Mungu nipe macho nione sawa sawa, ni kweli wizara ya elimu hakuna mawaziri mizigo?

Makala Jr

JF-Expert Member
Aug 25, 2011
3,395
1,110
Ndugu zangu sina papara za x-mass wala mwaka mpya.Papara zangu ni kutafuta kitambaa cheusi cha kujifutia machozi endapo msiba wa anguko la elimu mwaka 2012/2013 halitajirudia tena kwa msimu wa 2013/2014. Nakumbuka fika mwezi mei, 2013 pindi mjadala wa matokeo mabaya ya kidato cha nne uliposhika kasi, matokeo yakafutwa na masahihisho kufanywa upya lakini bado hakikubadilika kitu, nilimuenzi Mzee Chinua Achebe kwa kusema 'No Longer At Easy'. Sababu zilizotolewa kwa matokeo mabaya ya 60% ya wahitimu kupata daraja 0 (sifuri) ni pamoja na kubadilishwa viwango za ufaulu,upungufu wa vitendea kazi shuleni, mazingira magumu ya kufundishia, mitaala mibovu n.k. Matokeo yake tunajenga taifa la watu feki (plastic surgery), dawa feki, maziwa feki, usalama wa taifa feki n.k. Mwezi uliopita wizara ya elimu ilitangaza kufuta daraja sifuri ili liitwe daraja la tano.Ni ajabu CCM hawajaona mizigo wizara ya elimu na licha ya elimu yetu kuporomoka, chanzo ni nini nje ya mizigo?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom