Chaliifrancisco
JF-Expert Member
- Jan 17, 2015
- 23,489
- 70,276
Ni kweli mkuu hakuna ajuaye kesho yake lakini kuna wanaofanya mambo kama wana hakika ya kesho yao. Sabay alikuwa mmoja wa watu wa aina hiyo.Hakuna ajuaye kitakachomtokea, tusimlaumu
Hii iwe somo kwa sisi wote tuliobaki. Be humble hujui kesho itakuwaje. Ukijiona wewe ndio mwamba na kutesa na kudharau wengine hakika ipo siku utalia na kusaga meno.
Najaribu kumhurumia huyu jamaa lakini ndio hivyo tena anamalizia kitabu chake alichoanza kukiandika muda mrefu. Matukio yake ya nyuma ndio yamempeleka alipo. Kama unabisha jiulize kwanini sio wengine ni yeye? Kwanini kila mtu alie nae?
Mwisho wa unaya ni majonzi na aibu. Hukumu hii na maswahibu haya ya Sabaya yatukumbushe kuishi vizuri bila kujali mamlaka na nguvu tulizonazo.