MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,183
- 2,304
Mara nyingi nikimwona Katibu mkuu wa CCM kwenye TV huwa nabadilisha chaneli mara moja kwani huwa sielewi kama anahutubia,anagombana, ni majigambo, mahubiri au amekuja pale kuchekesha kama wajukuu zake akina Masanja.
Mara nyingi naona kama hayuko serious kwani akiongea anategemea tusikilize kwa makini kama watoto wa chekechea wakisimuliwa hadithi za Sindbad baharia, abunuwasi au hadithi za hisopo.
Juzi aliniudhi alipokuwa anasisitiza kule Igunga eti wataleta maji !!!!. Kama Rostam aliyekuwa karibu na JK ameshindwa kufanya hayo kwa miaka aliyokuwa mbunge ni ndoto kwa Kafumu kufurukuta kwani ni sawa na kudanganya watu kuwa mkokoteni utaweza kubeba mzigo ulioshindikana kubebwa na FUSO. Huu ni utani hasa unaofanywa na Mukama na ni dharau kubwa si tu kwa watu wa Igunga bali kwa waTZ wote.
Kama ni kweli kwanini walisubiri wakati wa Kampeni ndo waje na hizo hoja kwani tatizo la maji limetokea baada ya Rostam kujiuzulu au lilikuwepo siku zote?
Hii inanikumbusha incidence moja wakati huyu Mukama akiwa mkurugenzi wa jiji la Dar aliwahi ulizwa na mwandishi mmoja kwenye TV jiji la Dar lina wastani wa wakazi wangapi akajibu kiurahisi kuwa " HAJUI"
Hapo anakwenda Igunga na kuwasomea wananchi kipande cha karatasi alichoandika mikakati ya uongo ili tu wapate jimbo jambo ambalo ni DHAMBI
Huyu bwana haeleweki na mara nyingi speech zake huwa na makelele na majigambo, uzushi , kujidefend, kukashifu badala ya kutoa mambo yenye contents ambazo waTZ wanataka kuzisikia ili angalau matumaini yao kwa Mafisadi yarejee.
MI NAMTAKIA MAFANIKIO KATIKA KUIZAMISHA VEMA " MV SPICE MAGAMBA" ikiwa imejaza kupita kiasi mafisadi ambao wamekataa kuachia meli ili wengine wa safiri salama na kuamua kama ni kuzama basi tuzame tufe wote wote.
Mara nyingi naona kama hayuko serious kwani akiongea anategemea tusikilize kwa makini kama watoto wa chekechea wakisimuliwa hadithi za Sindbad baharia, abunuwasi au hadithi za hisopo.
Juzi aliniudhi alipokuwa anasisitiza kule Igunga eti wataleta maji !!!!. Kama Rostam aliyekuwa karibu na JK ameshindwa kufanya hayo kwa miaka aliyokuwa mbunge ni ndoto kwa Kafumu kufurukuta kwani ni sawa na kudanganya watu kuwa mkokoteni utaweza kubeba mzigo ulioshindikana kubebwa na FUSO. Huu ni utani hasa unaofanywa na Mukama na ni dharau kubwa si tu kwa watu wa Igunga bali kwa waTZ wote.
Kama ni kweli kwanini walisubiri wakati wa Kampeni ndo waje na hizo hoja kwani tatizo la maji limetokea baada ya Rostam kujiuzulu au lilikuwepo siku zote?
Hii inanikumbusha incidence moja wakati huyu Mukama akiwa mkurugenzi wa jiji la Dar aliwahi ulizwa na mwandishi mmoja kwenye TV jiji la Dar lina wastani wa wakazi wangapi akajibu kiurahisi kuwa " HAJUI"
Hapo anakwenda Igunga na kuwasomea wananchi kipande cha karatasi alichoandika mikakati ya uongo ili tu wapate jimbo jambo ambalo ni DHAMBI
Huyu bwana haeleweki na mara nyingi speech zake huwa na makelele na majigambo, uzushi , kujidefend, kukashifu badala ya kutoa mambo yenye contents ambazo waTZ wanataka kuzisikia ili angalau matumaini yao kwa Mafisadi yarejee.
MI NAMTAKIA MAFANIKIO KATIKA KUIZAMISHA VEMA " MV SPICE MAGAMBA" ikiwa imejaza kupita kiasi mafisadi ambao wamekataa kuachia meli ili wengine wa safiri salama na kuamua kama ni kuzama basi tuzame tufe wote wote.