Mungu wa kweli hahitaji haya tunayoaminishwa




Mkuu, ni kweli kabisa wala siyo utani, katika wanyama ni Jamii ya nyani (primates)== apes na monkeys pamoja Nguruwe ndiyo hufanya ngono za jinsia moja (homosexuality) na wataalamu wa lishe wanasema "you are what you eat" yaani mwili wako upo kutokana na kile unachokula, sasa kama utakula sana nyama ya nguruwe (staple food) moja kwa moja mwili wako utaambukizwa mazingira ya USHOGA kutokana na matumizi ya hiyo nyama ya nguruwe.

Mungu hakuiharamisha nyama ya nguruwe bila sababu of course kuna sababu nyingi sana ambazo zote ni mkusanyiko wa madhara.
 
Acha kudanganya watu , hao hao wanaosema hawali nguruwe ndiyo wanaongoja kwa huo usodoma, tunajua sana tatizo huwa tuna staha ya maneno, nakukaribisha nina ninafuga hao nguruwe nitafutiage wateja mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Soma Matendo ya mitume 10 labda uwe ni wale wanyofoa vifungu vinavyokufunga mwenyewe


Samahani kwa kueleza ukweli unaohatarisha biashara yako ya kiti moto, lakini ukisoma katika walawi , kuna maelezo juu ya nyama ya nguruwe. Nasi tunamuogopa Mungu zaidi kuliko wanadamu== Tunamuogopa yule anayeweza kudhuru mwili na roho kuliko yule anayeweza kudhuru mwili pekee.
 
Unadhani misikiti na makanisa yataendeshwa vipi tusipotoa zaka na sadaka?
masheikh na mapadre watakula wapi?

Ndo wajiongeze sasa!
Watafute wahisani halafu wawekeze wavune returns!
Huko dini zilikotoka Watu walishaachaga kwenda kusali makanisani sijui Kwanini !
Kwa hiyo kule wachungaji Wao hawaishi?
Wanaishi kwa kuwa wamejiongeza !
 
Sasa Mungu akimuadhibu kiumbe wake aliyemuumba mwenyewe kosa lipo wapi??, si kamuimba yeye mwenyewe na anajua mapungufu yake!!.

Vipi we dogo!!
Ahahahahaaaahahhahhaaha sasa akili imekukaa ", jibu maswali haya
1.kuua ni ubaya au uzuri ?
2. Unapoutia ugumu moyo wa mtu hapo kuna fair play ?
 
Ahahahahaaaahahhahhaaha sasa akili imekukaa ", jibu maswali haya
1.kuua ni ubaya au uzuri ?
2. Unapoutia ugumu moyo wa mtu hapo kuna fair play ?



Tatizo lako wewe dogo unasoma vitu nusunusu pia huwa hautafakari vya kutosha na hilo linathibitika kutokana na hayo maswali yako, eti unauliza:-

(1) kuua ni ubaya au uzuri??, jibu lake ni kwamba, kuua bila sababu inayopasa ni ubaya lakini kuua kwa sababu inayopasa ni vizuri, mfano kama kaja jambazi na silaha nyumbani kwako jambazi kwa dhamira ya kukuua ili apore mali zako na wewe ukamuwahi kumuua hapo unasemaje juu ya hayo mauaji??!!.

Unauliza swali la (2) kwamba, "unapotia ugumu moyo wa mtu hapo kuna fair play?"

Jibu ni kwamba, ama umesoma hiyo habari (kuhusu Firauni na nabii Musa as), nusunusu au kitabu ulichosoma kina mapungufu juu ya hiyo habari, sasa nakufungulia Qur'an uone ni kwa vipi Firauni alipewa moyo mgumu (au moyo wake ukawa mgumu kutokana na matendo yake).

Quran Suratul (Yunus:88-89), inasema:-

Na Musa akasema; Mola wetu mlezi hakika wewe umempa Firauni na wakuu wake mapambo na mali katika maisha ya dunia, hivyo wanapoteza watu katika njia yako. Mola wetu mlezi zifutilie mbali mali zao na ZIFUNGE NYOYO ZAO,wasiamini mpaka waione adhabu chungu. (10:88)


Mwenyezi mungu akasema; Maombi yenu yamekubaliwa. Basi simameni sawasawa ,wala msifuate njia za wale wasiojua. (10:89).


👆🏻Hiyo ndiyo habari yote kwa mukhtasari ilivyokuwa jinsi ilivyoeleza ndani ya Qur'an tukufu kuhusu Firauni aliyepata moyo mgumu.
 
Tatizo lako wewe dogo unasoma vitu nusunusu pia huwa hautafakari vya kutosha na hilo linathibitika kutokana na hayo maswali yako, eti unauliza:-

(1) kuua ni ubaya au uzuri??, jibu lake ni kwamba, kuua bila sababu inayopasa ni ubaya lakini kuua kwa sababu inayopasa ni vizuri, mfano kama kaja jambazi na silaha nyumbani kwako jambazi kwa dhamira ya kukuua ili apore mali zako na wewe ukamuwahi kumuua hapo unasemaje juu ya hayo mauaji??!!.

Unauliza swali la (2) kwamba, "unapotia ugumu moyo wa mtu hapo kuna fair play?"

Jibu ni kwamba, ama umesoma hiyo habari (kuhusu Firauni na nabii Musa as), nusunusu au kitabu ulichosoma kina mapungufu juu ya hiyo habari, sasa nakufungulia Qur'an uone ni kwa vipi Firauni alipewa moyo mgumu (au moyo wake ukawa mgumu kutokana na matendo yake).

Quran Suratul (Yunus:88-89), inasema:-

Na Musa akasema; Mola wetu mlezi hakika wewe umempa Firauni na wakuu wake mapambo na mali katika maisha ya dunia, hivyo wanapoteza watu katika njia yako. Mola wetu mlezi zifutilie mbali mali zao na ZIFUNGE NYOYO ZAO,wasiamini mpaka waione adhabu chungu. (10:88)


Mwenyezi mungu akasema; Maombi yenu yamekubaliwa. Basi simameni sawasawa ,wala msifuate njia za wale wasiojua. (10:89).


👆🏻Hiyo ndiyo habari yote kwa mukhtasari ilivyokuwa jinsi ilivyoeleza ndani ya Qur'an tukufu kuhusu Firauni aliyepata moyo mgumu.
Huo mfano wako mzuri kweli, aya sasa tuurudishe kwa namna tunavyojadili ubaya na uzuri wa uuaji wa Mungu ;

1.kwa vile umeleta mfano kuwa kuna uuaji mzuri na uuaji mbaya, ebu tuonyeshe sasa uuaji upi wa Mungu ni mzuri na uuaji upi mbaya ?

2.Musa ameomba dua ili firauni afanywe mgumu moyo wake, kitendo hicho cha kufanywa mgumu firauni moyo wake , maana yake firauni anakosa utashi wa kufanya jambo kwa matakwa yake kwa sababu Mungu ametumia Uungu wake kumfanya firauni awe mgumu wa moyo , sasa firauni iweje awe nakosa kutowaruhusu waisrael waondoka wakati Mungu mwenyewe kaufanya moyo wa firauni kuwa mgumu iko wapi fair play ?
 
Huo mfano wako mzuri kweli, aya sasa tuurudishe kwa namna tunavyojadili ubaya na uzuri wa uuaji wa Mungu ;

1.kwa vile umeleta mfano kuwa kuna uuaji mzuri na uuaji mbaya, ebu tuonyeshe sasa uuaji upi wa Mungu ni mzuri na uuaji upi mbaya ?

2.Musa ameomba dua ili firauni afanywe mgumu moyo wake, kitendo hicho cha kufanywa mgumu firauni moyo wake , maana yake firauni anakosa utashi wa kufanya jambo kwa matakwa yake kwa sababu Mungu ametumia Uungu wake kumfanya firauni awe mgumu wa moyo , sasa firauni iweje awe nakosa kutowaruhusu waisrael waondoka wakati Mungu mwenyewe kaufanya moyo wa firauni kuwa mgumu iko wapi fair play ?



Ndiyo maana nikasema wewe bado ni "dogo sana" kifikra. Njia rahisi ya wewe, nadhani, ni kutumia mifano tu ili uelewe hekima za Mungu.

Wewe mbele ya Mungu ni chini zaidi kuliko wewe jinsi unavyommiliki mbuzi wako, leo ukiamua kumchinja mbuzi wako na kupika supu nani atakuuliza??, halikadhalika kama Mungu angeamua kukufanya wewe uwe kitoweo chake ungeropoka " that's unfair ??!!" wakati huna lolote la kumfanya kwani yeye atabaki kuwa Muumba wako na wewe utabaki kuwa kiumbe chake, full stop.sasa kiburi cha kumjudge Mungu eti, kawa muuaji unakitoa wapi??, naam, Mungu atawaua wale ambao ni majeuri na waharibifu na mafedhuli katika ardhi kama Firauni alivyokuwa.

Eti, unaendelea kumkosoa Mungu kwanini kamfanya Firauni awe na moyo mgumu na kisha kumuadhibu.

Nimesema upeo wako wa kuelewa falsafa ya maneno ya Mungu ni mdogo na inaonekana umetawaliwa na jazba (emotions).

Firauni alikuwa ni jeuri mno na hakukubali kabisa jambo lolote aliloambiwa na Musa (as) na kilichompa jeuri na kiburi ni mali, ufalme na kuogopwa na raia na hasa Waisraeli, Musa akamuomba Mungu aangamize mali zake na hatua hii ilikuja baada ya hatua mbalimbali kushindwa na inaonyesha kamwe Firauni asingekubali kunyenyekea mbele ya Musa, ndipo Mungu akakubali maombi ya Musa kwa kumdhoofisha katika mali jambo lililomfanya Firauni awe na kiburi na jeuri zaidi kuliko hapo kabla kwasababu musa alimueleza kuwa kuanguka kwa mali zake ilitokana na hasira za mungu juu yake. Hivyo maneno "kutia ugumu moyoni" maana yake ni jeuri na kiburi na hasira na adhabu za Firauni zilizidi dhidi ya waisraeli kutokana na yale matokeo ya adhabu ya Mungu na hatimaye Mungu akamgharikisha baharini. Sasa huo ndiyo ufafanuzi wa habari hiyo.

Nikupe mfano mmoja; unapowinda chui "(a feral leopard)" anaponasa kwenye mtego ili kumuua kirahisi wawindaji humsogelea karibu na kumsakizia mti "(a poking pole)" ili kumpandisha hasira na mara moja ataung'ata huo mti na hapo inakuwa rahisi kumtwanga risasi, hapo kwa fikra zako utauliza kwanini apandishwe hasira halafu auawe??!!, mfano huo ndiyo jinsi Firauni alivyotiwa ugumu wa moyo na Mungu ili aangamizwe kwa sababu hatua aliyofikia ni "point of no return" na hakuwa tena mtu wa kheri.
 
Ndiyo maana nikasema wewe bado ni "dogo sana" kifikra. Njia rahisi ya wewe, nadhani, ni kutumia mifano tu ili uelewe hekima za Mungu.

Wewe mbele ya Mungu ni chini zaidi kuliko wewe jinsi unavyommiliki mbuzi wako, leo ukiamua kumchinja mbuzi wako na kupika supu nani atakuuliza??, halikadhalika kama Mungu angeamua kukufanya wewe uwe kitoweo chake ungeropoka " that's unfair ??!!" wakati huna lolote la kumfanya kwani yeye atabaki kuwa Muumba wako na wewe utabaki kuwa kiumbe chake, full stop.sasa kiburi cha kumjudge Mungu eti, kawa muuaji unakitoa wapi??, naam, Mungu atawaua wale ambao ni majeuri na waharibifu na mafedhuli katika ardhi kama Firauni alivyokuwa.

Eti, unaendelea kumkosoa Mungu kwanini kamfanya Firauni awe na moyo mgumu na kisha kumuadhibu.

Nimesema upeo wako wa kuelewa falsafa ya maneno ya Mungu ni mdogo na inaonekana umetawaliwa na jazba (emotions).

Firauni alikuwa ni jeuri mno na hakukubali kabisa jambo lolote aliloambiwa na Musa (as) na kilichompa jeuri na kiburi ni mali, ufalme na kuogopwa na raia na hasa Waisraeli, Musa akamuomba Mungu aangamize mali zake na hatua hii ilikuja baada ya hatua mbalimbali kushindwa na inaonyesha kamwe Firauni asingekubali kunyenyekea mbele ya Musa, ndipo Mungu akakubali maombi ya Musa kwa kumdhoofisha katika mali jambo lililomfanya Firauni awe na kiburi na jeuri zaidi kuliko hapo kabla kwasababu musa alimueleza kuwa kuanguka kwa mali zake ilitokana na hasira za mungu juu yake. Hivyo maneno "kutia ugumu moyoni" maana yake ni jeuri na kiburi na hasira na adhabu za Firauni zilizidi dhidi ya waisraeli kutokana na yale matokeo ya adhabu ya Mungu na hatimaye Mungu akamgharikisha baharini. Sasa huo ndiyo ufafanuzi wa habari hiyo.

Nikupe mfano mmoja; unapowinda chui "(a feral leopard)" anaponasa kwenye mtego ili kumuua kirahisi wawindaji humsogelea karibu na kumsakizia mti "(a poking pole)" ili kumpandisha hasira na mara moja ataung'ata huo mti na hapo inakuwa rahisi kumtwanga risasi, hapo kwa fikra zako utauliza kwanini apandishwe hasira halafu auawe??!!, mfano huo ndiyo jinsi Firauni alivyotiwa ugumu wa moyo na Mungu ili aangamizwe kwa sababu hatua aliyofikia ni "point of no return" na hakuwa tena mtu wa kheri.
Ahahahahaaaahahhahhaaha mkuu usilalamike hapa kila jambo linaweza jadiliwa , pamoja na kushindwa kujibu maswali yangu na kuanza kuzunguka na maelezo kibao yasiyo na msingi , maelezo yako yatakubana mwenyewe
"Point of no return", aliyofikia firauni Mungu aliijua kabla firauni ajafikia hatua hiyo au aliijua baada ya firauni kufikia hatua hiyo ? taratibu tutaelewana tu
 
Ahahahahaaaahahhahhaaha mkuu usilalamike hapa kila jambo linaweza jadiliwa , pamoja na kushindwa kujibu maswali yangu na kuanza kuzunguka na maelezo kibao yasiyo na msingi , maelezo yako yatakubana mwenyewe
"Point of no return", aliyofikia firauni Mungu aliijua kabla firauni ajafikia hatua hiyo au aliijua baada ya firauni kufikia hatua hiyo ? taratibu tutaelewana tu


Mungu alijua kuwa Firauni hasingegeuka kumkubali Musa (as), na hilo ni kutokana na majivuno na kiburi chake, njia ambayo aliichagua mwenyewe.
 
Mungu alijua kuwa Firauni hasingegeuka kumkubali Musa (as), na hilo ni kutokana na majivuno na kiburi chake, njia ambayo aliichagua mwenyewe.
Ujajibu swali , Mungu alijua wakati gani kuwa sasa firauni hawezi kuwa mwema? ni baada ya maombi ya musa au kabla ya maombi ya musa ?
 
Ujajibu swali , Mungu alijua wakati gani kuwa sasa firauni hawezi kuwa mwema? ni baada ya maombi ya musa au kabla ya maombi ya musa ?


Inaonekana kwamba umekwisha elewa maana ya Firauni kupewa moyo mgumu, sasa umekuja na mada nyingine unapotaka kujua; eti, Mungu alijua lini kwamba Firauni hataongoka?!!--Jibu ni "Mungu alijua hata kabla hajamuumba huyo Firauni kwamba asingeongoka kutokana na upumbavu, kiburi, jeuri, ujinga na ufedhuli wake mwenyewe.

Mungu alijua kabla hata hajamuumba huyo Firauni kwamba hataongoka.
 
Samahani kwa kueleza ukweli unaohatarisha biashara yako ya kiti moto, lakini ukisoma katika walawi , kuna maelezo juu ya nyama ya nguruwe. Nasi tunamuogopa Mungu zaidi kuliko wanadamu== Tunamuogopa yule anayeweza kudhuru mwili na roho kuliko yule anayeweza kudhuru mwili pekee.
Umesoma matendo 10 niliokwambia? Wala sitishiki na biashara biashara kuna mwezi mmoja lakin mingine ni wanunuzi ndiyo wanapigana vikumbo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaonekana kwamba umekwisha elewa maana ya Firauni kupewa moyo mgumu, sasa umekuja na mada nyingine unapotaka kujua; eti, Mungu alijua lini kwamba Firauni hataongoka?!!--Jibu ni "Mungu alijua hata kabla hajamuumba huyo Firauni kwamba asingeongoka kutokana na upumbavu, kiburi, jeuri, ujinga na ufedhuli wake mwenyewe.

Mungu alijua kabla hata hajamuumba huyo Firauni kwamba hataongoka.
Mungu alitaka kujidhihirisha kwao ili wamjue kama yeye ndiye Mungu niko ambaye niko, acha wamjaji ,
atawapigia tu anawasikia vizuri sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaonekana kwamba umekwisha elewa maana ya Firauni kupewa moyo mgumu, sasa umekuja na mada nyingine unapotaka kujua; eti, Mungu alijua lini kwamba Firauni hataongoka?!!--Jibu ni "Mungu alijua hata kabla hajamuumba huyo Firauni kwamba asingeongoka kutokana na upumbavu, kiburi, jeuri, ujinga na ufedhuli wake mwenyewe.

Mungu alijua kabla hata hajamuumba huyo Firauni kwamba hataongoka.
Ahahahahaaaahahhahhaaha sasa kama alijua kabla ajamuumba firauni kuwa atakuwa jeuri , sasa firauni kosa lake liko wapi ? kumbe ule ujeuri ni mipango ya huyo Mungu mwenyewe sasa hapa kuna fair play? mwacheni firauni wala hana tatizo kabisa
 
Ahahahahaaaahahhahhaaha sasa kama alijua kabla ajamuumba firauni kuwa atakuwa jeuri , sasa firauni kosa lake liko wapi ? kumbe ule ujeuri ni mipango ya huyo Mungu mwenyewe sasa hapa kuna fair play? mwacheni firauni wala hana tatizo kabisa



Hoja yako ni ya ajabu sana!!, Mungu kujua kwamba Firauni atakuwa jeuri hakuhusiani na yeye Firauni kuwa jeuri, yaani hali hiyo siyo "cause and effect", mfano wa "cause and effect" ni huu hapa; mtu uking'atwa na mbu mwenye vimelea vya malaria matokeo yake utapata malaria, hapo cause ni kung'atwa na mbu na effect ni kupata malaria. Sasa Mungu kujua kama Firauni angekuwa jeuri siyo cause ya Firauni kuwa jeuri, ujeuri wa Firauni au mtu yeyote ni kazi ya dhamira ya matendo ya mtu mwenyewe.

Hapa naomba nifafanue zaidi, ni kwamba hata mtu yeyote atende wema naye atahukumiwa kwa malipo mema kutokana na wema aliotenda, swali ni hili kwanini Mungu asilipwe thawabu kutokana na huo wema wa huyo mtu kwasababu ni Mungu ndiye aliyemuumba huyo mtu huku akijua kuwa huyo mtu angekuwa mwema.------- hapo ninakuonyesha "counter argument" ya hoja yako.

Hilo Swali lako wewe siyo mtu wa kwanza kuuliza na unayo mapungufu fulani ya MSINGI katika elimu ya dini ndiyo yamepelekea wewe kutoa hiyo hoja dhaifu nikipata wasaa nitajaribu kuweka hiyo misingi ndipo utaelewa hekima yote.

Ila lazima utambue, mtu atakaye hukumiwa mbele ya Mungu ni yule aliyefanya mema au mabaya huku akitambua kuwa anachofanya ni wema au ubaya, na kutokana na wema mtu atalipwa thawabu na kutokana na ubaya mtu ataadhibiwa. Mtu hawezi kuhukumiwa kwa kulipwa thawabu au adhabu akitenda wema au ubaya bila kujua/bila kudhamiria.

Bottom line ni kwamba, mema au mabaya ya mtu ni kutokana na utashi wa mtu mwenyewe na Kujua kwa Mungu hakuna mahusiano yoyote na utashi na dhamira ya huyo mtu.

Mimi ninakujua wewe "dogo" Sasa utauliza swali hili, "kwanini Mungu aumbe watu ambao anajua hatimaye watakuwa watu waovu??"😁😁😁

Mimi ninakuita "dogo" kwa sababu maswali yako ni madogo.
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom