Mulugo: Mwaka Kesho Serikali itashindwa kuwapeleka watoto Sekondari

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,445
7,813
Naibu Waziri wa zamani wa Elimu na Mbunge wa Songwe, Philip Mulugo leo Bungeni amesema mwaka kesho serikali itashindwa kuwapeleka watoto Form one kwenye shule za serikali kwasababu mpango wa elimu bure ulianza miaka sita iliyopita hivyo watoto waliopo leo darasa la sita ni takribani 1.8 milioni ilhali madarasa na madawati ya shule za serikali uwezo wake ni kuchukua wanafunzi laki saba na nusu.

Amesema serikali itabidi ijenge shule jambo ambalo hadhani kama itawezekana, ameiomba serikali ije na mpango wa PPP kwani shule binafsi zina kila kitu lakini zinakosa wanafunzi na nchi ni ya wote hivyo ameomba wawe pamoja.

Mulugo ame-declare interest kwamba yeye ni mdau wa elimu na mmiliki wa shule binafsi.

 
Amekuwa muwazi kwamba anamiliki shule inaitwa "Southern High land"

Pia issue ya capacity ya miundombinu ya kubeba form one in the comming years ni ndogo sana. Sijui kama itawezekana. Halafu tatitizo litakuwa endelevu hata kwenda A-level pia vyuo.
 
Ila ana hoja nzuri, je kwa miundombinu ya watoto laki saba wakiingia 1.5 million Itawezekana?

Hakuna anayekosa hoja nzuri kwenye kutetea ugali wake

Angetoa ushauri huu ukiwa na suluhu kwa kuzingatia gharama za shule yake huku akilinganisha na uwezo wa watanzania haswa wale wapiga kura wake pale jimboni. Angekuja na ushauri wa jinsi ya kuisaidia serikali kuendelea kutoa elimu kwa kugharamia kila kitu ili watoto wa kitanzania waelimike katika usawa

Yeye kama mtu aliyeamua kuwekeza kwenye elimu anaweza kuendelea kupokea wanafunzi wachache wenye uwezo wa gharama zake

Pia ni muda muafaka kwake kuangalia mahitaji ya taifa hili kwenye elimu kwa level nyingine kama Ufundi stadi, kilimo na ufugaji akawekeze huko
 
Back
Top Bottom