Mungu akulipe kheri nyingi Mwanadada Maria Sarungi

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,498
51,090
Mwanadada Maria, umeendelea kwa juhudi kubwa kuutahadharisha umma uchukue tahadhari juu ya ugonjwa wa Korona.

Tangu miezi kadhaa nyuma ambapo serikali ya awamu ya tano ilikuwa ikiutangazia ulimwengu kuwa nchini hakuna Korona, hukuchoka kuutahadharisha umma ujikinge maana kiukweli Korona nchini ipo

Wakati unapaza sauti ulikejeliwa na wana MATAGA na mashabiki maandazi wa hata mambo ya kijinga yafanywayo na watawala

Leo ugonjwa wa "changamoto za kupumua" umeanza kupiga "pabaya", Taifa limekuwa kama limezinduliwa kutoka usingizini kuwa hii kitu ipo!

Ndugu Watanzania wenzangu, Hii vita hatuiwezi mtu mmojammoja maana ni kama Mtumbwi, huwezi kuwa unaziba tobo moja halafu mwingine anatoboa kwingine!.

Bila serikali kuchukua nafasi yake na kuact responsibly kama mamlaka kuu yenye dhamana ya kuchukua hatua za kuthibiti hili janga kwa kuwashirikisha wananchi, basi Janga hili litatuacha nyang'anyang'a.

Ndiyo maana nampongeza huyu binti Sarungi kwa jitihada kubwa za kunusuru maisha ya wananchi.

Binti alifikia hatua ya kuziandikia jumuia za kimataifa barua ziokoe Wataanzania dhidi ya denial na hatua za kusuasua za serikali hii kulinda uhai wa watu wake. Kwa hakika huyu binti anastahili pongezi, Kazi zake za kutetea watu na haki zao ni kazi nzuri sana.

Namuomba asikate tamaa aendelee hivyohivyo, maana jitihada zake zinasaidia
 
20210217_234209.jpg
 
Mwanadada Maria, umeendelea kwa juhudi kubwa kuutahadharisha umma uchukue tahadhari juu ya ugonjwa wa Korona.

Tangu miezi kadhaa nyuma ambapo serikali ya awamu ya tano ilikuwa ikiutangazia ulimwengu kuwa nchini hakuna Korona, hukuchoka kuutahadharisha umma ujikinge maana kiukweli Korona nchini ipo

Wakati unapaza sauti ulikejeliwa na wana MATAGA na mashabiki maandazi wa hata mambo ya kijinga yafanywayo na watawala

Leo ugonjwa wa "changamoto za kupumua" umeanza kupiga "pabaya", Taifa limekuwa kama limezinduliwa kutoka usingizini kuwa hii kitu ipo!

Ndugu Watanzania wenzangu, Hii vita hatuiwezi mtu mmojammoja maana ni kama Mtumbwi, huwezi kuwa unaziba tobo moja halafu mwingine anatoboa kwingine!.

Bila serikali kuchukua nafasi yake na kuact responsibly kama mamlaka kuu yenye dhamana ya kuchukua hatua za kuthibiti hili janga kwa kuwashirikisha wananchi, basi Janga hili litatuacha nyang'anyang'a.

Ndiyo maana nampongeza huyu binti Sarungi kwa jitihada kubwa za kunusuru maisha ya wananchi.

Binti alifikia hatua ya kuziandikia jumuia za kimataifa barua ziokoe Wataanzania dhidi ya denial na hatua za kusuasua za serikali hii kulinda uhai wa watu wake. Kwa hakika huyu binti anastahili pongezi, Kazi zake za kutetea watu na haki zao ni kazi nzuri sana.

Namuomba asikate tamaa aendelee hivyohivyo, maana jitihada zake zinasaidia
Mungu azidi kumpa nguvu katika mapambano yake. Watanzania tujifunze kutoka kwa wanaotupambania pia tuchukue tahadhari, ugonjwa umeshaenea kwa Kasi sana nchi na sasa tunakula matunda ya ukaidi wetu.
 
Hata yule mrithi wa Nkurunzizah sikuhizi ana fuata ushauri wa WHO kuhusu covid. Amechanganya zake na za kuambiwa.
 
Back
Top Bottom