunua hilo baada ya mwezi rangi inababuka yote.

6. Epuka gari lililooshwa engine: Ukikagua gari ukiona limeoshwa engine ogopa sana. Mara nyingi magari yanaoshwa engine kuficha 'leakage', yaani oil na vitu vingine vinavyovuja kutoka sehemu mbalimbali za engine.

7. Jaribu gari wewe mwenyewe: Ni muhimu kuendesha na kuijaribu gari wewe mwenyewe hata ukienda na fundi. Ipitishe njia mbovu usikie jinsi ilivyo chini, chochote kinachogonga kuwa makini, usisikilize ukiambiwa ni tatizo dogo, kwanini hakurekebisha. Ingawa yapo matatizo madogomadogo ila kuwa makini.

8. Usiangalie plate Namba: Usibabaishwe na namba, eti hii C, D etc. Kuna gari namba A ziko vizuri kuliko namba C. Muhimu ni hali ya gari husika kwa muda huo.

9. Nenda TRA kujiridhisha: Ni muhimu kujua ukweli na status ya gari na mwenye gari. Jiridhishe anaekuuzia ndio mwenye gari. Akuonyeshe nyaraka zote halisi hata za kodi aliolipia.

10. Mwisho kabisa ukilipenda gari fanyeni makabidhiano kwa kuandikishana kwa mwanasheria. Ukiweza lipia benki na ubaki na risiti kama ushahidi wa malipo kupitia akaunti yake. Epuka kubeba cash kumpelekea muuzaji mahali alipo.

Haya machache naamini yanaweza kuwa msaada kwa watu wanaonunua magari yaliyotumika nchini,wengine mnaweza kuongezea mawili matatu na kurekebisha nilipokosea.



Naomba nifahamishe kuhusu Toyota Alphard 2400cc ulaji mafuta kwa long Safari na mizunguko ya mjini. Weakness zake na ubora wake.
 
Kwa kuwa inaonekana wabongo wengi wanapotaka kununua magari yalotumika ndani ya bongo kitu kikubwa wanachoangalia ni mileage ambayo gari imetembea basi nawaasa ndugu zanguni kuweni makini sana,kuna huu utapeli wa kurudisha km za maga, na wengi hurudisha nyuma chini ya km laki moja na nusu au chini ya laki moja!Cha kufanya: Zingatia zaidi uzima wa injini kwa kuwa gari ni injini asikudanganye mtu,ukitaka kununua tafuta mtu mwenye weledi wa magari akukagulie gari,kuna gari zimetembea km nyingi lkn ziko well maintained na kuna gari zina km ndogo lkn vimeo!Pia km gari unalotaka kununua huyo mmiliki aliliagiza mwenyewe toka nje,mwambie akuoneshe inspection document zilizokuja na gari huwa zinaonesha gari imeingia ikiwa inasoma km kadhaa,hivyo km amebadilisha km utajua!Kila la kheri wanunuzi!
 
Unalolisema ni kweli kabisa. Wabongo sio waaminifu kabisa. Unakuta mtu anakwambia anauza gari yake, alilinua toka Japan likiwa used miaka zaidi ya mitano iliyopita, lakini leo anapotaka kuliuza anasema limetembea Km chini ya laki moja!!
 
Kwa kuwa inaonekana wabongo wengi wanapotaka kununua magari yalotumika ndani ya bongo kitu kikubwa wanachoangalia ni mileage ambayo gari imetembea basi nawaasa ndugu zanguni kuweni makini sana,kuna huu utapeli wa kurudisha km za maga, na wengi hurudisha nyuma chini ya km laki moja na nusu au chini ya laki moja!Cha kufanya: Zingatia zaidi uzima wa injini kwa kuwa gari ni injini asikudanganye mtu,ukitaka kununua tafuta mtu mwenye weledi wa magari akukagulie gari,kuna gari zimetembea km nyingi lkn ziko well maintained na kuna gari zina km ndogo lkn vimeo!Pia km gari unalotaka kununua huyo mmiliki aliliagiza mwenyewe toka nje,mwambie akuoneshe inspection document zilizokuja na gari huwa zinaonesha gari imeingia ikiwa inasoma km kadhaa,hivyo km amebadilisha km utajua!Kila la kheri wanunuzi!
Hebu nielekeze jinsi ya kuzipunguza.
 
Labda hzo odometer isiwe digital
Lakini kama ni digital hata ukirudusha nyuma ukitembea umbali flan zina retain kwenye original milage mkuu hapo ndo utamkamata mwizi wako.
Wazungu sio wajinga.
 
Labda hzo odometer isiwe digital
Lakini kama ni digital hata ukirudusha nyuma ukitembea umbali flan zina retain kwenye original milage mkuu hapo ndo utamkamata mwizi wako.
Wazungu sio wajinga.
Una amini katikati digital?
 
Back
Top Bottom