Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
niliapa beki tatu ndani ya nyumba yangu marufuku....nsijepata kesi bure
Huyo mume anabaki mpaka sa sita ili iweje?
Aache kumpa house girl kazi za usiku, afanye kazi mchana kutwa na usiku pia? Ahakikishe akiingia kulala h'girl nae anaingia kulala manake huyo mumewe anamvizia h'g.
hahahaahhahhahhah nakaba mpaka kivuli aisee sio unaweka beki tatu halafu kijoka anazima taa :lol: hizi nywele mtihani na naona nilivyoweka bayana ndo zimepukutika kiukweli saa hizi ngozi nje nje:hatari: sasa likija beki tatu la kigunya nna changu mie!
Acha hizi Shosti!!!! ndio maana Nywele zimegoma kuota...Weka beki tatu lakini kula naye sahani moja kuhakikisha hazimi taa akimuona Baba mwenye nyumba na ukifanikiwa kumpata tu baada ya miezi miwili utaona nywele zimeota tena kwa kasi ya kutisha maana stress za kazi za nyumbani zitakuwa zimepungua sana na hivyo kupata wakati wa kupumua.
Mie sijaona shida hapo kabisa yaani mie niache kulala kisa eti namsubiria mume
akiangalia mpira?? Mweeehhh wanawake tuna kazi sana ila mie ahaaahhh
Sasa mke anataka mume alale saa tatu amekuwa kuku? Anakaa na wanume wenzake saa ngapi ? Acheni kuwabana waume zenu kwa visingizio vya kitoto.
...mmeona ee? ....yaani mume akiwa type ya mkaaji nyumbani, lawama ati halali mapema...
akiwa type ya kurudi majogoo, lawama!...duuuh....