Mukama nilimsikia katika taarifa ya habari ya usiku ya TBC1 kuwa maazimio ya kikao hayakutaja majina ya watu. Nikajiuliza kama hapakuwa na majina ya watu mafisadi wanaopigana nao wako wapi? Kama hawakuwataja kwa majina ni kwa sababu hawajawafahamu au hawapo? Maazimio yalikuwa ya nini na yalikuwa yakiwalenga kina nani?