Mungu hasamehi Dhambi; tuache kudanganyana

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,034
50,942
MUNGU HASAMEHI DHAMBI; TUACHE KUDANGANYANA

Kwa Mkono wa, Robert Heriel

Haya nayo niliandika, kusudi usije ukasema hukuambiwa. Nami najua siwezi kuukimbiza muda, nao umekuwa mchache, umeniacha wala siuoni tena. Basi ikiwa muda wetu wa kuishi Duniani ni mdogo yafaa tuishi kwa tahadhari.

Ni mimi Taikon mwana kutoka Nyota ya Tibeli yenye mbawa mbili, Irukayo huku na huku.

Nami nimechunguza mienendo ya muda. Tena mienendo ya nguvu za nishati nimezidadisi. Hata mabadiliko ya Maada nimeyatafakari. Nako sikupata la ziada isipokuwa nalipata huzuni na uchovu.

Mungu hasamehi dhambi bali husamehe Makosa

Ipo tofauti ndogo ila ya muhimu baina ya MAKOSA na DHAMBI ingawaje yote hufanana katika utendaji.

Makosa ni kitendo au hali ya kutofanya kitu kilichosahihi pasipo kujua au kama ajali.

Dhambi ni kitendo au hali ya kutofanya kitu kwa usahihi ukiwa unajua sio sahihi.

Dhambi haitokei kama ajali.

Makosa yanatokea kama ajali

Dhambi ni mchakato unaohitaji kupangwa

Makosa sio mchakato, hauhitaji kupanga

Kisayansi Makosa huitwa Errors

Kwa mfano ninapoandika hapa ninaweza kukosea kuandika bila dhamiri huitwa typing Errors.

Dhambi ni dhamiri/kusudi linalohitaji utayari.

Makosa sio Dhamiri

Kisheria; wale watu wa sheria kama Wanasheria, mahakimu na Majaji wataungana na mimi kuwa kuna Makosa ya kukusudia na yale yakutokukusudia.

Makosa ya Kukusudia huitwa Uhalifu

Na Mahakamani huwezi samehewa kwa uhalifu lakini unaweza samehewa kwa Makosa.

Kwa upande wa kiroho. Mungu hajawahi kusamehe Dhambi na kamwe hatakuja kusamehe dhambi zetu.

Dhambi ni Uasi wa makusudi kabisa.

Ndio maana vitabu vinaeleza usimjaribu Bwana Mungu wako.

Viongozi wa Dini hutufundisha kuwa Mungu anasamehe dhambi jambo ambalo ni uongo wa mchana. Mungu hajawahi kusamehe dhambi na hatakuja Awahi kusamehe dhambi.

Mshahara wa dhambi ni mauti. Haki ya dhambi ni kifo.

Wote tunajua Mungu ni mwenye Haki. Kusema Mungu anasamehe ni kumuondolea sifa ya kuwa na HAKI. Jambo ambalo sio kweli.

Sitajali kama utanikubalia au utakataa ukweli upo hivyo Mungu hasamehi dhambi. Labda tujidanganye.

Ndio maana watoto wadogo hawana dhambi, ila wanamakosa wao hufanya pasipo kujua hivyo haziitwi dhambi bali Makosa.

Nilishasema dhambi ni dhamiri. Makusudi.

Halikadhalika na wema ni dhamiri ya mtu. Mtu anaweza akafanya wema lakini asijue ni wema. Huo hauitwi wema. Halikadhalika mtu anaweza akafanya Dhambi asijue ni dhambi hiyo haiitwi dhambi bali makosa

Mtu asiye na dhamiri ni kama mnyama tuu. Hana wema wala hana ubaya

Ni kama kichaa au mwendawazimu. Hakuna dhambi au wema kwa kichaa au mwendawazimu kwani hawafanyi kwa dhamiri.

Ndio maana hata Mahakamani kichaa hata hatia. Au mnyama hana hatia isipokuwa anayemmiliki.

Ukiona unafanya jambo lolote baya kwa kukusudia jua hutasamehewa Milele zote.

Watu hujidanganya na kudanganywa kuwa Mungu anasamehe hivyo hufanya dhambi makusudi kwa maana wanajua Wataomba msamaha.

Mbona hawafanyi hivyo hata kwenye mahakama za Duniani?

Ikiwa duniani haipo hivyo sembuse kwa Mungu!!

Kufanya kosa kwa Makusudi(Dhambi) ni kukufuru Mungu. Na hili hata Yesu alilitolea maelezo kuwa dhambi ya Kukufuru haina Msamaha. Akiwamaanisha dhambi ya Makusudi.

Nimeshaeleza dhambi ni mchakato

Ukitaka kuzini lazima upange na uweke mikakati.

Lazima utumie gharama na wakati unafanya hayo kuna nafsi yako inakuonya lakini unaamua kukaidi.

Kinachomfanya mtu ajifiche atendapo dhambi ni nafsi yake kuwa na hatia.

Dhambi ni aibu

Makosa ni sehemu ya kujifunza

Ndio maana watoto wadogo wakoseapo hawaoni aibu kwani bado hawana dhamiri.

Dhambi ni Uamuzi

Makosa ni ajali

Mungu hakumsamehe na hatamsamehe Shetani kwa sababu alidhamiria

Mungu hakumsamehe Adam na Hawa kwa sabab walidhamiria.

Mungu sio mpumbavu yaani atuambie jambo Fulani ni kosa tusifanye alafu kwa ukaidi wetu tunafanya alafu atusamehe😀😀😀 hizo tunaita dharau.

Huwezi mdharau Mungu kwa kisingizio cha Msamaha.

Fundishola Msamaha linafundishwa na kutumika vibaya kwa maslahi ya waovu

Yesu alipokuwa msalabani alisema; wasamehe kwa kuwa hawajui walitendalo.

Hii ni kusema wasiojua walitendalo ndio husamehewa.

Kuna aina mbili ya Kutokujua jambo;

1. Kutokujua kabisa

2. Kutokujua kwa kusahau

1. Kutokujua Kabisa

Hii ni ile hali mtu hajui kitu kabisa yaani hajawahi kufundishwa au kujifunza. Hajawahi kusikia wala kuona

2. Kutokujua kwa Kusahau
Hii ni ile hali mtu alikuwa anajua jambo lakini kwa udhaifu wa kibinadamu akasahau

Asiyejua kabisa na aliyesahau ni sawa sawa tuu.

Ndio maana kwenye mtihani wale ambao hawajui kabisa na wale waliosahau walivyofundishwa hufeli.

Hata hivyo mambo hayo mawili kiroho hupimwa na dhamiri.

Dhamiri haidanganyi

Mtu aliyefanya dhambi utamjua kwani lazima atarudia hata mara Mia licha ya kuomba msamaha

Mtu aliyefanya Makosa; harudii akishambiwa jambo hilo ni dhambi.

Kuomba msamaha mara kwa mara kwa kosa lile ni kumdhihaki Mungu. Na Mungu hadhihakiwi.

Kama neno msamaha lisingekuwepo Duniani bas dhambi zingekuwa chache sana.

Lakini kadiri fundisho la msamaha linavyoenezwa ndivyo dhambi zinavyozidi kuongezeka.

Msamaha ni neno ambalo linatumiwa vibaya na viongozi wa dini au hawalielewi vyema.

Mungu hatatusamehe dhambi zetu.

Unazini kwa makusudi kabisa alafu unategemea Mungu a kusamehe? Acha dhihaka

Unaua kwa makusudi alafu Mungu a kusamehe?

Unaiba, unagonga wake za watu kwa makusudi licha ya kujua ni dhambi bado utake msamaha?

Mwisho; Tusifanye dhambi kwani kusamehewa hakupo

Wale wa Neema waendelee kujidanganya.

Note: Kizazi hiki sio Bora kama kizazi kilichopita. Na kinyume chake ni sahihi pia.


Robert Heriel

Taikon wa Fasihi

0693322300

Kwa sasa Morogoro
 
Toa mstari mmoja wa Biblia au aya ya korani inayosema dhambi haisamehewi.

Kuna mstari katika biblia unasema;

"Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu kama bendera zitakuwa nyeupe kama theluji asema bwana"

Ikimaanisha kuwa kuna msamaha wa Dhambi.

So biblia nayo inadanganya?

Kwahiyo Yesu alikuja hapa ulimwenguni bure.

Angalia isijekuwa unatumiwa na shetani bila kujijua.
 
Toa mstari mmoja wa Biblia au aya ya korani inayosema dhambi haisamehewi.

Kuna mstari katika biblia unasema;

"Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu kama bendera zitakuwa nyeupe kama theluji asema bwana"

Ikimaanisha kuwa kuna msamaha wa Dhambi.

So biblia nayo inadanganya?

Kwahiyo Yesu alikuja hapa ulimwenguni bure.

Angalia isijekuwa unatumiwa na shetani bila kujijua.

Yesu alikuja kwa ajili ya Makosa sio dhambi

Kama lengo lingekuwa dhambi ambaye angepaswa adhibitiwe ni shetani mwenyewe.

Unapofanya Dhambi unakuwa shetani
Unapofanya Makosa unaendelea kubaki binadamu

Nafikiri waandishi na watafsiri wa Biblia ndio walipuyanga
 
Uongo mtupu, anasamehe sababu anajua kuwa sisi viumbe wake ni dhaifu na dhambi tunazaliwa nazo mkuu unaposema mtoto hana makosa ni uongo. Tukikiri imani tunasema tumezaliwa katika hali ya dhambi ndo maana tunaungama na ndo sababu ya kuwepo kwa ubatizo sababu mtoto anazaliwa na dhambi ya asili ambayo walifanya adam na hawara yake hawa.
 
Uongo mtupu, anasamehe sababu anajua kuwa sisi viumbe wake ni dhaifu na dhambi tunazaliwa nazo mkuu unaposema mtoto hana makosa ni uongo. Tukikiri imani tunasema tumezaliwa katika hali ya dhambi ndo maana tunaungama na ndo sababu ya kuwepo kwa ubatizo sababu mtoto anazaliwa na dhambi ya asili ambayo walifanya adam na hawara yake hawa.

Sawa mimi muongo

Endelea kufanya dhambi usubiri msamaha wa Mungu
 
Toa mstari mmoja wa Biblia au aya ya korani inayosema dhambi haisamehewi.

Kuna mstari katika biblia unasema;

"Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu kama bendera zitakuwa nyeupe kama theluji asema bwana"

Ikimaanisha kuwa kuna msamaha wa Dhambi.

So biblia nayo inadanganya?

Kwahiyo Yesu alikuja hapa ulimwenguni bure.

Angalia isijekuwa unatumiwa na shetani bila kujijua.
Isaya 1:18
 
MUNGU HASAMEHI DHAMBI; TUACHE KUDANGANYANA

Kwa Mkono wa, Robert Heriel

Haya nayo niliandika, kusudi usije ukasema hukuambiwa. Nami najua siwezi kuukimbiza muda, nao umekuwa mchache, umeniacha wala siuoni tena. Basi ikiwa muda wetu wa kuishi Duniani ni mdogo yafaa tuishi kwa tahadhari.

Ni mimi Taikon mwana kutoka Nyota ya Tibeli yenye mbawa mbili, Irukayo huku na huku.

Nami nimechunguza mienendo ya muda. Tena mienendo ya nguvu za nishati nimezidadisi. Hata mabadiliko ya Maada nimeyatafakari. Nako sikupata la ziada isipokuwa nalipata huzuni na uchovu.

Mungu hasamehi dhambi bali husamehe Makosa

Ipo tofauti ndogo ila ya muhimu baina ya MAKOSA na DHAMBI ingawaje yote hufanana katika utendaji.

Makosa ni kitendo au hali ya kutofanya kitu kilichosahihi pasipo kujua au kama ajali.

Dhambi ni kitendo au hali ya kutofanya kitu kwa usahihi ukiwa unajua sio sahihi.

Dhambi haitokei kama ajali.

Makosa yanatokea kama ajali

Dhambi ni mchakato unaohitaji kupangwa

Makosa sio mchakato, hauhitaji kupanga

Kisayansi Makosa huitwa Errors

Kwa mfano ninapoandika hapa ninaweza kukosea kuandika bila dhamiri huitwa typing Errors.

Dhambi ni dhamiri/kusudi linalohitaji utayari.

Makosa sio Dhamiri

Kisheria; wale watu wa sheria kama Wanasheria, mahakimu na Majaji wataungana na mimi kuwa kuna Makosa ya kukusudia na yale yakutokukusudia.

Makosa ya Kukusudia huitwa Uhalifu

Na Mahakamani huwezi samehewa kwa uhalifu lakini unaweza samehewa kwa Makosa.

Kwa upande wa kiroho. Mungu hajawahi kusamehe Dhambi na kamwe hatakuja kusamehe dhambi zetu.

Dhambi ni Uasi wa makusudi kabisa.

Ndio maana vitabu vinaeleza usimjaribu Bwana Mungu wako.

Viongozi wa Dini hutufundisha kuwa Mungu anasamehe dhambi jambo ambalo ni uongo wa mchana. Mungu hajawahi kusamehe dhambi na hatakuja Awahi kusamehe dhambi.

Mshahara wa dhambi ni mauti. Haki ya dhambi ni kifo.

Wote tunajua Mungu ni mwenye Haki. Kusema Mungu anasamehe ni kumuondolea sifa ya kuwa na HAKI. Jambo ambalo sio kweli.

Sitajali kama utanikubalia au utakataa ukweli upo hivyo Mungu hasamehi dhambi. Labda tujidanganye.

Ndio maana watoto wadogo hawana dhambi, ila wanamakosa wao hufanya pasipo kujua hivyo haziitwi dhambi bali Makosa.

Nilishasema dhambi ni dhamiri. Makusudi.

Halikadhalika na wema ni dhamiri ya mtu. Mtu anaweza akafanya wema lakini asijue ni wema. Huo hauitwi wema. Halikadhalika mtu anaweza akafanya Dhambi asijue ni dhambi hiyo haiitwi dhambi bali makosa

Mtu asiye na dhamiri ni kama mnyama tuu. Hana wema wala hana ubaya

Ni kama kichaa au mwendawazimu. Hakuna dhambi au wema kwa kichaa au mwendawazimu kwani hawafanyi kwa dhamiri.

Ndio maana hata Mahakamani kichaa hata hatia. Au mnyama hana hatia isipokuwa anayemmiliki.

Ukiona unafanya jambo lolote baya kwa kukusudia jua hutasamehewa Milele zote.

Watu hujidanganya na kudanganywa kuwa Mungu anasamehe hivyo hufanya dhambi makusudi kwa maana wanajua Wataomba msamaha.

Mbona hawafanyi hivyo hata kwenye mahakama za Duniani?

Ikiwa duniani haipo hivyo sembuse kwa Mungu!!

Kufanya kosa kwa Makusudi(Dhambi) ni kukufuru Mungu. Na hili hata Yesu alilitolea maelezo kuwa dhambi ya Kukufuru haina Msamaha. Akiwamaanisha dhambi ya Makusudi.

Nimeshaeleza dhambi ni mchakato

Ukitaka kuzini lazima upange na uweke mikakati.

Lazima utumie gharama na wakati unafanya hayo kuna nafsi yako inakuonya lakini unaamua kukaidi.

Kinachomfanya mtu ajifiche atendapo dhambi ni nafsi yake kuwa na hatia.

Dhambi ni aibu

Makosa ni sehemu ya kujifunza

Ndio maana watoto wadogo wakoseapo hawaoni aibu kwani bado hawana dhamiri.

Dhambi ni Uamuzi

Makosa ni ajali

Mungu hakumsamehe na hatamsamehe Shetani kwa sababu alidhamiria

Mungu hakumsamehe Adam na Hawa kwa sabab walidhamiria.

Mungu sio mpumbavu yaani atuambie jambo Fulani ni kosa tusifanye alafu kwa ukaidi wetu tunafanya alafu atusamehe hizo tunaita dharau.

Huwezi mdharau Mungu kwa kisingizio cha Msamaha.

Fundishola Msamaha linafundishwa na kutumika vibaya kwa maslahi ya waovu

Yesu alipokuwa msalabani alisema; wasamehe kwa kuwa hawajui walitendalo.

Hii ni kusema wasiojua walitendalo ndio husamehewa.

Kuna aina mbili ya Kutokujua jambo;

1. Kutokujua kabisa

2. Kutokujua kwa kusahau

1. Kutokujua Kabisa

Hii ni ile hali mtu hajui kitu kabisa yaani hajawahi kufundishwa au kujifunza. Hajawahi kusikia wala kuona

2. Kutokujua kwa Kusahau
Hii ni ile hali mtu alikuwa anajua jambo lakini kwa udhaifu wa kibinadamu akasahau

Asiyejua kabisa na aliyesahau ni sawa sawa tuu.

Ndio maana kwenye mtihani wale ambao hawajui kabisa na wale waliosahau walivyofundishwa hufeli.

Hata hivyo mambo hayo mawili kiroho hupimwa na dhamiri.

Dhamiri haidanganyi

Mtu aliyefanya dhambi utamjua kwani lazima atarudia hata mara Mia licha ya kuomba msamaha

Mtu aliyefanya Makosa; harudii akishambiwa jambo hilo ni dhambi.

Kuomba msamaha mara kwa mara kwa kosa lile ni kumdhihaki Mungu. Na Mungu hadhihakiwi.

Kama neno msamaha lisingekuwepo Duniani bas dhambi zingekuwa chache sana.

Lakini kadiri fundisho la msamaha linavyoenezwa ndivyo dhambi zinavyozidi kuongezeka.

Msamaha ni neno ambalo linatumiwa vibaya na viongozi wa dini au hawalielewi vyema.

Mungu hatatusamehe dhambi zetu.

Unazini kwa makusudi kabisa alafu unategemea Mungu a kusamehe? Acha dhihaka

Unaua kwa makusudi alafu Mungu a kusamehe?

Unaiba, unagonga wake za watu kwa makusudi licha ya kujua ni dhambi bado utake msamaha?

Mwisho; Tusifanye dhambi kwani kusamehewa hakupo

Wale wa Neema waendelee kujidanganya.

Note: Kizazi hiki sio Bora kama kizazi kilichopita. Na kinyume chake ni sahihi pia.


Robert Heriel

Taikon wa Fasihi

0693322300

Kwa sasa Morogoro
Isaya 43:25 Naam, mimi ndimi niyafutaye makosa kwa ajili yangu mwenyewe wala sitazikumbuka dhambi zako...
 
Yesu alikuja kwa ajili ya Makosa sio dhambi

Kama lengo lingekuwa dhambi ambaye angepaswa adhibitiwe ni shetani mwenyewe.

Unapofanya Dhambi unakuwa shetani
Unapofanya Makosa unaendelea kubaki binadamu

Nafikiri waandishi na watafsiri wa Biblia ndio walipuyanga
Wewe ni wakala wa shetani.
 
Biblia imebadilika boss? Em tupe mafungu mapya hayo.
 
Kuna wakati asee naogopa tunakoelekea Mungu watu watamchukulia kama Mshikaji.

Mtoa mada Dhambi zinasamehewa.

Kitu pekee ambacho hakisamehewi ni kukufuru
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom