Issue ya wamachinga imekuwa covered na ujinga mwingi na ndio maana linaendelea kuwa tatizo badala ya kuonyesha hata nia ya kutatuliwa.
Wamachinga ni matokeo ya aina ya ajira zilizotengenezwa katika miaka takribani 60 ya uhuru na hasa hii miaka 35 ya karibuni. Kibaya zaidi 95% ya bidhaa wanazochuza ni kutoka viwanda vya China na mitumba ya Ulaya.
Mfumo wa kutengeneza ajira za uhakika kama kilimo na uzalishaji mwingine umeuawa na huu mfumo wa kinafiki wa kujipendekeza kwa walio na channels ili 'kukutupia' walau makombo. Kibaya zaidi karibia 50% ya population wanaangukia kwenye hili kundi la miaka 35 (ambao ndio wamachinga) wamekuwa brainwashed kwa elimu duni isiyotoa mwelekeo wa ni wapi pa kwenda mbali na kuwafuata wanaofaidi keki ya taifa walipo (mijini).
Kwa hiyo kuwafukuza walipo itatumika nguvu ambapo ilitakiwa nguvu hiyo hiyo au zaidi itumike pia kuwa assure wanakokwenda/pelekwa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.