Mungu najua ananitaarifu kuhusu jambo muhimu ila naona simuelewi

pureman2

JF-Expert Member
Aug 21, 2019
1,494
2,538
Wakuu njooni mnisaidie kwenye hali hii inayonitatiza.

Siku za hivi karibuni nimekua nikipitia hali flani ambayo Siwezi kuitafsiri vyema na hivyo kupelekea kushindwa kuchukua hatua yoyote.

Kifupi ni kuwa, nimekua nikipatwa na hali ya uzuni na mfadhaiko moyoni kila niamkapo kitandani asubuhi. Hali hii uendelea mpaka mida ya sita mchana, kisha upotea kidogo.

Kutokana na hali hii nimekua nikichelewa kazini, na Sina drive ya kazi na passion ya maisha inapotea.

Mimi ni mpenzi wa social media, nina rafiki kadhaa na wengi ni she. Mara nyingi nikiwa down Ila akitokea mmoja akinipa campany nzuri mood yangu urudi kwa kasi. Lakini mbinu hii imeshindwa kabisa kunitosheleza kuondoa hisia ya uzito wa moyo ninayoipitia recently.

Nimekua najiuliza maswali nisiyokuwa na majibu nayo. Wakati mwingine nadhani Mungu ana-communicate na mimi ila nahisi nimeshindwa kupambanua anataka kunipa ujumbe gani maishani mwangu.

Wakuu ikiwa umewahi kupitia hali hii please nakaribisha uzoefu wako kwenye hili.

Karibuni mnisaidie JF family.
 
Kwa nini unahisi Mungu anacommunicate na wewe? Huyo sio shetani kweli? Mungu hukupa raha na faraja. Hebu ingia kwenye maombi. Jiombee mwenyewe, jisogeze kwa Mungu maana hali uliyonayo inaonyesha Mungu yuko mbali na wewe! Pigania furaha yako mwenyewe! tupa mbali mawazo, simanzi na huzuni.

Kula vizuri, lala mapeeema, amka mapema kwa uchangamfu!
 
Mungu uongea na binadamu kwa kutumia viashiria, maono, na ndoto. Kama kiashiria cha uzuni ujakielewa omba aongee nawe kupitia ndoto. Kama unaota ndoto usiku alafu ukiamka unakuwa na uzuni ujumbe huko kwenye hiyo ndoto. Kama unaota alafu ukumbuki omba ukiota ukumbuke maana shetani anakusahaulisha! Best wishes
 
Acha kufanya vitu nafsi yako haiwezi, mfano usilazimishe kunywa pombe au kudanganya wakati nafsi yako haitaki hii itaondoa mgogoro na nafsi ulionao sasa, pia jifunze kuishi kwa ratiba na uwe na muda wa mazoezi asubuhi na jioni, uwe jirani na Kanisa, Msikiti au Mila na desturi kilingana na imani yako
 
Energy yako inategemea watu wengine na social media kama ulivyotanabaisha. Hali unayopitia ni ya kawaida na ni kipindi cha mpito, isipokuwa unapaswa kubadilika na kujifunza kupata energy kutoka ndani kwako mwenyewe.
 
Jaribu Kufunga na kuomba na kusoma vitabu vya Mungu, acha mambo ya kushinda kwenye social media hakuna msaada wa tatizo lako.
Jibu utalipata ndani ya siku tatu tu.

Yawezekana ni jambo baya linalokunyemelea, maana bila shaka utakuwa mtu wa totoz.
 
Jaribu Kufunga na kuomba na kusoma vitabu vya Mungu, acha mambo ya kushinda kwenye social media hakuna msaada wa tatizo lako.
Jibu utalipata ndani ya siku tatu tu.

Yawezekana ni jambo baya linalokunyemelea, maana bila shaka utakuwa mtu wa totoz.
Asante Kwa ushauri

But totoz are just friends
 
Energy yako inategemea watu wengine na social media kama ulivyotanabaisha. Hali unayopitia ni ya kawaida na ni kipindi cha mpito, isipokuwa unapaswa kubadilika na kujifunza kupata energy kutoka ndani kwako mwenyewe.
Noted
 
Acha kufanya vitu nafsi yako haiwezi, mfano usilazimishe kunywa pombe au kudanganya wakati nafsi yako haitaki hii itaondoa mgogoro na nafsi ulionao sasa, pia jifunze kuishi kwa ratiba na uwe na muda wa mazoezi asubuhi na jioni, uwe jirani na Kanisa, Msikiti au Mila na desturi kilingana na imani yako
Mara nyingi niko really
 
Hii hali iliniandama sana kipind fulan lkn ilikuja kupotea yenyewe yaan moyo ulikuwa hauna amani pia furaha inakosekana kabisa na ukiangalia sababu inayopelekea hivyo huioni
 
Mungu uongea na binadamu kwa kutumia viashiria, maono, na ndoto. Kama kiashiria cha uzuni ujakielewa omba aongee nawe kupitia ndoto. Kama unaota ndoto usiku alafu ukiamka unakuwa na uzuni ujumbe huko kwenye hiyo ndoto. Kama unaota alafu ukumbuki omba ukiota ukumbuke maana shetani anakusahaulisha! Best wishes
Ninaendelea kuomba
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom