Najiandaa ku-claim hii ngoma
Mimi namfahamu mheshimiwa mmoja aliye"liwa" kwa ujumbe kama huu. Hatimye alitoa USD 3,000 jamaa wakaingia mitini. Alipokuwa anawaandikia hawampi jibu, ndipo alipoanza kugoogle, akagundua mtandao supposedly fedha zinakotoka, ulikuwa katika lugha ya Kispanish. Alinifuata kutaka kujua kulikoni, jawabu yangu kwake hata kabla ya kumalizia mkasa wenyewe nilimwambia "Mheshimiwa, Wanaigeria wamekuzidi akili".Imekula kwako rafiki! Hii ni scamming made simple. Imejaa sana facebook. Wanigeria hawa.Kitakachofuata watakuambia utume $20 ili kulipia gharama ya ' kuprocess' malipo. Ukituma watakuambia utume $xyz gharama za benk. Ukituma watakuambia utume $klm as transfer cost. Hivyo hivyo watakusumbua mpaka uote kipara, na hakuna hela yoyote utakayoiona! Pole rafiki! Nasema hivyo kwa sababu ylishanipata.
Nilipokea e-mail moja mwaka jana mwezi wa tano nafikiri, ikiniarifu kwamba namba yangu ya airtel imeshinda kwenye ' uk nokia promo.' Nilichofanya, niligoogle 'uk nokia promo' na nilichogundua kilinistua. Watu kutoka nchi mbalombali walikuwa wanalalamika kwamba wamelizwa na hio 'uk nokia promo'. Kuona hivyo, wala sikujibu e-mail zao zilizofuata!
Hebu na wewe jaribu kugoogle hilo jina la mashindano yaani face book award promotional' uone mambo.
Najiandaa ku-claim hii ngoma