The Transporter
JF-Expert Member
- Aug 26, 2016
- 3,475
- 6,854
Ipo hivi nina rafiki yako ambae shughuli zake ni dereva sasa amenipa mkasa wake na kuomba ushauri.
Jamaa mwanzo mwa miaka ya 2000s alimpata Binti wakakubaliana na kuamua kuishi pamoja wakabahatika wakapata watoto watatu wakiume wawili wa kike mmoja. Ila kutokana na sababu kadhaaa wakawa wametengena watoto wakaenda kwa babu yao (baba wa mshikaji).
Wao kila mtu akaendelea na shughuli zake jamaa amehangaika kwa wanawake kadhaa na kufanikiwa kupata watoto huko wawili na katika hao wanawake mmoja kajifungua mwanzoni mwa mwaka huu huko kote alikuwa anafanya taratibu zote kama kwenda kupima afya na alikuwa salama.
Sasa mwaka jana akarudisha mapenzi kwa mzazi mwenzie wa awali( mama wa watoto watatu) na kupelekea kuanza kuishi wote pamoja kwani huyo mama watoto wake alikuwa single tu.
Sasa juzi kanipigia simu kadata nikamuuliza shida nini?
Akaniambia ana anishi na huyo mwanamke ila kuna siku aliona vidogo vya ajabu na hakuweza kujua ni vidogo vya aina gani kwani alijaribu kuvipiga picha na kumshirisha mtu wake ila hawakuweza kujua kwani havikuwa na jina!
Sasa juzi mkewe akiwa katoka kuna nguo alikuwa anaitafuta katika pekuapekua ndio akakuta kadi ya clinic ya waathirika wa HIV na kadi inamuonesha huyo mama watoto wake toka mwaka 2018 amekuwa mwanachama wa ARV na kinachomuuma zaidi ni kuwa hakumuambia hivyo hiyo ina maana mkewe yupo tayari wafe wote na watoto wabaki yatima!
Na katika maisha aliyoishi naye kwa miezi hii mitatu walikuwa wakiwa wanazungumzia mambo ya HIV mkewe huyo alikuwa anawakashfu sana waathirika kumbe na yeye ni mmoja wapo.
Hivyo ameniomba ushauri je amuambie mkewe au auchune tu mpka na yeye akapime?
Majibu akipata akiwa anao afanye nini na huyo mkewe na akiwa hana maisha yaende vipi hapo?
Jamaa mwanzo mwa miaka ya 2000s alimpata Binti wakakubaliana na kuamua kuishi pamoja wakabahatika wakapata watoto watatu wakiume wawili wa kike mmoja. Ila kutokana na sababu kadhaaa wakawa wametengena watoto wakaenda kwa babu yao (baba wa mshikaji).
Wao kila mtu akaendelea na shughuli zake jamaa amehangaika kwa wanawake kadhaa na kufanikiwa kupata watoto huko wawili na katika hao wanawake mmoja kajifungua mwanzoni mwa mwaka huu huko kote alikuwa anafanya taratibu zote kama kwenda kupima afya na alikuwa salama.
Sasa mwaka jana akarudisha mapenzi kwa mzazi mwenzie wa awali( mama wa watoto watatu) na kupelekea kuanza kuishi wote pamoja kwani huyo mama watoto wake alikuwa single tu.
Sasa juzi kanipigia simu kadata nikamuuliza shida nini?
Akaniambia ana anishi na huyo mwanamke ila kuna siku aliona vidogo vya ajabu na hakuweza kujua ni vidogo vya aina gani kwani alijaribu kuvipiga picha na kumshirisha mtu wake ila hawakuweza kujua kwani havikuwa na jina!
Sasa juzi mkewe akiwa katoka kuna nguo alikuwa anaitafuta katika pekuapekua ndio akakuta kadi ya clinic ya waathirika wa HIV na kadi inamuonesha huyo mama watoto wake toka mwaka 2018 amekuwa mwanachama wa ARV na kinachomuuma zaidi ni kuwa hakumuambia hivyo hiyo ina maana mkewe yupo tayari wafe wote na watoto wabaki yatima!
Na katika maisha aliyoishi naye kwa miezi hii mitatu walikuwa wakiwa wanazungumzia mambo ya HIV mkewe huyo alikuwa anawakashfu sana waathirika kumbe na yeye ni mmoja wapo.
Hivyo ameniomba ushauri je amuambie mkewe au auchune tu mpka na yeye akapime?
Majibu akipata akiwa anao afanye nini na huyo mkewe na akiwa hana maisha yaende vipi hapo?