Mungu wa kweli hahitaji haya tunayoaminishwa

Habari wakuu!

Mungu wa kweli, mwenye uweza wote, na aliyeumba kila kitu hahitaji mambo yafuatayo:-

1. Hahitaji Zaka wala Sadaka
Mungu wa kweli si mhitaji, uhitaji ni karba ya viumbe. Mungu hana anachohitaji kutoka kwa kiumbe. Yeye ndiye huamua nini kiwe na nini kisiwe. Mungu wa kweli hahitaji sadaka kama watu wengi wanavyoaminishwa. Hahitaji zaka kama wachungaji wanavyosema. Wachungaji wanamsingizia Mungu mambo mengi ikiwemo hili la zaka na sadaka. Wanachoshindwa kusema ni kuwa wao ndio wanahitaji hizo zaka na sadaka kama sehemu ya huduma yao. Ni uongo na dhambi kubwa kusema Mungu anataka sadaka na zaka jambo ambalo linamdhalilisha Mungu muweza wa yote.

Wachungaji, mashehe na viongozi wote wa dini kwa majina yao. Muache kuhadaa watu na kumdhalilisha Mungu. Tutatoa sadaka na zaka kwa kujua kuwa mnatupa huduma za kiroho na si kusema kuwa Mungu anahitaji sadaka na zaka tena fungu la kumi. Kama tunawalipa waalimu, madaktari, wanasheria na kada zingine iweje tusiwalipe nyie. Kwa nini mumsingizie Mungu mambo ya uongo. Eti fungu la kumi ni la Mungu. Si kweli. Mtu atatoa zaka na sadaka kulingana na umuhimu wa huduma anayoipata na si kumtishia vitisho vya uongo.

2. Kafara si ondoleo la dhambi
Watu wameaminishwa kuwa eti ili mtu asamehewe dhambi basi sharti amwage damu. Zamani walimwaga damu ya wanyama lakini sasa hivi wanaamini kuwa Yesu(mtu ninayemheshimu sana) alikufa kwa ajili ya watu jambo ambalo ni uongo. Mungu wa kweli hawezi kufikiri achilia mbali kutenda jambo kama hilo. Hiyo ni mila za kuabudu miungu ya Kiyahudi ambayo msingi wake mkuu umetokana na Abrahamu aliyechukua baadhi ya mila za Kiashuru( kwa sasa ni Syria). Miungu ya Abrahamu ndiyo ilimtaka amtoe Isaka kafara kama ilivyodesturi.

Mungu wa kweli hahitaji mchakato huo kusamehe dhambi, na kumwaga damu si suluhu ya dhambi kuishi. Kwa kutambua hili jambo hili moja kwa moja linaonekana ni wazo la kibinadamu zaidi kuliko la Mungu.

3. Maombi hayabadili chochote kwa Mungu mwenye uweza.
Wachungaji, mashehe na viongozi wa dini wengine kwa majina yao wanawadanganya watu kuwa ukimuomba Mungu jambo lolote anaweza akakupa kitu ambacho si kweli hata kidogo. Vile Mungu alivyopanga kabla hajakuumba ndivyo itakavyokuwa. Kusema kuwa ukimuomba Mungu anabadili mipango yake ni kujidanganya na kupoteza muda. Kumuomba Mungu ni kumfundisha namna ya kufanya mambo yake. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaoonyesha kuwa mtu akiomba jambo kwa Mungu hupewa isipokuwa ushahidi uliowazi ni kuwa Mtu akifuata maagizo ya Mungu na sheria zake ndio hupata akitakacho. Mungu anataka watu wafuate sheria zake na si kuomba omba tuu.

Hii inamaanisha kuwa viongozi wa dini jukumu lao ni kuwafundisha watu sheria za Mungu na si kuwadanganya waombe au kuwaombea. Kuwaombea watu ni kuwafundisha uvivu. Na kuamini katika hamna.

Ukitaka uamini nikisemacho, kaa ndani omba alafu usiende kufanya kazi uone kama Mungu atakupa ukitakacho, alafu mwenzako asiombe aende kufanya kazi uone nani atapewa/atapata. Hakuna sheria ya Mungu mahali popote kwenye torati inayomtaka mtu aombe. Tafsiri yake nadhani mnaelewa ni nini. Usishangae kwa nini bara la Afrika ni masikini ilhali ndilo linaloongoza kwa waumini wenye kuomba makanisani na misikitini. Jibu unalo.

4. Wachungaji/mashehe na viongozi wa dini si watu pekee wanaotakiwa kuheshimiwa.
Kuna dhana watu huaminishwa kuwa kundi fulani la watu ndilo linalotakiwa kupewa heshima kuliko kundi jingine. Huu ni uongo mkubwa. Mchungaji ni mtumishi kama walivyo watumishi wengine. Anahudumia watu kama wanavyohudumia wengine. Hana uspesho wowote zaidi ya wao kuwahadaa watu wenye akili ndogo na wasioujua ukweli ndio maana wamegeuka watumwa wa makuhani na mashehe. Kila mtu duniani anahitaji heshima ikiwa anafanya kazi ya kuhudumia wengine. Iwe ni fundi nguo, fundi magari, mbunge, mwalimu, muuguzi, mhandisi wote wapo sawa na wote wanategemeana. Kumpa mtu fulani heshima kuliko mwingine si tu kwamba ni ukosefu wa maarifa bali ni kuonyesha hali ya kutoujua ukweli.'

Viongozi wa dini wamejipa hadhi kubwa na kujiona wao ndio wenye mamlaka. Usishangae kiongozi wa dini mjinga akisema kuwa anakulaani kwa Mungu. Nikisiaga hivi huwa nacheka sana. Mtu hupata laana kwa kuacha sheria za Mungu na si maneno ya Mchungaji au mzazi. Kwa ujumla ni kuwa mtu hujilaani yeye mwenyewe ikiwa ataacha sheria za Mungu.

Hivyo watu wamejikuta wakiwaogopa wanadamu wenzao kwa kutoujua ukweli. Unamuogopa mtu aliyezaliwa na mwanamke? Mtu anayehitaji chakula ili apate nguvu ya kuishi. Unakuta mtu anaenda kanisani anaitwa na mchungaji mbele ya kanisa na kutabiriwa vitu vya uongo na yeye anasema kweli wakati sio kweli. Kwa mfano;
Mchungaji: wewe unatatizo la ugumba
muumini: Kweli
Mchungaji: Mama yako anakuloga
Muumini: Kweli
wakati yote ni uongo, anasema kweli kwa uoga na utumwa wa kifikra.

Wito wangu, lazima watu waishi kwa kupendana na kuzishika amri na sheria za Mungu ili wapate kuwa huru na maisha. Vinginevyo tutabaki kuwa watumwa na kuona sisi ni wasindikizaji wakati wengine ndio walioumbiwa huu ulimwengu jambo ambalo si kweli
Msingi wa hoja zako ni nini?
 
Sijakuelewa,,, kwa hiyo anaitaj Mambo tan?
Habari wakuu!

Mungu wa kweli, mwenye uweza wote, na aliyeumba kila kitu hahitaji mambo yafuatayo:-

1. Hahitaji Zaka wala Sadaka
Mungu wa kweli si mhitaji, uhitaji ni karba ya viumbe. Mungu hana anachohitaji kutoka kwa kiumbe. Yeye ndiye huamua nini kiwe na nini kisiwe. Mungu wa kweli hahitaji sadaka kama watu wengi wanavyoaminishwa. Hahitaji zaka kama wachungaji wanavyosema. Wachungaji wanamsingizia Mungu mambo mengi ikiwemo hili la zaka na sadaka. Wanachoshindwa kusema ni kuwa wao ndio wanahitaji hizo zaka na sadaka kama sehemu ya huduma yao. Ni uongo na dhambi kubwa kusema Mungu anataka sadaka na zaka jambo ambalo linamdhalilisha Mungu muweza wa yote.

Wachungaji, mashehe na viongozi wote wa dini kwa majina yao. Muache kuhadaa watu na kumdhalilisha Mungu. Tutatoa sadaka na zaka kwa kujua kuwa mnatupa huduma za kiroho na si kusema kuwa Mungu anahitaji sadaka na zaka tena fungu la kumi. Kama tunawalipa waalimu, madaktari, wanasheria na kada zingine iweje tusiwalipe nyie. Kwa nini mumsingizie Mungu mambo ya uongo. Eti fungu la kumi ni la Mungu. Si kweli. Mtu atatoa zaka na sadaka kulingana na umuhimu wa huduma anayoipata na si kumtishia vitisho vya uongo.

2. Kafara si ondoleo la dhambi
Watu wameaminishwa kuwa eti ili mtu asamehewe dhambi basi sharti amwage damu. Zamani walimwaga damu ya wanyama lakini sasa hivi wanaamini kuwa Yesu(mtu ninayemheshimu sana) alikufa kwa ajili ya watu jambo ambalo ni uongo. Mungu wa kweli hawezi kufikiri achilia mbali kutenda jambo kama hilo. Hiyo ni mila za kuabudu miungu ya Kiyahudi ambayo msingi wake mkuu umetokana na Abrahamu aliyechukua baadhi ya mila za Kiashuru( kwa sasa ni Syria). Miungu ya Abrahamu ndiyo ilimtaka amtoe Isaka kafara kama ilivyodesturi.

Mungu wa kweli hahitaji mchakato huo kusamehe dhambi, na kumwaga damu si suluhu ya dhambi kuishi. Kwa kutambua hili jambo hili moja kwa moja linaonekana ni wazo la kibinadamu zaidi kuliko la Mungu.

3. Maombi hayabadili chochote kwa Mungu mwenye uweza.
Wachungaji, mashehe na viongozi wa dini wengine kwa majina yao wanawadanganya watu kuwa ukimuomba Mungu jambo lolote anaweza akakupa kitu ambacho si kweli hata kidogo. Vile Mungu alivyopanga kabla hajakuumba ndivyo itakavyokuwa. Kusema kuwa ukimuomba Mungu anabadili mipango yake ni kujidanganya na kupoteza muda. Kumuomba Mungu ni kumfundisha namna ya kufanya mambo yake. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaoonyesha kuwa mtu akiomba jambo kwa Mungu hupewa isipokuwa ushahidi uliowazi ni kuwa Mtu akifuata maagizo ya Mungu na sheria zake ndio hupata akitakacho. Mungu anataka watu wafuate sheria zake na si kuomba omba tuu.

Hii inamaanisha kuwa viongozi wa dini jukumu lao ni kuwafundisha watu sheria za Mungu na si kuwadanganya waombe au kuwaombea. Kuwaombea watu ni kuwafundisha uvivu. Na kuamini katika hamna.

Ukitaka uamini nikisemacho, kaa ndani omba alafu usiende kufanya kazi uone kama Mungu atakupa ukitakacho, alafu mwenzako asiombe aende kufanya kazi uone nani atapewa/atapata. Hakuna sheria ya Mungu mahali popote kwenye torati inayomtaka mtu aombe. Tafsiri yake nadhani mnaelewa ni nini. Usishangae kwa nini bara la Afrika ni masikini ilhali ndilo linaloongoza kwa waumini wenye kuomba makanisani na misikitini. Jibu unalo.

4. Wachungaji/mashehe na viongozi wa dini si watu pekee wanaotakiwa kuheshimiwa.
Kuna dhana watu huaminishwa kuwa kundi fulani la watu ndilo linalotakiwa kupewa heshima kuliko kundi jingine. Huu ni uongo mkubwa. Mchungaji ni mtumishi kama walivyo watumishi wengine. Anahudumia watu kama wanavyohudumia wengine. Hana uspesho wowote zaidi ya wao kuwahadaa watu wenye akili ndogo na wasioujua ukweli ndio maana wamegeuka watumwa wa makuhani na mashehe. Kila mtu duniani anahitaji heshima ikiwa anafanya kazi ya kuhudumia wengine. Iwe ni fundi nguo, fundi magari, mbunge, mwalimu, muuguzi, mhandisi wote wapo sawa na wote wanategemeana. Kumpa mtu fulani heshima kuliko mwingine si tu kwamba ni ukosefu wa maarifa bali ni kuonyesha hali ya kutoujua ukweli.'

Viongozi wa dini wamejipa hadhi kubwa na kujiona wao ndio wenye mamlaka. Usishangae kiongozi wa dini mjinga akisema kuwa anakulaani kwa Mungu. Nikisiaga hivi huwa nacheka sana. Mtu hupata laana kwa kuacha sheria za Mungu na si maneno ya Mchungaji au mzazi. Kwa ujumla ni kuwa mtu hujilaani yeye mwenyewe ikiwa ataacha sheria za Mungu.

Hivyo watu wamejikuta wakiwaogopa wanadamu wenzao kwa kutoujua ukweli. Unamuogopa mtu aliyezaliwa na mwanamke? Mtu anayehitaji chakula ili apate nguvu ya kuishi. Unakuta mtu anaenda kanisani anaitwa na mchungaji mbele ya kanisa na kutabiriwa vitu vya uongo na yeye anasema kweli wakati sio kweli. Kwa mfano;
Mchungaji: wewe unatatizo la ugumba
muumini: Kweli
Mchungaji: Mama yako anakuloga
Muumini: Kweli
wakati yote ni uongo, anasema kweli kwa uoga na utumwa wa kifikra.

Wito wangu, lazima watu waishi kwa kupendana na kuzishika amri na sheria za Mungu ili wapate kuwa huru na maisha. Vinginevyo tutabaki kuwa watumwa na kuona sisi ni wasindikizaji wakati wengine ndio walioumbiwa huu ulimwengu jambo ambalo si kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Itakuaje kama Mungu ndio kafanya wale wawe waharifu kwa uwezo wake aliokuwa nao ?



Mungu hana sifa ya kutenda ubaya au kusababisha ubaya au kumfanya mtu atende ubaya, matendo yote mabaya ni mkono wa shetani au unaweza sema ni msukumo wa tamaa mbaya za nafsi yake, na hapo ndipo mtu anaposhikwa na hatia kwamba alifanya mabaya kwa nafsi yake huku akijua kuwa hayo anayofanya ni mabaya na hapo Mungu ahusiki aslani.
 
Mungu hana sifa ya kutenda ubaya au kusababisha ubaya au kumfanya mtu atende ubaya, matendo yote mabaya ni mkono wa shetani au unaweza sema ni msukumo wa tamaa mbaya za nafsi yake, na hapo ndipo mtu anaposhikwa na hatia kwamba alifanya mabaya kwa nafsi yake huku akijua kuwa hayo anayofanya ni mabaya na hapo Mungu ahusiki aslani.
Una uhakika kijana na unalo andika humu

UBAYA KAFANYA MUNGU, MWENYEWE

HESABU 21:6
"; Bwana akatuma nyoka za moto, kati ya watu , wakawauma, watu wengi wakafa";


Kwa kitendo cha Mungu kutuma nyoka kuua watu huo ni uzuri au ubaya ?

HUU KAUSABABISHA kwa PHARAO mpaka pharao akawa mkaidi na jeuri

KUTOKA 4:21
";Bwana akamwambia Musa, utakaporudi Misri , angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini NITAUFANYA MGUMU MOYO WAKE, naye HATAWAPA ruhusa hao watu waende zao";

Kwanini unamlaumu farao kutokuwaruhusu waisrael waende, kumbe ule ugumu kaufanya Mungu mwenyewe kwenye moyo wa Farao ?
 
Una uhakika kijana na unalo andika humu

UBAYA KAFANYA MUNGU, MWENYEWE

HESABU 21:6
"; Bwana akatuma nyoka za moto, kati ya watu , wakawauma, watu wengi wakafa";


Kwa kitendo cha Mungu kutuma nyoka kuua watu huo ni uzuri au ubaya ?

HUU KAUSABABISHA kwa PHARAO mpaka pharao akawa mkaidi na jeuri

KUTOKA 4:21
";Bwana akamwambia Musa, utakaporudi Misri , angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini NITAUFANYA MGUMU MOYO WAKE, naye HATAWAPA ruhusa hao watu waende zao";

Kwanini unamlaumu farao kutokuwaruhusu waisrael waende, kumbe ule ugumu kaufanya Mungu mwenyewe kwenye moyo wa Farao ?



Sasa Mungu akimuadhibu kiumbe wake aliyemuumba mwenyewe kosa lipo wapi??, si kamuimba yeye mwenyewe na anajua mapungufu yake!!.

Vipi we dogo!!
 
Sielewi nini hapo, kwani unapochinja hao wanyama wao wanapenda kuchinjwa??!! na mbaya zaidi huwa wanapiga kelele kwa uchungu lakini binadamu bila huruma anawapiga kisu, na anakula nyama zao utasikia " loo, nyama ya huyu kuku imenona kweli kweli" lakini kasahau kwamba kabla ya kuchinja alikuwa ni kiumbe mwenye roho kama yeye.
Loo! Hunishawishi ng'0! Hata kwa ndumba nyama siachi kula aisee!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo maana inaitwa imani ya mtu, hujawahii ona mtu anasema katupa hela nyingi kwa waganga wa kienyeji hadi ng'ombe katoa, lakini kanisni anataka asitoe hata mia tano eti Yesu alisema toeni bure, tunawatajirisha wachungaji mie huwa siwamalizi kabisa, hivi wale WALAWI walikuwa wanafanya kazi gani? Wakati imeandikwa usiende nyumbana mwa Bwqna Bwana mikono mitupu, Yesu mwenyewe baada ya kuwaponya aliwambia nenda katoe sadaka yako na usitende dhambi tena,

embu mtu mmoja asome hapa 2 Corinthians 9:6-11, Isaya 3:7, Kumbukumbu 12:17-19, Malaki3:10-12, Mithali 3:9-10, kama mtu anakula kila siku anashindwa nini kutenga sadaka angalau ya siku moja, bora usiende kanisan
:D:D:D:D:D:D
Sasa utaendaje kanisani bila kutoa zaka na sadaka huo si ujuha. Yaani ukienda kilabuni ulipie pombe, shule ulipie ada, kwenye usafiri ulipe nauli alafu kanisani useme sio lazima huo ndio ujuha wenyewe watu wasioujua. Tatizo kanisani hawasemi ukweli wangesema tu kwamba kama huna sadaka au zaka usije kanisani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo usipotoa sadaka au hizo zaka kanisa litaendeshwa vipi?
Mchungaji na familia yake wataishi vipi? Kumbuka ile ndo kazi yake.
Mtumishi wa Mungu riziki yake hupatikana madhabauni na si vinginevyo.
Labda useme hawa manabii uchwara ndo wanazingua harakati za kanisa la Yesu coz wana warubuni nakuwahadaa waumini wao kwa tamaa ya pesa
 
Mkuu, amini nakuambia. Mzazi hawezi kukufanya lolote kama hukuvunja sheria za Mungu. Kwanza unazjua sheria zenyewe?
Kwani heshima kwa mzazi si ipo katika amri kumi za Mungu? Kama unajitambua sizazi kama unaweza kukubali jambo baya ambalo mzazi atakwambia wewe ukajua sio sahihi akatoa laana na ikashika hapana, vitu vingine ni kujiongeza tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1.Fungu la kumi linahitajika kama shukrani kwa MUNGU mkuu nakushauri usome biblia vizuri.
3, Nabishana na wewe.
Mungu kamuumba binadamu ili amtumikie na kumpa uhuru wa kuchagua yeye mwenyewe.
Hata Yesu alifunga kwa hiyo utaona maombi ni muhimu.
Ufalme wa mbingu unapatikana vigumu ndugu so pambana kuutafuta ufalme wa mbinguni.
Kwa namna uliyoweka hapo sidhani kama kungekua na haja ya uwepo wa MUNGU.
Yesu mwenyewe alikuwa anafunga na kuomba, je kama maombi hayakuwa na nguvu kwanini alikuwa anafunga na kuomba? Hapo hapo aliwambia wanafunzi wake mapepo mengine sio rahisi kutoka isipokuwa kwa kufunga nakuomba, hapa kuna watu wanadanganya ili Mungu asahaulike ili atukuzwe shetani wao, washindwe tu kwajina la Yesu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom