Mulugo: Tumekamata vijana walio taka kuharibu mfumo wa BVR wakijifanya maafisa wa NEC

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
52,173
41,979
Wasalaam wana jamvi!
Bila shaka mtakuwa mnajua fika zoezi ya uandikishaji wa wapiga kura kwenye daftari jipya linaendelea kwenye mikoa tofauti mwanza ukiwemo!

Nakumekuwa na kelele nyingi kuwa zoezi limekwama kabisa na halito wezekana kabisa pamoja na changamoto hizo tume imekuwa ikituhakikishia kuwa zoezi litakamilika hivi karibuni!Na mwenye macho atakubaliana nami kuwa pamoja na changamoto zilozopo watu wana jiandikisha na zoezi litakamilika!

Zoezi hili likiendelea mkoa wa Mwanza kumejitokeza vijana ambao wamekuwa wakijifanya ni wataalam wa mfumo wa BVR kutoka NEC hivyo uenda kwenye vituo na kujifanya wanafanya marekebisho kwenye machine kumbe wana vuruga na kuharibu machine ili ionekane zoezi limekwama! Lakini wasimamizi na jeshi la polisi walifanikiwa kuwanasa na wako mikononi mwa polisi!

Ni wazi kuna watu hawataki kuona zoezi hili linafanikiwa hivyo wanatumia njia zozote ili kulikwamisha na lionekane limeshindikana...hakika ina sikitisha sana!

Bado najiuliza nani aliwatuma hao vijana na anapata faida gani? kwanini?

Nalishukuru jeshi la polisi mwanza na watumishi kwa kuwatia nguvuni hao vijana na watasema walio watuma!

Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Afrika!

Karibuni wana jamvi!

Chanzo: Channel 10
 
Sasa tunajadili nini kabla ya ripoti ya polisi kutoka?
Au unataka tuanze kupiga ramli ya watu waliohusika?
Kwa vyovyote watakuwa ni ccm wametumwa kutoka lumumba kuja kuharibu utaratibu kama walivyofanya Arusha
Na jaji Lubuva akajitokeza kuwaulia soo!!!
 
Sasa tunajadili nini kabla ya ripoti ya polisi kutoka?
Au unataka tuanze kupiga ramli ya watu waliohusika?
Kwa vyovyote watakuwa ni ccm wametumwa kutoka lumumba kuja kuharibu utaratibu kama walivyofanya Arusha
Na jaji Lubuva akajitokeza kuwaulia soo!!!

Kwani wewe hujui ni wakina nani hawataki zoezi lifanikiwe?
 
Rutta, kweli wewe huna tofauti na Mulugo! Huyo Mulugo alipovuliwa Uwaziri ndio akapelekwa Mwanza kuwa Mkuu wa Mkoa!
 
Wasalaam wana jamvi!
Bila shaka mtakuwa mnajua fika zoezi ya uandikishaji wa wapiga kura kwenye daftari jipya linaendelea kwenye mikoa tofauti mwanza ukiwemo!

Nakumekuwa na kelele nyingi kuwa zoezi limekwama kabisa na halito wezekana kabisa pamoja na changamoto hizo tume imekuwa ikituhakikishia kuwa zoezi litakamilika hivi karibuni!Na mwenye macho atakubaliana nami kuwa pamoja na changamoto zilozopo watu wana jiandikisha na zoezi litakamilika!

Zoezi hili likiendelea mkoa wa Mwanza kumejitokeza vijana ambao wamekuwa wakijifanya ni wataalam wa mfumo wa BVR kutoka NEC hivyo uenda kwenye vituo na kujifanya wanafanya marekebisho kwenye machine kumbe wana vuruga na kuharibu machine ili ionekane zoezi limekwama! Lakini wasimamizi na jeshi la polisi walifanikiwa kuwanasa na wako mikononi mwa polisi!

Ni wazi kuna watu hawataki kuona zoezi hili linafanikiwa hivyo wanatumia njia zozote ili kulikwamisha na lionekane limeshindikana...hakika ina sikitisha sana!

Bado najiuliza nani aliwatuma hao vijana na anapata faida gani? kwanini?

Nalishukuru jeshi la polisi mwanza na watumishi kwa kuwatia nguvuni hao vijana na watasema walio watuma!

Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Afrika!

Karibuni wana jamvi!

Chanzo: Channel 10

Sasa Tume haijui watumishi wake mpaka ikaribishe wahuni kugusa mashine zake? Hawana utambulisho maalumu wa watumishi?Inakuwaje kila mtu anakuwa na access ya mitambo hiyo?Kutakuwa kuna tatizo katika utendaji.
 
Back
Top Bottom