munaotafuta wachumba jf jihadharini na chuma ulete.

Watunduru

Senior Member
Dec 29, 2011
170
39
wadau kwa nia ya dhati niliweka bango la kuhitaji mchumba hapa jf na kweli nilipata,kwa muda mfupi tu baada ya kukutana nilibaini hatuwezi kuishi,na kwa kuwa lengo ilikuwa nipate mke basi nikaamua kujinasua mapema ili nisimpotezee muda wake na mimi nisipoteze lengo langu la kupata mke wa ndoa.

Siku ya kwanza na dakika ya kwanza kukutana nae aliniomba nimtoe kwa lunch pamoja na rafiki yake,nilikubali bila kinyongo lakini ktk notebook yangu nikatia x kwa kitendo kile,wakati tunakula mimi nikiwa sivuti hata sigara mwenzangu akaitisha Tusker nikatia x nyingine.

Wakati tunaendelea kupata mara akapita chinga na viatu akaitisha na wakati tunaagana nikapewa ombi nimnunulie simu yenye fast internet,nilichoka mwili na roho Nilivotoka hapo nikajisemea mwenye kwamba huyu si tu kwamba hatoshi kuwa mke bali hafai hata kupajua nyumbani kwangu.namshukuru mungu nilifanikiwa kujinasua na japo bado sijapata mke nimelazimika kujipa muda zaidi na tafakuri mpya maana hali ile ilinitia hofu na kunichanganya hasa ikizingatiwa hitaji langu ni mke wa maisha na sio gonga niondoke.
Karibuni wadau tusaidiane mawazo.
 
ooooh no....hebu nitafute tuongee vizuri....huyo mwanamke hakufai.....ni gubegube......
na kwa nini akufanyie hivyo....hustahili kabisa.......
 
duu chezea viburudisho wewe wanamambo we acha 2 bila shaka huyo kazoea kuchuna kwa sana na kugawa kwa sana siri ya mwanamke ukitaka kujua tabia yake mwangalie ile cku ya kwanza unapo mtongoza hapo utagundua kitu kama kweli hutaki kuchezea unataka kuoa
 
enzi za mwalimu mchumba alitakiwa umjue tangu baba yake, mama yake na ndugu zake wengine kabla ya kutangaza ndoa lakini siku hizi imekua vululu,vululuuuuu tu ndio maana ndoa zetu hazidumu.
 
Kumbe wewe sio jemedari.
Mimi mwenzako mke wangu shopping ni Paris, watoto wanasoma Cambridge, mke anatembelea Aston Martin model ya 2012, kwa biashara hii hiii ya kuuza juisi na ubuyu.
Usije ukanidharau ukiniona nakatiza mitaani na kandambili na nguo mbovumbovu.
Nafanya kila kitu kwa wale niwapendao.
Mimi ni JEMEDARI wa mapenzi
wadau kwa nia ya dhati niliweka bango la kuhitaji mchumba hapa jf na kweli nilipata,kwa muda mfupi tu baada ya kukutana nilibaini hatuwezi kuishi,na kwa kuwa lengo ilikuwa nipate mke basi nikaamua kujinasua mapema ili nisimpotezee muda wake na mimi nisipoteze lengo langu la kupata mke wa ndoa.

Siku ya kwanza na dakika ya kwanza kukutana nae aliniomba nimtoe kwa lunch pamoja na rafiki yake,nilikubali bila kinyongo lakini ktk notebook yangu nikatia x kwa kitendo kile,wakati tunakula mimi nikiwa sivuti hata sigara mwenzangu akaitisha Tusker nikatia x nyingine.

Wakati tunaendelea kupata mara akapita chinga na viatu akaitisha na wakati tunaagana nikapewa ombi nimnunulie simu yenye fast internet,nilichoka mwili na roho Nilivotoka hapo nikajisemea mwenye kwamba huyu si tu kwamba hatoshi kuwa mke bali hafai hata kupajua nyumbani kwangu.namshukuru mungu nilifanikiwa kujinasua na japo bado sijapata mke nimelazimika kujipa muda zaidi na tafakuri mpya maana hali ile ilinitia hofu na kunichanganya hasa ikizingatiwa hitaji langu ni mke wa maisha na sio gonga niondoke.
Karibuni wadau tusaidiane mawazo.
 
Hahaha! Sikucheki ila hvyo vitendo vinanipa mshangao unanonipa kicheko, atleast she didnt hide, umemjua mapema ukakimbia mapema hongera kwa hilo! Wishn u the best ktk kumpata wa ukweli
 
ooooh no....hebu nitafute tuongee vizuri....huyo mwanamke hakufai.....ni gubegube......
na kwa nini akufanyie hivyo....hustahili kabisa.......
Preta kwani kuna ubaya gani mwanamke kuomba atolewe lunch yeye na rafiki yake?, Je kuna ubaya gani mwanamke akiomba anywe Tusker bariiiiidi moja tu? Kuna ubaya gani ukimnunulia mwanamke viatu vya WAMACHINGA?
Huyo ni mwanamke mwenye akili sana, alikuwa nategemea mwanamume ambaye hapo siku za usoni atakuwa baba wa nyumba ampe mwongozo, "usifanye hiki", "viatu hatununui leo, haviko kwenye bajeti"
Jamaa yangu Watunduru umeonyesha u Tunduru wako kwa kushindwa kumuelewa binti wa JF.
Nakushauri urudi kwenu Tunduru, ukatambike, uiombe MIZIMU YA MABABU IKUTAFUTIE MKE
 
Ha ha ha ha unatafuta mke kwa ininternet wewe umechelewa Kabisa aisee. Ndo ukome umeshindwa kutongoza wale unaokutana nao mpaka utafute hapa? Pole wewe umefundishwa vizuri sana.

Halafu acha ubahiri wewe Lu nch tu unapiga Kelele ukiambia Mark II itakuwaje?
 
Ha ha ha ha unatafuta mke kwa ininternet wewe umechelewa Kabisa aisee. Ndo ukome umeshindwa kutongoza wale unaokutana nao mpaka utafute hapa? Pole wewe umefundishwa vizuri sana.

Halafu acha ubahiri wewe Lu nch tu unapiga Kelele ukiambia Mark II itakuwaje?

mmmh, upo mamito....?xmass hiyo yapiga hodi........naandaa mapokezi
 
Bahili Hapati Mke!!!!!!!!!!! Mke asie n matumizi kamfate Kijijini kwao, na hapo akikaa mjini mwezi tu hakawii kuitisha Viatu vya GLADIATORS!, Carolite, skin jeans na madera ya isha mashauzi!!!!!!!!!
 
Dah.. Pole sana kaka..! Usikate tamaa, utampata tuu ambaye mtaendana..!! Kila la heri..!!
 
wadau kwa nia ya dhati niliweka bango la kuhitaji mchumba hapa jf na kweli nilipata,kwa muda mfupi tu baada ya kukutana nilibaini hatuwezi kuishi,na kwa kuwa lengo ilikuwa nipate mke basi nikaamua kujinasua mapema ili nisimpotezee muda wake na mimi nisipoteze lengo langu la kupata mke wa ndoa.

Siku ya kwanza na dakika ya kwanza kukutana nae aliniomba nimtoe kwa lunch pamoja na rafiki yake,nilikubali bila kinyongo lakini ktk notebook yangu nikatia x kwa kitendo kile,wakati tunakula mimi nikiwa sivuti hata sigara mwenzangu akaitisha Tusker nikatia x nyingine.

Wakati tunaendelea kupata mara akapita chinga na viatu akaitisha na wakati tunaagana nikapewa ombi nimnunulie simu yenye fast internet,nilichoka mwili na roho Nilivotoka hapo nikajisemea mwenye kwamba huyu si tu kwamba hatoshi kuwa mke bali hafai hata kupajua nyumbani kwangu.namshukuru mungu nilifanikiwa kujinasua na japo bado sijapata mke nimelazimika kujipa muda zaidi na tafakuri mpya maana hali ile ilinitia hofu na kunichanganya hasa ikizingatiwa hitaji langu ni mke wa maisha na sio gonga niondoke.
Karibuni wadau tusaidiane mawazo.

hahhahaha kama yuko humu sijui atajiskiaje aftr reading dis thread maskini...ulimtoa out bar?? teh teh
 
Inategemea ulijitambulishaje kwake!
Mimi nilompata, kwa mara ya kwanza alipokuja ili tuonane; jambo la kwanza alinikuta niko kazini, hivyo alinambia anatafuta chumba akapumzike then atanijulisha ni wapi alipopumzika - nikamkubalia.
Kwa kuwa ilikuwa Jumamosi; kazi ilikuwa nusu siku; ilipofika saa saba alinipigia sm na kuniuliza ni wapi wanachoma vizuri samaki. Nilimwelekeza na kumwambia tukutane hapo ili tukapate wote samaki choma.
Kweli tulikutana hapo na wote tulikuwa tunatumia Kil (bia). Tuliongea mengi na nilifufrahia kampani yake kwa sana. Ilipofika mida ya saa 2 aliniomba nimsindikize alipochukua chumba, kabla hatujaondoka niliomba bill - zikaletwa mbili - ya jikoni na ya vinywaji. Alichukua ya vinywaji akalipia na kunambia hivi - si wote tunafanya kazi? wacha tugawane majukumu. Sikuwa na wasiwasi naye hadi tunaenda chumbani kuendelea na maongezi.

Niko naye hadi sasa japo hatujafunga mkataba.
 
Hakuna ulimbukeni duniani kama mwanamke kujifanya kama bidhaa!
Wapo wanaume wanaopenda kuwagharamia sana wanawake lakini sio katika style ya kulazimisha au kukomoa hasa kwenye First impression.
 
hahahaha wewe hapa huwezi pata mke ng'oo wapo hapa wenzio kupoteza muda tuu.....ila asante sana ebu niPM nimtafute huyo shosti nikale nae maraha.
 
Back
Top Bottom