Mungu alipoona kiburi chetu, kaamua kutupatia mtihani wa miaka 10

Mtarban

JF-Expert Member
Jan 14, 2015
3,818
5,007
Wale Wa sodoma na Gomola aliamua kuwatupia moto baada ya kuona maovu yamezidi katika nchi ile, hali kadhalika gharika wakati wa Nuhu. sasa sisi Mungu kaamua kutuonjesha kidogo tu kwa kutupa mtihani Wa miaka kumi, amini nakuambia ukiweza kufaulu mtihani huu kwa miaka hii wewe utakuwa ama shujaa/mwoga. Nasema hivyo kutokana na sababu mbalimbali.

ngoja niendelee na mtihani nisije nakafeli maana mtihani wenyewe mgumu
 
Yaani eti nao walikaa wakamteua! Duuh they need to be examined in their heads.
 
Wale Wa sodoma na Gomola aliamua kuwatupia Gharika baada ya kuona maovu yamezidi katika nchi ile. sasa sisi Mungu kaamua kutuonjesha kidogo tu kwa kutupa mtihani Wa miaka kumi, amini nakuambia ukiweza kufaulu mtihani huu kwa miaka hii wewe utakuwa ama shujaa/mwoga. Nasema hivyo kutokana na sababu mbalimbali.

ngoja niendelee na mtihani nisije nakafeli maana mtihani wenyewe mgumu
Sorry,rekebisha sehemu ya uzi wako uliposema,sodoma na gomora walipata gharika,siyo hivyo,Mungu aliwaadhibu kwa moto na kibiriti(sulphur) soma ripoti hii Mwanzo19:24-25,na habari ya gharika inahusu wakati wa Nuhu,soma repoti hii katika mwanzo7:7-23,samahani,kama nimekosea kwa marekebisho,MH,wangu
 
Samahani tujikumbusshe ,yafuatayo kisha kije kisa chenyewe na hatimaye swali
1)Mtu mnyonge,hulipiza kisasi
2)Mwenye nguvu husamehe
3)mwenye akili hupuuza anayotendewa
HADITHI YA KWELI KUHUSU MTU MWENYE NGUVU,
Nikiwa mtoto wa darasa la tatu hivi mwaka wa 1976 nilisimuliwa kisa kimoja na baba yangu
kuwa katika kijiji kilichokuwa jirani na kijiji chetu,yaani pawaga aliishi mtu mmoja aliyeitwa
Mnyawasa,mtu huyu alikuwa na utajiri wa mifugo kiasi cha ng'ombe elfu kumi(10,000)aliowapata kwanjia ya kuwinda wanyama wa pori,inasemekana alikuwa na nguvu sana kiasi kwamba wanyama kama tembo alikuwa anaua kwa kuingia kwenye makundi ya tembo na kutoboa matumbo
kisha kung'oa meno,aidha akiwa na wenzake chui wakija alikuwa anawakataza wasiwaue kwa mishale akiwaambia wataharibu ngozi kwa sauti ndogo ya chini,maana ndivyo alivyokuwa ameumbika kwa sauti ya chini sana,na hapo yeye alikuwa anauwezo kuwauwa chui kwa mikono tu kwa kuwakaba shingo zao na kisha kuchuna ngozi zao hao wanyama,ifahamike kwamba wakati wa utoto akiwa anafanya kibarua kwa
wazungu,aliwahi kumuua nyapara wa kikoloni kwa teke moja kwa kuvunja mbavu tatu,
mtoto huyu inasemekana alipata hasira baada ya kuendelea kutumwatumwa sana bila kupumzika na akawa amechoka sana,nyapara alipomtuma tena mtoto alimjibu nimechoka kwasauti ya upole sana,na nyapara akamzaba kibao akisema ana kiburi
na mtoto huyo akarudisha teke moja akamua yule nyapara,nguvu hizi ziwatisha sana watu wa kijij kile taarifa zilipoenea
Wazazi waktafuta matibabu au uwezekano wa kupunguza nguvu hizo hatarishi,inasemekana ;wakati ule zilipungua,lakini kwavile alipunguzwa akiwa mtoto mdogo zikarejea vilevile na kuzidi Paka wakinywa maziwa alikuwa anapiga kwa Kidole tu nakupasua vifuvu vyao hadi ubongo nje
Sehemu aliyoishi waliishi pia wamasai,ambao sikumoja waliiba ng'ombe wake 100(miamoja)
alichofanya,alitengeneza mishale miamoja yenye sumu na kuenda usiku akalenga ng'ombe 100,kama alioibiwa,na wamasai walipoamka asubuhi walikuta ng'ombe 100 wamekufa ; wakamua kuchukua ng'ombe 100 na kuenda kutubu;aidha wake zake wakisumbua alikuwa hapigi,ila alichokuwaanafanya
ilikuwa anachukua ng'ombe kadhaa wa kutosha anawarudisha kwa wazazi wao na kwa sauti yake ileile ya upole anawaambia tunaomba mtutunzie wametushinda kisha anatoa wale ng'ombe kisha anaondoka na kuwaachia wazazi wao

.
Swali;Je MNYAWASA alikuwa na nguvu zipi , za kimwili au za kiakili?
 
Sorry,rekebisha sehemu ya uzi wako uliposema,sodoma na gomora walipata gharika,siyo hivyo,Mungu aliwaadhibu kwa moto na kibiriti(sulphur) soma ripoti hii Mwanzo19:24-25,na habari ya gharika inahusu wakati wa Nuhu,soma repoti hii katika mwanzo7:7-23,samahani,kama nimekosea kwa marekebisho,MH,wangu

asante ndugu! uko sahihi
 
Mungu anachukia sana wanafiki.
Ufipa kumejaa wanafiki watupu,kiufupi hawajui lipi hasa wanalotaka katika maisha yao,polen sana.
 
Tulishauri kwamba kwakuwa huyu kiumbe anatoka kwenye jamii yetu, basi tufuatilie ukoo wake wakoje? Tukasema tuanzie kwa babu yake kisha kwa baba ili tujiridhishe kwamba hawana tatizo. Tatizo mpaka sasa hakuna mtu anayetaka kujua hilo. Lakini ushauri ule una maana yake.
 
Miaka kumiiiiii!!!aaaah mkuu,acha utani bwana. Kwani mapumziko baada ya dakika 45 yamefutwa? Na ule muda wa mapumziko haturuhusiwi kubadilisha mchezaji??? Kama tunaweza, kumi kivipi sasa???
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom