Mukama aviabisha vyombo vya Usalama: Adai CDM imeingiza mamluki toka ng'ambo

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
1,221
1,788
Akizungumza na vyombo vya habari leo mjini Igunga,katibu mkuu wa ccm Mukama,amejidhalilisha yeye na serikali yake,kwa kusema et chadema wameingiza makomandoo 30 waliofanyiwa mafunzo ya kikomandoo huko Afganistan.

Ni aibu kwa Mukama na serikali yake ya ccm,na leo tumejuwa rasmi kuwa hatuna usalama wa Taifa,inawezekanaje chama kisicho na dola kuingiza makomandoo nchini na dola kukaa kimya?Huyu Mukama ameonyesha jinsi gani upeo wake wa kufikiri ulivyo mdogo.

Tuna taarifa za uhakika kuwa baada ya Nape na uongozi wote wa ccm kukubaliana kutumia wale vijana wao waliokuwa kwenye makambi haramu mkoani Singida,sasa wamekuja na hoja kuwa chadema ndio wameingiza ili kupotosha umma,kimsingi ni kwamba wao sasa ndio wanawatumia hawa vijana wao baada ya Umma wa Igunga wa kuwakataa,na sasa moja ya option pekee ni kutisha wananchi.

Chadema tunamtaka Mukama na chama chake atambue alama za nyakati,Igunga imeenda,na aache mara moja kutishia wananchi,kwa propaganda za kihuni.Tuna taarifa za uhakika za ccm kufanya uhuni na kisha kuisingizia chadema ili kupata kura za huruma,Tunawatahadharisha ccm kuwa kamwe hawataweza,kwani haki na ukweli vitashinda daima.

Wakati ccm wakiendelea kukorogana na kuja na propaganda za kihuni,Chadema kwa upande wake imeendelea kufanya mikutano mitatu kila kata huku mgombea ambaye ni mbunge anayesubiri kuapishwa akifanya mikutano minne.

ALUTA CONTINUA
 
We have just enough religions to make us hate, but not enough to make us love one another.

I believe Chadema will overcome this kind of cheap CCM politics.


Chadema Motto "Whenever you are confronted with an opponent in politics with religion issues. Conquer him with love."
 
CCM ni chama cha Kikenge. Wanafikiri hata leo bado wanaweza kuwafool watanzania kwa uongo na wakawaamini kama wazee wetu waliokuwa wanaamini kila kitu ili mradi tu kimetangazwa redioni au na kiongozi. Kizazi cha sasa ni cha Dotcom lazima walielewe hilo.
 
Kazeni msuli kuwaelimisha wananchi kukataa kuhadaiwa,Mh Diwani na wewe story zako unatuambiya kama wote tuko Igunga tupe ile stori tamu kwa mfano sasa tunaona wamama na vidole viwili tuu wazee wakiume na vidole viwili vipi wanasenaje kuhusu CCM danganya toto
Waambie wananchi wakae mbali na Mukama tawalowesha na mate anayotematema
all the best guys GOd bless the nation is behind you
 
Sasa mukama ndio kabisaa akili yake
ni mgando atoe ushahidi la sivyo
usalama wa taifa umedhalilishwa
kuwa wapo likizo kwa Kauli za
mukama ccm wanaunda bomu la
kuwauwa wenyewe mukama na ccm tunasema
mkubwa hatishiwi nyau .
 
Akizungumza na vyombo vya habari leo mjini Igunga,katibu mkuu wa ccm Mukama,amejidhalilisha yeye na serikali yake,kwa kusema et chadema wameingiza makomandoo 30 waliofanyiwa mafunzo ya kikomandoo huko Afganistan.

Ni aibu kwa Mukama na serikali yake ya ccm,na leo tumejuwa rasmi kuwa hatuna usalama wa Taifa,inawezekanaje chama kisicho na dola kuingiza makomandoo nchini na dola kukaa kimya?Huyu Mukama ameonyesha jinsi gani upeo wake wa kufikiri ulivyo mdogo.

Tuna taarifa za uhakika kuwa baada ya Nape na uongozi wote wa ccm kukubaliana kutumia wale vijana wao waliokuwa kwenye makambi haramu mkoani Singida,sasa wamekuja na hoja kuwa chadema ndio wameingiza ili kupotosha umma,kimsingi ni kwamba wao sasa ndio wanawatumia hawa vijana wao baada ya Umma wa Igunga wa kuwakataa,na sasa moja ya option pekee ni kutisha wananchi.

Chadema tunamtaka Mukama na chama chake atambue alama za nyakati,Igunga imeenda,na aache mara moja kutishia wananchi,kwa propaganda za kihuni.Tuna taarifa za uhakika za ccm kufanya uhuni na kisha kuisingizia chadema ili kupata kura za huruma,Tunawatahadharisha ccm kuwa kamwe hawataweza,kwani haki na ukweli vitashinda daima.

Wakati ccm wakiendelea kukorogana na kuja na propaganda za kihuni,Chadema kwa upande wake imeendelea kufanya mikutano mitatu kila kata huku mgombea ambaye ni mbunge anayesubiri kuapishwa akifanya mikutano minne.

ALUTA CONTINUA
Hili swala la makomandoo ni swala zito kwa kweli, Polisi wanapaswa kumuhoji mukama juu ya ili na awe shaidi namba moja coz yeye ndo wa kwanza kulizungumzia hili.
 
Watacheza sana rafu lakini haitawasaidia, wanadhani miaka yote wabongo wataendelea kudanganywa kama ule mwaka Walivyotangaza kwamba CUF wameingiza Kontena la visu. najaribu kujiuliza hivi kwa sasa kuna Mwana-CCM anaweza kujitambulisha waziwazi mbele ya watu makini? Maana CCM imekuwa kituko sasa, huwezi ukaongozwa na mtu kama JK utegemee chama chako ku-prosper
 
Hili swala la makomandoo ni swala zito kwa kweli, Polisi wanapaswa kumuhoji mukama juu ya ili na awe shaidi namba moja coz yeye ndo wa kwanza kulizungumzia hili.
Angekuwa ni mpinzani ametoa hayo madai ya kiendawazimu, tayari angekuwa ameshafikishwa kwa Afande Manumba kujieleza. Lakini kwa kuwa na Magamba, hata yatoe tuhuma nzito kiasi gani kuhusu usalama wa taifa watabaki wanachekelea tu kama mwenyekiti wao.
 
Huyu mjita ni kutumia masaburi kufikiri au kachanganyikiwa kuona mahela yore waliyomwaga yataenda kwa wahuni wenye sera ya kula magamba na kulala magwanda. Wajita wenzake hebu muelimisheni huyu mjinga. Interahamwe na mungiki hawajawakamata na Leo wanaleta makomandoo, how come?
 
Mkuu Nanyoro, Naomba ufikishe huu mtazamo wangu kwa viongozi wa chadema walioko Igunga

"Think out of the Box please..."

jamani kuweni makini na huyu mzee pengine anaongea kinyumenyume kumbe CCM ndo imeleta watu wake waje wafanye ulipuaji isemekane ni CDM . Guys please don't take this message for granted, it may have a maxmum impact for our people in Igunga. Tumeshaona attempt za CCM kumwagia tindikali, kuchoma nyumba na vituko vingine vingi ambavyo vimeshindwa kuleta matokeo tarajio.

Mimi moyoni napata wasiwasi kwamba kuna kitu kikubwa kinataka kufanywa na CCM ili kuvuruga uchaguzi Igunga na hasa siku ya uchaguzi au siku chache kabla.
Chadema lazima waongezee inteligence na ulinzi maana inaonekana CCM hawahitaji tena uchuguzi ufanyike tarehe 2 ila wanataka kuvuruga uchaguzi ili CDM ibebeshwe lawama za vurugu na baadaye uchaguzi urudiwe upya na watu watakuwa scared.

Jamani naomba CDM wawe waangalifu sana na hizi statement, Mukama ni mtu mkubwa sana na anajua kila kitu kwenye hii nchi hivyo hawezi kuongea maneno haya bila kuwa na siri kubwa iliyofichika na hatachukuliwa hatua yoyote zaidi ya polisi kuzuga tu kuwa wameshamhoji.

CCM inataka kufanya kitu cha hatari sana pale Igunga kama CDM hawatakitegua mapema kabla hakijatokea.

Jamani we need to pray na hata mlioko huko field mwombeni Mungu sana kwa wale Wakristo mnaweza kufunga hata siku chache mkiliombea swala hili ili Mungu awaabishe madui zenu.

Haki itatendeka tu pale Mungu akiwa upande wetu.

Mungu irehemu Igunga na watu wake. Pia warehemu watu
 
Tunaomba kama kweli usalama Wa taifa kama wapo wamhoji Mkama la sivyo itaonyesha usalama Wa taifa uko nyuma ya ccm.
 
Komandoo Malaria Sugu ameishaelekea Igunga kwa ajili ya ughaidi na kuwafundisha vijana wa kiislamu kubeba mabomu na kujitoa muhanga. Wao magmata ndio wameingiza maghaidi Igunga, akiwemo MS
 
Kunauhusiano gani kati ya kauli za mwaka jana kuwa CDM chama cha wakristo na leo Afganistan ambako ni nchi ya Kiislamu?. Nisawa na kusema gari is not equal to jiwe. Alitoka MAkamba na sasa Mukama. KAzi iko. HAya mambo waachie vijana na sio hawa wazee ambao shule waliiacha miaka 40 iliyopita!!
 
Usalama wa taifa au usalama wa ccm?tusijidangdnye kuwa na usalama wa taifa haupo kwa kuwa twiga wasingetoroshwa ,magogo yasingesafirishwa sukari ,mahindi visingevuka mipaka madawa ya kulevya yasingeingia nchini ,watu wasingetoa wala kupokea rushwa ,na mafisadi wasingekuwepo
 
Mkuu Ngonini,Haya ya kutishia watu kwa mgongo wa CHADEMA mara makomandoo,mara magaidi hayana tofauti kubwa na zile propaganda za mwaka jana za Shimbo!.Na inasadikika vile vitisho ni moja ya sababu ya watu wachache kujitokeza kupiga kura,kwa hiyo CHADEMA inabidi wajitahidi kuwapiga dozi ya kudumu(elimu),ili hawa jamaa wasiweze kuwayumbisha wana Igunga katika maamuzi yao,maana CCM wamekata tamaa,wako desparate kuja na upuuzi wowote katika kipindi kilichobaki-Akili zao ziko likizo.
Mkuu Nanyoro, Naomba ufikishe huu mtazamo wangu kwa viongozi wa chadema walioko Igunga

"Think out of the Box please..."

jamani kuweni makini na huyu mzee pengine anaongea kinyumenyume kumbe CCM ndo imeleta watu wake waje wafanye ulipuaji isemekane ni CDM . Guys please don't take this message for granted, it may have a maxmum impact for our people in Igunga. Tumeshaona attempt za CCM kumwagia tindikali, kuchoma nyumba na vituko vingine vingi ambavyo vimeshindwa kuleta matokeo tarajio.

Mimi moyoni napata wasiwasi kwamba kuna kitu kikubwa kinataka kufanywa na CCM ili kuvuruga uchaguzi Igunga na hasa siku ya uchaguzi au siku chache kabla.
Chadema lazima waongezee inteligence na ulinzi maana inaonekana CCM hawahitaji tena uchuguzi ufanyike tarehe 2 ila wanataka kuvuruga uchaguzi ili CDM ibebeshwe lawama za vurugu na baadaye uchaguzi urudiwe upya na watu watakuwa scared.

Jamani naomba CDM wawe waangalifu sana na hizi statement, Mukama ni mtu mkubwa sana na anajua kila kitu kwenye hii nchi hivyo hawezi kuongea maneno haya bila kuwa na siri kubwa iliyofichika na hatachukuliwa hatua yoyote zaidi ya polisi kuzuga tu kuwa wameshamhoji.

CCM inataka kufanya kitu cha hatari sana pale Igunga kama CDM hawatakitegua mapema kabla hakijatokea.

Jamani we need to pray na hata mlioko huko field mwombeni Mungu sana kwa wale Wakristo mnaweza kufunga hata siku chache mkiliombea swala hili ili Mungu awaabishe madui zenu.

Haki itatendeka tu pale Mungu akiwa upande wetu.

Mungu irehemu Igunga na watu wake. Pia warehemu watu
 
Walipomuweka Mukama kuwa katibu mkuu nilifikiri ana busara kidogo anaweza kukisaidia chama lakini anazidi ku prove ndivyo sivyo.

Naungana na Ngonini hapo juu kuwa tamko hili lisipuuzwe limetoka kwa kiongozi mkubwa inawezekana kabisa kuna kitu kikubwa CCM imepanga kukifanya likiwemo la kujilipua, lazima wapenda amani na si CDM pekee tuwe na tahadhali kubwa ikiwa ni pamoja na CDM kuriporti polisi.

Haijawahi kutokea CCM ikawa na wasiwasi wa kushindwa kama wakati huu maana kushindwa kwa asilimia 80 kwa chama kongwe kama CCM si aibu tu ni fedheha kwa hiyo wako radhi kufanya kitu chochote ilmradi uchaguzi usifanyike.
 
huyu mukama naye vipi? maskini ya mungu wee kwa kauli hizi za mukama kama huu uchaguzi ungekuwa unafanyika majimbo ya watu wenye upeo tayari ccm wangeshashindwa. Hivi mukama anaweza kusema haya maneno kwenye maeneo kama Kawe, Mwanza mjini au Arsuha? Si watu watamuona tu mzee mpuuzi tu asiyejua kusoma alama za nyakati?

Badala ya kujibu maswali kwa nini Igunga ni miongoni mwa majimbo maskini sana Tanzania pamoja na kusimamiwa na mbunge wa ccm mwenye ukwasi wa kutisha aliyepita ambaye hata hivyo hajawahi hata siku moja kuwakilisha matatizo ya wana igunga bungeni yeye analeta vitisho vya ugaidi? Hivi wana igunga mnahitaji sababu gani nyingine ya kuwatosa ccm na mbunge wao zaidi ya kauli hizi za huyu mzee mukama anayeleta dharau kwenu kana kwamba hamuwezi kupambanua uongo na ukweli na kuwaletea vitisho vya afghanistan?
 
naungana na waliosema chadema izungumze na waandishi iseme ccm wathibitishe madai yao la sivyo aibu kwao na kwamba inawezekana wanataka kufanya fujo ila wanaanza kujenga mazingizi chadema ionekane ndio wamefanya. taarifa kama hizo wangetoa polisi, mara intarahamwe, al quida etc
 
Back
Top Bottom