Mume anakuletea mke mwenza ndoa Kikristo, Ungefanyaje?

MzalendoHalisi

JF-Expert Member
Jun 24, 2007
4,519
1,367
Nimekuta hii habari kule Michuzi Blog- Je ungekuwa wewe ungemshauri vipi huyu mama?

Bwana Michuzi,

Naomba usome mail hii kisha ukiona inafaa uiweke kwenye blog yako wadau wanisaidie/wanishauri. Ila kama utaona haistahili, basi achana nayo, ila tafadhali usiweke e-mail yangu hadharani.

Mimi ni Mama nimeolewa na nina watoto watatu, ninaishi hapa Tanzania ninafanya kazi shirika lisilo la Kiserikali. Nimeishi na mume wangu kwa miaka mingi sasa kwa raha na karaha pia. Mume wangu alikuwa akifanya kazi shirika fulani, lakini kwa bahati mbaya aliachishwa kazi miaka miwili nyuma kutokana na sababu flani flani.

Wakati mume wangu akifanya kazi, tulikuwa tukiishi nyumba ya shirika alilokuwa akifanyia kazi, na baada ya kuachishwa, nikaomba nyumba ya shirika na nikapewa ambayo tunaendelea kuishi mpaka sasa.

Let me cut the story short;

Ni kwamba miezi kama sita baada ya mume wangu kuachishwa kazi, mara siku moja jioni natoka kazini nakuta watoto wawili wameongezeka wakiwa na bag kabisa, nikamuuliza mwenzangu ugeni wa wapi huu, akadai ni habari ndefu japo baadae alikiri ni watoto wake/wetu mtu mzima nikajua haya ni matunda ya zile siku alikuwa akilala nje nikawapokea na kuwatambulisha kwa watoto wangu kwamba na hao ni ndugu zao.

Kama hiyo haikutosha, baada ya kama miezi miwili hivi akaletwa Mama wa watoto hao (mke mwenzangu)!, Nikauliza itakuwa vipi na sisi ni wakristo wa ndoa moja tu, tutaiambiaje jamii? Yule Mama akadai hapo haondoki kwani kaja kulea wanawe na hana imani na mimi kumlelea watoto wake. Nikabeba mzigo kwamba sawa na akae lakini kwa kivuli kwamba ni ndugu wa mume wangu (nakiri udhaifu kwa hili).

Siku zikaenda kificho nje lakini ndani inajulikana na yeye ni Mama kwani hakukuwa na kificho hicho hata kwa watoto! Tuliita wazazi wa pande zote mbili kusuluhisha, siwezi kuwalaumu kwa kufuata sheria za dini kwani walidai katika kiapo cha Ndoa tuliapa kutokuachana mpaka kifo kitapotutenganisha, na kwamba nivumilie ndio mitihani katika maisha.

Nikavumilia kwamba huu ni msalaba wangu niubebe mwenyewe. Kinachoniuma sasa ni kwamba ndani ya nyumba hakuna tena maelewano kati yangu na Mume wangu, na tumegeuka maadui mimi na mkwe mwenzangu, kiasi hata kile kificho kwamba ni ndugu wa mume wangu hakipo tena kwani mbali na watu kuhisi, yeye alikuwa mstari wa mbele kutamba kwamba na yeye ni mke kama nilivyo mimi, hivyo ana haki na mamlaka ndani ya nyumba, kuwekeana nyimbo za vijembe na kuvaliana kanga za mafumbo zinazonunuliwa kwa hela yangu! Kero ni nyingi ndani ya ndoa yangu nyingine hata aibu kuzisema hadharani, na nikisema tuachane Mume wangu anakuja na visingizio kwamba ninamnyanyasa vile hana kazi na mimi nina kazi, wazazi nao wanadai sio vizuri watoto kulelewa upande mmoja, Jamani nimeshindwa na sina raha ya maisha tena nifanyeje?

Mke mwenzangu nikampa ushauri walau apange chumba nje ya nyumba yetu tutamlipia hataki, anadai atakuwa pale mume wake na watoto wake watakapokuwepo! Sijui, labda mimi sio mvumilivu vya kutosha, lakini kweli niko njia panda naomebi uhsuri nifanyeje jamani.
Sina raha tena na ndoa yangu, na maisha nayaona machungu. Ieleweke, sio kwamba vile hana kazi ndio maana nafanya hivi, hapana ila manyanyaso na vituko ndani ya nyumba nimechoka.

Samahani kwa kuwapotezea muda kuwaelezea shida zangu, naomebi msaada wenu Watanzania wenzangu.
Kwa Mume wangu, najua ukisoma ujumbe huu utajua ni wewe na familia yetu naiongelea, nisamehe kwa kuchukua uamuzi huu ni kwa sababu sina pa kukimbilia tena, acha tusikie wanajamii wengine wanasemaje then we can act on the advise.
natanguliza shukrani.
 
Huyu mama nampa pole na hongera kwa uvumilivu na mapenzi ya kweli kwa huyo bwana. Kwa kizazi cha sasa ni wanawake wa kuhesabu ambao wanaweza kuvumilia hali hiyo.

Kwa kuangalia naona idadi ya wategemezi ilivyoongezeka na usawa wenyewe huu ulivyo mgumu.

Pili inaonekana Mr. na mama yake hawampendisana huyu bi mkubwa ndio maana huyu bi mdogo ameweza kupata kiburi cha namna hiyo.

Mimi namshauri huyu dada, usawa wa sasa ni wa hatari, amwambie huyu Mr, mkewe na hao watoto wao wakapange, na yeye akae na wanae.

Kama atasema sijui ndoa ya kanisa, jamii itanionaje n.k, atakuja kufa na presha na na virusi halafu akaacha watoto bado wadogo. Kwanza amshukuru mungu kama bado hajapata. (ili watoto wapatikane ni kwamba mtu alikuwa peku) na vema pia akamuuliza Mr anao watoto wangapi wengine nje ya ndoa.

Na mali za familia/ndoa kama wana aaccount ya pamoja, nyumba n.k, aannze kuangalia sasa, ikiwezekana hati ya maandishi ya umilik/ugawaji wa mali.

Nampa pole sana, ingekuwa ni mimi nimeshamtimua kitambo yeye, mkewe, mama yake and the likes.
 
Kasana,

Kwa wanawake wa leo- basi ktk 100 yuko mmoja kama huyu mama! Ni mvumilivu sana!

Huyu jamaa ni kicheche- na kama unavyosema huenda ana watoto zaidi nje!

Mimi saa ingine dini ya wakristo inananipa taabu maana 60% ya waliooa wana nyumba ndogo- na hatari kubwa ya ukimwi ipo hapo! Huyu jamaa angekuwa Mwislamu angempangishaia tu chumba huyu mke wake!

Muhimu-- huyu mama mgeni akubali tu kupangishiwa chumba ili aondoke kwa hali ya amani!

Huyu jamaa atafute kazi, hata ya kubangaiza ili alete pesa kulea watoto wake- manake watoto watano, na watu wazima 3 nyumba- jumla 8 nyumba moja na mapato ni ya mama!

Huyu jamaa ni free rider- sii mwanamme wa nguvu- heshima ya baba ni kubeba majukumu ya kutunza familia!
 
Nimekuta hii habari kule Michuzi Blog- Je ungekuwa wewe ungemshauri vipi huyu mama?

Huyu mama nampa HONGERA haya ni matokeo ya Imani za DINI ambazo haziruhusu UHURU wa Mtu na KUHESHIMU uhalisia wa BINADAMU,

Kabla hatuja mshauri kuna maswali madogo ya kujiuliza hili ni tokeo la jambo Flani ambalo hatulijui sote inawezekana huyu jamaa anaetwa kicheche leo hapa kuna vitu vilipelekea yeye kuamua kua na NYUMBA NDOGO kama wengi manvoita na hii ni matokeo ya ukoloni kutu aminisha ndoa ni mmoja tu while mila zetu zilitufundisha na kutupa uhuru wa kua na wake zaidi ya mmoja bila matatizo.

Hayo ya juu ni angalizo tusije jadili matokeo na kutua conclussion bila kutafuta root ya tatizo.

MSIMAMO/USHAURI

Mama huyu naamini ni muafrika akumbuke mila zetu wazee walikua na wake zaidi ya mmoja na waliishi sehemu mmoja bila tatizo sasa kwanza alikubali hilo baada ya hapo kama kuna tatizo la utulivu huyo mzee alitatue kama no solution aje JF tutampa ushauri.

MWISHO
Nampongeza huyo jamaa kwa kudumisha mila na utamaduni masuala ya dini tuliletewa tu huyo mama asikariri hilo akubali mila yetu ya mume mmoja wake wengi na kuishi kwa kukubaliana.(tusisahau si rahisi watu zaidi ya mmoja kuweka maji ktk chupa moja na then kila mmoja kupata maji yake aliyo weka ktk chupa hiyo mmoja lakini ni rahisi na inawezekana mtu mmoja kuweka maji ktk chupa tofauti na baadae kupata maji yake aloweka.)thats why utamaduni wa mume mmoja unakubalika agaist mke mmoja waume wengi.
 
Mkuu
Mapenzi hayawezi kuwa kama ya mwanzo tena, hapo tayari doa limeshaingia.

Yule mama amesema atakaa pale alipo mumewe, sasa inabidi na huyo mume aende, na inaonekana huyo bi mdogo aliyekuja hajaenda shule au kakulia uswahilini.

Kwa mazingira ya vijembe, taarabu, n.k anaweza kupata tabu (au kuuawa kwa sumu au kwa ndumba na ngai).
Sababu na mume na yeye inaonekana amekolea kwa huyo mdogo, wacha waende wote.

Inanikumbusha movie ya 'waiting to exhale'. Namshauri kwa mara nyingine kipindi cha sasa si cha kubembelezana yeye a EXHALE tu, watoto watakua tu.
 
Nampongeza huyo jamaa kwa kudumisha m ila na utamaduni masuala ya dini tuliletewa tu huyo mama asi kariri hilo akubali mila yetu ya mume mmoja wake wengi na kuishi kwa kukubaliana

1. Hayo hayakuwa makubaliano yao tangia awali.
2. Kwa mila za kwetu, mume alikuwa natakiwa awe na kihamba na kuwaweka katika hicho kihamba chake (labda kama anatoka morogoro anakubali kuishi ukweni).
3. Hata mila za wenzetu/(hata waislamu) huwezi kuoa bila kumshirikisha mkeo, ni lazima mukubaliane wote.
4. Hata kama yule mama alikuwa na makosa, staili ya walivyokuja haikuwa sawa.
 
Mama inabidi atafute msaada wa kisheria kumtoa huyo "mkewenza" kwenye nyumba yake.Hata kama wameamua kuondoa maadili ya kikristo ya ndoa, bado mama ana haki ya kumtoa mtu asiyemtaka katika nyumba yake.
 
Mama inabidi atafute msaada wa kisheria kumtoa huyo "mkewenza" kwenye nyumba yake.Hata kama wameamua kuondoa maadili ya kikristo ya ndoa, bado mama ana haki ya kumtoa mtu asiyemtaka katika nyumba yake.

Pundit,
Amtoe mama aende wapi wakati ni yeye aliyemkaribisha kwa kuficha siri atamwita dada wa mume?

Muhimu huyu jamaa atafute kazi- ampangie huyu mke mwingine nyumba! Hilo ndo jambo la hekima!
 
Hii ndo garama ya dhambi ya unafiki! Kitendo cha huyo mama kufanya dhambi ya unafiki kutaka mbele za watu aonekane ni mkristo safi ndo kinacho mgharimu!, Unafiki ni dhambi mbaya sana, nauchukuia sana unafiki na madhara yake ni makubwa sana ndo kama haya ambayo yanampata huyu mama!

Ushauri wangu, aachane na dhambi ya unafiki, aweke wazi jambo hili kwamba mumewe kaanguka si mkristo wa ndoa moja tena, na hivo mumewe aamue jinsi ya kuwatunza hao wakeze, akiona hawezi hilo ni juu yake, ila asiendelee kuwa msalaba wa huyo mama kwa ajili ya unafiki wake wa kutosema ukweli!

Katu si jukumu la huyo mama kumtunza mke mwenzie!!
 
Hii ndo garama ya dhambi ya unafiki! Kitendo cha huyo mama kufanya dhambi ya unafiki kutaka mbele za watu aonekane ni mkristo safi ndo kinacho mgharimu!, Unafiki ni dhambi mbaya sana, nauchukuia sana unafiki na madhara yake ni makubwa sana ndo kama haya ambayo yanampata huyu mama!

Ushauri wangu, aachane na dhambi ya unafiki, aweke wazi jambo hili kwamba mumewe kaanguka si mkristo wa ndoa moja tena, na hivo mumewe aamue jinsi ya kuwatunza hao wakeze, akiona hawezi hilo ni juu yake, ila asiendelee kuwa msalaba wa huyo mama kwa ajili ya unafiki wake wa kutosema ukweli!

Katu si jukumu la huyo mama kumtunza mke mwenzie!!

Lets not blame the victim.Mama kachemsha lakini inaonekana amechemsha kutokana na udhaifu wake wa kuwa "too nice". Inabidi asaidiwe ili hili dume na huyu bimdogo wasim-exploit zaidi.

Anaweza kuwasiliana na TAMWA na wanasheria wengine kuangalia anaweza kufanya nini.
 
This woman is too good to be TRUE, Unbelivable, yaani kuna wanawake wenye roho nzuri hivi duniani! kweli Mungu kaumba, nampa maksi zote za upendo na uvumilivu, I just can't imagine...I might be too strict that's why I find it difficult to believe! Yaani mwaanume umtunze halafu akuletee timu; yaani mke na watoto siamini wala sitaki kuelewa how I could handle the situation. Well, nakutakia kila la kheri bibie ila nafikiri unahitaji msaada wa kisheria kabla huyo mama mdogo pamoja na mumeo kipenzi(fungua friji) hawajakutoa nje ya picha.P'se think twice and do something NOW!(usijifikirie mwenyewe ktk hili wafikirie watoto wako pia) You are too nice, nakupongeza sana hasa katika ulimwengu wa sasa!
 
Stori hii naona ni ya kubuni haiwezekani mtu ukawa ni mtakatifu kiasi hicho. Jamaa aliyetunga ni mbunifu mzuri wa hekaya.
 
Kama hii sio ubunifu, nampa hongera huyo mama kwa kuwa na upendo wa kupitiliza.

Kaandika kwamba anataka waachane na huyo bwana ila wazazi/ndugu wanasema ameshakula kiapo kuishi katika shida na karaha (katika ndoa ya kanisani).... katika mazingira haya huyo mama hafungwi tena na kiapo kile kwa sababu mume ameshavunja dhana nzima ya ndoa yenyewe (mke/mume mmoja).
Pia kaandika akitaka waachane mume anadai kwamba anamwacha sababu amepigika... hicho ni kisingizio tu. Huyo bwana anajua fika udhaifu wa mkewe..anatafuta kuonewa huruma hata anapoboronga.

Kama mama yuko tayari kuishi ndoa ya mume 1 wake wengi, ni sawa ila sioni kinachombana kutaka waachane na mume wake. Anyway, sometimes you have to scarifice your hapiness for the ones you love.
 
Stori hii naona ni ya kubuni haiwezekani mtu ukawa ni mtakatifu kiasi hicho. Jamaa aliyetunga ni mbunifu mzuri wa hekaya.

Bubu, sio lazima huyu mwanadada akawa mbunifu ama ni hadithi tu za kubuni. Watu tuna mitazamo ya aina tofauti kwa kila suala na kwa kila tatizo, sio lazima tuwe na mtazamo mmoja. Mfano, mtu anapotembea porini, akakutana na gogo ambalo limezuia njia anayopita, kuna mmoja ataliruka (bila kulikanyaga) na kuendelea na safari. Mwingine atapita pembeni na kuendelea na safari. Mwingine ataliondoa na kuondoa kadhia, na ataendelea na safari pia. Mwingine atalipitia kwa juu, kwa kulikanyaga na kuendelea na safari. Mwingine atajiuliza, lile gogo limefikaje pale, na kadhalika. Kuna watu ambao "Ukimpiga shavu la kushoto, anakugeuzia na la kulia" na wengine "Ukimpiga shavu la kushoto naye anakurudishia". Sasa huenda huyu mwanamama yuko hilo kundi la kwanza, sitashangaa. Kuna watu wana roho za ajabu sana. Kuna wengine anamfumania mpenziwe "Live" anaamua kumuua,kwa kufikiri kwamba katatua tatizo na mwingine anamfumania mpenziwe na anamsamehe na yanaisha hapo hapo! Wote hawa wanatatua tatizo moja, ila kwa njia tofauti. Kuna mwingine akipatwa na matatizo makubwa anajiua, na mwingine akipatwa na tatizo hilo hilo anaomba ushauri kabla hajaamua afanye nini ili kulitatua. Huu ndio utofauti wetu wanadamu.
Huyu mwanadada anaweza akachukuliwa kama mjinga fulani vile kwa kumsamehe mumewe mzinzi, lakini huenda yeye kaangalia madhara ya muda mrefu ya kuwa bila mume, akilinganisha na madhara ya kushi katika uke wenza wa kunyanyasika. hivyo tusimshangae sana kwa kuomba ushauri wakati "UTATUZI" anao!
Naamini anajua analolifanya kwa sababu ni mtu mzima, shime tumsaidia kama kuna ushauri wa maana, ila sio kumkatisha tamaa!
 
mnapoishi pamoja kama mume na mke ni vyema mkajuana tabia. mwanamme kamsoma mke wake vizuri sana na alijua ana roho ya u-malaika ndio maana alimletea timu ya mpira ndani ili wote walishwe na mkewe. ndio maana huyu mama anaomba ushauri hapa maana u-malaika wake unamfanya asijue cha kufanya. ingekua ni mwanamke kichaa kama wengine, mwanamme asingethubutu kumletea mwanamke na watoto ndani, au hata kuwapitisha karibu na nyumbani. kama wengine walivyoshauri, atafute ushauri wa kisheria kama nguvu hiyo anayo, maana inaelekea ana mapenzi makubwa sana kwa mumewe ambaye hana haja naye.
 
wadau wa JF naomba muingie kwenye blog ya MICHU msome majibu ya MUME wa huyu mama. Hope he's telling the truth. kazi kweli kweli, ndoa hizi, mungu saidia.
 
wadau wa JF naomba muingie kwenye blog ya MICHU msome majibu ya MUME wa huyu mama. Hope he's telling the truth. kazi kweli kweli, ndoa hizi, mungu saidia.

Sal,
Mume wa huyo mama kaandika hivi,

Michuzi mimi ndo mume wa huyo mama aliyeandika kulalama kuhusu mke mwenza. Mbona hatoi upande mwingine wa habari? Mbona hasemi katika watoto watatu aliozaa mmoja si wangu; alimpata nilipokuwa masomoni? Anatafuta public sypathy isiyo na justification! After all si kwamba sina kazi; I am a consultant. Nimejiajiri. I take care of my family. Muulizeni alikuwa akifanya nini hadi nikajikuta naenda nje? Anyway, haya yalikuwa ya ndani ya familia. Sikutarajia atayaleta huku. Sasa tutaona kama ana jeuri aliyotamba katika waraka wake kwamba anayo, nyo!

Sasa tunaweza kujadili kuanzia hapa.
Ingependeza sana kama huyu 'Mume' angetoa story nzima ili sie wanajamii tu-balance mambo.
 
Woman! lots of respect and admiration for you, you are every man's dream, I mean what more can a man ask for? Hii ndio wazungu wanaita 'true love' na kweli ume prove kale ka msemo ka kiswahili kanakosema 'ukilipenda boga- upende na maua yake' You are perfect.
USHAURI-Kama bado unampenda mumeo banana hapohapo na upiganie ndoa yako-kwa ngumi na mateke, kwa msaada wa majirani, polisi, wataalamu wa sheria na hata ukishindwa nenda Bagamoyo ukampige kipapai mke mwenzio aione nyumba kama kambi ya majambazi! Usisikilize manungayembe hapa yanayokushauri umuache mumeo, wanataka kuona ndoa yako ikivunjika tu ili uwe kama wao!
 
Du kumbe wote sii waaminifu? Halafu mnafanya ngono za nje bila kinga wakati mna watoto -je hamwogopi kuacha yatima?

Basi mkapime kwanza wote watatu- kabla ya yote ili kujua afya zenu!
 
Back
Top Bottom