Mungu najua ananitaarifu kuhusu jambo muhimu ila naona simuelewi

Sonona
Wakuu njooni mnisaidie kwenye hali hii inayonitatiza.

Siku za hivi karibuni nimekua nikipitia hali flani ambayo Siwezi kuitafsiri vyema na hivyo kupelekea kushindwa kuchukua hatua yoyote.

Kifupi ni kuwa, nimekua nikipatwa na hali ya uzuni na mfadhaiko moyoni kila niamkapo kitandani asubuhi. Hali hii uendelea mpaka mida ya sita mchana, kisha upotea kidogo.

Kutokana na hali hii nimekua nikichelewa kazini, na Sina drive ya kazi na passion ya maisha inapotea.

Mimi ni mpenzi wa social media, nina rafiki kadhaa na wengi ni she. Mara nyingi nikiwa down Ila akitokea mmoja akinipa campany nzuri mood yangu urudi kwa kasi. Lakini mbinu hii imeshindwa kabisa kunitosheleza kuondoa hisia ya uzito wa moyo ninayoipitia recently.

Nimekua najiuliza maswali nisiyokuwa na majibu nayo. Wakati mwingine nadhani Mungu ana-communicate na mimi ila nahisi nimeshindwa kupambanua anataka kunipa ujumbe gani maishani mwangu.

Wakuu ikiwa umewahi kupitia hali hii please nakaribisha uzoefu wako kwenye hili.

Karibuni mnisaidie JF family.
 
Kwa nini unahisi Mungu anacommunicate na wewe? Huyo sio shetani kweli? Mungu hukupa raha na faraja. Hebu ingia kwenye maombi. Jiombee mwenyewe, jisogeze kwa Mungu maana hali uliyonayo inaonyesha Mungu yuko mbali na wewe! Pigania furaha yako mwenyewe! tupa mbali mawazo, simanzi na huzuni.

Kula vizuri, lala mapeeema, amka mapema kwa uchangamfu!
Roho wa Mungu aniongoze nikivuke kipindi hiki kizito
 
Kwa wakistro waraka wa Paulo (sikumbuki jina) anasema "huzuni ya Mungu humpeleka mtu kwenye Toba Bali huzuni ya dunia hii hufanya mauti " (Sina halina Kama nimenukuu vyema) ila general meaning yake ndo hiyo hapo kwamba Kama huzuni inatoka kwa Mungu basi inakudai ufanye Toba ila Kama huzuni hiyo inatokana na dunia hii basi inakua inakupeleka kwenye mauti


My take : fanya Toba kwa Mungu maana yeye huyajua yote


Asante
 
Mkuu Roho wa Mungu anaongea na wewe kuna kitu hakipo sawa piga magoti muulize Mungu anataka ufanye nini omba kwa kumaanisha kabisa ongea nae muulize anataka ufanye nini naimamani utapata jibu na ukishapata utapata amani moyoni mwako,viashiria vya roho Mtakatifu ni pamoja na huzuni ya Mungu kama una kiongozi was kiroho karibu yako mshirikishe pia atakuongoza.
 
Mkuu Roho wa Mungu anaongea na wewe kuna kitu hakipo sawa piga magoti muulize Mungu anataka ufanye nini omba kwa kumaanisha kabisa ongea nae muulize anataka ufanye nini naimamani utapata jibu na ukishapata utapata amani moyoni mwako,viashiria vya roho Mtakatifu ni pamoja na huzuni ya Mungu kama una kiongozi was kiroho karibu yako mshirikishe pia atakuongoza.
Thanks kwa ushauri mzuri toka moyoni mwako
 
Mkuu kwa nini unakua lonely?je una miaka 35-45 hawa huwa wanapitia kitu kinaitwa 'mid life crisis' huu umri ndio watu huwaza kama wamefanya right career choice ..if they have right and supportive partner and whether kupata familia kumewafanya wawe na furaha...sasa kama kuna mahali wanaona hawafurahii choices walizozofanya then wanakua 'depressed' ..dalili ni kama zako..kuto enjoy 'normal things' ulizokua unafanya kama kufika kazini na kufanya unayotakiwa kufanya kazini...na dalili nyingine ni 'avoidance' huku kuspend more time on social media ni ku avoid reality...vitu unaweza kufanya moja,kutembelea kituo cha magonjwa ya akili kupata tiba ,pili ni kuchunguza wapi which area of your life your are not happy with and then work on it..kila la kheri...
 
Mkuu kwa nini unakua lonely?je una miaka 35-45 hawa huwa wanapitia kitu kinaitwa 'mid life crisis' huu umri ndio watu huwaza kama wamefanya right career choice ..if they have right and supportive partner and whether kupata familia kumewafanya wawe na furaha...sasa kama kuna mahali wanaona hawafurahii choices walizozofanya then wanakua 'depressed' ..dalili ni kama zako..kuto enjoy 'normal things' ulizokua unafanya kama kufika kazini na kufanya unayotakiwa kufanya kazini...na dalili nyingine ni 'avoidance' huku kuspend more time on social media ni ku avoid reality...vitu unaweza kufanya moja,kutembelea kituo cha magonjwa ya akili kupata tiba ,pili ni kuchunguza wapi which area of your life your are not happy with and then work on it..kila la kheri...
Asante mtaalamu
 
Back
Top Bottom