Mungu wetu;
Ulitupatia Tanzania na watu wake (nikiwemo mimi, na wengine), mbona sasa unaruhusu watu wako wapigwe mabomu kisa wamechagua UPINZANI? Je, wapinzani si wa Tanzania? Je, hakuna sehemu mume na mke wana vyama tofauti? baba na babu vyama tofauti? Shangazi na mjomba vyama tofauti? Islaam na Ukristu vyama tofauti? Wahindi na wajaruo vyama tofauti?
Kwani polisi hawana ndugu zao wapinzani? Kwani JWTZ hawana ndg zao CCM na CHADEMA? Mungu, uko wapi uzuie mabomu kwa watu wako maskini? Tazama, waliambiwa, mkichagua upinzani mtaleta vita, kumbe ndo hii vita? Sikuwahi kuijua? Nilichokuwa nadhani ni kuwa wapinzani wakishinda tu wanaanza kutupiga mabomu, ndiyo maana siku zote nilisita kuwachagua; maskini kumbe ndo wanaoonewa! Maskini Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo, SHUKA SASA uzuie mabomu haya. Hata kama tumekutenda dhambi, tunaomba utusamehe.
Kuna watu wanatulazimisha tuamini kuwa sisi wa Tanzania ni wadini. Nilianza kuamni hivyo; kumbe ni ujinga wangu. Nilianza kumchukia jirani yangu bure; mbona ndo kawa wa kwanza kuja kuniangalia jana hospitalini nilipopigwa mabomu nikidhaniwa nimeandamana! Shuka Mwenyezi Mungu uzuie mabomu na umweke RAIS mwenye uchungu na Taifa hili...Amina.
Ulitupatia Tanzania na watu wake (nikiwemo mimi, na wengine), mbona sasa unaruhusu watu wako wapigwe mabomu kisa wamechagua UPINZANI? Je, wapinzani si wa Tanzania? Je, hakuna sehemu mume na mke wana vyama tofauti? baba na babu vyama tofauti? Shangazi na mjomba vyama tofauti? Islaam na Ukristu vyama tofauti? Wahindi na wajaruo vyama tofauti?
Kwani polisi hawana ndugu zao wapinzani? Kwani JWTZ hawana ndg zao CCM na CHADEMA? Mungu, uko wapi uzuie mabomu kwa watu wako maskini? Tazama, waliambiwa, mkichagua upinzani mtaleta vita, kumbe ndo hii vita? Sikuwahi kuijua? Nilichokuwa nadhani ni kuwa wapinzani wakishinda tu wanaanza kutupiga mabomu, ndiyo maana siku zote nilisita kuwachagua; maskini kumbe ndo wanaoonewa! Maskini Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo, SHUKA SASA uzuie mabomu haya. Hata kama tumekutenda dhambi, tunaomba utusamehe.
Kuna watu wanatulazimisha tuamini kuwa sisi wa Tanzania ni wadini. Nilianza kuamni hivyo; kumbe ni ujinga wangu. Nilianza kumchukia jirani yangu bure; mbona ndo kawa wa kwanza kuja kuniangalia jana hospitalini nilipopigwa mabomu nikidhaniwa nimeandamana! Shuka Mwenyezi Mungu uzuie mabomu na umweke RAIS mwenye uchungu na Taifa hili...Amina.