Muonekano wa chuo cha veta kilichozinduliwa leo na rais dkt magufuli wilaya ya namtumbo mkoani ruvuma

esther mashiker

JF-Expert Member
May 29, 2018
616
552
1063585


Mjini Namtumbo, Mhe. Rais Magufuli amezindua Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) kilichojengwa na Serikali ya Tanzania kwa gharama ya shilingi Bilioni 6.5 na ambacho kitakuwa na uwezo wa kutoa mafunzo kwa wanafunzi 600 wa kozi ndefu na fupi kwa mwaka.

Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa kwake na gharama kubwa zilizotumika ikilinganishwa na thamani ya majengo yaliyojengwa na ameitaka VETA na viongozi wote wa Serikali kutambua umuhimu wa kubana matumizi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Joyce Ndalichako amesema pamoja na chuo cha VETA Namtumbo, Serikali imejenga vyuo vingine vya VETA katika Mikoa ya Njombe, Rukwa, Geita na Simiyu. Pia imejenga vyuo vya maendeleo ya jamii 20 ambavyo vitaongezeka hadi kufikia 34 ifikapo mwaka 2020.
1063586


1063587

1063588
 
Back
Top Bottom