figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,491
- 54,884
Ni katika kijiji cha Kishanda. Bibi mmoja anaejulikana kama Makoleta, ameuawa kwa kukatwakatwa mapanga na kuchomwa moto pamoja na nyumba yake pia imechomwa.
Inadaiwa bibi huyo kamuua mtoto wa shule ya msingi alopotea ni siku ya 12 zilizopita.
Inadaiwa Mjukuu wa huyo bibi akiwa shuleni akawaambia wenzake kwamba yule mtoto anayetafutwa kwamba kapotea, yupo kwao bibi yake kamficha nyuma ya mlango
Inadaiwa Kijijini hapo tetesi za bibi huyo kuwa mchawi ni za miaka mingi.
Wananchi waliamua kuanza msako kwenye hiyo nyumba.
Inadaiwa walikuta mwili wa mtoto umezikwa kwenye shamba la huyo bibi na mtoto kashaanza kuoza lkn nguo alizopotea nazo zinaonekana bado
Ndipo walipochukua sheria mkononi. Bado tunasubiri taarifa kamili kutoka mwenye mamlaka husika kwani tukio linetokea jana jioni.
======
Mtoto Ismail Hamis mweye umri wa miaka 7 aliyepotea tangu Aprili 5 mwaka huu akitokea shule, jana usiku amekutwa akiwa amefariki kwenye shamba la bibi mmoja akiwa amefukiwa kwenye shimo
Tukio hilo lililotokea katika Kata ya Kishanda Wilayani Muleba limesababisha baadhi ya Wananchi wa maeneo hayo kukata migomba ya bibi huyo na kumuua kwa kumchomo moto akiwa ndani ya nyumba yake
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Revocatus Malimi amesema tangu kupotea kwa mtoto huyo hakuonekana tena hadi mwili wake ulipogundulika umefukiwa katika shamba la bibi huyo, ukiwa na sare zake za shule
Aidha, Kamanda Revocatus amesema taratibu za kiuchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo zinaendelea kufanyika
Inadaiwa bibi huyo kamuua mtoto wa shule ya msingi alopotea ni siku ya 12 zilizopita.
Inadaiwa Mjukuu wa huyo bibi akiwa shuleni akawaambia wenzake kwamba yule mtoto anayetafutwa kwamba kapotea, yupo kwao bibi yake kamficha nyuma ya mlango
Inadaiwa Kijijini hapo tetesi za bibi huyo kuwa mchawi ni za miaka mingi.
Wananchi waliamua kuanza msako kwenye hiyo nyumba.
Inadaiwa walikuta mwili wa mtoto umezikwa kwenye shamba la huyo bibi na mtoto kashaanza kuoza lkn nguo alizopotea nazo zinaonekana bado
Ndipo walipochukua sheria mkononi. Bado tunasubiri taarifa kamili kutoka mwenye mamlaka husika kwani tukio linetokea jana jioni.
======
Mtoto Ismail Hamis mweye umri wa miaka 7 aliyepotea tangu Aprili 5 mwaka huu akitokea shule, jana usiku amekutwa akiwa amefariki kwenye shamba la bibi mmoja akiwa amefukiwa kwenye shimo
Tukio hilo lililotokea katika Kata ya Kishanda Wilayani Muleba limesababisha baadhi ya Wananchi wa maeneo hayo kukata migomba ya bibi huyo na kumuua kwa kumchomo moto akiwa ndani ya nyumba yake
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Revocatus Malimi amesema tangu kupotea kwa mtoto huyo hakuonekana tena hadi mwili wake ulipogundulika umefukiwa katika shamba la bibi huyo, ukiwa na sare zake za shule
Aidha, Kamanda Revocatus amesema taratibu za kiuchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo zinaendelea kufanyika